Na Habari MAELEZO
Katika kuadhimisha miaka 53 ya
Mapinduzi ya Zanzibar Idara ya Habari – MAELEZO ilipata fursa ya kufanya
mahojiano na Waziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mwenye
dhamana ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Hamad Rashid
Mohammed, kuhusiana na maadhimisho hayo. Yafuatayo ni maswali na majibu
katika mahojiano hayo:
SWALI: Zanzibar imetimiza miaka 53 ya Mapinduzi una lipi la kuwaeleza Wazanzibar?
JIBU:
Unapoongelea Mapinduzi ya
Zanzibar, wote tukumbuke ndio chanzo cha Muungano wetu wa Tanganyika na
Zanzibar, bila Mapinduzi Muungano usingekuwepo, haya yote ni katika
kuzingatia umoja. Umoja ni jambo la msingi sana kwa Wanzanzibar kwa kuwa
Serkali ya Kikoloni ilitubagua na kupanda mbegu ya kubaguana hata kwa
sisi Wafrika wenyewe.
Ni vema kuyaenzi Mapinduzi haya
kwa kuwa ndio chanzo cha Muungano wetu, Amani yetu, Umoja wetu, Utulivu
wetu na Mshikamano wetu. Hivyo tunakila sababu ya kushukuru uwepo wa
Mapinduzi ya mwaka 1964 yameweza kutuunganisha tukawa na Umoja.
Awamu ya kwanza ya Uongozi wa
Rais wa Zanzibar Marehemu Shekhe Abeid Amani Karume alifanya mambo
mengi makubwa mfano ujenzi wa nyumba bora za makazi za wananchi, kutoa
elimu bure, huduma za afya, maji na kufuta kabisa ubaguzi wa kila aina
ambao ulikuwa umeota mizizi hapa Zanzibar kabla ya Mapinduzi.
Aidha, Awamu ya pili Serikali ya
Zanzibar chini ya uongozi wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Marehemu Abood
Jumbe, iliandika Katiba ya Zanzibar, kuundwa kwa Baraza la Wawakilishi,
kutengeneza muundo wa Baraza la Wawakilishi na kuanza kazi kwa kuwa na
wakikilishi Zanzibar na Katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Awamu ya tatu mpaka ya Saba ni muendelezo wa:
Tatu, Uchumi wa Zanzibar umekua,
kama kuzalisha mazao zaidi hapa visiwani, mfano asilimia 80 ya matunda
yalikuwa yanatoka Tanzania Bara lakini sasa katika Awamu ya saba ya
Mheshimiwa Dkt Ali Mohammed Shein, uzalishaji wa matunda umeongezeka
asilimia 80 inatoka Zanzibar na 20 tu ndio yanatoka Tanzania Bara.
Ujenzi wa barabara kila mkoa,
miundombinu mbalimbali imeongezeka kama hospitali, bandari imeimarishwa
ambapo kwa sasa kuna meli nyingi zaidi za mizigo na Uvuvi ukilinganisha
na miaka ya nyuma.
Nne, suala la kubadilishana
uongozi kutoka awamu ya kwanza mpaka ya saba, tofauti na uongozi wa
kisultani ambao ulikuwa ni wakurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine
katika familia moja tu.
SWALI: Mheshimiwa Hamad Rashid
wewe ni kati ya watu wachache waliobobea katika siasa na umeitumikia
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na Bunge la Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania. Unadhani muelekeo uliopo mpaka sasa unaleta hali halisi ya
matarajio ya Mapinduzi yaliyofanyika mwaka 1964?
JIBU:
Muelekeo upo na madhumuni makubwa
ya mapinduzi ni kutaka kujitawala wenyewe, unapojitawala utaepuka
kudharauliwa, kunyanyaswa na kuondoa ubaguzi uliokuwa umekidhiri katika
utawala wa Wakoloni enzi hizo.
