Thursday, May 9, 2013

‘ Watanzania sasa changamkieni mikopo ya nyumba’

Mwanasheria Mkuu wa Kwanza wa Serikali, Jaji Mark Bomani, 
Na Mwandishi wetu, Mwandishi  (email the author)

Kwa ufupi
“Bila kutumia fursa hii, ni vigumu kujenga kwa kukusanya fedha kidogokidogo. Ukikopa benki unapata fursa nzuri ya kupata nyumba bora huku ukilipa taratibu, kwa ujumla mikopo hii ni mkombozi wa kupambana na makazi holela kwa kutupatia makazi bora yaliyopimwa na yenye huduma zote muhimu,” alisema.


Mwanasheria Mkuu wa Kwanza wa Serikali, Jaji Mark Bomani, amewashauri Watanzania kuchangamkia fursa za mikopo ya nyumba zinazotolewa na benki hapa nchini ili kupata makazi bora.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Jaji Bomani alisema fursa hiyo ni njia bora na sahihi ya kupata makazi bora kwa kuwa Watanzania wengi wataweza kununua nyumba katika maeneo yaliyopimwa na yenye mfumo mzuri kuanzia barabara, umeme na maji.

Jaji Bomani aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa mradi wa nyumba zilizopo eneo la Goba Kunguru jijini Dar es Salaam, zilizojengwa na kampuni ya Greystone Holdings.

“Bila kutumia fursa hii, ni vigumu kujenga kwa kukusanya fedha kidogokidogo. Ukikopa benki unapata fursa nzuri ya kupata nyumba bora huku ukilipa taratibu, kwa ujumla mikopo hii ni mkombozi wa kupambana na makazi holela kwa kutupatia makazi bora yaliyopimwa na yenye huduma zote muhimu,” alisema.

Kwa mujibu wa Jaji Bomani, wananchi wanaweza kununua nyumba zilizozinduliwa kwenye eneo kwa kukopa fedha katika Benki Biashara za Kenya (KCB), Commercial Bank of Africa (CBA) na Bank of Africa (BOA).

“Eneo hili lina barabara, umeme, maji yaliyochimbwa na bustani nzuri za kupumzikia, kwa ujenzi wetu wa kudunduliza, ni vigumu kutenga eneo zuri la bustani, hivyo ni muda mwafaka sasa kwa Watanzania kununua nyumba kama hizi kupitia mikopo ya nyumba,” alisema.

Nyumba hizo ni zenye vyumba vitatu vya kulala, stoo, jiko na maegesho ya magari.

No comments :

Post a Comment