Monday, January 23, 2023

UCHUMI WA TANZANIA UNAENDELEA KUIMARIKA-MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO

DODOMA


MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Philip Isdori Mpango amesema, uchumi wa Tanzania umeendelea kuimarika licha ya changamoto iliyoikumba Dunia ya UVIKO-19 na vita kati ya Urusi na Ukraine.

Hayo yamesemwa leo Januari 20, 2023 kupitia hotuba ya Makamu wa Rais iliyosomwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe.Angellah Kairuki (Mb) katika hafla ya kuufahamisha umma mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita katika Mkoa wa Dodoma.

"Nina furaha kujumuika nanyi leo hapa Dodoma katika Ukumbi huu wa TAG kushirikiana na nanyi kuufahamisha Umma wa Watanzania na dunia kwa ujumla mambo makubwa ambayo kwa neema za Mwenyezi Mungu na juhudi za watanzania hususan wana-Dodoma zimetuwezesha kupiga hatua kubwa ya maendeleo.

"Jambo la kwanza, sisi sote ni mashahidi kuwa uchumi wa nchi yetu umeendelea kumaimarika. Tanzania ni nchi ya mfano duniani katika usimamizi wa uchumi ambapo, licha ya majanga ikiwemo changamoto za UVIKO 19 na vita inayoendelea baina ya Urusi na Ukraine,"amesema Mhe.Kairuki kwa niaba ya Makamu wa Rais Dkt.Mpango.

Amefafanua kuwa, tathimini ya Benki ya Dunia inaonesha kuwa uchumi wa Tanzania uko imara. Kulingana na taarifa za Benki Kuu, katika robo ya kwanza ya mwaka 2022 uchumi umekua kwa asilimia 4.8 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 3.8 katika kipindi kama hicho mwaka uliotangulia 2021.

"Hata hivyo, kutokana na mipango kabambe iliyowekwa na Serikali, tunatarajia uchumi utakua zaidi hadi kufikiaw wastaniwa asilimia 5.0.


Chanzo; OR-TAMISEMI

No comments :

Post a Comment