Pili makazi na maisha ya
Wanzanzibar waliowenngi yalikuwa duni na umaskini ulikuwepo wa hali ya
juu kwa jamii za kiafrika na; Tatu Uchumi wa Zanzibar ulikuwa mikononi
mwa wakoloni hakuna Mzanzibar aliyeruhusiwa kumiliki sehemu ya uchumi wa
nchi. Kutokana na kadhia hiyo utamaduni wetu ulidharauliwa utu wetu
ulipuuzwa na ushiriki wetu wa uchumi ulikuwa haupo.
Hivyo madhumuni makubwa ya
mapinduzi ni kuleta umoja, usawa, utulivu na mshikamano miongioni mwa
wanzanzibar hilo limefanikiwa kwa asilimia kubwa ukilinganisha na hali
ya mwaka 1964.
SWALI: NIni maoni yako kuhusu Serikali ya Mapinduzi ya Zanznibar kuelekea kwenye uchumi wa viwanda vidogo, vya kati na vikubwa?
JIBU:
Tukubali kuwa uchumi ndio msingi
wa maendeleo wa Taifa lolote. Sera zinazoandaliwa ni lazima zilenge
katika kuleta maendeleo ya nchi kiuchumi. Rais anaposema anataka Taifa
liondokane na umasikinini ni kweli tutaondokana nao, kama tutakuwa na
viwanda vichache vyenye manufaa kwa nchi kwa kuwa eneo la kisiwa ni
dogo. Hivyo, tutaongeza ajira Wakulima watapata soko la uhakika la mazao
yao na bidhaa zitakazozalishwa zitauzwa ndani na nje ya nchi kwa kuwa
zimeongezewa dhamani.
Ni vema Wazanzibar tukadhamini vitu vinavyozalishwa nchini mwetu na kupenda kushiriki katika kufanya kazi.
SWALI: Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inalipi la kujivunia katika miaka 53 ya Mapinduzi Tukufu ya Zanzibar?
JIBU:
Yapo mengi ya kujivunia, leo hii
hakuna wakutupuuza, kutudharau na kutunyanyasa, tunatembea kifua mbele
kwa marefu na mapana katika kila jambo liwe lakijamii, kiuchumi, elimu,
miundombinu, afya, michezo au utamaduni kila Mzanzibar ana haki ya
kushiriki katika maendleo ya Zanzibar. Hapa la msingi kila Mzanzibar
ajiulize atafanya lipi kwa Zanzibar ili kuleta maendeleo, kila raia
anatambua maendeleo yetu yataletwa na sisi wenyewe. Maana ukitaka au
kudai haki lazima ujue wajibu wako kwa nchi katika kuleta maendeleo.
Mambo ya msingi ya kujivunia
yanabaki kuwa ni Umoja wetu, Mshikamano wetu Amani yetu, Utulivu wetu
na hali ya kuvumiliana katika siasa hasa uvumilivu wa kufanya siasa za
vyana vingi.
SWALI: Suala la Nidhamu kwa
Watumishi wa Umma, Taasisi, Mashirika na Idara za Serikali linatiliwa
mkazo sana na Rais wa Zazibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein hili
unalizungumziaje?
JIBU:
Ni kweli Mheshimiwa Rais Dkt. Ali
Mohammed Shein, anasisistiza nidhamu na kufanya kazi kwa bidii na
kujituma. Amesema kabisa hataki tufanye kazi kwa mazoea, anasisistiza
kabisa kwenda kwa wananchi na kufanya kazi nao ili kujua wanachofanya,
changamoto zao ili viongozi waweze kuzitatua pamoja na wananchi.
Anatuhimiza tutoke tuende kwa wananchi na kuona ni jinsi gani tunaweza
kufanya nao kazi kwa pamoja ili kuleta maendeleo bila kubagua rangi,
kabila, dini, Jinsia na uwezo.
ADC tunasema asilimia 70 kazi na
asilimia 30 tutakaa maofisini. Kwa sasa watumishi wote waone umuhimu wa
kufanya kazi badala ya kupiga maneno maneno tu, tabia hii haitatusaidia
Wazanzibar.
SWALI: Nini nafasi ya Vyama vya Upinzani katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar?
