Friday, April 28, 2017

RAIS DKT. MAGUFULI APOKEA TAARIFA YA ZOEZI LA UHAKIKI WA VYETI KWA WATUMISHI WA UMMA KATIKA UKUMBI WA CHIMWAGA MKOANI DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinyanyua juu Taarifa na vitabu vye majina 9,932 ya watumishi wenye vyeti vya kugushi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia viongozi mbalimbali, wanafunzi wa UDOM, pamoja na watumishi wa Umma mara baada ya kupokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa watumishi wa umma kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisoma moja ya  vitabu vya Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa watumishi wa umma awamu ya kwanza alivyopokea kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angela Kairuki, (kulia) katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma leo Aprili 28, 2017. Katikati ni Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa Watumishi wa umma kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe na kufungua boksi kubwa lenye majina ya watumishi zaidi ya 9,932 waliobainika kuwa na vyeti vya kugushi mara baada ya kupokea Taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti  kwa watumishi wa umma kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa , Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako, Spika wa Bunge Job Ndugai, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Angela Kairuki wakiminya kitufe kuashiria maadhimisho ya miaka 10 ya Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na watumishi mbalimbali wa umma, viongozi pamoja wanafunzi wa UDOM mara baada ya kumaliza kuhutubia katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.


Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia katika Ukumbi wa Chimwaga.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akihutubia katika hadhara hiyo katika Chuo kikuu cha Dodoma UDOM.



Baadhi ya viongozi mbalimbali wakifatilia kwa makini Hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika maadhimisho ya miaka 10 ya Chuo cha UDOM toka kuanzishwa kwake.


Baadhi ya Makatibu wakuu pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, wanafunzi pamoja na walimu wa  UDOM wakipiga makofi wakati wakimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akiwasili katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Taarifa ya miaka 10 ya Chuo kikuu cha Dodoma UDOM kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Idris Kikula, katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma. (PICHA NA IKULU)

No comments :

Post a Comment