Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wajumbe wa bodi mpya
ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), mara baada ya kuizindua
rasmi, jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi mpya ya Mamlaka
ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jones Kilimbe (katikati),
akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa
Makame Mbarawa (kushoto), wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo, jjini Dar es
Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Faustine Kamuzora
akizungumza na bodi, menejimenti na wafanyakazi wa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA), (hawapo pichani), wakati wa uzinduzi wa
bodi hiyo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani),
alipoongea na wafanyakazi wa Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA), wakifurahia jambo mara baada ya uzinduzi wa
bodi mpya ya Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
No comments :
Post a Comment