JIBU:
Vyama vya Upinzabni vina nafasi
kubwa katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na nje ya serikali katika
masuala muhimi kwa wananchi ya kuleta maendeleo. Nitakupa mfano binafsi
na chama chetu cha “Alliance for Democratic Change” – ADC tulishirikiana na wananchi kutafuta wafadhili kama chama cha siasa na kujenga uwanja wa mpira Pemba sikuwa Waziri wala Diwani.
Pia ni fadhaa kumsingizia
Mheshimiwa Rais eti hatoi nafasi kwa vyama vingine vya siasa. Mimi
mwenyewe nipo ndani ya serikali tunakaa kwenye vikao mpaka saa 6 usiku
kila mhusika natoa mawazo yake katika kuwaletea maendeleo Wazanzibar.
Kama hoja unayotoa ni ya msingi lazima itakubalika, inapofikia suala la
maendeleo Mheshimiwa Rais Shein haangalii chama anaangalia masilahi ya
Zanzibar kwanza.
Kila Mzanzibar ana wajibu wa
kujiuliza ameifanyia nini Zanzibar ili kuleta maendeleo na sio kusifiwa
kwa malumbano ambayo hayana masilahi kwa maendeleo.
SWALI: Ni kweli Serikali ya SMZ
Ikiongozwa na Chama cha Mapinduzi – CCM inakandamiza demokrasia na
kubagua Vyama Vingine vya siasa?
SWALI: Ni kweli Serikali ya SMZ Ikiongozwa na Chama Tawala cha CCM inakandamiza demokrasia na kubagua Vyama Vingine?
JIBU:
Hili la kubaguliwa na
kukandamizwa demokrasia halina ukweli hata kidogo, Katika Awamu ya
kwanza ya uongozi niliwahi kupendekeza jambo ambalo idadi kuwa ya
washiriki walilikataa, lakini kutokana na uzito wa hoja, Serikali
ililipima na kulichukua hii ndio demokrasia, kama suala lina masilahi
kwa nchi ni vema likafanyika kwa masilahi ya nchi.
Mimi ni mwanachama wa “Alliance for Democratic Change” katika
utendaji wa kazi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mheshimiwa Dkt Shein sijawahi kubaguliwa au kutengwa kwa
sababu natoka chama kingine cha sIasa.
Mhe. Rais anatushirikisha katika
kila jambo na katika vikao tunaongea na kutoa mawazo na mapendekezo yetu
ambayo yanachukuliwa na kufanyiwa kazi kama ambavyo yangeweza kutolewa
na muwakilishi wa chama chake cha CCM.
SWALI: Una wito gani kwa wanzanzibar na Watanzania kwa ujumla?
JIBU:
Mosi, Umoja wetu, Usawa kwa kila Raia na Mshikamano wetu ni masuala ya msingi sana katika nchi yetu.
Pili, tunataka nchi hii ibaki
salama, mnapokuwa na amani katika nchi yenye rasilimali za kutosha
mtaweza kujipanga vema na kuzitumia rasilimali hizo kwa faida ya wote,
hivyo ni lazima tuhakikishe kuna Amani na pale wachache wanapohatarisha
amani hiyo kwa pamoja tushirikiane kusuluhisha ili kurejesha hali ya
utulivu na amani.
Serikali ipo imara katika kuleta
Maendeleo lakini wewe Mzanzibar ni lazima utimize wajibu wako. Mfanya
biashara alipe kodi na afanye biashara ya halali. Mkulima afanye kazi
kwa bidii na Serikali ihakikishe inampatia pembejeo kwa wakati na zenye
ubora.
Tatu, sisi wanasiasa njia za
kurekebisha makosa zipo tukubali kukaa chini na kuzungumza, lawama
hazina nafasi, Chama cha siasa ni lazima kuwa na mipango ya maendeleo na
mipango hiyo ifanyike hata kama hauko katika uongozi.
Nne, tunao viongozi wetu wa dini
kama Mashekhe, Mapadri Wachungaji tuwe karibu nao tuongee nao waweze
kutuelekeza pale tunapokosea na kwenda katika mwenendo sahihi. Mwisho
nawapongeza kwa dhati kabisa Wazanzibar kutimiza miaka 53 ya Mapinduzi.
No comments :
Post a Comment