Mkurugenzi mkuu
wa PSPF Adam Mayingu
Pensheni
zinatolewa na mifuko iliyopo hapa nchini hazitoshelezi mahitaji ya watanzania
wakiwemo wastaafu na familia zao. Takwimu zilizotolewa mwaka 2012 zinaonesha ya
kuwa ni watu milioni 1.7 tu ndio waliojiunga na
mifuko ya hifadhi ya jamii wakati idadi ya watanzania wote ni milioni 44.9 hii
ikiwa ni asilimia 6.5 tu ya nguvu kazi yote ya watu milioni 23.7. Hivyo ni kwamba asilimia 93.5 ya watanzania
wote wanaotegemewa kuwa ni milioni 44.9 hawana kinga ya hifadhi ya jamii ya
aina yeyote.
Hifadhi ya Jamii ni haki ya kila Mtanzania. Haki hii imeanishwa wazi katika Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 11(1) na Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003.
Haki
hii pia imeiainishwa kwenye mkataba wa kimataifa wa haki za binadamu wa mwaka
1948 pamoja na mikataba ya shirika la kazi duniani (ILO) ibara ya 102 ya mwaka
1952.
Idadi
kubwa ya watanzania hawana elimu ya hifadhi ya jamii inayoweza kuwaelemisha juu
ya mafao yanayotolewa, wajibu wao, na haki zao za pensheni kwa ujumla. Kuna
haja kubwa hata kuelemishwa juu umma juu ya kujiunga na mifuko ya pensheni ya
ziadi ya kujiunga kwa hiari hata kama ni wanachama wa wachangiaji wa mifuko hii
ya lazima kisheria. Kufuatia kupitishwa na sheria ya
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Sheria Na. 8 ya
mwaka, 2008 mtu yeyote anaweza kujiunga na mfuko wowote wa pensheni ya hifadhi
ya jamii.
Uanachama kwenye mifuko ya ziada iliyoruhusiwa na SSRA kuanzishwa na mifuko hii
ya pensheni ya hifadhi ya jamii ni ya hiari kwa mtu yeyote aliyeajiriwa au
kujiajiri mwenyewe, mwanachama aliye katika mifuko mingine, na kwamba
mwanachama wa mpango wa hiari anayo fursa ya kuhamia kwenye mpango wa uchangiaji
kwa mujibu wa sheria.
Mfuko wa pensheni wa PSPF ni taasisi
ya hifadhi ya jamii iliyoanzishwa kwa sheria Namba 2 ya mafao la hitimisho la
kazi kwa watumishi wa umma ya mwaka 1999
Mabadiliko katika sekta ya hifadhi
ya jamii nchini yamepelekea kuwepo na mabadiliko ya sheria ya mfuko wa
pensheni wa (PSPF). Sheria ya Mfuko wa pensheni wa
PSPF sasa unaruhusu kusajili wanachama katika sekta zote za umma na binafsi. Na
kwa sasa mfuko una mipango miwili ya uchangiaji wa lazima yaani PSPF Mandatory Scheme na mpango
wa uchangiaji wa hiari yaani PSPFSupplementary
Scheme yaani kwa kifupi PSS
Adam Mayingu ambaye ndiye Mkurugenzi mkuu anasema
mwanachama wa mpango huu anastahili kulipwa michango pamoja na faida
itakayopatikana kutokana uwekezaji ambayo huwekwa katika akiba mara mbili kwa
mwaka yaani kwa mwezi wa Januari na Julai.
Anaongezea
kwa kusema ya kuwa mpango huu wa hiari ni mahususi kwa ajili ya kuwapatia
huduma ya hifadhi ya jamii wale wote ambao awali kutokana na matakwa ya
kisheria hawakuweza kujiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. “Watanzania wachukue fursa hii
kujiwekea akiba ya ziada hata kwa wale ambao tayari wamo katika mifuko
mabalimbali ya hifadhi ya jamii hii itawasaidia kujiongezea na kutunisha na
hivyo kunufaika na mafao ya muda mrefu na ya muda mfupi wakati wanapoendelea
kufanya kazi na baada ya kustaafu,” anasema mkurugenzi mkuu.
Katika mpango huu wa uchangiaji wa hiari wa wa pensheni wa PSPF, mwanachama anapaswa kuchangia si chini ya Tshs 10,000 kwa mwezi. Michango inaweza kuwasilishwa kwa siku, wiki, mwezi au awamu. Mwanachama anawekewa gawio la akiba yake kwa kila mwaka mara moja. Uanachama ni kwa watanzania wote na wasio watanzania wanaofanya kazi nchini na hata waliopo nje ya nchi. Wanachama waliokwisha kujiunga na mifuko mingine ya hifadhi ya jamii ikiwemo mfuko wa pensheni wa PSPF wanaweza kujiunga na mpango huu. “Hivyo wananchi wote mnakaribishwa kujiunga ili kufaidika na mpango huu hiari wa mfuko wa pensheni wa PSPF” mkurugenzi mkuu anasema.
