Friday, November 3, 2017

WAKULIMA WILAYA YA BUKOMBE WALILIA MBEGU ZA MAHINDI YA WEMA 2109 YANAYOSTAHIMILI UKAME

Mshauri wa Jukwaa la Matumizi ya Bioteknolojia katika kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange (kulia), akimkabidhi mbegu ya mahindi ya Wema 2109, Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Bukombe, Joseph Bachibya kwa ajili ya kupanda katika shamba darasa katika Kijiji cha Msasa kilichopo Kata ya Runzewe wilayani humo leo. Wengine kutoka kulia ni Mtafiti wa Mazao ya Mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibula na Mtafiti, Dk. Beatrice Lyimo  kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)
Maofisa Ugani wakiandaa shamba darasa la mahindi ya Wema  katika Kijiji cha Kabagole kilichopo Kata ya Busonzo litakalosimamiwa na Kikundi cha Igembensabho.
Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Bukombe, Joseph Bachibya, akizungumza na wakulima wa Kikundi cha Igembensabho.
Wanakikundi cha Igembensabho wakiwa wameshosha mikono ikiwa ni ishara ya mshikamano.
Mshauri wa Jukwaa la Matumizi ya Bioteknolojia katika kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange (kulia), akimkabidhi mbegu ya mhogo aina ya Mkombozi, Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Bukombe, Joseph Bachibya kwa ajili ya kupanda katika shamba darasa katika Kijiji cha Msasa kilichopo Kata ya Runzewe wilayani humo leo. Wengine kutoka kulia ni Mtafiti wa Mazao ya Mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibula na Mtafiti, Dk. Beatrice Lyimo  kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)
Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Bukombe, Joseph Bachibya akikmabishi mbegu ya Wema Ofisa Ugani wa Kijiji cha Kabagole, Ponsian Pancras.
Mtafiti wa Kilimo kutoka Kituo cha Utafiti wa Ilonga mkoani Morogoro, Ismail Ngolinda, akiwafundisha wakulima wa Kijiji cha Kabagole namna ya kupanda mahindi ya Wema. Kulia ni Ofisa Ugani, David Makabila kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.
Katibu wa Kikundi cha Igembensabho, Jacob Nsunzu akizungumza na waandishi wa habari.
Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Bukombe, Joseph Bachibya akikmabishi mbegu ya Wema Ofisa Ugani wa Kijiji cha Msasa, Mohamed Mwangeni. Katikati ni Mshauri wa Jukwaa la Matumizi ya Bioteknolojia katika kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange.
Mtafiti wa Kilimo kutoka Kituo cha Utafiti  Ilonga mkoani Morogoro, Ismail Ngolinda, akiwafundisha wakulima wa Kijiji cha Msasa, namna ya kupanda mahindi ya Wema.

Na Dotto Mwaibale, Bukombe Geita

No comments :

Post a Comment