Thursday, August 1, 2013

Malengo na mfumo wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii nchini Tanzania




 SSRA Director General Irene Isaka

Mkurugenzi Mkuu wa chombo cha kudhibiti na kusimamia mifuko ya hifadhi ya jamii nchini (SSRA) Irene Isaka

 Na Christian Gaya majira 30 Julai 2013
Lengo kubwa la hifadhi ya jamii ni kuzuia umasikini, kupunguza au kuondoa umasikini, kuifidia jamii, kugawanya mapato sawasawa kwa wanajamii. Masuala mengi yanayogusa hifadhi ya jamii ni ya nyeti sana, yanagusa ni kiini muhimu sana cha wafanyakazi kwenye sekta rasmi na sekta zisizo rasmi hasa za watu masikini pamoja na sekta ya bima za jumuiya za waajiri


Hifadhi ya jamii ina maana ni aina ya hatua madhubuti au shughuli zilizobuniwa za kuhakikisha kuwa wananchi wa jamii hiyo wanapata mahitaji yao ya lazima na ya msingi  na wanapewa kinga ya hifadhi ya kutokana na majanga ili kuwawezesha kuwa na kiwango cha maisha ya kuishi kulingana na mila na desturi za jamii


Mpaka sasa hapa nchini kuna mifuko sita ya hifadhi ya jamii ambayo imeanzishwa kwa sheria za bunge mifuko ambayo ni: Mfuko wa taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF), Mfuko wa pensheni wa wafanyakaziwa serikali za mitaa(LAPF), Mfuko wa akiba wa wafanyakazi wa serikali (GEPF), Mfuko wa pensheni wa watumishi wa serikali (PSPF), Mfuko wa pensheni kwa mashirika ya umma(PPF), Mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF).


Mifuko hii ya hifadhi ya jamii ina wajibu wa Kuandikisha wanachama, Kukusanya michango kutoka kwa wanachama, Kuwekeza michango ya wanachama, Kuwekeza michango ya wanachama, Kulipa mafao kwa wanachama yanayoendana na ukali wa maisha au mfumuko wa bei kiuchumi ya wakati huo. Na kuhakikisha ya kuwa inakuwa na malengo pamoja na mikakati madhubuti  ya kuwaelimisha wanachama,  waajiri na  wananchi kwa ujumla ingawa Kumekuweko na ongezeko dogo sana la kuelewa juu ya mfumo wa hifadhi ya jamii hasa juu ya mafao yanayotolewa, jinsi ya kujiunga kuwa wanachama, vitega uchumi na shughuli mbalimbali za sekta.


Mapungufu yaliyomo kwenye mfumo huu wa hifadhi ya jamii ambayo yanahitajika kutatuliwa na sera hii ya hifadhi ya jamii  chini ya msimamizi na mdhibiti wa mifuko hii hifadhi ya jamii yaani SSRA. Na idadi kubwa ya watu ambao ni wanachama katika mifuko hii ya hifadhi ya jamii ni wale tu ambao wameajiriwa kwenye sekta iliyo rasmi kwa sababu inakisiwa kuwa ni milioni 1.0 hii ni asilimia 6% ya nguvu kazi yote ambayo ni kama milioni 16 ya Watanzania wote. Hii ina maana yakuwa karibu milioni 15 ya nguvu kazi inashughulika na sekta isiyo rasmi na wote wako katika hali hatarishi kwa vile hawana kinga yeyote ya hifadhi ya jamii

.
Mtu yeyote aliyejiajiri, mkulima, mvuvi, mfanyakazi wa ndani, wafanya biashara wadogo wanaweza kujiandikisha kwa hiari na kulipa kadri ya uwezo wake na mifuko hii ya hifadhi ya jamii na akisha anza kuchangia mwanachama wa hiari naye atakuwa na haki ya kupata mafao yote yatolewayo na mfuko wowote wa hifadhi ya jamii atakaopendelea kujiunga nao ingawa hakuna mikakati ya makusudi inayoridhisha ya utekelezaji wa jambo hili inayofanywa na mifuko hii ya hifadhi ya jamii hapa nchini. 


Kwa kawaida mipango ya mifuko ya hifadhi ya jamii huchangiwa kati ya mwajiri na mfanyakazi kwa kiwango cha asilimia 20 ya mshahara wa mfanyakazi ikijumuishwa na marupurupu mengine. Moja kati ya viwango vifuatavyo vinaweza  kutumika kutegemeana na maamuzi ya mwajiri na mwanachama: asilimia 10 kwa mfanyakazi na asilimia 10 kwa mwajiri au asilimia 5 kwa mfanyakazi na asilimia 15 kwa mwajiri na asilimia 20 yote kuchangiwa na mwajiri


Baadhi ya changamoto kwa serikali ni kama vile kujaribu kuangalia jinsi ya kufikia watu wengi zaidi au wote nchini, kwa ajili ya kukidhi mahitaji yao ili kila mtu aishi kwa heshima na utu. Kulingana na sera za masuala ya nchini Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya kama vile sura ya 11 (1) inaainisha wajibu wa serikali na jamii ulinzi kwa raia wake juu ya majanga ya kijamii kama vile,magojwa ulemavu na uzee.


Ni wajibu wa mifuko hii ya hifadhi ya jamii kuhakikisha ya kuwa mwanachama anaelemishwa kama mchangiaji pamoja na mwajiri wake ili kila mmoja ajue wajibu wake kwenye mfuko hii ya hifadhi ya jamii. Mifuko hii ya pensheni wa hifadhi ya jamii lazima uweke wazi juu ya haki za wanachama hasa zile za kumruhusu mwanachama kukata rufaa kwenye bodi ya sheria au mahakamani atakapoona kwamba pale hajatendelewa haki inavyotakiwa na mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii. Siyo hivyo mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii ina wajibu wa kuweka wazi kwa wanachama mchangiaji jinsi ya kuwashirikisha kwa vitendo kwenye maamuzi na jinsi ya uendeshwaji wa mifuko. mwisho

No comments :

Post a Comment