Waziri wa Fedha Dkt. William Mgimwa (wa kwanza kulia), Mkurugenzi Mkuu
wa PPF William Erio (wa pili kulia), Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na
Vijana Dkt. Makongoro Mahanga (wa tatu kulia), na Mwenyekiti wa Kamati
ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mh. Zitto Kabwe wakitazama nembo mpya ya
Mfuko wa Pensheni wa PPF mara baada ya kuzinduliwa mwanzoni mwa Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanachama na Wadau wa PPF kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa AICC jijini Arusha.
Mfuko wa Pensheni wa PPF mara baada ya kuzinduliwa mwanzoni mwa Mkutano Mkuu wa 23 wa Wanachama na Wadau wa PPF kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa AICC jijini Arusha.
Waziri
wa fedha Dkt. Mgimwa akiwa mgeni rasmi
kwa niaba ya serikali ya Tanzania alianza kwa kuwakaribisha washiriki wote
kwenye mkutano wa 23 wa mwaka wa wanachama na wadau wa Mfuko wa Pensheni kwa
Mashirika ya Umma (PPF) uliofanyika hivi karibuni jijini Arusha.
Dkt.Mgimwa
aliupongeza Mfuko huo) kwa kutimiza miaka 35 tangu kuanzishwa kwake,ambapo
alisema hatua hiyo ni mafanikio makubwa siyo tu kwa kutimiza miaka hiyo, lakini
pia kwa kutimiza mafanikio ya utendaji.
Alipongeza
mfuko huo kukua mwaka hadi mwaka kama taarifa za Mfuko za kila mwaka
zinavyoonyesha kama vile mtaji wa mfuko kuanza na milioni 50 kwa mwaka
1992 mpaka kufikia trilioni 1.09
mwishoni mwaka 2012 ambapo mpaka mwaka
kufikia mwisho wa mwaka 2013 mfuko unategemea kuwa na mtaji wa trilioni 1.3.
Mfuko
wa Pensheni wa PPF ulianzishwa Julai 1978 kwa sheria Namba 14 ya mwaka 1978
ambayo sasa inafahamika kama “PPF Pensions Fund Act” Sura ya 372 ya
sheria za nchi yetu kama ilivyorekebishwa na sheria namba 5 ya mwaka 2012 kwa
madhumuni ya kutoa mafao ya uzeeni na mafao mengine kwa wanachama wa
Mfuko. PPF ilianza ikiwa chini ya
usimamizi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) kama Mfuko wa
kwanza wa kuchangia wa Pensheni Tanzania.
Waziri
fedha aliyataja mbele ya wanachama, wadau na wageni mbalimbali kutoka ndani na
nje ya Tanzania ya kwamba mambo yafuatayo yamethibitisha utendaji wa hali juu
ya mfuko wa pensheni wa PPF kama vile:-
Kuweza
kutimiza majukumu ya mfuko ya kulipa pensheni na mafao mengine bila kukopa wala
kulazimika kuuza rasilimali za mfuko wa pensheni wa PPF, waziri aliendelea
kusisitiza ya kuwa hili ni jambo la kutia moyo sana kwani mfuko unadhihirisha
wazi kabisa ya kuwa unaendeshwa kisayansi na viongozi na wafanyakazi kazi wa
PPF kwa kushirikiana na wanachama na wadau wote wa mfuko kwa ujumla.
Waziri
aliupongeza Mfuko wa pensheni wa PPF kwa kuweza kutoa huduma kwa wadau wa ndani
ya mfuko na wale wa nje kwa asilimia 80 ukitumia mtandao wa kompyuta hii
ikimaanisha ya kuwa asilimia 80 ya mifumo ya TEHAMA itumikayo na Mfuko wa
PPF imetengenezwa na wafanyakazi wa ndani.
Alisema
jambo hili la kutumia kompyuta ni muhimu siyo tu kwa vile dunia ya sasa ndiyo
inakoelekea lakini pia inaitaiwezesha mfuko wa pensheni wa PPF kuendelea kutoa
huduma kwa haraka zaidi na pia kwa wanachama na wadau wengine kuweza kupata
huduma kama vile taarifa za hesabu kwa
haraka zaidi na kwa gharama nafuu.
Pamoja
na hayo Mgimwa ambaye ni waziri wa fedha vile vile aliipongeza kuanza kutumia
mawasiliano mapya kwa PPF kwa njia ya ‘facebook’ ambayo pamoja na mengine
aliyazindua nembo mpya ya mfuko wa pensheni wa PPF na tofuti iliyoboreshwa
ikiwemo facebook siku hiyo ya ufunguzi
wa mkutano huo wa mwaka wa 23
viongozi
wa PPF, na wadau mbalimbali wakishuhudia uzinduzi wa NEMBO mpya ya mfuko wa
pensheni wa PPF
Alisema
kuwa ushiriki wa mfuko katika shughuli
mbalimbali za uwekezaji ambazo zimeleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika
Taifa kwa kushirikiana na Mifuko mingine
ya hifadhi na taasisi za fedha kama vile mabenki.
