Wednesday, November 25, 2015

PAPA FRANCIS AKILAKIWA NA RAIS UHURU KENYATA JIJINI NAIROBI LEO PA1

PA1
Papa Francis akisalimiana na Rais wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta wakayi alipowasili nchini Kenya leo ambapo atakuwa na ziara ya siku sita katika nchi za Afrika. Kushoto ni Mke wa Rais Kenyatta, Magret Kenyatta.
PA2

WENGI WAJITOKEZA KATIKA UZINDUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE JIJINI DAR ES SALAAM

Maelfu wajitokeza katika maandamano ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, hapa wakiendelea na matembezi ya kupinga ukatili wa Kijinsia
  Maandamano yakipokelewa na Mkurugenzi wa shirika la misaada la Marekani USAID  Daniel Moore, Mwakilishi wa Balozi wa Ireland
nchini Maire Matthews, Mwakilishi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa Wanawake
Lucy Melele, Mkurugenzi wa shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo
barani Afrika – WiLDAF, Dr. Judith Odunga, pamoja na wawakilishi wa mashirika
wahisani na viongozi mbalimbali.
 Dr. Judith Odunga kutoka WiLDAF akiwakaribisha wageni.
 Mwanaharakati mama Siwale, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Anna Mghwira(wa kwanza kulia) ni miongoni mwa waliohudhuria maadhimisho hayo.
 Wageni mbalimbali
 Maigizo kuhusu uchapaji wa viboko kwa wanafunzi
 Mwakilishi wa Balozi wa Ireland Maire Matthews akizungumza
  Lucy Melele kutoka shirika la UN Women akizungumza
 Mwalimu akitoa ushuhuda
  Paulina Mkonongo(wa kwanza kulia), Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Akisikiliza jambo
 Mgeni rasmi Bi. Paulina Mkonongo Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi akitembelea sehemu za maonyesho kutoka kwa mashirika mbalimbali.
 Baadhi ya wadau wakitembelea mabanda
 Wadau mbalimbali waliohudhuria maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake.
Maadhimisho
ya Siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake leo yamefunguliwa rasmi kwa
kuanza na maandamano ya amani yaliyoanzia uwanja wa Tipi Sinza darajani hadi
ukumbi wa hoteli ya Blue Pearl iliyopo jengo la Ubungo Plaza jijini Dar es
salaam.
 
Maandamano
hayo yalihudhuriwa na maelfu ya watu yaliongozwa na bendi ya jeshi la polisi
kupitia njia za Shekilango kisha barabara ya Morogoro hadi katika jengo la
Ubungo Plaza ambapo yalipokelewa na Mkurugenzi wa shirika la misaada la
Marekani USAID  Daniel Moore, Mwakilishi wa
Balozi wa Ireland nchini Maire Matthews, Mwakilishi kutoka shirika la Umoja wa
Mataifa Wanawake Lucy Melele, Mkurugenzi wa shirika la Wanawake katika Sheria
na Maendeleo barani Afrika – WiLDAF, Dr. Judith Odunga, pamoja na wawakilishi
wa mashirika wahisani na viongozi mbalimbali.
 
Akitoa
neno la ukaribisho, Dr. Judith Odunga alisema kampeni ya siku 16 kwa mwaka huu
imelenga zaidi kuzungumzia suala zima la usalama mashuleni. Lengo kuu ikiwa
kuhamasisha umma kuhusu ukubwa wa ukatili wa kijinsia kwa vijana na watoto wetu
mashuleni.
 
“Ni
kutokana na unyeti wa tatizo la ukatili wa kijinsia mashuleni, WILDAF na wadau
mbalimbali tumeona kuna umuhimu wa kushirikisha Wizara ya elimu na ufundi stadi
ili kuzungumzia ukatili wa kijinsia mashuleni na kujenga mikakati ya kuzuia
ukatili huo” Aliongezea.
 
Dr.
Odunga aliitaja kauli mbiu ya mwaka huu kuwa ni FUNGUKA! CHUKUA HATUA, MLINDE
MTOTO APATE ELIMU. “Kauli hii inalenga kumshawishi mtu binafsi, kuwashawishi
walimu, wanafunzi, wazazi na jamii kwa ujumla, kuwalinda watoto dhidi ya
ukatili wa kijinsia na kuhakikisha kwamba shule ni mahala salama. Ni vyema
kutafakari kwa kina jinsi vitendo vya ukatili wa kijinsia mashuleni
vinavyoathiri maendeleo ya watoto wetu kielimu.” Alisema Dr. Odunga.
 
