Saturday, April 29, 2017

RAIS MAGUFULI AONDOKA DODOMA NA KUELEKEA KILIMANJARO





Mkuu wa mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana akimshukuru  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kabla ya kuondoka uwanja wa ndege wa Dodoma kuelekea mkoani Kilimanjaro leo Aprili 29, 2017. Pamoja na mambo mengine Rais anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za Mei Mosi zinazofanyika kitaifa mkoani humo  (PICHA NA IKULU)








WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagamaametoa wito kwa waajiri wote nchini kujisajili kwenye Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF) kama sheria inavyotaka.




SHAMIMU NYAKI-WHUSM.
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) linaaanda mpango mkakati  wa kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kulinda Haki za Watoto kwa kuandaa vipindi mbalimbali vya redio na luninga kama njia ya haraka ya kufikisha ujumbe kwa jamii.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mwakilishi Mkazi
wa Shirika hilo hapa nchini Bi Maniza Zaman alipokutana na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe ambapo amesisitiza kuendeleza ushirikiano na Serikali katika Miradi na Programu za kulinda Watoto.
“UNICEF itaendelea kuandaa vipindi vya luninga na redio kwa ajili ya kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kulinda haki za watoto ili itambue watoto wanahitaji nini katika maisha yao ya kujenga Taifa la kesho” Alisema Bi Maniza.
Kwa upande wake Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe ameahidi kutoa ushrikiano kwa UNICEF katika mpango huo ambao una malengo ya kusaidia watoto   kutambua haki zao ikiwemo haki ya kupata taarifa.
“Watoto ndio viongozi wa kesho hivyo ni vyema kuwalinda na kuwapatia haki zao wanazostahili ikiwemo ya kuwapa taarifa sahihi na kwa wakati sahihi ili kuwajengea Utamaduni wa kupenda kuwasilisha mawazo yao”.Alisema Mhe.Mwakyembe.
Aidha Mhe. Waziri Mwakyembe amevitaka vyombo vya habari kutoa ushirikiano kwa UNICEF wakati itakapowasilisha vipindi hivyo vya kuelimisha kuhusu haki za watoto ili wananchi wapate elimu itakayosaidia kutoa malezi yanayostahili kwa watoto wao.
Mazungumzo hayo pia yamelenga kuimarisha ushirikiano katika Sekta za Sanaa na Utamaduni zilizopo Chini ya Wizara   kwa lengo la kutambua fursa zinazoweza kutumika kwa manufaa ya pande mbili hizo.

No comments :

Post a Comment