Tuesday, June 27, 2017

‘Dunia Maridhawa’ ya TBL Group yaendelea kunyanyua wakulima wa Shayiri nchini

tiz1
Meneja wa TBL kiwanda cha Arusha,Joseph Mwaikasu akimpatia maelezo
Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi,Dk Charles Tizeba utekelezaji wa kushirkiana na wakulima unavyofanyika
tiz2.Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi,Dk Charles Tizeba(kushoto)akimsikiliza Afisa Ugani kutoka TBL Group,Joel Msechu(kulia)
tiz3
Wakulima wa Shahiri  kanda ya kaskazini wakijifunza mbinu za kilimo bora katika maadhimisho ya siku yao15.Waziri wa Kilimo,Dk.Charles Tizeba akiongea na baadhi ya wakulima wilayani Monduli
tiz4
Wakulima wa Shahiri  kanda ya kaskazini wakijifunza mbinu za kilimo bora katika maadhimisho ya siku yao15.Waziri wa Kilimo,Dk.Charles Tizeba akiongea na baadhi ya wakulima wilayani Monduli
tiz5
Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi,Dk Charles Tizeba(kushoto)akimsikiliza  akitoa maelezo kwa wakulima wa zao la shayiri
……………………………………………………………………………………………
-Wakulima wa shahiri waanika mafanikio waliyoyapata
Wakulima wa zao la Shayiri kanda ya Kaskazini wanaoshirikiana na kampuni ya TBL Group wameeleza kuwa ushirikiano huo umewawezesha kupiga  hatua mbalimbali za maendeleo kwa
kuwa wanafanya kilimo wakiwa na uhakika wa kuuza mazao yao kwa bei nzuri.
Akiongea kwa niaba ya wakulima wenzake katika maadhimisho ya Siku ya Wakulima wa Shayiri kanda ya kaskazini yaliyofanyika katika Kijiji cha  Emairete wilayani Monduli juzi,
Mwenyekiti wa umoja wa wakulima hao ,Bariki Kivuyo,alisema kuwa wanawezeshwa kuanzia kupatiwa mbegu,utaalamu wa kutunza mashamba na kupatiwa madawa na pembejeo za kilimo.
“Uwekezaji wa kampuni ya TBL Group katika kilimo ni mkakati ambao umesaidia wakulima wengi ambao hivi sasa wanafanya kilimo cha Shahiri kwa njia za kisasa na uzalishaji umeongezeka zaidi ambapo kwa sasa wanavuna  gunia kumi hadi 16 kwa heka moja badala ya gunia tano walizokua wanapata na kwa kuwa soko ni la uhakika  maisha ya wakulima wengi yamebadilika kuwa bora kwa kujenga nyumba nzuri,kusomesha watoto wao na kununua pembejeo za kisasa za kilimo”.Alisema Kivuyo.
Hata hivyo alizitaja changomoto zinazowakabili kuwa ni  pamoja  na miundombinu mibovu ya barabara inayoongeza  gharama za ziada kwa wakulima kusafirisha mazao kutoka shambani kwenda kiwandani na kuiomba serikali iimarishe barabara zinazoingia na kutoka kwenye mashamba makubwa.
“Tunaomba mapato yanayolipwa kwa halmashauri sehemu yake irudishwe kwenye vijiji vinavyolima Shayiri kwa wingi ili kuhamasisha zao hili ili kuchochea kilimo kikubwa zaidi na kuwapunguzia wakulima mzigo na kufanikisha mkakati wa  serikali ya awamu ya tano wa kuwawezesha  wananchi hususani wenye kipato cha chini,”alisema Kivuyo
Kwa upande wake Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi,Dk Charles Tizeba,ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ameitaka kampuni ya  TBL Group kwa kushirikiana na halmashauri za wilaya ambapo kuna kilimo cha  Shayiri kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji ili serikali isitishe kuagiza kimea nje ya nchi na aliwataka maafisa kilimo kuweka mipango madhubuti ya kilimo hicho ili kuwawezesha wakulima kunufaika zaidi.
Alipongeza juhudi za kampuni ya  TBL kuwawezesha wakulima pembejeo na utaalamu katika kilimo cha mikataba kinachowahakikishia wakulima soko la mazao yao na kutaka halmashauri kupitia vyama vya ushirika wa wakulima kuwawezesha wakulima kuingia mikataba yenye tija kwao.
Awali Meneja wa kiwanda cha TBL mkoa wa Arusha,Joseph Mwaikasu, alisema jitihada za kuwawezesha wakulima kuongeza ubora na kiwango cha Shayiri unaendelea kwani wamekua wakipata zao hilo chini ya kiwango cha mahitaji yao.
Alisema mahitaji ya kampuni kwa mwaka ni tani 18,000 lakini wakulima wanaweza kuzalisha tani 10,000 pekee na zinazobaki wanaagiza nje ya nchi hivyo kuwataka wakulima kuongeza uzalishaji kwa manufaa yao na taifa kwa ujumla.
Alisema katika kipindi cha mwaka 2016 TBL imewalipa wakulima katika mikoa hiyo Sh 14.7 bilioni zilizotokana na tani 12,700 wakati mwaka huu wameshawakopesha wakulima Sh 2.1 bilioni ziwawezeshe katika maandalizi ya shamba pamoja na pembejeo.
Mwaikasu alisema TBL Group kupitia mkakati wake wa ‘Dunia Maridhawa’ moja ya malengo yake ni kujenga dunia inayokua hivyo itaendelea kufanya kazi na wakulima  kama ambavyo hatua hii imeanza kuleta mafanikio kwa kuboresha maisha ya wakulima,kupanua wigo wa ajira kutokana na mpango huu na kampuni kunufaika wa kupata malighafi bora inayozalishwa hapa nchini.

No comments :

Post a Comment