Tuesday, June 24, 2014

Umuhimu wa mafao ya pensheni kwa wazee wastaafu



 Some of the retired teachers who had TSC over their dues. Photo/FILE
Baadhi ya wazee wastaafu wakihojiwa na waandishi habari hawapo pichani picha na mitandao

Na Christian Gaya Majira Juni 24, 2014

Kadiri tunavyo kuwa wazee tunafanya kazi, tunazalisha na kipato chetu kinazidi kuwa kidogo zaidi na hivyo basi tunahitaji kupata kipato kutoka sehemu nyingine ili kuhakikisha ya kuwa tunaendeleza maisha yetu. Jamii na serikali mbalimbali za hapa Afrika na za huku ulaya ikiwemo nchi yetu ya Tanzania wameweza kuwa na vyombo mbalimbali kwa ajili kuwapa kinga kwa njia ya kuwapa kipato fulani kwa raia wake wanapofikia hali ya uzeeni kama sehemu ya kinga kwa ajili ya kupunguza umasikini kwa watu wastaafu na watu wengine waliofikia umri wa uzee ambayo ni kuanzia miaka sitini kwa mtanzania.

Lakini mipango hii inatugusa sisi wote kwani haijalishi kwa sasa wewe in tajiri au maskini,  halijalishi wewe ni mtoto au mtu mzima au una umri wa miaka mingapi kwa sasa mipango hii iiliyoiridhiwa inaweza kusaidia malengo hayo au ikawa ndiyo kizuizi cha kukua kwa maendeleo ya uchumi na kijamii nchini

Ikumbukwe ya kuwa idadi ya watu wanaofikia umri wa uzee inavyozidi kuongozeka kila siku, kinga ya hifadhi ya jamii ya wazee nayo inazidi kuingia kwenye matatizo zaidi. Kwa sababu sekta isiyo rasmi ya kijamii na mfumo wa hifadhi ya jamii unaotolewa na familia unazidi kupungua na kuwa dhaifu siku hadi siku. Na mfumo wa hifadhi ya jamii ulio rasmi kama vile unaotolewa na taasisi hizi zetu za hifadhi ya jamii za kuchangia na zile zisizo za kuchangia zinakabiriliwa na utumiaji ovyo wa michango ya wanachama kwa kuwekeza kwa kufuata maangizo ya wanasiasa bila kutumia vitego vya kitaalamu na kuwa na matumizi makubwa ya michango ya pensheni za wanachama bila vile vile bila ya kufuata kanuni na utaratibu wa uwekezaji michango ya pensheni ya wanachama. 

Kwa ujumla ni kwamba mifuko haina utaratibu wa kufuata utawala bora wa jinsi ya kuendesha taasisi hizi za hifadhi ya jamii, na matokeo yake idadi kubwa ya wazee ambao wamekuwa wakichangia katika kujenga taifa hili kwa muda mrefu hawana hata kinga ya uzee yaani kupatiwa mafao ya kustaafu ya kutosheleza mahitaji muhimu ya maisha yao ya kila siku.  Wakati huo huo utaratibu wa undeshaji wa mifuko ya jamii unaendelea kuwa uleule wa zamani badala kuja na mikakati ya kisayansi ili kuleta mabadiliko ya kisasa ya jinsi ya kuendesha mifuko hii ya hifadhi ya jamii. Cha kushangaza ni kuwa hakuna mfuko wa hifadhi ya jamii unaotoa maelezo halisi ya mwenendo wa hifadhi ya jamii. Leo ukidadisi juu ya idadi ya wazee wanaopata pensheni kila mwezi ni idadi ndogo sana ukilinganisha na idadi ya wazee wanaostaafu kila siku. 

Hii ina maana ya kuwa wengi wanaishia kuondoa mafao yao au kwa njia halali au ya udanganyifu na hii inawezekana kufanywa kwa makusudi au kwa mwoga wa taasisi hizi kwa lengo la kukwepa kusimamia mafao haya ya uzee. Matokeo yake ni kwamba idadi ya wastaafu inazidi kupungua kila siku na wakati huo huo umaskini  unazidi kuingia kwa kasi kwa wazee. 

