Daktari Ramadhani Dau
Mkurungenzi mkuu wa NSSF
Na Christian Gaya majira 14 januari 2014
Mfuko wa taifa wa hifadhi ya
jamii wa NSSF ulianza kama idara ya serikali mwaka 1964 kabla ya kuanzishwa
kama shirika la taifa la akiba ya wafanyakazi (NPF) kwa sheria Na 36 ya mwaka
1975. Shirika hili liliendelea hadi pale serikali ilipopitisha sheria Na 28 ya mwaka
1997 iliyoanzisha shirika la taifa la hifadhi ya jamii (NSSF) kama mpango
kamili wa hifadhi ya jamii unaozingatia kanuni za kimataifa za hifadhi ya jamii
Mabadiliko
hayo yameiwezesha NSSF kutoa mafao mengi na bora zaidi yakiwemo pensheni ya
ulemavu na fao la kuumia kazini na magonjwa yatokanayo na kazi kwa wanachama
wake na kuongoza kwa afrika mashariki na kati. Sheria hii ya kuumia kazini ya
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (Na. 28 ya 1997), ilianza kutekelezwa mwaka
2002.
Tanzania imeanza kuwahusisha
wafanyakazi wa sekta zisizo rasmi katika sheria za kazi ili kuwapatia kinga
kama vile za hifadhi ya jamii au haki za msingi kama vile likizo ya uzazi,
likizo ya ugonjwa na ruzuku ya serikali pindi wanapokuwa hawana kazi. Hata hivyo,
inaweza kuwa vigumu sana kutekeleza sheria hii katika nchi yetu kama vile OSHA
ambacho ndicho chombo cha kusimamia wa sheria za kazi hawana vitendea kazi au
rasilimali za kutosha za kufanyia kazi zao na mifumo ya taarifa/habari ni
duni.Aidha, wafanyakazi wengi wa hawajui haki zao, hivyo hawawezi kudai ulinzi
au haki zao kutoka kwa waajiri wao.
Tanzania
imeridhia Mkataba wa Ukaguzi Kazini, 1947 (Na. 81), na Itifaki Na. 81 ya 1995
katika Mkataba wa Ukaguzi wa Kazi, na sheria nyingine husika. Mfumo wa kisheria
uliopo unaundwa na Sheria ya Afya na Usalama Kazini ya mwaka 2003 na Sheria ya
Fidia kwa Wafanyakazi ya mwaka 2008. Kwa mara nyingine, kuwepo kwa mfumo huu na
hatua hizi zilizochukuliwa na Serikali kunaonyesha maendeleo yaliyo katika jambo
hili.
Kwa upande wa sheria na kanuni za
afya na usalama katika maeneo ya kazi (OHS), Tanzania kama nchi endelevu.
Tanzania hivi karibuni ilipitisha sera ya Afya na Usalama Katika Maeneo ya Kazi
(OHS) ambayo inafuata Mkataba 155 wa ILO yaani Shirika la Kazi Duniani katika
kufafanua sehemu yoyote ambayo watu wanapata maisha au kipato kama mahali pa
kazi.
Tanzania imeanzisha mfumo wa huduma
za msingi za afya ya umma ambao unajumuisha huduma za afya na usalama makazini
kwa wafanyakazi wote, iwe rasmi au isiyo rasmi, na inatakiwa kuwa na mfumo wa
ukaguzi wa kazi ambao unajumuisha sehemu zote za sekta rasmi na zisizo rasmi.
Katika
viwanda, idadi ya ajali kazini iliongezeka ghafla kutoka 90 mwaka 1999 hadi 309
mwaka 2008, kuanzia yale yenye idadi ndogo hadi yale yenye idadi kubwa ya ajali
miongoni mwa sekta tatu zilizochunguzwa. Kinyume chake, sekta ya biashara, na
hususan sekta ya huduma, imeonesha mwelekeo wa kupungua kwa ajali katika miaka yote,
ingawa kuna mabadiliko kila mwaka.
Idadi kubwa
ya ajali zilizoripotiwa hazikusababisha vifo, na hakukuwa na mfululizo wa ajali
kazini zilizosababisha vifo katika miaka hiyo, hii ilikuwa wastani wa karibu
ajali 22 kwa mwaka, vilevile kukiwa na mabadiliko kila mwaka. Wakati wote katika
miaka hiyo, viwanda vimekuwa na idadi kubwa zaidi ya ajali zilizoripotiwa
kusababisha vifo, kwa wastani wa ajali 12 kila mwaka. Kwa kuwa sekta ya kilimo ambayo
huajiri idadi kubwa ya wafanyakazi inajulikana kuwa na viwango vikubwa vya
ajali, kama ingeingizwa ingeonesha idadi ya ajali kuwa kubwa.
Idadi ya
wakaguzi wa kazi ni ishara ya uwezo wa Serikali kusimamia kanuni, sheria na
taratibu za usalama kazini. Mamlaka ya Usalama na Afya Kazini (OSHA), chini ya
Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana, inaendesha ukaguzi wake wa viwanda.
