Njia mojawapo ya wadau wa
mifuko ya hifadhi ya jamii ni kufuatilia na kujua utendaji wa mifuko hii
inayosimamiwa na bodi za wadhamini kwa njia ya mikutano mikuu inayofanyika kila
mwaka. Ambapo wadau kama vile wanachama ambao ndio wachangiaji na waaajiri
ambao mara nyingi ndio waliodhaminiwa au wakala wa kuhakikisha ya kuwa
wanashirikiana na mifuko hii kama vile kusimamia ukataji na kupeleka michango
kwenye mifuko ya hifadhi na kuhakikisha ya kuwa wanatunza kumbukumbu za
wafanyakazi wao, pamoja na wawakilishi kutoka katika vyama mbalimbali vya
wafanyakazi nchini na baadhi ya taasisi za serikali na zisizo za kiserikali.
Kwa kawaida hii inakuwa nafasi ya kipekee na muhimu sana kwa wadau kama
wanachama wa mifuko hii ya hifadhi ya
jamii kuhudhuria kwa ajili ya kuzungumzia mambo muhimu yanayogusa afya na ustawi wa mifuko zinazohusiana na
taarifa za hesabu, taarifa za ukaguzi wa mahesabu, zinazohusiana na taarifa za
bodi ya wadhamini wa mifuko na kujua nafasi na uwezo wa mfuko kifedha.
Lakini pamoja na hayo wadau
wanakuwa na haki ya kujua maamuzi muhimu yaliyoamuliwa kwa mfano na mkutano wa
mwaka jana ambayo yalipewa kipa umbele pamoja na yatokanayo ambapo tumeona mara
nyingi wadau kama mwanachama inakuwa nafasi nadra sana kwao kama wachangiaji au
mwana hisa kuitumia vizuri.
Kwa mfano mfuko wa pensheni wa PPF unategemea
kuwa na mkutano wa 23 wa wanachama wa mfuko na wadau mbalimbali wa sekta ya
hifadhi ya jamii utakao anza tarehe 2-4 Oktoba 2013. Wanachama na wadau wakiwa
kama vile Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi, Maofisa Watendaji Wakuu (CEO), Maofisa
wanaoshughulika na Raslimali Watu na Utawala, Sheria, Uhasibu, Fedha,
Teknolojia na Mawasiliano na Bima, kutoka Serikali Kuu na Taasisi za Serikali,
Mashirika ya Umma, Makampuni binafsi, Mashirika yasiyo ya Kiserikali pamoja na
Wawakilishi wa Vyama vya Wafanyakazi kutoka sehemu za kazi, vyama vya waajiri
na watu wengine wowote watakaopenda kushiriki kwa lengo la kujua na kupata
elimu ya masuala ya hifadhi ya jamii. Mkutano huu utafanyika
Arusha katika ukumbi wa
Simba, AICC – Arusha ukiwa na mada kuu ya 'PPF na Wadau; Miaka 35 ya Kukua
Pamoja'.
Hivyo basi hima kwa
wanachama na wadau kuhakikisha ya kuwa mnaitumia nafasi ya nadra inayotokea
mara moja kwa kila mwaka kwa kuchambua ustawi na afya ya mfuko wenu huu wa PPF
ili kuondoa dukuduku zenu na kuboresha utendaji wa mfuko. Kuwawezesha wanachama
na wadau kutekeleza haki, wajibu na nguvu walizopewa katika mkutano mkuu wa
mwaka kama huu wanatakiwa kuandaliwa mapema kwa muda muafaka na kupewa habari
bora na za hali ya juu na isipofanyika
hivyo basi uwezo wa nguvu wa kisheria waliopewa unakuwa hauna nguvu yeyote kwa
wanachama, waajiri na hata kwa wadau wengine. Ni wajibu wa bodi ya wadhamini ya
PPF kuhakikisha ya kuwa taarifa za kuwapasha wadau zinawafikia wadau wa mfuko
huu juu ya kufanyika mkutano mkuu wa mwaka kwa muda muda muafaka na siyo
vinginevyo. Maswali ya kujiuliza ni kama vile taarifa au habari hizo
zinazotolewa na PPF zina ubora gani na je zimewafikia wadau wanaohusika kwa
muda muafaka?