Kwa mwaka 1990 nusu ya bilioni ya watu ambao ni kama zaidi ya asilimia tisa (9) ya watu wote duniani  walikuwa zaidi ya umri wa miaka 60. Na inakisiwa ya kuwa kufikia mwaka 2030, idadi hiyo itaongezeka mara tatu (3) mpaka kufikia bilioni 1.4. na haya mabadiliko ya kuongezeka yatatokea kwa nchi zinazoendelea ikiwemo nchi yetu Tanzania, ingawa zaidi ya nusu ya ongezeko hili itatokea nchi za Asia na zaidi ya robo itatokea huko China.

Na ikumbukwe ya kuwa mahitaji ya bima ya afya yanaongezeka zaidi pale nchi inapozidi kuwa na idadi kubwa wa wazee, kama unavyojua kuwa matatizo ya ugonjwa kwa umri wa uzee na teknolojia ya matibabu mara nyingi inafikiriwa kutumika zaidi kwa ajili ya kupambana na wazee zaidi.  Na wakati huo huo mifuko hii ya hifadhi ya jamii fedha ambazo zinatakiwa kuweka na kuwekeza pembeni kwa ajili ya  wazee watakao staafu mara nyingi zimelalamikiwa kutumika ovyo kwa kukosa uongozi na utawala wa bora wa mifuko ya hifadhi ya jamii kama ilivyoelezwa hapa juu. Kwa mfano inaonesha ya kuwa idadi kubwa ya michango ya pensheni iliwekezwa kwenye hatifungani na hivyo kupoteza kiwango kikubwa cha fedha za michango kwa mwaka. 

Na karibu idadi kubwa ya michango ya pensheni inayokusanywa inaonesha kutumika kwa ajili ya kuendeshea gharama za mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii. Pamoja na hayo karibu pensheni zote zinazotolewa mara chache sana zinafanyiwa marekebisho kulingana na mfumuko wa maisha ya kila siku kwa kurekebisha kwa kwa sababu labda mshahara kuongezeka au kurekebisha kufuatana na mfumuko wa bei ya bidhaa au huduma mstaafu anazonunua sokoni. 

Kwa hiyo ni kinga ndogo au hakuna kabisa kinga yeyote inayotolewa kwa wazee hawa waliostaafu. Na serikali inaweka bajeti kubwa sana kwa kuwalipa pensheni kubwa kwa wanasiasa na baadhi ya viongozi wa ngazi za juu ambao wao hawachangii hata kidogo  katika mapato yao ya mishahara minono wanayopata na hivyo kubebesha mzigo mkubwa kwa serikali kwa kutumia kodi za wananchi wanazotozwa badala ya kuwaboreshea huduma za kijamii na kiuchumi  nchini. Ingawa serikali imepanga kuwalipa wazee kiasi cha shilingi elfu kumi kwa wazee wote watakaokuwa wanafikia umri wa miaka 60 na kuendelea, kwa maana hii serikali inahitaji kuliangalia sana jambo hili kiundani ili kuleta usawa katika kugawana sawa mapato ya taifa bila ubaguzi wowote na kuibebesha serikali mzigo mkubwa. Kwa sababu unaweza ukakuta baadaye ukawaambiwa pensheni ya wazee ya shilingi elfu kumi inapunguzwa kwa sababu serikali haina fedha za kutosha kwa ajili ya wazee ambao kila siku idadi ya watanzania wengi wanafikisha umri wa kustaafu wa miaka sitini (60) inaongezeka. Lakini pamoja na hayo mipango ya kuwapatia kiwango hicho kidogo mpaka leo haijaanza kutekelezwa tangia itangazwe. 

Utafiti wa kuwianisha mapato kwa kuhakikisha ya kuwa mapato ya makusanyo ya taifa kutoka watu wenye uwezo zaidi na kuyagawanya upya kwa watu wenye pato la chini yaani maskini, na wakati huo huo lazima ijulikane ya kuwa watu wenye uwezo au matajiri huishi miaka mingi zaidi kuliko watu maskini  yaani wenye pato la chini kabisa na hivyo hao matajiri au wenye uwezo wakifikia umri wa kustaafu na kuanza kupata pensheni hupata kwa muda mrefu zaidi ukilinganisha na masikini

