Sunday, April 30, 2017

CRISTIANO RONALDO AFUNGA NA KUZIDI KUWEKA REKODI ULAYA

Real Madrid imefunga goli la dakika za mwisho na kufanikiwa kuifunga Valencia kwa magoli 2-1 katika hatua muhimu ya kuwania taji la Ligi ya Hispania ya La Liga.

Katika mchezo huo Cristiano Ronaldo aliifungia Real, goli la kwanza na kumfanya kuwa mfungaji anayeongoza kufunga magoli mengi katika ligi tano za juu Ulaya.

Katika mchezo huo ambao Ronaldo alikosa penati, Valencia walisawazisha goli kupitia kwa Dani Parejo dakika ya 82, kisha baadaye Marcelo akafunga goli la ushindi kwa Real.
   Cristiano Ronaldo akiruka juu na kuupiga mpira kwa kichwa na kufunga goli la kwanza
   Dani Parejo akipiga mpira wa adhabu uliopaa juu ya ukuta wa Real na kufunga goli

No comments :

Post a Comment