Dr.
Odunga alitumia nafasi hiyo kuiomba serikali kufanya yafuatayo:
 
1.
Kufutwa kabisa kwa adhabu ya viboko mashuleni na
waalimu kufundishwa au kutafuta mbinu za kutoa adhabu mbadala.
2.
Kutengeneza mwongozo wa utekelezaji wa sera ya
elimu ya mwaka 2014 utakaoelekeza upatikanaji wa elimu ya msingi iliyo bora na
salama.
3.
Kuboresha miundombinu rafiki ya elimu ikiwa ni
pamoja na kuwa na madarasa ya kutosha, madawati, vyoo na sehemu za kujisitiri
watoto wa kike, mabweni, uzio pamoja na kuwa na usafiri wa uhakika kwa
wanafunzi.
4.
Serikali kuweza kuunda na kusimamia mabaraza
yatakayo kuwa yanasikiliza malalamiko ya wanafunzi mashuleni.
5.
Tunaomba Wizara ya elimu na ufundi stadi kushirikiana
na wizara ya Katiba na Sheria na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
kutunga Sheria ya Ukatili wa Majumbani sambamba na kubadilisha Sheria ya Ndoa
ya mwaka 1971 inayoruhusu ndoa kwa mtoto chini ya miaka 18.
 
 
Akifungua
rasmi kampeni hizi, mgeni rasmi Paulina Mkonongo ambaye ni Mkurugenzi wa Elimu
ya sekondari kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi aliyemuwakilisha
Katibu mkuu wa wizara hiyo alisema, “ukatili wa kijinsia huleta athari hasi
katika utoaji na upatikana wa fursa mbalimbali za kijamii ikiwemo fursa ya
elimu kwa watoto wetu, hivyo kuwa ni kikwazo katika kujenga usawa wa kijinsia
nchini.
 
Aidha
Mkonongo alisema serikali imefanya juhudi za makusudi kuzuia ukatili na kuleta
usawa katika kupambana na ukatili wa kijinsia kwa kuweka sera na mipango
inayozingatia usawa na kupinga ukatili kwa makundi mbalimbali, katika jamii
ukiwemo ukatili wa kijinsia.
 
Mkonongo
alitoa wito kwa wananchi wote kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili na
kwamba kila mtoto ana haki ya kulindwa popote anapokuwepo iwe nyumbani,
shuleni, kwenye vyombo vya usafiri, michezoni na njiani wanapokwenda na kurudi
shuleni pia kuwapa mbinu za kujilinda wenyewe.
 
Naye
mwakilishi wa Balozi wa Ireland nchini Bi. Maire Matthews alisema kuwa takwimu
za hivi karibuni zinaonyesha kuwa wastani wa asilimia 45 ya wanawake Tanzania wenye
umri kati ya miaka 15 – 49 waliripoti kuwahi kufanyiwa ukatili wa kimwili au
kingono katika maisha yao. Alisema takwimu nyingine zinakadiria kiwango hicho kuwa
kati ya 41 – 56%.
 
Kwa
upande wake Lucy Melele kutoka shirika la UN Women aliyemwakilisha Mwakilishi
wa shirika hilo hapa nchini Anna Collins alisema wanawake na wasichana
ulimwenguni kote wanapitia aina mbalimbali za ukatili ambayo inawanyima haki
zao za msingi, ni tishio la demokrasia na ni kizuizi cha amani ya kudumu. Hata
hivyo alisema shirika la umoja wa mataifa litaendelea kufanya kazi kwa ukaribu
na wadau wa maendeleo, serikali, mashirika mbalimbali, na jamii katika kampeni
ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
 
Kampeni
ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia pia inafanyika kikanda katika kanda
ya ziwa (Mwanza, Mara na Shinyanga, kanda ya Kaskazini (Manyara, Arusha,
Kilimanjaro na Tanga), kanda ya kati (Dodoma, Morogoro na Singida), kanda ya
Kusini (Mtwara, Songea, Mbeya, Iringa na Lindi, Kanda ya Pwani (Dar es salaam
na Pwani) zikisimamiwa na wadau mbalimbali wakiwemo mashirika ya Kivulini,
CWCA, NAFGEM, Morogoro Paralegal,  Mtwara
paralegal, WiLDAF, TWCWC pamoja na jeshi la Polisi.
 

 

HATIMA YA MWILI WA MAWAZO KUAGWA AMA KUTOAGWA JIJINI MWANZA KUJULIKANA KESHO.

Na:George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imeahirisha
kesi ya madai ya kuomba ridhaa ya kufanya ibada ya Mazishi ya aliekuwa
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoani Geita Marehemu
Alphonce Mawazo iliyowasilishwa na Mchungaji Charles Lugiko ambae ni baba mlezi
wa marehemu Mawazo.
Katika kesi
hiyo, mlalamikaji anaiomba mahakama kuondoa zuio la jeshi la polisi Mkoani
Mwanza la kutoruhusu shughuli ya kuuaga mwili wa marehemu Mawazo kufanyika
Jijini Mwanza, kabla ya kwenda kuzikwa Mkoani Geita.
 
