Tuesday, February 27, 2018

MO DEWJI AAHIDI KUONGEZA IDADI YA WANAFUNZI WANAOPATA UFADHILI WA TAASISI YAKE

Mohammed Dewji akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao wanafadhiliwa na Taasisi ya Mo Dewji katika hafla ya kutangaza washindi wa mpango wa ufadhili kwa wanafunzi wa elimu ya juu (Mo Scholars).
Taasisi ya Mo Dewji, Mohammed Dewji akikabidhi zawadi kwa baadhi ya wanafunzi wa elimu ya juu waliopata ufadhili kutoka katika taasisi hiyo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 kupitia mpango wa Mo Scholars.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao wanafadhiliwa na Taasisi ya Mo Dewji wakisikiliza kwa makini katika hafla ya kutangaza washindi wa mpango wa ufadhili kwa wanafunzi wa elimu ya juu (Mo Scholars).

Taasisi ya Mo Dewji imetangaza orodha ya wanafunzi 22 wa elimu ya juu waliopata ufadhili kutoka katika taasisi hiyo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 kupitia mpango wake wa Mo Scholars.

Wanafunzi hao ni Neema Charles, Winfrida Mrope, Henritha Rwegasira, Monica Ubushimbali, Suzana Mkindi, Hamisa Selemani, Beatrice Shupa, Phoebe Mwankemwa, Amon Abraham, Venance Makambe na Amos Ntandu.

Wengine ni Benjamin Mkondya, Ally Mashaka, Amuniri Sebarua, Iddi Mbilinyi, Samwel Ponda, Eram Temu, Busumilo Tumaini, Cosmadeus Mayunga, Amos Kashinje, Kelvin Ernest na Barnaba Barnaba ambao wote ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Akizungumza kuhusu ufadhili huo, Mwanzilishi wa Taasisi ya Mo Dewji, Mohammed Dewji aliwapongeza washindi kwa kufanikiwa kupata ufadhili huo, lakini akiwataka kujituma ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea katika maisha yao.

No comments :

Post a Comment