
Afisa anayeshughulikia Masuala
ya Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA) Dorice Mhimbila akizungumza na watu wasiosikia wa mkoa wa Simiyu
wakati mamlaka hiyo ilipokwenda kutoa elimu ya utumiaji wa mawasiliano.

Baadhi watu wasiosikia (viziwi) wakiwa katika mafunzo ya utumiaji wa mawasiliano .
*********************************
Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa imeendesha semina ya siku
moja kwa watu wenye matatizo ya kutosikia (Viziwi) katika Mkoa wa Simiyu
yenye lengo la kuwajengea
uelewa juu ya matumizi sahihi na salama ya
mawasiliano.
Mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ambapo zaidi ya viziwi 50 wameshirikia mafunzo hayo.
Akizungumza
na waandishi wa habari Mkuu wa Kanda ya Ziwa wa TCRA , Mhandisi
Francis Mihayo amesema kuwa TCRA imeandaa mafunzo hayo kwa viziwi ili
waweze kuepuka na madhara ambayo wanaweza kupata ikiwa watatumia vibaya
mawasiliano.
Mihayo
ameongeza kuwa viziwi ni moja kati ya watu ambao wameendelea kukumbwa na
tatizo la matumizi mabaya ya mitandao kama facebook, instagram, whatsap
na twitter kwa kurusha vitu ambavyo siyo sahihi.
“ Mara nyingi
wamekuwa wakijikuta wakichukuliwa hatua kali za kisheria kwa kikuka
sheria zilizopo za matumizi sahihi ya mawasiliano, kutokana na hali
tumeona ni vyema tukawapa elimu jinsi gani ya wanaweza kuepuka kwa
kuzitambua sheria,” amesema Mhandisi Mihayo.
Aidha Mihayo
amesema kuwa amekuwa wakipata malalamiko mengi kutoka kwa viziwi juu ya
kutapeliwa kupitia simu, ambapo kupitia mafunzo hayo wataweza
kuwafundisha namna bora ya kuepuka hali hiyo.
“
Tunawaelimisha pia umuhimu wa kusajili laini zao kwa njia ya alama za
vidole, tunatambua changamoto wanazozipata katika zoezi hili, ndiyo
maana tumewaita hapa ili kuwapatia elimu na kutatua changamoto hiyo,”
alisema Mihayo.
Akiongea kwa
niaba ya viziwi hao Makamu mwenyekiti wa viziwi mkoa, Alex Benson viziwi
wameeleza kukumbwa na tatizo la mawasiliano baina yao na watu
wanaohusika katika zoezi la kusajili laini za simu kwa njia ya alama za
vidole (Biometric Registration).
Wamesema kuwa
tatizo hilo limesababisha viziwi wengi katika mkoa huo kushindwa
kujisajili, kutokana na kushindwa kuelewana na watoa huduma wa makampuni
mbalimbali ya simu wakati wa kujisajili kwa mfumo huo.
Bensoni
alisema kuwa mbali na tatizo hilo, Bado Viziwi wameendelea kukumbwa na
tatizo la kutapeliwa na watu wenye nia mbaya kupitia simu, ambapo
alisema kupitia mafunzo hayo wataweza kutatuliwa changamoto hizo.
Akifungua
mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga ameipongeza TCRA
kwa kuona umuhimu wa zoezi hilo, kwani viziwi wanayo haki ya kupata
elimu ya mawasiliano kama watu wengine.
No comments :
Post a Comment