Mohammed Dewji akizungumza na
wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao wanafadhiliwa na
Taasisi ya Mo Dewji katika hafla ya kutangaza washindi wa mpango wa
ufadhili kwa wanafunzi wa elimu ya juu (Mo Scholars).
Taasisi ya Mo Dewji, Mohammed Dewji
akikabidhi zawadi kwa baadhi ya wanafunzi wa elimu ya juu waliopata
ufadhili kutoka katika taasisi hiyo kwa mwaka wa masomo 2017/2018
kupitia mpango wa Mo Scholars.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao wanafadhiliwa na
Taasisi ya Mo Dewji wakisikiliza kwa makini katika hafla ya kutangaza washindi wa mpango wa
ufadhili kwa wanafunzi wa elimu ya juu (Mo Scholars).
Taasisi ya Mo Dewji imetangaza
orodha ya wanafunzi 22 wa elimu ya juu waliopata ufadhili kutoka
katika taasisi hiyo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 kupitia mpango wake
wa Mo Scholars.
Wanafunzi hao ni Neema Charles,
Winfrida Mrope, Henritha Rwegasira, Monica Ubushimbali, Suzana
Mkindi, Hamisa Selemani, Beatrice Shupa, Phoebe Mwankemwa, Amon
Abraham, Venance Makambe na Amos Ntandu.
Wengine ni Benjamin Mkondya, Ally
Mashaka, Amuniri Sebarua, Iddi Mbilinyi, Samwel Ponda, Eram Temu,
Busumilo Tumaini, Cosmadeus Mayunga, Amos Kashinje, Kelvin Ernest na
Barnaba Barnaba ambao wote ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM).
Akizungumza kuhusu ufadhili huo,
Mwanzilishi wa Taasisi ya Mo Dewji, Mohammed Dewji aliwapongeza
washindi kwa kufanikiwa kupata ufadhili huo, lakini akiwataka
kujituma ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea katika maisha yao.
No comments :
Post a Comment