John Mallya
ambae ni miongoni mwa Mawakili watatu wa Chadema ambao wanaitetea kesi hiyo,
amebainisha kuwa Mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi kesho majira ya saa saba
mchana, ambapo Jaji wa Mahakama hiyo Mhe.Lameck Mlacha anatarajiwa kutoa
maamuzi yake baada ya leo kusikiliza utetezi wa pande zote mbili zinazohusika.
 
Kaimu Katibu
Mkuu wa Chadema bara Salum Mwalimu, amewasihi wanafamilia pamoja na wafuasi wa
chama hicho kuendelea kuwa watulivu, wakati maamuzi ya mahakama hiyo yakisubiriwa
ambapo ameeleza kuridhika na mwenendo wa kesi hiyo.
 
Nje ya
Mahakama, ulinzi ulikuwa umeimarishwa zaidi ambapo kulikuwa na polisi wa
kutuliza ghasia waliokuwa na bunduki za risasi za moto, mabomu ya machozi
pamoja na mbwa ambapo baada ya kesi hiyo kuahirishwa, umati mkubwa wa wananchi
uliokuwa umetanda mita chache kutoka Mahakamani hapo ulianza kuimba nyimbo za
maombolezo na kuwasindikiza viongozi mbalimbali wa chedema hadi katika hoteli
waliyofikia. 

BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA BINAGI RADIO-HABARI 
John Mallya ambae ni mmoja wa Mawakili wa Chadema akizungumza baada ya kesi kuahirishwa
Katibu Mkuu Msaidizi Chadema bara, Salum Mwalimu akizungumza baada ya kesi kuahirishwa
Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe akizungumza baada ya kesi kuahirishwa
Viongozi na makada wa Chadema wakiwa mahakamani
Viongozi na makada wa Chadema wakiwa mahakamani
Mawakili na Viongozi/Makada wa Chadema wakitoka Mahakamani
Wananchi na wafuasi wa Chadema wakitoka Mahakamani huku wakiimba nyimbo za maombolezo
Wananchi na wafuasi wa Chadema wakitoka Mahakamani huku wakiimba nyimbo za maombolezo
Wananchi hawa waliwasindikiza viongozi wa chadema hadi hotelini.

HAKIELIMU YAZINDUA JOPO LA WASHAURI MABINGWA

Timu
ya Menejimenti ya HakiElimu ikiwa katika picha na Mwenyekiti wa Bodi ya
HakiElimu na Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa jopo la washauri
bingwa
Wafanyakazi wa Shirika la HakiElimu waliohudhuria uzinduzi katika picha ya pamoja na jopo la washauri bingwa
Waliosimama ni Prof. J. Galabawa (kushoto) Prof. Kitila Mkumbo (katikati) na Prof. Elias Jengo (kulia) Waliokaa ni John Kalage (Mkurugenzi wa HakiElimu) Prof. G.Mmari (katikati) na Prof. Prof. Martha Qorro (Kulia).
Mgeni
rasmi Prof. Geofrey Mmari,akizungumza jambo katika hafla fupi ya
uzinduzi wa jopo la washauri mabingwa akitoa neno la ufunguzi.
Prof. Kitila Mkumbo mmoja wa wajumbe wa ThinkTank akitoa neno kwa niaba ya jopo la washauri bingwa wa HakiElimu.
Mwakilishi
wa Kamishna wa Elimu Bi, Joyce Sekimanga kutoka Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi akiwasilisha ujumbe kutoka serikali katika uzinduzi wa
jopo la washauri wa HakiElimu
Prof. Martha Qorro mmoja wa wajumbe wa jopo la washauri
mabingwa akipokea mpango mkakati wa HakiElimu kutoka kwa mgeni Rasmi
Prof Geofrey Mmari
Prof. J. Galabawa mmoja wa wajumbe wa jopo la washauri mabingwa akipokea mpango mkakati wa HakiElimu
Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu John Kalage akielezea lengo la kuanzishwa kwa Think Tank
Washiriki katika uzinduzi wa jopo la washauri mabingwa wa HakiElimu
…………………………………………………………………………………….
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
 
SHIRIKA la HakiElimu
limezindua Jopo la Washauri Mabingwa
linaloundwa na maprofesa 10 waliobobea katika fani ya elimu ili  kuleta mabadiliko katika sekta ya elimu kwa
watoto kupata elimu bora.
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es
Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu , John Kalage amesema kazi ya jopo
hilo itakuwa kutoa ushauri wa kitaalam juu ya masuala ya elimu kadri
litakavyoombwa na  HakiElimu.
 