Inasemakana kuwa wakaguzi wa kazi, ukiondoa wale walioajiriwa na OSHA, wamebaki
kuwa wachache kwa idadi ya wastani 70 nchini Tanzania katika kipindi kuanzia
mwaka 2005 hadi 2009. Vilevile, kama wakipangwa kulingana na ajira, idadi ya
wakaguzi wa kazi ni ndogo sana na inazidi kupungua: Tanzania (bara) ilikuwa na
0.33 ya wakaguzi wa kazi kwa kila wafanyakazi 10,000 wa kulipwa, au wakaguzi wa
kazi 0.04 kwa kila watu 10,000 walioajiriwa.
Hii inaonyesha kuwa
wakaguzi wa kazi bado hawatoshi nchini Tanzania. Hii inatoa nafasi ya ajali
nyingi kutokea au mazingira mengine ya kazi yasiyo salama kutokea bila
kuripotiwa ili hatua sahihi ziweze kuchukuliwa ili kuimarisha mazingira ya kazi
yenye staha.
Licha ya kuwepo
Sheria ya Usalama na Afya Kazini ya mwaka 2003 yaani OSHA na kuundwa kwa Wakala
wa Usalama na Afya Kazini, suala la kazi salama halijashughulikiwa vya kutosha,
kama inavyoshuhudiwa na kuwepo kwa wakaguzi wachache sana wa kazi na ukosefu wa
raslimali
Hapo awali, maafisa
kazi walitakiwa kwa upande mmoja, kuendesha ukaguzi na uchunguzi wa kazi na, ikibidi,
kuwashtaki waajiri katika mahakama na, kwa upande mwingine, kuwa wenyeviti wa tume
za usuluhishi na maamuzi ambazo zilikuwa zikiwabana waajiri. Kazi za wakaguzi
wa kazi kwa sasa zimetenganishwa na zile za wasuluhishi na waamuzi. Kuna haja
ya kuajiri zaidi wakaguzi wa kazi, kuamsha ufahamu miongoni mwa wafanyakazi na
waajiri kuheshimu sheria.
Mapato ya chini na na ukosefu wa
ulinzi au uzingatiwaji wa haki unamaanisha kwamba wafanyakazi wengi hapa nchini
wapo katika mazingira magumu. Endapo itatokea wakaugua au kuumia na hivyo
kushindwa kuja kazini, wengi wanapoteza mishahara au ujira wao au kufukuzwa
kazi.
Na mara nyingi wanakuwa hawana kinga
ya hifadhi ya jamii au akiba ili kulipa bili za matibabu na kuwafanyia
ukarabati wa viungo bandia au kuwafanya waendelee na maisha mpaka watakapopata
kazi mpya. Hali hii inaweza kuonekana isiyo ya haki kabisa hususani kwa
wafanyakazi ambao awali ya yote, chanzo cha ugonjwa au kuumia ni hiyo kazi
yenyewe.
Wamiliki wa mahali au sehemu za
kazi ambapo wafanyakazi wanafanyia kazi zao wanaweza kufikiri mahali pa kazi
zao ni maeneo salama, lakini sehemu hizo hizo zinaweza kuwasilisha matatizo
kadhaa ya kiafya na ki-usalama kwa watu wanaofanya kazi ndani mwake.
Wafanyakazi wa sekta zisizorasmi
wanatambua kwamba kazi zao zinaweza kuwa hatari kwa afya zao. Utafiti wa hivi
karibuni huko California ulionyesha karibu wafanyakazi wawili kati ya watatu wa
sekta zisizo rasmi walioshiriki wanachukulia kazi zao kuwa “zenye
hatari/hatarishi” (Smith 2001).
Taratibu au sheria za Afya na
Usalama katika Maeneo ya Kazi yaani OHS, ambazo zimelenga katika kuzuia hatari
za kuumia au kupata ugonjwa katika sehemu za kazi, mara nyingi zinawalinda
wafanyakazi rasmi waliopo katika mazingira rasmi ya kazi kama vile migodini,
viwandani, ofisini na madukani.
Kanuni hizi haziwalindi wafanyakazi
ambao wanafanya kazi katika sekta zisizokuwa rasmi, kitu ambacho kinamaanisha kwamba
japokuwa kazi za sekta zisizo rasmi ni chanzo muhimu cha ajira, na ingawa kuna
hatari nyingi za kiafya na kiusalama katika kazi hizo, na japokuwa wafanyakazi
hao wapo katika mazingira magumu ya umasikini endapo wataugua au kuumia,
taratibu au sheria za OHS katika nchi hii ya Tanzania haziwazingatii.
