Friday, September 2, 2016

WAZEE WATAKA USHIRIKI WA WAZI KATIKA SERA NA MIPANGO YA MAENDELEO



 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (kushoto) akiongoza na mwenyeji wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za ESRF kufungua warsha ya nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs)  iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International.
  Mkurugenzi Mkazi Shirika la kimataifa la kusaidia wazee (Help Age International), Amleset Tewodros (wa kwanza kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (wa pili kulia) ofisini kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (katikati). Wengine kushoto ni Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Anna Mwasha na Mkurugenzi Mkazi Msaidizi wa Shirika la kimataifa la kusaidia wazee (Help Age International), Smart Daniel (wa pili kushoto).
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi na washiriki wa warsha ya nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs)  iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akifungua warsha kuhusu nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi wa Jukwaa la Wazee Tanzania, Samson Msemembo (85) akizungumzia changamoto wanazokutana nazo wazee katika vituo vya huduma za afya kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (katikati), Kaimu Kamishna Ustawi wa Jamii Bw.Rabikira Mushi kutoka Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida waliopo meza kuu.
 Mtafiti Mkuu Mshiriki kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) na Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Oswald Mashindano akizungumzia nafasi ya wazee katika sera ya kitaifa kwenye warsha kuhusu nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mkazi Shirika la kimataifa la kusaidia wazee (Help Age International), Amleset Tewodros akishiriki kutoa maoni kwenye warsha kuhusu nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akifafanua jambo kwenye warsha ya nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs)  iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International. Kushoto ni Mkurugenzi Mkazi Shirika la kimataifa la kusaidia wazee (Help Age International), Amleset Tewodros.
  Mshauri wa Masuala ya Ushirikiano wa Kanda ya Afrika Mashariki, Kati na Magharibi wa Shirika la Help Age International, Roseline Kihumba akizungumzia hali ya uzee na wazee duniani na ushirikishwaji wa wazee katika maendeleo endelevu kwenye warsha ya nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs)  iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International.

Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Anna Mwasha akichangia mada kwenye warsha ya nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International.
  Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Uchambuzi wa Sera na Utafiti wa Wizara ya Fedha na Mipango, Mudith Cheyo akifafanua jambo kwa washiriki wa warsha kuhusu nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs)  iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International.
 Mkurugenzi wa Mtandao wa Watu Waishio na Virusi vya Ukimwi Tanzania (SHDEPHA), Joseph Katto akizungumzia changamoto zinazowakabili wazee wanaoishi na VVU katika kupata huduma mbalimbali nchini kwenye warsha kuhusu nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya washiriki waliohudhuria warsha kuhusu nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam
  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa mikutano wa ESRF wakati wa warsha kuhusu nafasi ya wazee katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) iliyoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na Shirika la Help Age International
 Picha ya pamoja

 Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Kanali Martin Mkisi akikagua gwaride maalum la wahitimu wa mafunzo ya JKT yaliyofanyika katika kikosi cha 825 JK Mtibila ambapo vijana 1140 walifuzu na kumaliza mafunzo hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Kanali Martin Mkisi akipokea heshima kutoka kwa wahitimu.
 Wahitimu wakipita mbele ya mgeni rasmi kutoa heshima.
 Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Kanali Martin Mkisi akizungumza na wahitimu hao wa mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Kanali Martin Mkisi akiangalia madawati yaliyotengenezwa na vijana hao wa JKT.
**************
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Col Martin Eliah Mkisi katika hotuba yake, amewataka vijana waliohitimu mafunzo ya JKT Oparesheni Magufuli Kundi la nne Kwa Mujibu wa sheria, kuiamini, kuitekeleza na kuiishi kaulimbiu ya HAPA KAZI TU. 

Amesema vijana hao waliobahatika kupata mafunzo ya JKT katika kambi ya 825 KJ Mtabila kuja na mbinu mbadala na mawazo chanya ktk kutatua changamoto mbalimbali za maisha badala ya kulalamika.

 Amewataka kuwa kielelezo cha nidhamu na uzalendo ktk maisha yao ya vyuoni na mahali pa kazi hapo baadaye kama walivyofundishwa na Wakufunzi Mahiri wa JKT. 

Aidha, Col Mkisi amelipongeza JKT kwa kutekeleza wajibu wake adhimu wa kuwalea na kuwafundisha vijana wa Tanzania, stadi za maisha, uzalenda na ujasiliamali.Vijana wapatao 1140 walifuzu mafunzo hayo yaliyochukua miezi mitatu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Doto James kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Fedha na Mipango Doto James mara baada ya kuapishwa.(PICHA NA IKULU)

Shindano la Ulimbwende la "Ozona Miss Lake Zone 2016" linaloshirikisha Walimbwende 18 kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa limezinduliwa rasmi hii leo Jijini Mwanza.
Shindano hilo litakalofanyika jumamosi Septemba 10,2016 katika Ukumbi wa Rock City Mall, limeandaliwa na Flora Promotions na kupewa nguvu na wadhamini mbalimbali akiwemo mdhamini mkuu, Kampuni ya vipodozi ya Ozona ambayo imetoa zawadi ya gari lenye thamani ya shilingi Milioni 12 kwa mshindi wa kwanza.
Katika picha, kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Ozona, Dr.Thobias Mkina, akizungumza katika uzinduzi wa shindano hilo ambapo kushoto ni Mkurugenzi wa Flora Promotions, Flora Lauwo.
Na BMG
Wadau mbalimbali Ozona Miss Lake Zone wakiwa kwenye uzinduzi wa shindano hilo hii leo
Wadau mbalimbali Ozona Miss Lake Zone wakiwa kwenye uzinduzi wa shindano hilo hii leo
Mkurugenzi wa Flora Promotions, Flora Lauwo, akiteta jambo kwenye uzinduzi wa shindano la Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Mzee wa Masauti, Christian Bella pamoja na Mchekeshaji Erick Omond wanatarajiwa kuungana na watumbuizaji wengine pamoja na wadau wengine kwenye kufanikisha Usiku wa Ozona Miss Lake Zone 2016.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto)akizungumza na  Makamu wa Rais wa Angola Mhe. Manuel Domingos Vicente wakati wa kuhitimisha mkutano wa 36 wa nchi za SADC mjini Mbabane Swaziland.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka saini katika moja ya makubaliano yaliofanywa na nchi za SADC kwenye mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliofanyika Lozitha, Mbabane nchini Swaziland.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa kwenye mkutano wa 36 wa nchi 15 za SADC uliofanyika mjini Mbabane Swaziland, kulia ni Makamu wa Rais wa nchi ya Angola Mhe. Manuel Domingos Vicente na kushoto ni Waziri Mkuu wa Madagascar Mhe.Mahafaly Solonandrasana Olivier.
 Mwenyekiti wa SADC Mfalme Mswati wa III(kulia) akizungumza na Katibu Mkuu Mtendaji wa SADC Dr. Stergomena L. Tax wakati wa kuhitimisha mkutano wa 36 wa SADC mjini Mbabane,Swaziland.
 Mwenyekiti wa SADC Mfalme Mswati wa III akihutubia wakati wa kufunga mkutano 36 wa SADC mjini Mbabane ,Swaziland.
                                                    ............................................

No comments :

Post a Comment