NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
BENKI
Kuu ya Tanzania (BoT) imesimamisha ajira ya Mkurugenzi Mtendaji wa TIB
Corporate Bank, Bw. Frank Nyabundege kuanzia Julai 13, 2019 kutokana na
ufanisi mbovu wa benki.
ufanisi mbovu wa benki.
Taarifa
iliyotolewa na Idara ya Uhusiano na Itifaki ya BoT leo Julai 14, 2019
imesema uamuzi huu umechukuliwa baada ya BoT kutoridhishwa na utendaji
wa benki hiyo kama inavyopasa.
Taarifa
hiyo imefafanua, kuwa uamuzi huo wa BoT umechukuliwa chini ya Kifungu
namba 33 (1) na 33 (2) (f) vya Sheria ya Usimamizi wa Mabenki na Taasisi
za Fedha ya mwaka 2006.
Aidha
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), chini ya kifungu cha 33 (2) (b) cha Sheria
za Mabenki na Taasisi za Fedha, imeamua kumteua Bw. Fred Luvanda kutoka
Kurugenzi ya Usimamizi wa Mabenki kusimamia shughuli za kiutendaji za
kila siku za benki hiyo kama Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Corporate
Bank.
Taarifa kamili ya BoT inapatikana hapo chini.

No comments :
Post a Comment