Amesema jopo hilo litatatoa ushaufri juu ya mikakati
,taratibu na mbinu za kuhakikisha ushiriki madhubuti katika kukuza na kutetea
ubora wa elimu nchini.
 
Kalage aliwataja maprofesa wanaounda jopo hilo kuwa ni
Abel Ishumi,Herme Mosha,Justinian Galabawa,Kitila Mkumbo,Suleiman
Sumra,Martha  Qorro, Mwajabu
Possi,Akundaeli Mbise, Masalukulangwa pamoja na Elias Jengo.
 
Amesema kuanzishwa kwa jopo hilo litasaidia shirika
kupata mawazo mapana zaidi ya kitafiti na uchambuzi wa changamoto za sekta ya
elimu.
 
Kalage amesema kuwa jopo hilo litakwenda sambamba na
jitihada za serikali kuwa na mikakati mingi ya kuboresha elimu na azma ya
serikali kutekeleza maazimio mbalimbali ya kimataifa kama  Malengo Maendeleo Endelevu (SDGs)na Incheon ya
uboreshaji wa elimu.
 

VIPODOZI FEKI VYAKAMATWA BANDARINI ZANZIBAR

E3
 Maafisa wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar wakifungua moja ya Boxi lenye Vipozi vyenye Kemikali ambavyo vimepigwa marufuku kutumika duniani baada ya kuvikama Bandarini vikitokea Marekani na Italy.
e285815f-59f6-4535-8772-619d5b24bede
Baadhi ya Vipozi vyenye Kemikali ambavyo vimepigwa marufuku kutumika duniani vikiwa vimetolewa katika Maboxi ambayo yalitumika kuviihifadhi. Vipodizi hivyo Vinasubiri kuteteketezwa na Maafisa wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
…………………………………………………………………………………………
Na Miza Kona Maelezo -Zanzibar 
Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi imekamata vipodozi haramu katika Bandari Kuu ya Malindi Zanzibar ambavyo vimepigwa marufuku kuingizwa nchini.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari huko Ofini Mombasa Mkaguzi wa Bodi hiyo Nassir Buheti amesema vipodozi hivyo haramu vimepigwa marufuku kuingizwa nchini kutokana na kuwa Viambata vyenye kemikali vinavyoweza kuleta madhara Mtumiaji ikiwemo Kansa, Ulemavu pamoja na uharibifu wa ngozi.
Amevitaja vipodozi hivyo kuwa ni pamoja na Movet Crèame kutoka Itali na Medical Fade Crème kutoka Marekani vyenye uzito wa tani tatu na kuhifadhiwa katika Makontena yaliyochanganyishwa na vitu vingine bandarini hapo.
Aidha amefahamisha kuwa vipodozi vya aina Movet Cream hutumika kwa matibabu ya ngozi lakini inahitajika kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia ili kuepukana na madhara.
Mkaguzi huyo ameeleza mawakala wa vipodozi hivyo wamedai kuwa  havikukusudiwa kuingizwa nchini jambo ambalo vipodozi vya aina hiyo vimepigwa marufuku dunia nzima.
Amesema Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi inafanya juhudi ya kutaka kudhibiti kuingiza bidhaa haramu nchini hivyo inaomba mashiriano makubwa kwa jamii ili iweze kufikia lengo lililokusudiwa.
Aidha Mkaguzi Buheti amesema Sheria inasema si ruhusa kuingiza, kuuza, kusambaza vipodozi haramu na kuwataka wafanyabiasha wa vipodozi, dawa pamoja na Chakula kutofanya udanganyifu wa bidhaa wanazoingiza ili kuepuka madhara yasiongezeke nchini.

TIGO YADHAMINI ONESHO LA MWANAMUZIKI MOUSSA DIALLO KUTOKA NCHINI MALI LITANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM KESHO

Meneja wa Mawasiliano wa Kampuni ya Simu ya Tigo, John Wanyanja (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu kampuni hiyo kudhamini onesho la mwanamuziki Mousa Diallo kutoka nchini Mali litakalofanyika kesho katika Mgahawa wa Chakula na Vinywaji wa Samaki Samaki, Masaki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Mkuu wa Masoko wa Mgahawa wa Samaki Samaki, Saum Wengert na katikati ni Mwanamuziki, Moussa Diallo.
 
Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Simu ya Tigo, John Wanyanja (kushoto), akizungumza na Mwanamuziki, Moussa Diallo (kulia). Katikati ni Mmiliki wa Mgahawa wa Samaki Samaki, Carlos Bastos.
Mwanamuziki Moussa Diallo wa nchini Mali anayeishi Denmark (katikati), akiimba mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akijitambulisha ambapo leo atafanya onesho lake Ukumbi wa Samaki Samaki, Masaki jijini Dar es Slaam. Kulia ni Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Simu ya Tigo, John Wanyanja ambao wamewezesha ujio wa mwanamuziki huyo na kushoto ni Ofisa  Mkuu wa Masoko wa Mgahawa wa Samaki Samaki, Saum Wengert.
Ofisa Mkuu wa Masoko wa Mgahawa wa Samaki Samaki, Saum Wengert (kushoto), akizungumza katika mkutano huo kuhusu onesho hilo.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Warembo wa Samaki Samaki wakifuatilia matukio mbalimbali ya mkutano huo.
…………………………………………………………………………………………..
Na Dotto Mwaibale
MWANAMUZIKI maarufu toka Afrika Magharibi anayeishi Denmark, Moussa Diallo, leo anatarajia kufanya onesho lake hilo leo (Novemba 26) katika Mgahawa wa Chakula na Vinywaji wa  Samaki Samaki uliopopo Masaki jijijini Dar es Salaam ambapo litaenda sanjari na ziara ya kutembelea  miradi mbalimbali ya kijamii hapa nchini.


Onesho hilo lililodhaminiwa na Kampuni  ya simu za mikononi ya Tigo ikishirikiana na Mgahawa huo wa  Samaki Samaki litafanywa na Mwanamuziki huyo toka nchini Mali mwenye asili ya Denmark, ambaye amewasili nchini leo.


 Akizungumza Dar es Salaam leo asubuhi kwenye mkutano wa waandishi wa habari, Ofisa Mkuu wa Masoko wa Samaki Samaki, Saum Wengert, alisema mwanamuziki huyo anapiga muziki wa aina ya soul iliyochanganywa na vionjo vya kiafrika na muziki wa Magharibi unaopendwa ulimwenguni kote.


 Alisema onesho hilo pia linatarajiwa kufanyika kesho kutwa (Novemba 27) katika Hoteli ya Melia jijini Zanzibar na baadae watafanya Full Moon Party kwenye Hotel ya Kendwa Rocks iliyopo jijini Zanzibar. 


Moussa alizaliwa jijini Paris nchini Ufaransa na kukulia Bamako nchini Mali ambapo hivi sasa anamakazi yake Copenhagen nchini Denmark.


Katika juhudi za kukuza utamaduni, Diallo anachanganya muziki wake kwa kushirikisha vikundi mbalimbali vya utamaduni ikiwemo; Dawda Jobarten (Kora, Mwimbaji), Preben Carlsen (gitaa), Salieu Dibba (Percussions, Sauti), na Marco Diallo (Ngoma).


Kwa upande wake, Meneja uhusiano wa Tigo, John Wanyacha alisema kampuni hiyo na wadhamini wengine wamekubali Diallo kufanya onesho nchini ikiwa ni pamoja na kuweka mahusiano mazuri yaliyopo na maonesho yanayokuja.


Alisema kuwa wanafahamu wanachopenda wateja wao kwenye muziki na kwamba wana eneo ambalo linaweza kuwawezesha kuzuia miziki wasioyoipenda hivyo ujio wa Diallo nchini utaendeleza makubaliano mazuri kati ya kampuni hizo kwa kuwapa wateja wanachokihitaji ikiwa ni pamoja na vionjo. 


Wengine waliodhamini ziara hiyo ni pamoja ni; Johnnie Walker, French Kiss, Heineken na Ledger Plaza Bahari Beach.


(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
 

MKEMIA MKUU WA SERIKALI AANDAA WARSHA

PRO
Beatrice Lyimo 
Dar es Salaam
Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeandaa warsha ya mafunzo juu ya kujiandaa kukabiliana na dharura ya kemikali hatari na zenye madhara kwa afya na mazingira kwenye maeneo ya bandari.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mkemia mkuu wa serikali Prof. Samweli Manyele amasema kuwa lengo la warsha ya mafunzo hayo ni kuwasilisha na kusambaza matokeo ya utafiti kwa kuhamasisha matumisi salama ya kemikali katika ukanda wa afrika.
“kufundisha nchi za ukanda wa Afrika Mashariki juu ya namna ya kushughulika na kusimamia kemikali hatari na zenye madhara, namna ya kujiandaa na kukabiliana na matukio ya kemikali pamoja na kubadilisha uzoefu wa ushughulikiaji salama wa kemikali hizo kati ya nchi na nchi” aliongeza Prof Manyele.
Pia kujadili mahitaji ya nchi na kikanda pamoja na kutambua hatua za kuelekea njia bora Zaidi ya kujianda na kukabiliana na matukio ya kemikali katika maeneo ya bandari na njia za usafirishaji ni moja ya lengo ya warsha hiyo.
“Ni matumaini yangu warsha ya mafunzo hayo yatakuwa muhimu katika kuongeza uelewa wa washiriki na kujenga uwezo wao wa kushughulikia mizigo ya kemikali hatari kwa usalama na hivyo kulinda afya, mazingira na mali dhidi ya madhara ya kemikali hizo” alifafanua Prof. Manyele.
Warsha hiyo itafanyika kwa muda siku mbili kuanzia tarehe 26 hadi 27 Noverma, 2015 kwenye ukumbi wa Protea Courtyard Hotel iliyopo jijini dar es salaam na kuhusisha nchi mbalimbali.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UGONJWA WA MNYAUKO FUSARI WA PAMBA NA MBEGU ZISIZOOTA