Ili
kutatua tatizo hili la kuumia na kupatwa na ulemavu na magonjwa yatokanayo na
mahali pa kazi shirika la taifa la hifadhi ya jamii yaani NSSF linatoa mafao ya
kuumia kazini na magonjwa yatokanayo na kazi. Sheria hii ya kuumia kazini ya
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (Na. 28 ya 1997), ilianza kutekelezwa mwaka
2002;
Mkurugenzi
mkuu daktari Dau Ramadhani anasema mafao haya hulipwa kwa mwanachama aliyepata
ajali akiwa kazini au magonjwa yatokanayo na kazi anayoifanya na anazitaja sifa
zake zinazotakiwa ya kuwa awe tayari alishaandikishwa na NSSF kama mwanachama
na awe ameumia kutokana na kazi anayoifanya au kupata magonjwa yatokanayo na
kazi yake.
Pamoja
na haya yote ni kwamba NSSF hutoa fedha taslimu kama mojawapo ya mafao kwa
mwanachama aliyepata maumivu ya muda. Mafao yanayotolewa ni 60% ya wastani wa
mapato yake ya siku, na mafao haya hulipwa kwa muda usiozidi wiki 26 tangu tarehe
ya kuumia au kupata ugonjwa, na kwamba kwa mwanachama aliyepata maumivu ya
kudumu yaani maumivu ya 100% ya uwezo wake wa kufanya kazi, mafao yanayotolewa
ni 70% ya wastani wa mapato yake ya mwezi. Malipo hufanyika kutegemea viwango
vya kuumia kama vilivyoelewa katika Kanuni za NSSF za mafao haya Daktari Dau
anasisitiza
Daktari
Dau ambaye ndiye mkurugenzi mkuu wa NSSF anasema vile vile Shirika hutoa viungo
bandia kwa ajili ya kumsaidia mwanachama iwapo vitahitajika kama
vitakavyoelezwa na Madaktari wanaohusika. Viungo hivi ni vile vinavyopatikana
katika hospitali zilizopo ndani ya Tanzania
Anaongezea
na kusema ya kuwa siyo tu shirika hutoa mafao ya kuumia kazini na kupatwa na magonjwa
yatokanayo na kazi NSSF vile vile hutoa hata pensheni ya ulemavu pale
mwanachama anapogundulika ya kuwa amepatwa na ulemavu kwa sababu ya kazi
aliyokuwa akifanya, anasema ya kuwa pensheni
hii hulipwa kwa mwanachama aliyepoteza angalau 2/3 ya uwezo wake wa kufanya
kazi kutokana na ulemavu wa kimwili au kiakili kama utakavyothibitishwa na Bodi
ya Madaktari
Mkurugenzi mkuu anaainisha sifa zinazotakiwa
ya kwamba kunahitajika kuwa na uthibitisho
wa Bodi ya Madaktari wa kupoteza 2/3 ya uwezo wa kufanya kazi. Michango 180 au angalau 36 kati yake
michango 12 iwe imelipwa karibu na kupata ulemavu na awe chini ya umri wa kustaafu yaani miaka 60 ya kustaafu kwa
lazima
Dau anaeleza kwa kina ya kwamba mafao
yanayotolewa chini ya pensheni ya ulemavu ukokotoaji
ni wake ni sawa na ule wa pensheni ya uzee isipokuwa huongezwa 1% kwa kila
michango 12 inayozidi kiwango cha michango 180, na mafao yanayotolewa ni sawa pia na mafao ya pensheni ya uzee
yaani pensheni ya kila mwezi, mkupuo wa awali na mkupuo maalum kwa aliyekosa
sifa zinazotakiwa na pensheni hulipwa hadi mwanachama atakapofariki au
atakapotimiza umri wa kustaafu na kuhamia pensheni ya uzee.
Anasema ingawa Waajiri
wanaohusika kisheria kuandikishwa katika mfumo wa taifa wa hifadhi ya jamii wa
NSSF ni waajiri wote walio katika sekta binafsi, taasisi zisizokuwa za
kiserikali, ofisi za kibalozi zinazoajiri watanzania, taasisi za kimataifa
zinazofanya shughuli ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, taasisi za
wizara za serikali zinazoajiri wafanyakazi kwa masharti ya muda, mashirika ya
umma yanayoajiri wafanyakazi kwa mashari ya muda. Watu binafsi waliojiajiri
wenyewe, sehemu yoyote ya shughuli kama mwajiri mlipa michango na kupewa namba
ya uandikishaji mara tu anapoanza shughuli zake
“Lakini hata mtu yeyote
aliyejiajiri, mkulima, mfanyakazi wa ndani, wafanya biashara wadogo wanaweza
kujiandikisha kwa hiari na kulipa kadri ya uwezo wake kuanzia shilingi 20,000
kwa mwezi asilimia 20 ya mshahara wa kima cha chini (KCC) wa serikali na
atapata mafao yote saba yatolewayo na mfuko wa hifadhi ya jamii ikiwa na pamoja
na kunufaika na mafao ya kuumia kazini na magonjwa yatokanayo na kazi na
pensheni ya ulemavu” Daktari Dau anasistiza
No comments :
Post a Comment