Tuesday, March 3, 2020

SIMBACHAWENE ASHANGAA MTUHUMIWA KUACHIWA NA MAHAKAMA ZANZIBAR KWA KUKOSEKANA MKALIMANI




Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza na Watendaji Wakuu wa Jeshi na Polisi Zanzibar, katika ukumbi wa mikutano wa Jeshi hilo, Mjini Unguja, leo. Simbachawene amesema atafuatilia kwa viongozi baada ya kupokea taarifa ya Jeshi lake, kuwa mtuhumiwa wa dawa za kulevya mjini humo kuachiwa huru na mahakama kwasasabu ya kukosekana kwa mkalimani. Pia alishangazwa na baadhi watuhumiwa wa dawa za kulevya kuachiliwa huru na mahakama kwa kupewa adhabu ndogo ambacho hakiendani na ukubwa wa kosa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akisalimana na wananchi walinaosubiri kuhudumiwa na Maafisa Uhamiaji Makao Makuu, Zanzibar, leo, wakati alipokuwa anawasili katika ofisi hizo kwa ajili ya kuzungumza na Watendaji Wakuu wa Uhamiaji. Pia, Waziri huyo alikutana na Viongozi wa Polisi na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa katika ziara yake ya siku moja mjini humo
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kulia) akimsikiliza Afisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Ofisi ya Zanzibar, Khadija Kheir Othman, wakati alipokuwa anafanya ziara katika ofisi hizo, leo. Waziri huyo aliwataka maafisa hao kufanya kazi kwa uadilifu pamoja na kushirikiana.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati meza kuu) Mkuu wa Sheria Uhamiaji Zanzibar, Kamishna Msaidizi wa Idara hiyo, Hosea Kagimbo, wakati alipokuwa anazungumza na Watendaji Wakuu wa Idara hiyo, leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza na Watendaji Wakuu wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar, katika kikao kilichofanyika ukumbi wa mkutano wa Idara hiyo, leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed, alipomtembelea ofisini kwake Vuga, Mjini Zanzibar, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments :

Post a Comment