Ndoto na shauku ya
kijana Ahmed Albaity alieteseka kwa zaidi ya Miaka 10 Kitandani kwa
kushindwa kumudu gharama za matibabu leo imebadilika kuwa furaha baada
ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kumkabidhi Tiketi za
Ndege za watu Wanne kwaajili ya safari ya kwenda kupatiwa matibabu
Nchini China kwenye Hospital ya Beijing Puhua International huku
akijitolea pia kugharamia fedha za Matibabu na Malazi.

RC Makonda alitoa
ahadi kumsaidia Ahmed Albaity wakati wa Zoezi la Upimaji Afya Bure
kwenye Meli ya Jeshi la China mwishoni mwa Mwaka Jana baada ya
kugundulika Ahmed anahitaji Matibabu Maalum ambayo hayapatikani kokote
kule duniani isipokuwa China, jambo lililomfanya RC Makonda kutokwa na
Machozi na Kuhaidi Kumpeleka kwenye matibabu kwa gharama yoyote ile
Maumivu na Mateso anayopitia kijana huyo.

Ahmed Albaity
anasumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo baada ya kuanguka na kuvunjika
Shingo alipokuwa akiogelea ambapo kwa sindano moja pekee inagharimu
Dollars 26,000/= sawa na shillingi million 52.
RC Makonda amesema
Ahmed atasafiri Nchini China Siku ya Jumapili akiongozana na watu watatu
wa kumsaidia kumuhudumia ambapo gharama zake ni zaidi ya Shilingi
Million 100.

Aidha RC Makonda
amesema Shauku yake ni kugusa maisha ya Mwananchi hata kama ni mmoja
atakaekwenda mbele za Mungu na kusema Asante Mungu kwa kutupatia
viongozi wetu, ifike mahali tumtumikie Mungu katika nafasi zetu, na
katika hilo watu wote watakuwa Sawa na tutawahudumia bila kutarajia
chochote kutoka kwao kama sehemu ya utumishi wetu ambapo amewashukuru
watu wote waliomchangia na kufanikisha matibabu.
Hata hivyo RC Makonda
ametoa wito kwa wananchi wa dini zote kumuombea Ahmed ili aweze kupona
na kuendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa.
Kwa upande wa Ahmed
Albaity amemshukuru RC Makonda kwa moyo wa ukarimu aliouonyesha ambapo
ameeleza kuwa ameishi kwa mateso muda mrefu kutokana na kukosa uwezo wa
kumudu gharama za matibabu.
Aidha amesema
alipokuwa akiomba watu wamchangie wapo waliokuwa wakimvunja moyo kwa
kumwambia hawezi kupona lakini RC Makonda ameonyesha moyo wa kipekee.
No comments :
Post a Comment