Wednesday, March 20, 2013

Waajiri wapeni mifuko hifadhi ya jamii fursa sawa ya kuandikisha wafanyakazi wapya kuwa wanachama wa mifuko ya pensheni




Na Christian Gaya: Majira: Machi 19, 2013
Sheria ya msimamizi na mdhibiti wa sekta ya hifadhi ya jamii hifadhi  SSRA  ilitungwa na kupitishwa  na sheria namba 8 ya mwaka 2008 ili kusimamia na kudhibiti shughuli zote za hifadhi za jamii hapa nchini kwa kuanza na mifuko yote ya hifadhi  ya jamii iliyopo hapa nchini kwa sasa kama  vile mfuko wa pensheni wa mashirika ya umma yaani Parastatal Pension Fund (PPF) ulioundwa kwa ajili ya kutoa huduma ya pensheni ya hifadhi ya jamiii kwa wafanyakazi wote wa mashirika ya umma na wa sekta ya watu binafsi na sekta ilisiyokuwa rasmi.  Mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii (NSSF) wa sheria namba 28 ya mwaka 1997

Mfuko wa pensheni wa serikali za mitaa yaani Local Authorities Pensions Fund (LAPF) mfuko wa taifa wa bima ya afya yaani National Health Insurance Fund (NHIF) unaotoa huduma ya bima ya afya kwa watumishi wote wa serikali. Na mfuko wa akiba ya wafanyakazi kwa watumishi wa serikali yaani Government Employees Provident Fund (GEPF). Pamoja na mfuko wa pensheni wa watumishi wa serikali ya Public Service Pensions Fund (PSPF)

Mpaka sasa mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya hifadhi ya jamii (SSRA)  ameanza kuleta marekebisho ya baadhi ya vifungu vya sheria  kwa awamu kwa mfano waajiri wote katika utumishi wa umma na sekta binafsi wanapaswa kuzingatia matakwa ya sheria hii kwa kuwapa fursa watumishi wapya kujiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya lazima wanayoitaka. Bado ni changamoto kubwa sana kwa SSRA kuleta na kufanya marekebisho haya yote.  kwani  mpaka sasa haya mashirika ya hifadhi ya jamii kila moja ina wizara yake inayoisimamia na kuwa utaratibu na kanuni tofauti za uendeshaji wa mifuko hii. Matokeo yake ni kwamba kiwango cha michango, mfumo wa mafao, na sifa za kupata mafao na hata mipako na vipa umbele vinatofautiana kabisa kwa kila mfuko.

Mpaka sasa hakuna utaratibu ulioanzishwa wa kuruhusu haki za mafao ya mwanachama kuhamishwa kutoka mfuko mmoja hadi mwingine. Matokeo yake wafanyakazi wamekuwa wakipoteza baadhi ya haki zao za mafao wakati wakihama kutoka sehemu moja ya mwajiri hadi mwajiri mwingine. Pia hii imechangia sana kuongezeka kwa tabia ya kuondoa michango ya pensheni kabla haijakomaa. 

Kumekuwa hakuna soko huru la hifadhi ya jamii ambalo linaweza kumruhusu hata taasisi za watu binafsi au sekta za watu binafsi kuendesha mifuko ya hifadhi ya jamii kwa muda mrefu ingawa kwa sasa wameruhusu lakini muundo rasmi haujatoka bado kutoka kwa mdhibiti na msimamizi wa hifadhi ya jamii (SSRA)

Miongozo ya uwekezezaji wa rasilimali za mifuko hii ya hifadhi ya jamii ingawa imetolewa tayari lakini haijaanza kutumika mpaka sasa. Mapungufu yaliyomo kwenye mfumo huu wa hifadhi ya jamii ambayo yanahitajika kutatuliwa na sera hii ya hifadhi ya jamii. Watu waliomo katika mifuko hii ya hifadhi ya jamii ni wale tu ambao wameajiriwa kwenye sekta iliyo rasmi
Jumla ya idadi ya wanachama wa mifuko hii ya pensheni ya hifadhi ya jamii kwa Tanzania ni watu 871,000 na imegawanywa kama ifuatavyo NSSF ni 363,000, PSPF 193,000, na kwa NHIF 180,000, 90,000 PPF, na kwa LAPF 45,000. Hii inawakilisha kama asilimia 85 ya watu wote waliajiriwa kwenye sekta iliyokuwa rasmi