Na kwa upande mwingine mtu
anaweza kujiuliza ya kwamba chukulia ya kuwa mwanachama amepelekewa habari na
kupata taarifa mapema juu ya kuhudhuria mkutano mkuu wa 23 wa wanachama na
wadau wa PPF. Je baada ya hapo inafuatiliwa ili kuhakikisha ya kuwa hawa
wanachama na wadau watakaochaguliwa kuwawakilisha wenzao kwenye mkutano huo
watawajibika kama inavyotakiwa. Hivyo kwa upande mwingine unaweza kusema ya
kuwa wadau kupatiwa taarifa na bora kwa muda muda muafaka hiyo haitoshi
kabisa kinachotakiwa hapa ni kwa hali na
mali mdau kuwa tayari kujua au kuelewa kilichoandaliwa kwenye makabrasha ambalo
ni jambo linaloonekana kuwa ni tatizo kubwa kwa wanachama na wadau wengi wa
mifuko ya hifadhi ya jamii
Mtu mwingine anaweza kuwa na
mashaka na kilichopo ndani ya makabrasha kama siyo pambo tu la kuvutia mfuko wa
pensheni kwa idadi kubwa ya wadau na wanachama. Kwa upande mwingine wanachama
mara nyingi wameonekana kuwa ni kundi ambalo halina nguvu kabisa kwa kusimamia
utendaji na uendeshaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii ikiwemo kufuatilia tabia
na utaratibu wa utendaji wa wadhamini au bodi hizi za hifadhi ya jamii na hata inaonekana wanatofautiana katika
mitazamo kwa upande mwingine
Hapa ikumbuka kwamba uhai na
ustawi wa mifuko ya hifadhi ya jamii siyo kweli ya kwamba inategemewa na
mikutano mikuu ya mwaka ya mifuko kama huu utakaofanyika wiki ijayo huko arusha
na PPF ingawa ni mojawapo ya mlango muhimu wa ufahamu kama mfuko wa pensheni wa
hifadhi ya jamii. Wadau wa mifuko ya hifadhi ya jamii wametawanyika karibu
mikoa yote ya Tanzania kuanzia ngazi za vitongoji, vijiji, wilaya, kimkoa na
hadi kitaifa hivyo kwa maana hii inalazimisha kuwepo na uwakilishi katika
kuhudhuria kwenye mikutano mikuu hii ya mwaka.
Kutokana na msambaratiko huu
wa wanachama au wadau na hatimaye kuwakilishwa na watu wachache kutoka kila
kampuni za umma na za watu binafsi, na
taasisi mbalimbali kwa hiyo hata mahudhuria ya wadau na wanachama kwenye
mkutano mkuu wa mwaka umekuwa wa matatizo kwa kuhudhuriwa na wanachama na wadau
wachache wawakilishi. Kwa sababu hii imesababisa mpaka kuwepo na uwakilishi katika
mkutano mkuu ya kila mwaka badala ya wanachama kuhudhuria. Jambo la kujiuliza
ni kwamba je hawa wawakilishi kutoka kwa waajiri mbalimbali wanakutana na
wafanyakazi wenzao au kama ni mwajiri je
naye anahakikishaje kutoa taarifa kwa ukamilifu na ubora ule ule uliotolewa
wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa wanachama au wadau wa mfuko wa pensheni wa
hifadhi ya jamii kama PPF.
Kwa kifupi ni kwamba je
wanachama hupewa taarifa na wawakilishi mara tu baada ya kutoka kwenye
mahudhurio ya mkutano mkuu wa mwaka wa wadau wa mfuko? Na kama hawapewi
kunakuwepo na maana gani ya kuwa na mwakilishi? Hivyo kuna haja ya kuwa na malengo na mikakati ya makusudi ya
kuhakikisha ya kuwa waajiri, wafanyakazi, na taasisi mbalimbali kuchagua
mwakilishi ambaye atakuwa ni mtu ambaye atashiriki kwa malengo ya kuelewa na
kujua mambo muhimu ya mkutano mkuu hasa yanayogusa uhai, afya na ustawi wa
mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii kwa malengo ya kuboresha kinga ya
wanachama wake wachangiaji wakati wanapofanya kazi na baada ya kustaaafu na
siyo vinginevyo
Wawakilishi wa wanachama na
wadau mbalimbali wa PPF tumieni fursa hii ya kuwa na utahitaji wa kujifunza
zaidi utendaji wa mifuko ya pensheni kutoka kwa wataalamu wa PPF na mamlaka
inayohusika kama vile mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii (SSRA) wakati wa mkutano
mkuu wa mwaka wanachama wa PPF
Manejimenti ya PPF ikumbuke kuwa kuendesha na kusimamia
mfuko wa hifadhi ya jamii kama vile kuwa na mkutano mkuu wa mwaka wa wadau
haukuanza jana mfuko huu una uzoefu wa muda mrefu tangia miaka 23 iliyopita
kuendesha mikutano kama hii hivyo ni mfuko wa kwanza wa pensheni ya hifadhi ya
jamii kuanzisha wa mfumo huu kuwashirikisha wanachama na wadau wa hifadhi ya
jamii.