PA
Serikali imewataka wachambuaji na wasambazaji  wa mbegu za pamba kuacha kuwasambazia wakulima mbegu zilizozalishwa katika maeneo yaliyobainika kuwa na ugonjwa wa mnyauko fusari (Fusarium Wilt Disease).  Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Huduma za Usimamizi, Bodi ya Pamba Tanzania, Bwana James Shimbe.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Bwana Shimbe amesema, ugonjwa wa mnyauko fusari unaweza kudhibitiwa ikiwa wakulima wa pamba watatumia mbegu bora kutoka kwa wasambazaji wanaotambulika na Bodi ya Pamba Tanzania.
Akizungumzia tatizo la kuenea kwa ugonjwa huo Bwana Shimbe amesema kwa kiasi fulani limetokana na baadhi ya wachambuaji wasio waaminifu kuendelea kusambaza mbegu za pamba za kupanda ambazo zinaweza kuwa zimetoka katika maeneo yaliyobainika kuwa na  ugonjwa wa mnyauko fusari.
“Tulishatoa maelekezo kwa kuwataka wasambazaji wa mbegu za pamba za kupanda kutosambaza mbegu zilizozalishwa katika maeneo yenye ugonjwa.”
Hivyo tunaendelea kusisitiza kuwa wakulima wawe makini wanapo nunua mbegu kutoka kwa wasambazaji wasiotambulika na watoe taarifa haraka kwa Bodi wanapoona mbegu hizo hazioti ili hatua za haraka zichukuliwe za kupeleka mbegu zingine mbadala ili kuendana na msimu wa kilimo.
Aidha, Bwana Shimbe amewataka wachambuaji wa pamba ambao ndio wasambazaji wa mbegu kuacha mara moja kuwasambazia wakulima mbegu ambazo zimetoka kwenye maeneo yaliyobainika kuwa na ugonjwa na badala yake mbegu za pamba hizo zisindikwe kuzalisha mafuta ya kula kama walivyokuwa wameelekezwa na Bodi hapo awali.
“ Bodi ilishatoa maelekezo kwa wachambuaji wote wa pamba kote nchini,  kutenga mbegu za pamba za kupanda  msimu huu wa kilimo kutoka maeneo yaliyo salama kwa kuziwekea lebo ili  kuzitofautisha na zile zinazotoka kwenye maeneo yaliyobainika  kuwa na ugonjwa, ambapo  zile zinazotoka katika maeneo yenye ugonjwa zisitumike kama mbegu za kupanda, bali zisindikwe kupata mafuta ya kula kama sehemu ya kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa, na zile mbegu ambazo zimetoka kwenye maeneo yasiyo na ugonjwa zisambazwe kwa wakulima kwa ajili ya kupanda kwenye mashamba yao baada ya kufanyiwa majaribio ya uotaji (seed germination test) na taasisi inayohusika na udhibiti wa ubora wa mbegu (TOSCI)”
 Aidha, mbegu zinazofaa kutumika kwa sasa ni UKM08 iliyofanyiwa utafiti na Kituo chetu cha Utafiti cha Ukiriguru, ambayo ubora wake umethibitishwa na Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu (TOSCI) na inauwezo wa kuhimili magonjwa pamoja na uzalishaji wenye tija zaidi. Mbegu hiyo itakuwa inaiondoa kwenye uzalishaji ile ya zamani  ya UK 91 ambayo imepungua ubora wake. Katika msimu huu wa kilimo wa 2015/16 Mbegu ya UKM08 itaendelea kuzalishwa kwa wingi (seed multiplication) katika maeneo salama yasiyo na ugojwa wa mnyauko fusari katika mkoa wote wa Singida na wilaya ya Nzega na Igunga, mkoa wa Tabora.
Bwana Shimbe ametoa wito kwa wakulima na wadau wote wa pamba nchini kufuata kanu
ni za kilimo bora cha pamba ikiwa ni pamoja na kutumia mbegu bora za pamba.  Aidha, baadhi ya mawakala wa ununuzi wa pamba mbegu na wakulima wenye tabia ya kuchanganya pamba mbegu na maji, mchanga, chumvi na kemikali zingine kama vile “mafuta ya kenge” kwa madai ya kuongeza uzito kwenye pamba yao waachane na tabia hiyo potofu, kwani kwa kufanya hivyo kunachangia kuoza kwa kiini cha mbegu na kuharibu ubora wake na hivyo kusababisha mbegu kutokuota.  
Imetolewa:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika

JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. OTHMAN CHANDE ATOA SOMO KWA WAANDISHI WA HABARI.