Mayingu ambaye ndiye mkurugenzi mkuu
wa PSPF anasema Mpango huu wa hiari umeanzishwa na mfuko wa pensheni wa PSPF
kwa ajili ya kupanua wigo wa uwanachama kwa kuandikisha wananchi waliojiajiri
au kuajiriwa katika sekta rasmi na isiyo rasmi mpango huu utawezesha wale wote
ambao hapo awali hawakuweza kupata huduma ya hifadhi ya jamii kutokana na
kutokua na ajira rasmi vilevile utawawezesha wananchi ambao tayari ni wanachama
katika mifuko ya hifadhi ya jamii iliyopo kuweza kuwa na akiba za ziada.
Anasema hifadhi ya jamii ni haki ya kila mtu na
si kwa wale tu walio katika ajira rasmi ila hata kwa wale waliojiajiri wenyewe
na hata kwa wale ambao ni wanachama wa katika mifuko ya hifadhi ya jamii nchini
kuweza kuwa na akiba ya ziada.
“Kwa sababu mpaka sasa kulingana na takwimu
zilizotolewa mwaka 2012 idadi ya watanzania wote ni milioni 44.9 ambao kati yao
watu milioni 1.7 tu ndio waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii, hii ikiwa
ni asilimia 6.5 tu ya nguvu kazi yote ya watu milioni 23.7”. Ananukuu
mkurugenzi mkuu.
Kwa vile hifadhi ya
jamii ni haki ya kila mtu mkurugenzi mkuu wa PSPF ndugu Mayingu anasema ndiyo
maana mfuko wa pensheni PSPF tuna mpango wa uanachama wa hiari kama mkakati wa makusudi juu ya kupanua
wigo wa hifadhi ya jamii ili kuhakikisha
ya kuwa hata wale waliojiajiri kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii kwa
hiari
na hata wale wanachama wa mifuko iliyopo kuweza kuwa na akiba ya ziada ya
kutosha kwa baadaye.
Hili ni jambo ambalo
liko wazi kabisa ya kwamba kila binadamu ana uhusiano mkubwa na hifadhi ya
jamii iwe kinadharia au kivitendo kutoka kuzaliwa kwake mpaka kufa, binadamu
mwenyewe lazima ajishughulishe na kazi hatarishi na kuugua magojwa
mbalimbali na kwa hiyo binadamu lazima
akumbane na majanga mbalimbali kama vile majanga ya kiuchumi na ya kijamii yanayosababishwa
na kukoma au kupungua kipato kutokana na maradhi, kujifungua mtoto, ajali za
kuumia kazini, ukosefu wa ajira, ulemavu, uzee, kifo na kuongezeka kwa gharama
za matibabu haya majanga yote ni matukio ya kila siku kwa binadamu ambayo
hayatabiriki na yote yanaaangukia kwenye mpango wa hifadhi ya jamii. Hivyo ni
kitu cha asili ya kwamba kila mtu lazima ajue hifadhi ya jamii ni nini kwa
sababu ni sehemu ya maisha ya mwanadamu
Na ndiyo maana mfuko wa
pensheni wa PSPF unakaribisha
wananchi wote wenye umri wa kufanya kazi, kuanzia miaka 18 na zaidi walioajiriwa
katika sekta iliyo rasmi hata kama wanachama kwenye mifuko iliyopo hapa
nchini au sekta isiyo rasmi yaani kwa wale waliojiajiri kama vile Wakulima,
wafanyabiashara ndogondogo,wasusi,vinyozi,mamalishe,mafundi cherehani n.k. kuwa wote wana haki ya kujiunga na mpango wa
uchangiaji wa hiari wa mfuko wa pensheni wa PSPF
Mkurugenzi
mkuu anasema uanachama wa mpango huu wa hiari wa PSPF ni kwa raia na asiye raia
wa Tanzania anayefanya kazi nchini na nje ya nchi hivyo hauna ubaguzi nchi wala
wa rangi ya mtu. Mayingu anakumbusha ya kuwa pamoja na hayo ni kwamba mfanyakazi anapaswa kuwa mwanachama wa mfuko
mmoja tu katika mpango wa lazima, lakini ana haki ya kujiunga na mpango wa
hiari zaidi ya mmoja kama huu wa mfuko wa pensheni wa PSPF.