Hiki ni kipengele mojawapo muhimu cha kuzingatia
utaratibu na kanuni za utawala bora hivyo tunaamini ya kuwa PPF utaendelea
kujenga imani zaidi wakati wa mkutano mkuu kwa wanachama na wadau kwa
kuwahakikishia ya kuwa mfuko unaendeshwa na kuongozwa na utawala bora na kwa
ufanisi wa hali ya juu zaidi kwa kuendesha mkutano kwa njia ya ukweli na uwazi
Kuna haja ya uongozi wa mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa
wazi kama kigezo muhimu cha utawala bora kuthibitisha pale uamuzi unapofanywa
kwa kuzingatia masilahi ya mfuko kwanza na siyo masilahi binafsi ya viongozi.
Uwazi ni matokeo ya mchakato na utaratibu wa uamuzi wa wazi wenye kuzingatia
vigezo maalumu vinavyotumika katika kufanya maamuzi ya kuchagua wajenzi,
makandarasi, kusaini mikataba, na viongozi kutoa taarifa nyeti zinazowasaidia
kuboresha shughuli za mfuko na kufanya kuwa endelevu kwa wanachama wachangiaji
na wadau wengine kwa njia mbalimbali kama vile kupitia magazeti, tovuti,
televisheni, redio na mitandao ya kijamii.
Nafikiri mmeshuhudia hata baadhi ya taasisi na makampuni
makubwa ya kimataifa kufilisika na kuanguka na mara nyingi makampuni haya
yamekuwa yakitoa taarifa za uongo za matumizi ya fedha na za kiutendaji, na
wizi uliokithiri, malipo na marupurupu yasiyo ya kawaida kwa viongozi, mifumo
ya ndani dhaifu ya udhibiti wa fedha, kushidwa kudhibiti hatari na majanga,
mawasiliano duni kati viongozi na wanachama na uendeshaji mbaya unaosababisha
wanahisa kupoteza mitaji yao na kupata hasara. Mara nyingi wanachama wamekuwa
wakijiuliza kuwa imekuwaje viongozi hawakujua kuwa kuna hatari ya kufilisika?
Tunaamini ya kuwa mfuko huu wa PPF unazingatia kanuni za
uongozi bora na kwa kufanya ndiyo maana hivyo kumekuwa na uwezekano mkubwa kwa
mfuko kuwa na utendaji mzuri unaofikia malengo na kukidhi matarajio ya
wanachama wake na familia zao.
PPF hivyo tumieni
nafasi hii ya mkutano mkuu wa wadau kwa kuhamasisha kuanza kupanua wigo zaidi wa hifadhi ya jamii
kwa kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wanachama, wadau na kwa umma wa
Tanzania kwa ujumla kwa njia ya kujenga ushirikiano kati ya wadau ili
kuhamasisha wananchi kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii nchin
i.
Hivyo mkutano huu mkuu
unategemewa kufanywa kwa ushirikiano mkubwa kati ya wanachama, wadau na mamlaka
ya usimamizi na udhibiti wa sekta ya hifadhi ya jamii SSRA na mifuko mengine ya
hifadhi ya jamii, shirika la kazi duniani (ILO), Hazina, Wizara ya kazi na
ajira, wakala wa huduma za ajira Tanzania (TAESA), shirika la tija la taifa
(NIP) na idara ya ajira pamoja na Baraza
la ushululisho na uamuzi (CMA)
Hivyo tunagemea PPF kama
mfuko wa pensheni ya hifadhi ya jamii kutumia vyombo vya habari kwa ajili ya
kuwahabarisha hata kwa wale wanachama, wadau na wananchi wengine ambao idadi
yao kubwa hawatapata nafasi ya kuhudhuria mkutano mkuu wa mwaka kuhamasishwa
kwa njia ya programu za redio, runinga na machapisho mbalimbali kama vile
magazeti, vipeperushi n,k, wakiwa majumbani mwao safarini Tanzania nzima na
nchi za nje. Watanzania wengine tumieni fursa hii ya wiki ya mkutano mkuu kwa
wanachama na wadau nchini kujifunza na kujielemisha juu ya uhai, utendaji, afya na ustawi wa mfuko wa pensheni wa taifa (PPF) juu ya
taarifa zinazohusiana na hesabu, taarifa za ukaguzi wa mahesabu, na taarifa za
bodi ya wadhamini wa mifuko na kujua nafasi na uwezo wa mfuko kifedha kwa njia
ya magazeti, redio, luninga, blog na njia zingine za mitandao kwani pensheni ni
haki yako
No comments :
Post a Comment