MO1
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akitoa ufafanuzi kwa wanabari (hawapo pichani) kuhusu uandishi bora wa habari za Mahakama wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama leo jijini Dar es salaam.
MO2
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande (kushoto) na Meneja wa Maadili wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Allan Lawa (kulia) wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari za Mahakama yaliyoandaliwa na Mahakama ya Tanzania leo jijini Dar es salaam.
MO3
Rais wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari namna wanavyoweza kuandika habari za Mahakama kwa kuzingatia weledi wa taaluma zao.
MO4
Washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama wakiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande leo jijini Dar es salaam.
MO5
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama leo jijini Dar es salaam.
Picha/Aron Msigwa –MAELEZO.
………………………………………………………………………………
Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
 Dar es salaam.
Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuzingatia weledi wa taaluma zao wanapoandika habari za Mahakama ili kuepuka kuandika habari zinazowatia hatiani watuhumiwa na kushindwa kutofautisha kati ya  mshitakiwa na mtuhumiwa pamoja na haki zake.
Akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa Habari za Mahakama leo jijini Dar es Salaam, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande  amesema waandishi wa habari  wanalojukumu la kuwapatia wananchi taarifa sahihi kuhusu masuala yanayowahusu na kuepuka uandishi wa habari zenye kuhukumu.
Amesema  kisheria mtuhumiwa huwa hana hatia mpaka itakapothibitishwa na mahakama kuwa ametenda kosa na kuongeza kuwa kukosekana kwa weledi katika uandishi wa habari za mahakama  huleta mkanganyiko  miongoni mwa jamii  kuhusu ukweli na kuondoa imani ya watu kwa mahakama.
Ameongeza kuwa baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa Vikitoa  habari zisizo mpatia mtu  fursa na haki ya kujibu tuhuma huku vingine vikitoa taarifa nusunusu na kushindwa kuwa na mwendelezo wa habari za mashauri mbalimbali mahakamani.
Mhe.Chande ameeleza kuwa waandishi wamejikita katika uandishi wa taarifa zenye mvuto kwa jamii na kusahau nyingine walizo anza nazo jambo  linalosababisha wananchi kuachwa  njia panda bila kupata taarifa za kina kuhusu mwisho wa mambo yanayoanzishwa.
” Mimi sitaki kuingilia utendaji wa kazi zenu za kila siku ila nachotaka kusema ni kuweka msisitizo wa utoaji wa habari za mashauri mbalimbali mnayoanza kuyaripoti kwa mwendelezo ili msiwachanganye wananchi” Amesisitiza.
Amewataka waandishi wa habari kuandika habari sahihi na kuepuka upendeleo na maslahi binafsi ili kulinda taaluma na imani katika jamii juu ya utendaji wa vyombo vya habari.
Mhe. Chande ametoa wito kwa waandishi wa habari kuepuka uandishi wa habari zilizojaa chuki zinazoweza kuleta mgawanyiko katika jamii na kusisitiza habari za kuisaidia jamii kukabiliana na changamoto mbalimbali.
Kuhusu Mahakama amesema itaendelea kuboresha huduma na miundombinu yake katika maeneo yasiyofikiwa ili kuendelea kutoa haki kwa wakati pia  kushirikiana na waandishi wa habari wa ndani ili kuimarisha utendaji wao.
Aidha amevipongeza vyombo vya habari kwa ukomavu  viliouonyesha wakati wa utoaji wa taarifa za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Kwa upande wake Rais wa Baraza la Habari Tanzania Mhe. Jaji Mstaafu Mhe.Thomas Mihayo akizungumza kwa niaba ya Baraza hilo ametoa wito kwa waandishi wa habari kuzingatia weledi katika uandishi wa habari za mahakama ili kuepusha madhara katika jamii.
Amewataka waandishi kujikita zaidi katika uandishi wa habari zenye uhakika kuliko kuwa na taarifa zenye mlengo wa kuuza gazeti.
Amesema kuwepo kwa mafunzo hayo ambayo yameandaliwa na Mahakama ya Tanzania ni ishara nzuri ya uboreshaji wa taaluma ya habari hasa uongezaji wa ushirikiano katika kutekeleza majukumu ya kimahakama hapa nchini.
Amewataka wanahabari kujifunza na kufuatilia miongozo na kufuatilia taarifa mbalimbali zinazoweza kuboresha uandishi wao kwa kupata maneno sahihi ya kimahakama.Amesema Semina hiyo itawasaidia waandishi wa habari kujenga weledi katika uandishi wa habari za mahakama.
Ametoa tahadhari kwa waandishi kuepuka uandishi wa habari zenye uchochezi ili kuepuka kushtakiwa na jamii, kuepuka lugha za kishabiki na upendeleo.
Naye Meneja wa Maadili wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Allan Lawa akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo amewataka kuepuka kuandika habari zinaonyesha upendeleo na  kubainisha kuwa kuwa ipo haja kwa vyombo vya habari kutenga maeneo madawati ya habari hizo