Ujenzi
wa Chuo Kikuu cha Dodoma na kile cha Kimataifa cha Sayansi na Ufundi cha Nelson
Mandela hapa Arusha, aliipongeza PPF kwa ujenzi wa nyumba za bei nafuu kule
Mwanza, utoaji wa mikopo katika sekta za kilimo na viwanda kama vile Kiwanda
cha Sukari cha Kagera na kile cha 21st Century pale Morogoro, mikopo
ya SACCOS kwa Wanachama wao, ujenzi wa majengo ya hoteli za kitalii Arusha na
kule Mwanza alisema ya kuwa ni uthibitisho kutosha wa mchango mkubwa wa
maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa taifa letu changa kama Tanzania.
Na
kwamba shughuli hizi za kiuwekezaji siyo tu zimekuwa na manufaa kwenu, bali pia
kwa Wanachama kwao, watanzania kwa
ujumla na Serikali, waziri alisisitiza.
Alisema
ya kuwa mfuko wa pensheni wa PPF wamewekeza kwa kuzingatia miongozo ya
uwekezaji iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya
Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA). Na kwamba kwa
kufanya hivyo siyo tu itahakikisha mfuko unapata faida nzuri ya uwekezaji wake
lakini pia kwa fedha za wanachama wake kuwa salama.
Na
jambo lingine muhimu ambalo waziri wa fedha
aliipongeza PPF ilikuwa juu ya PPF kuweza kubuni na kutoa fao la elimu
kwa watoto wa wanachama wake waliofariki wakiwa kazini kwa kipindi cha miaka 10
sasa mfuko umewawezesha watoto hawa kupata elimu na kwa rasilimali watu
iliyoelimika kwa siku za usoni kwa taifa.
Ambapo
kwa miaka kumi yote mfululizo fao limekuwa likitolewa kwa watoto tegemezi wa
wanachama waliofariki wakiwa kazini mpaka kidato cha nne na kuanzia mwakani
2014 PPF itaendelea kutoa mpaka kidato
cha sita.
Na
aliendelea kuupongeza mfuko ya kuwa umekuwa ukipata hati safi za hesabu
zilizokaguliwa na mkaguzi mkuu wa serikali
kila mwaka kwa mfululizo ukizingatia ukubwa na wingi wa shughuli za
mfuko huo wa pensheni. Na kwamba mambo yote sita aliyoyataja hapo juu ni ya
kupigiwa mfano na kuupongeza sana uongozi wa PPF, wafanyakazi, wanachama na
wadau wote kwa ushirikiano wao wa matokeo makubwa ya utendaji
Waziri
wa fedha aliupongeza mfuko pia kwa namna ya pekee kwa kufanya mikutano hii ya
Wanachama kwa miaka 23 mfululizo sasa.
Alisema
mikutano hii siyo tu inawapa wanachama na wadau fursa ya kukutana watendaji
wa mfuko na kupata taarifa mbalimbali za
utendaji za Mfuko wao bali inawawezesha kutoa maoni na mapendekezo ya kuboresha
zaidi huduma, mafao na kuhakikisha kuwa Mfuko unakuwa endelevu zaidi na
kusisitiza ya kuwa kikubwa zaidi ni kwamba inadumisha misingi ya uwazi na
uwajibikaji na kuimarisha utawala bora.
Dkt.Mgimwa alizungumzia pia juu ya changamoto kubwa
kuhusu waajiri kutowasilisha michango kwa wakati muafaka na pia kukwepa
kuandikisha baadhi ya wafanyakazi wao kwenye MfuKo.
Kwa
upande wa Waajiri, waziri anawakuwakumbusha kuwa suala la kuandikisha
wafanyakazi wao kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na pia kupeleka michango ni
suala la kisheria na siyo la hiyari.
Na
kutofanya hivyo ni kuvunja sheria na aliiagiza PPF isisite kuwachukulia hatua
kwa mujibu wa sheria waajiri hao.
Alisisitiza
ya kuwa ni vyema waajiri wakakumbuka kuwa kwa kutowaandikisha na kupeleka
michango yao kwenye Mifuko, kunawanyima wafanyakazi hao haki yao ya msingi ya
kupata pensheni wakati watakapostaafu.
Aliendelea
kuwahabarisha wanachama na wadau washiriki ya kuwa taarifa alizokuwa nazo ni
kwamba mchakazo wa maswala hayo unaendelea vizuri.
Hivyo
aliwaomba wanachama na wadau wote
kuendelee kuwa na subira wakati mamlaka husika zinaendelea na mchakato.
Pamoja
na haya yote waziri hakusahau
kuzungumzia juu ya changamoto za utoaji wa huduma ya hifadhi ya Jamii
kwenye sekta isiyo rasmi. Alisema mpaka sasa asilimia zaidi ya 90 ya wafanyakazi
katika nchi yetu wako katika sekta isiyo rasmi na kwamba bahati mbaya ni
wachache sana miongoni mwao wanapata huduma hii.
Lakini
alisisitiza na kuwakumbusha PPF kutumia
uzoefu wa miongoni mwa mada zilizokuwa zimewasilishwa na mtoa mada juu ya utoaji wa huduma hii kwa
sekta isiyo rasmi nchini kutoka Kenya kuona ni kwa namna gani watanzania
wanaweza kutoa huduma hiyo hapa nchini.
No comments :
Post a Comment