Anasema aina za mafao yanayo tolewa na mpango huu wa hiari chini ya
mfuko wa pensheni wa PSPF ni kama vile fao la uzeeni, fao ya kuumia kazini, fao
la kifo, fao la elimu, fao la ujasiriamali, fao ya urithi, fao ugonjwa/ulemavu,
na fao la kujitoa. Mayingu vile vile
anasema mafao haya hutolewa na kunufaika sawasawa bila kujali ya kuwa
mwanachama anachangia kwa hiari au kwa lazima kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii.
“Hivyo mtu yeyote aliyejiajiri, mkulima,
mvuvi, mfanyakazi wa ndani, wafanya biashara wadogo wanaweza kujiandikisha kwa
hiari na kulipa kadri ya uwezo wake wa mapato kwenye mfuko wa pensheni wa
PSPF. Uchangiaji katika mpango huu wa hiari wa PSPF Wanachama wana uhuru wa kuchagua jinsi ambavyo wanaweza
kuwasilisha michango yao, iwapo ni kwa wiki Mwezi au kwa msimu kutegemea na
upatikanaji wa kipato cha ziada kwa ajili ya akiba na michango huwasilishwa
moja kwa moja kupitia akaunti ya benki au wakala wa malipo wa M-pesa, Tigo-pesa
na Airtel money. Na kiwango cha uchangiaji ni kuanzia shilingi 10,000 za
kitanzania au zaidi”. Mkurugenzi mkuu
anabainisha.
“NIMEJIUNGA kuwa mwanachama wa hiari katika Mfuko
wa Pensheni wa PSPF, kwa kuwa kuna utaratibu baada miezi 12 unaweza kuchukua
fedha zako,” anaanza kueleza, Charles Lucas mpiga picha wa gazeti la majira ’
alipozungumza na Kituo cha HakiPensheni .
Lucas ambaye ni mwanachama wa mfuko wa hiari wa
PSPF na mpiga picha mwandamizi wa gazeti la majira, anasema ni muhimu kwa
wajasiriamali na watu wengine walio katika sekta isiyo rasmi kujiunga na mfuko
huu wa PSPF ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zilizopo kwa kwamba
yeye ana wasilisha michangi yake kwa
wiki, mwezi au msimu kutegemeana na upatikanaji wa kipato cha ziada kwa ajili
ya akiba.
Anasema mtu yeyote anaweza kuwa mwanachama
kwa kujiunga na mpango huu wa hiari kwa kujaza formu PSS FN.1 na kuambatanisha
picha moja ya rangi yaani passport size pamoja na taarifa muhimu za wanachama
kama vile; majina; tarehe ya kuzaliwa;
anwani na nambari za simu; shughuli au kazi na mara baada ya kukamilisha
usajili, mwanachama hupewa kitambulisho na nambari ya uanachama
“Katika mpango huu wa
uchangiaji hiari wa mfuko wa pensheni wa PSPF mwanachama akisha anza kuchangia naye anakuwa na haki ya kupata mafao yote yatolewayo
na mpango
huu wa hiari wa PSPF”.Mayingu
anabaisha wazi
Mkurugenzi mkuu anasema mafao katika
mpango huu wa hiari mwanachama huwa anastahili kulipwa michango pamoja na riba
inayokokotolewa kwa mujibu wa viwango vya riba vilivyoko katika soko kulingana
na mfumuko wa bei na kwamba riba ambayo ni asimilia sita (6) huongezwa katika
akiba ya mwanachama mara mbili kwa mwaka katika miezi ya Januari na Julai
Na anaendelea kubainisha ya kuwa mafao
yaliyopo katika mpango wa hiari ni ya aina sita
(6) kama vile fao la elimu ambalo litatolewa kwa mwanachama ambaye
amechangia kwenye mfuko kwa kipindi kisichopungua miezi 12.
“Nusu ya akiba ya mwanachama yaani
asilimia 50 ya mchango itatumika kulipa fao hili na nusu itabaki katika akaunti
ya mwanachama kwa ajili ya akiba ya uzeeni na mwanachama anapaswa kuandika
barua ya maombi.
Kwa upande wa fao la ujasiriamali
huwa linatolewa kwa mwanachama ambaye amechangia kwenye mfuko kwa kipindi
kisichopungua miaka kumi na mbili (12) na nusu ya akiba ya mwanachama yaani
asilimia 50 ya mchango inatumika kulipa fao hili na nusu yake inayobaki katika
akaunti ya mwanachama hutumika kwa ajili ya akiba ya uzeeni na vile vile
mwanachama atapaswa kuandika barua ya maombi.