Matumizi ya TEHAMA yaboresha ufanisi Serikalini.

KA1
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba akiwaeleza waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu utaratibu wa Serikali kutumia TEHAMA katika kufanya mikutano kwa kutumia mfumo wa Mawasiliano ya  (Video  comference) ambapo kikao kimoja kitawaunganisha pamoja washiriki kutoka  Mikoa 8 ambapo mada huwasilishwa na kutoa fursa ya kuwasiliana moja kwa moja (interactivity) kwa maswali na ufafanuzi leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bi Zamaradi Kawawa.
KA2
Mkurugenzi Msaidizi  wa Idara ya Habari  (MAELEZO) Bi Zamaradi Kawawa  akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano kati ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na vyombo vya habari uliofanyika leo jijini Dar es asalam.Kulia kwake ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Priscus Kiwango.
KA3
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi  kuhusu utaratibu wa Serikali kutumia TEHAMA katika kufanya mikutano ambapo mfumo wa Mawasiliano ya (Video comference)  utatumika ili kupunguza gharama za mikutano kwa Taasisi za Serikali.
KA4
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari kuhusu faida za kutumia TEHAMA ikiwemo kuokoa fedha zilizokuwa zinatumika awali kuandaa mikutano hiyo ambapo kwa sasa washiriki watashiriki mikutano hiyo wakiwa katika vituo vyao vya kazi leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Priscus Kiwango.
(Picha na Frank Mvungi-Maelezo)
..…………………………………………………………………………………………
Na Jovina Bujulu-MAELEZO
Uanzishaji wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Serikalini utaboresha na kuongeza ufanisi wenye tija ambao utapunguza gharama za utendaji na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Kupitia utaratibu huu wa vikao kazi ambavyo vitaendeshwa kwa kutumia mfumo wa mawasiliano ya video ambapo kikao kimoja kitaunganisha kwa pamoja washiriki kutoka mikoa nane ambapo mada huwasilishwa na kutoa fursa ya kuwasiliana moja kwa moja kwa maswali na ufafanuzi.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu matumizi ya TEHAMA katika kupunguza gharama za uendeshaji vikao kazi.
Mfumo wa mawasiliano ya video ni teknolojia inayowezesha mawasilano kutoka vituo mbalimbali kuwasiliana kwa njia ya sauti na picha kwa njia ya kielekroniki bila kuhitaji kukutana eneo moja.
“Teknolojia hii ya kutumia mfumo wa mawasiliano ya video itapunguza gharama mbalimbali za uendeshaji vikao Serikalini ambazo ni pamoja na kukodi kumbi za mikutano, usafiri na muda ambao hutumika nje ya vituo vya kazi” alisema Temba.
Aidha, Bw. Temba alisema kuwa utaratibu wa vikao ni rasmi kama ilivyo mikutano mingine ya kazi ambao ni salama kwa kuwa miundo mbinu yake inaratibiwa na Serikali.
Bw. Temba aliendelea kusema kuwa mwongozo wa mawasiliano kwa njia ya video umetolewa na unapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, “Mwangozo huu unahusu wajibu wa Wizara, idara, Wakala za Serikali na Mamlaka ya Serikali za Mitaa katika kuboresha mawasiliano kwa njia ya video” aliongeza Bw.Temba
Pia mwongozo huo unaainisha mazingira na vifaa ya kuendesha mawasiliano kwa njia ya video kuzingatia sifa na viwango vya chini na kuhakiki mfumo huo kabla ya matumizi.
Mfumo huo ulianzishwa na Serikali mwaka 2013/2014 katika mikoa ya Kilimanjaro, Kagera, Morogoro na Iringa kati ya utumishi na mamlaka za Serikali za mitaa ambapo kwa sasa mawasiliano hayo yanapatikana nchi nzima isipokuwa mikoa mipya ya Geita, Simiyu, Katavi na Njombe.

No comments :

Post a Comment