Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akisalimiana na Balozi wa Canada nchini Tanzania Bi.Pamela O’Donnell,
wakati akiwasili katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma, kufungua
Maonesho ya Wiki ya Azaki
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya AZAKI
yanayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akiangalia kitabu, wakati akitembelea mabanda, kabla ya kufungua
Maonesho ya Wiki ya AZAKI yanayofanyika katika uwanja wa Jamhuri,
jijini Dodoma Kutoka kushoto ni Msajili wa Mashirika Yasiyo ya
Kiserikali, Vickness Mayao, Mkurugenzi Mtendaji wa Wajibu Ludovick
Utouh, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy
Mwalimu.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akiangalia bidhaa, iliyotengenezwa na Mjasiriamali ambaye ni mlemavu wa
macho, Angela Sebastian, wakati akitembelea mabanda, kabla ya kufungua
Maonesho ya Wiki ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini
Dodoma
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akisalimiana na Mjasiriamali ambaye ni mlemavu wa macho, Angela
Sebastian, wakati akitembelea mabanda, kabla ya kufungua Maonesho ya
Wiki ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akisalimiana na Mkurugenzi wa Policy Forum, Semkae Kilonzo, kwenye
ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa
Jamhuri, jijini Dodoma,
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,
akizungumza na wananchi,wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya AZAKI
inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
Rais wa Foundation for Civil
Society, Dkt.Stigmata Tenga, akitoa taarifa kwenye ufunguzi wa Maonesho
ya Wiki ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma
Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu, akizungumza kwenye ufunguzi wa
Maonesho ya Wiki ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini
Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani
Jafo,akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya AZAKI
inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji ,Foundation
for Civil Society (FCS) ,akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Wiki
ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Mhe.Binilith Mahenge ,akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya
AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
Sehemu ya wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa
katika picha ya pamoja na viongozi wa AZAKI baada ya kufungua Maonesho
ya Wiki ya AZAKI inayofanyika katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.
…………………….
Na.Alex Sonna,Dodoma
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa
amezindua leo wiki ya Asasi za Kiraia(AZAKI) huku akisema serikali
itaendelea kujenga mazingira wezeshi ya utendaji kazi wa AZAKI ili
ziweze
kushiriki ipasavyo katika agenda ya maendeleo.
Aidha, amezitaka asasi za
kiraia kuhamasisha wananchi kuhusu umuhimu wa kupiga kura katika
uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, mwaka huu.
Akizungumza leo katika
uzinduzi wa wiki hiyo iliyoanza leo hadi Novemba 8, mwaka huu,Waziri
Mkuu Majaliwa amesema serikali ipo tayari muda wote kushirikiana na
AZAKI katika kuleta maendeleo kwenye jamii ya Watanzania.
Amesisitiza AZAKI kuhakikisha zinatekeleza majukumu kwa mujibu wa Sheria.
“Hivyo, hakikisheni
mnatekeleza majukumu yenu kwa kuzingatia sheria, taratibu, kanuni na
miongozo iliyopo na mnapotekeleza majukumu yenu hakikisheni mnazingatia
misingi ya uwazi na uwajibikaji na katika utekelezaji wa miradi na
programu wabainishe vyanzo vyao vya fedha,”amesema.
Waziri Mkuu amewataka
kujihusisha na mambo ambayo ni kinyume na Sheria na taratibu za Nchi na
badala yake wajikite kwenye mipango, miradi na mikakati kwa kuzingatia
vipaumbele vya Taifa.
Kadhalika, amesema serikali
itaendelea kuondoa vikwazo vinavyochangia kukwamisha dhamira ya
kuboresha maisha ya wananchi na hasa wanyonge huku akiwahakikishia kuwa
Serikali ya awamu ya tano inathamini sana mchango wa Asasi za Kiraia na
itaendelea kushirikiana nanyi katika kuboresha maisha ya wananchi wetu
hasa wanaoishi maeneo ya vijijini.
Ametoa rai kwa kwa watoa mada
na washiriki wa mijadala kwenye maonyesho hayo kuhakikisha wanazingatia
maslahi mapana ya Taifa sambamba na kutoa ushauri utakaosaidia kuweka
mikakati madhubuti ya kuendeleza Taifa letu kupitia utendaji mzuri wa
AZAKI.
Kuhusu uchaguzi wa serikali za
mitaa, Majaliwa amesema wananchi wengi wamejiandikisha kupiga kura
hivyo ni wajibu wa asasi kuhimiza kujitokeza kupiga kura ambapo
wapiga kura 19,681,259 sawa na
asilimia 86 ya makadirio ya wapiga kura 22,916,412 wamejiandikisha mwaka
huu ikilinganishwa na mwaka 2014 ambao ulifika asilimia 63 ya
makadirio.
Ametoa wito kwa watanzania
wote wenye sifa kujiandaa kushiriki kupiga kura kwa kuwa ni haki yao
kikatiba kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na serikali imejipanga
kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu.
Kwa upande wake Rais wa
Foundation for Civil Society, (FCS), Dkt Stigmata Tenga, kupitia wiki ya
asasi za kiraia zinapata fursa ya kuonesha shughuli wanazozifanya
katika maeneo mbalimbali hapa nchi na kauli mbiu ya wiki hiyo ni “ubia
kwa Maendeleo, ushirikiano Kama nguzo ya Maendeleo Nchini Tanzania”.
Ameongeza kuwa hapa
nchini kumekuwa na ongezeko la asasi za kiraia zipo takribani elfu 6000
na zimejikita katika maeneo mbalimbali hapa nchini na kujishughulisha
na mambo mbalimbali katika kazi za kitaifa, mikoa, wilaya, Tarafa, kata
na vijiji” amesema Dkt Stigmata.
Amesema wanashirikiana
na Serikali katika majukumu yao, na kwa ushirikiano mkubwa na wanatambua
kazi kubwa inayofanywa na Serikali katika nyanja mbalimbali kutika
kuwatumikia wananchi.
Ameiomba serikali katika
bajeti zao waone namna ya kutenga fungu kwa ajili ya asasi za kiraia
katika kuziwezesha Kama luzuku kutimiza majukumu yao na kuongeza ufanisi
zaidi katika shughuli zao za kila siku kuwatumikia wananchi.
Naye Waziri wa Afya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amesema Wizara
yake ndio msimamizi Mkuu wa shughuli zote za asasi za kiraia na
kunaidara maalumu ambayo inaratibu shughuli zote za asasi za kiraia na
wanashirikiana nao vyema.
Ameongeza kuwa ”
wanashirikiana vyema na asasi zote za kiraia na asasi nyingi
zimejipambanua kufanya kazi na jamii hasa zile za chini kabisa na watu
wasiojiweza, katika maswala mbalimbali Kama Afya,elimu,maji na msaada wa
kisheria vitu ambavyo vinaungwa mkono na Serikali” amesema Waziri Ummy.
No comments :
Post a Comment