Tuesday, February 19, 2013

Madhara ya kutoa michango ya pensheni mapema kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii

Kumruhusu mtu kuchukua michango yake kabla ya haikomaa au kufikia muda wake wa pensheni kuiva hii inaweza kuleta hali hatarishi kwa mwanachama mchangiaji. Kama mwanachama mchangiaji aliyewekewa bima anaweza kuruhusiwa kuchukua michango yake ya pensheni ya uzee inaweza kuleta mgongano wa hasi zaidi  hasa pale atakapoanza kuchagua kiwango cha kiasi gani cha pensheni yake atapata.

Kwa mfano sera ya hifadhi ya jamii Tanzania ya mwaka 2002 inataja rasmi kuwa mwanachama ataruhusiwa kupata mafao yake ya pensheni ya asilimia 25 kama mkupuo ambao hauna kodi kabla hajafikia umri wa miaka 55 ya hiyari au 60 ya lazima kustaafu. Kutoa michango yote sio jambo nzuri, kwa sababu michango ikisha tolewa baada ya hapo hufanyiwa nini? Kama inawekezwa kwenye vitega uchumi kama vile hatifungani, hisa, vipande na uwekezaji mwingine ni bora zaidi kuliko kwa ajili ya mahitaji ya leo tu. 

Hapa inaonyesha ya kuwa wafanyakazi wengi wanapendelea kuondoa michango yao kwa mkupuo bila ya hata kuelemishwa  juu ya matokeo ya pensheni yake ya mwisho yaani ya kustaafu. Hii tabia itawaweka watu wengi baada ya kustaafu kwenye hali au mazingira hatarishi hasa watakapo kuwa wanapata pensheni kidogo kuliko walivyokuwa wakitegemea kupokea baada ya kustaafu na pale muda wao wa kuishi utakapokuwa mkubwa zaidi kuliko pensheni waliyopata. Na kiutaratibu zaidi inatakiwa mchangiaji asisitoe michango yake yote ya pensheni. Inatakiwa kama atatoa theluthi ya michango yake ya pensheni basi theluthi mbili zibaki kwa ajili ya pale atakapokuwa hana uwezo tena kupata pato lake kwa njia ya kujiajiri au kuajiriwa tena.

Kwa sababu ya hali hii hatarishi, kuchukua michango kabla ya kufikisha umri wa kustaafu kwa hiyari yaani miaka 55 au lazima baada ya kufikisha miaka 60 kwa kweli imefikia muda msimamizi na mdhibiti wa mifuko hii ya hifadhi ya jamii yaani Social Security Regulatory Authority (SSRA) au kwa kila mfuko wa pensheni ya hifadhi ya jamii kuwa na mikakati ya makusudi ya kuandaa programu za kuelemisha na kufundisha na kutoa ushauri kwa wananchi au mwanachama pamoja na familia zao juu ya matokeo au madhara ya kutoa michango yao ya pensheni kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kabla haijafikia muda wake.  SSRA inatakiwa kuhakikisha kuwa inaadaa programu iliyo kamili kwa ajili ya kutoa elimu kwa watu na wakati wowote inapohitajika iweze kupatikana. Lakini hata mifuko yote ya pensheni ya hifadhi ya jamii inatakiwa kutoa elimu ya juu

Na hii lazima ifahamike wazi ya kwamba karibu mifuko yote ya pensheni inayoendeshwa kwa utaratibu wa bima kama vile Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), shirika la pensheni kwa ajili ya mashirika ya umma (PPF), Mfuko wa Pensheni wa hifadhi ya jamii kwa ajili ya Watumishi wa Umma (PSPF), Mfuko wa Bima wa Taifa yaani (NHIF), mfuko wa pensheni ya hifadhi ya jamii kwa ajili ya wafanyakazi wa serikali za mitaa yaani (LAPF)

Michango ya wanachama wao yote huingizwa kwenye chungu au mfuko mmoja bila kujali ukubwa au udogo wa michango ya wanachama na huwekezwa kwenye mfuko mmoja. Kwa maana hii inakuwa vigumu kwa mfuko kama hii kutoa michango kwa wanachama kabla ya wakati wake. Kwa vile michango yote huingizwa kwenye akaunti moja tu. Ila pale mwanachama anapopatwa na janga lolote litalomfanya kupunguza pato lake kama vile kuumia akiwa kazini, kustaafu, kujifungua yaani uzazi, ugonjwa pale anapougua pamoja na familia yake gharama zote za matibabu zinachotwa kwenye akaunti hiyo hiyo.

Kuchukua michango ya pensheni kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kama NSSF, LAPF, PSPF, LAPF, NHIF, AU PPF ambayo michango wanachama huwekwa kwenye mfuko mmoja bila kujali umechangia kiasi  ngapi kunaweza kuharibu kabisa thamani ya mifuko hii na hata kupelekea baadaye kutokuwa endelevu. Na hii inaweza hata kuleta madhara makubwa hata kwa wanachama wengine wa mifuko hii ambao wataendelea kuchangia.  Kwa vile hakuna akaunti ya mwanachama mmoja mmoja hivyo kunafanya uchukuaji wa michango ya pensheni mapema kuwa vigumu zaidi. Lakini kwenye mifuko ya akiba ya wafanyakazi ya taifa kama ilivyokuwa NPF yaani National Provident Fund      kabla haujabadilishwa kuwa mfumo kamili wa hifadhi ya jamii yaani NSSF pamoja na Mfuko wa Akiba ya Wafanyakazi wa Serikali (GEPF) ambao wenyewe mpaka sasa kila mwanachama ana akaunti yake ya michango ya pensheni.  

itaendelea wiki ijayo









No comments :

Post a Comment