NA MWANDISHI MAALUM
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Dkt.
Alexander Kyaruzi amesema kuwa TANESCO inajipanga kufikisha Umeme wa
Gridi ya Taifa katika Mgodi wa STAMIGOLD Biharamulo ili kuokoa kiasi cha
Takribani Shilingi bilioni 8.4 zinazotumika kwa mwaka katika mgodi huo
kuzalisha umeme ghali wa mafuta mazito ya dizeli kwaajili kuendesha
mitambo ya Mgodi huo.
Kwa
upande wake Meneja Mkuu wa mgodi wa STAMIGOLD, Mhandisi Gilay Shamika
amesema kuwa, kutokana na kukosa umeme nafuu wa TANESCO, gharama za
kiuendeshaji ni kubwa lakini endapo mgodi utaunganishwa na umeme wa
TANESCO, itasaidia kukua kwa mgodi na kuongeza mapato pamoja mchango wa
mgodi Serikalini.
“Hivi
sasa tunatumia takribani Shilingi bilioni 1 kuzalisha umeme kwa mwezi
lakini kama tukiunganisha umeme wa TANESCO tutalipia takriban shilingi
milioni 300 kwa mwezi hivyo tutaokoa takriban bilioni 8.4 ambazo
zitaingia kwenye mapato ya Mgodi na Serikali” Alisema Mhandisi Shamika
No comments :
Post a Comment