Imefikia wakati sasa mifuko ya hifadhi ya jamii inahitaji kubadilika kimtazamo na kidira imefika wakati ambapo mteja huenda akaonekana ni mfalme. Mifuko ya jamii nchini inahitaji kujua hili ili kujipanga upya na kuhakikisha ya kuwa inajali wateja wao hasa kwa kutoa huduma bora kwa wanachama na wastaafu pamoja na washika dau wengine kama vile  wamama, wababa na watoto tegemezi. Mashirika ya hifadhi ya jamii yanahitaji kupokea malalamiko ya wanachama wao na kujibu kwa muda muafaka ili kuwaridhisha kama wenye wachagiaji wa michango hiyo. Wanahitaji kutimiza ahadi wanazotoa kwa wanachama kwa wakati muafaka na siyo vinginevyo.
Wakati umefika wa kubadilisha sheria zilizopitwa na wakati na ukiritimba, kila mmoja anahitaji kuingia uwanjani kwa kuuza sera zake ili kumvutia mteja. Waajiri wanahitajika kubadilika juu ya suara hili la mabadiliko ya marekebisho ya sheria ya hifadhi ya jamii ya kuwaruhusu wafanyakazi wapya walioajiriwa kutoka sekta iliyokuwa rasmi na isiyo kuwa rasmi kuchagua mfuko wowote anautaka mfanyakazi kujiunga nao na wale ambao wako kwenye ajira lakini walikuwa hawajawahi kuijiunga na mfuko wowote hapa nchini nao pia wapitiwa uhuru huo wa kuchagua siyo kuchaguliwa na mwajiri.

Ingawa kwa upande mwingine ni changamoto kubwa kwa waajiri hasa kwa kuongezeka kwa gharama kwa kuhakikisha ya kuwa michango yote ya wafanyakazi wao inapelekwa kwa muda muafaka kwa kila mfuko wa pensheni ambayo wafanyakazi wake hao wapya wamechagua kujiunga nayo. Lakini ijuilikana ya kuwa marekebisho haya yanafanyika ili kutimiza matakwa ya kifungu Na. 30 cha sheria iliyoanzisha Mamlaka ambayo inampa uhuru mfanyakazi na mfuko wowote ulioanzishwa kwa sheria ya bunge.na kwa upande wa mifuko ya pensheni naamini wanajua ya kuwa Kwa mujibu wa vifungu vya (29),( 2) na (3) vya Sheria ya Usimammizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2008 ni kinyume cha sheria na  ni kosa la jinai kwa mfuko wowote wa pensheni kuandikisha wanachama waliokwisha andikishwa na Mfuko mwingine; kutoa taarifa zisizo sahihi kwa lengo la kuaminika kwa wadau, waajiri na waajiriwa; kutoa nyaraka ukijua kuwa nyaraka hiyo ni ya kughushi; na kupata ridhaa ya wafanyakazi au waajiri kwa njia ya shinikizo au vitisho

Ni makosa makubwa kwa mfanyakazi mpya kujiunga au kujiandikisha kwenye mifuko zaidi ya mmoja wa pensheni kwa kufanya hivyo unaweza kupoteza haki yako ya msingi.pamoja na hayo kwa mujibu wa kifungu cha 30 cha Sheria ya Usimammizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii na Sheria za Mifuko kama zilivyorekebishwa, mfanyakazi ambaye hajawahi kujiunga na Mfuko wowote wa Pensheni au anayeajiriwa kwa mara ya kwanza anao uhuru wa kuchagua mfuko wowote kati ya mifuko tajwa hapo juu. Hii ina maana mfanyakazi anapaswa kuwa mwanachama wa Mfuko mmoja tu wa Pensheni. Ili kutekeleza kifungu hiki cha kufanya marekebisho SSRA kwa sasa imeanza kushirikiana pamoja  na vyombo mbalimbali kama kama vile Idara ya Utumishi wa Walimu (TSD), Idara ya Utumishi wa Umma (CSD), Idara ya Utumishi wa Serikali za Mitaa (LGSD) Idara ya Utumishi wa zimamoto (FRSD), Idara ya Utumishi Afya (HSD) na kuhakikisha ya kuwa vyama mbalimbali vya wafanyakazi vinazingatie pia masharti ya Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii kwenye maeneo yao.

No comments :

Post a Comment