Anasema mpango huu wa hiari
Mwanachama anapata hata fao la uzeeni ambalo hulipwa kwa mwanachama
aliyefikisha miaka 55 au zaidi. Mwanachama analipwa akiba yake ya asilimia mia
moja (100%) pamoja na riba itakayokokotolewa. Mwanachama anapaswa kuandika
barua ya maombi na kuambatanisha kitambulisho cha uanachama.
“Wakati fao la kifo hulipwa kwa
wategemezi wa mwanachama aliyefariki. Malipo yanayolipwa ni ya asilimia mia
moja (100%) ya akiba ya mwanachama na riba inayokokotolewa. Wategemezi
wanapaswa kuwasilisha cheti cha kifo, kitambulisho cha uanachama za marehemu
pamoja na nyaraka za mahakama zinazodhibitisha msimamizi wa mirathi na wategemezi
wa marehemu. Aidha mpango wa mirathi unahitajika kutoka mahakamani”. Mkurugenzi
mkuu anataja
Anaendelea kwa kusema ya kuwa fao la ugonjwa au ulemavu huwa
linatolewa kwa mwanachama ambaye kutokana na sababu za ugonjwa au ulemavu
hataweza tena kumudu kufanya kazi za uzalishaji kwa ajili ya kujipatia kipato
cha kila siku. Mwanachama analipwa asilimia mia moja (100%)
ya akiba yake pamoja
na riba inayokokotolewa. Mwanachama anawasilisha barua ya maombi, kitambulisho
cha uanachama na uthibitisho wa taarifa ya daktari
Kwa upande wa fao la kujitoa anasema fao
hili linalipwa kwa mwanachama anayetaka kujitoa. Mwanachama analipwa asilimia
mia moja (100%) ya akiba yake pamoja na riba itakayokokotolewa. Mwanachama
anatakiwa kuuarifu mfuko kuhusu kujitoa kwa njia ya barua na kurejesha
kitambulisho cha mfuko.
Anasema
mwanachama wa mpango huu wa hiari wa PSPF anapolazimika kuchukua michango yake
yote na faida kutokana na sababu zozote zile, anaweza tena kuchangia upya bila
masharti yoyote,” alisema.
Mkurugenzi
mkuu anasema ya kwamba uanachama ni wa
hiari kwa mtu yeyote aliyeajiriwa au kujiajiri mwenyewe, mwanachama aliye
katika mifuko mingine, na kwamba mwanachama wa mpango wa hiari anayo fursa ya
kuhamia kwenye mpango wa uchangiaji kwa mujibu wa sheria ya mfuko wa pensheni
wa PSPF
Akizungumzia
mwamko wa watu kujiunga na mpango huu wa hiari yaani wa PSS, Mkurugenzi mkuu
anasema kumekuwa na mafanikio makubwa kwani tangu kuzinduliwa kwake mapema
machi 7 mwaka 2013 tayari wanachama zaidi ya 5,000 wamejiunga na mpango huo.
“Makundi zaidi ya 25 yamejiunga na mfuko huu kutokana na ubora wa mafao yake na
mikopo inayotolewa kwa wanachama waliojiunga na mfuko huo kwa miaka mitano
tofauti na wakati wa nyuma ambapo mikopo ya nyumba ilitolewa kwa wanachama
waliobakiza miaka mitano ya kustaafu” anasema .
Anasema ya kuwa mfuko wa pensheni wa PSPF
una uzoefu wa muda mrefu katika sekta ya hifadhi ya jamii tangu ulipoanzishwa
mfumo wa hifadhi ya jamii usio wa kuchangia wa pensheni mwaka 1954 hadi mfuko
wa pensheni wa PSPF ulipobadilishwa mwaka 1999 kuwa mfuko wa pensheni
unaojitegeme. Mkurugenzi
mkuu anaongeza ya kuwa, watanzania
wasiwe na wasiwasi kwa kuwa thamani ya mfuko inaongezeka anatolea mfano ya
kuwa mwaka 2000 thamani ya mfuko ilikuwa fedha ya kitanzania shilingi bilioni
36, na mpaka mwaka huu 2014 imefika fedha za kitanzania shilingi trilioni
1.25
“Dira ya mfuko wetu wa PSPF ni kuwa mtoa huduma bora wa huduma za
hifadhi ya jamii nchini kwa dhima ya kutoa huduma zenye ushindani katika sekta
ya hifadhi ya jamii kwa wateja wao kwa kutumia watumishi wenye ari ya
kazi na teknolojia inayofaa. Maadili Yetu ni kuhakikisha ya kuwa
Mfuko unatoa huduma zake kwa wateja, wadau na umma kwa kuzingatia misingi ya
Uwajibikaji, Wajibu, Muitikio, Nidhamu, Juhudi. Uwazi na Unyenyekevu kwa wote”.
anataja
No comments :
Post a Comment