Lakini ikumbukwe  kuwa mfumo wa mifuko ya pensheni hapa nchini ina matatizo na changamoto nyingi mno kama vile utaratibu wa kuhamisha michango kutoka mfuko mmoja hadi mfuko mwingine pale mfanya kazi anapopata mwajili mwingine badala yake michango yote ya pensheni za wafanyakazi huishia kuiondoa kabla haijaiva na hivyo kuishia kuiondoa kabla haijaiva na hivyo kuishia kupunguza idadi ya michango  ya    mwanachama na baadae anapostaafu anaishiwa kuambiwa kuwa michango yake haitoshi kumpatia pensheni ya kila mwezi na kwa upande mwingine ni kwamba kunatofauti kubwa sana kwa upande wa idadi ya mafao yanayotolewa kulingana na idara ya 102 ya 1952 la shirika la kazi duniani ambalo lenyewe limeainisha mafao tisa kama vile fao la pensheni  ya uzee,pensheni ya ulemavu ,pensheni ya urithi ambayo ni mafao ya mda mrefu na mda mfupi ni kama vile ;fao la matibabu ,fao la kuumia kazini ,fao la msaada wa mazishi,fao la uzazi, fao la kutokuwa na kazi na la mwisho ni fao la msaada   kutunza kupunguza ukali wa utunzaji wa watoto. Na badala yake mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii inaishia kujumuisha pamoja na baadhi ya vivutio kwa wateja wao na kuitwa kama mafao jambo ambalo siyo kulingana na idara namba 102 ya mwaka 1952 ya ILO

Na kumekuwa na tofauti  kubwa na hata kwa upande wa fomula za ukokotoaji wa mafao, kwani kila mfuko wa pensheni ya hifadhi ya jamii ina fomula yake badala ya kutumia fomula zilizoainishwa na shirika la kazi duniani (ILO)kila mfuko unajitungia fomula zake za ukokotoaji. Ambayo inapelekea hata kuleta tofauti kubwa za pensheni wanazopata wastaafu madhalani unakuta katibu muhitasani anapata pensheni kubwa zaidi kulikomstaafu aliekuwa mkurugenzi mkuu wa kampuni nyingine .wakati huohuo ni asilimia 6 tu ya nguvukazi ndio wanachama wa mifuko hii ya hifadhi ya jamii.hivyo asilimia karbu 94 ya nguvu kazi hawana kinga ya hifadhi ya jamii.


Ingawa mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya hifadhi ya jamii anasema amesha fanyia kazi tayari na anasubiri maamuzi ya mwisho kutoka katika baraza la mawaziri kuamua utaratibu wa kuwa kutoka na fomula moja ya kukokotoa mafao kwa mifuko yote hapa nchini Tanzania bara

Mara nyingi ushirikishwaji wadau katika mifuko hii umekuwa kidogo sana kama siyo hakuna kabisa katika maamuzi ya  fedha zao za michango ambalo ni swala la utawala bora wa mifuko hii ya hifadhi ya jamii.


Hivyo kwa kukosa utawala bora umepelekea mara nyingi kuleta gharama kubwa za uendeshaji wa mifuko na hasa kuwekeza bila hata kufuata kanuni za uwekezaji na mara nyingine bila hata  na malengo dhabiti ya uwekezaji na kuishia kuwekeza kwenye maeneo yasiokuwa na tija hata kidogo. Na mwisho wa siku matatizo yote haya huishia kwa mchangiaji ambaye ndiye mwanachama kupatiwa pensheni hafifu na kupelekea kuzidisha janga la umaskini kila siku

Pensheni ni haki ya kila mtu hasa mwananchi yoyote awe anachangia au asichangie na hii inajulikana wazi na ndiyo maana hata katika idara ya 11 ya katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na sera ya taifa ya hifadhi ya hifadhi ya jamii ya mwaka 2003 inajieleza wazi na vilevile imeanishwa kwenye katiba wa shirika la kazi duniani ILO idara ya 102 ya mwaka 1952 na kwenye katiba ya kimataifa na haki za kibinaadamu ya mwaka 1948.


Na lengo kubwa la hifadhi ya jamii ni kuzuia umasikini, kupunguza au kuondoa umasikini, kuifidia jamii, kugawanya mapato sawasawa kwa wanajamii. Masuala mengi yanayogusa hifadhi ya jamii ni ya nyeti sana, yanagusa ni kiini muhimu sana cha wafanyakazi kwenye sekta rasmi na sekta zisizo rasmi hasa za watu masikini pamoja na sekta ya bima za jumuiya za waajiri

No comments :

Post a Comment