Thursday, December 29, 2016

NGULI WA HOLLYWOOD DEBBIE AMFUATA BINTIE CARRIE ALIYEFARIKI DUNIA

DELE ALLI ATIKISA NYAVU MARA MBILI WAKATI TOTTENHAM IKIUWA

REA AWAMU YA TATU KUJA NA NGUZO ZA ZEGE

mule
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt.Medard Kalemani, akizungumza jambo wakati wa Mkutano wake na wananchi wa Kijiji cha Kishuro,Kata ya Ngenge Wilaya ya Muleba, Mkoa wa Kagera. Dkt.Kalemani amefanya ziara Wilayani humo ya kukagua Mradi utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Pili na kueleza mipango ya Serikali kutekeleza Awamu ya Tatu ya mradi husika.
mule-1
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt.Medard Kalemani, akizungumza jambo wakati wa Mkutano wake na wananchi wa Kata ya Ngwanseri,wilaya ya Muleba, wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Pili.
mule-2
Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Ruyango,akizungumza jambo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt.Medard Kalema ni kukagua utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Pili.Wengine katika picha ni baadhi ya Viongozi wa Halmashauri hiyo,Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, REA,TANESCO, na Wakandarasi wanaotekeleza mradi husika.
mule-3
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt.Medard Kalemani, (Wa tatu kushoto) katika picha ya pamoja na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini, Prof.Anna Tibaijuka (wa pili kushoto),Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Ruyango,(wan ne kushoto)pmoja na Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, REA,TANESCO, na Wakandarasi wanaotekeleza mradi wa REA Awamu ya Pili.
mule-4
Mmoja wa Wananchi katika akiuliza jambo wakati wa mkutano wa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt.Medard Kalemani(hayupo pichani) katika Kata ya Ngwanseri.
mule-5
Wananchi wa Kata za Ngwanseri na Ngenge wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt.Medard Kalemani na ujumbe wake wakati wa ziara yake a kukagua utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Pili wilayani Muleba.
mule-7
Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Prof.Anna Tibaijuka (kulia) akiteta jambo na Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt.Medard Kalemani ( katikati) mara baada ya kumaliza mkutano wake na wananchi wa Kijiji cha Kishuro. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Ruyango.

GAZETI LA NIPASHE YAFANIKISHA WANAFUNZI KUONDOKANA NA PAA LA NYASI.

                                                                                                   Na Shushu Joel,BUSEGA.

WANANCHI wa kijiji cha Yitwimila A kilichopo kata ya Kiloleli wilaya ya Busega mkoani Simiyu wamelipongeza gazeti la NIPASHE kwa kuandika ukweli wa mambo yanayojitokeza katika sehemu mbali mbali ikiwemo habari yao ya kuezekwa kwa nyasi shule ya msingi Masanza kuonekana na kuchukua sura ya pekee katika jamii na nchi kwa ujumla.

Pongezi hizo zimekuja siku chache tu mara baada ya gazeti hilo lilipotangaza juu ya shule ya Masanza kuezekwa kwa nyasi na wazazi wa eneo hilo ili kuweza kuwasaidia watoto waliokuwa wakisoma katika hali ngumu ya kupigwa na jua kwa muda mrefu.

Samwel Abel ni mkazi wa kijiji hicho anaeleza kuwa ni juhudi za wananchi zilizofanikisha kumtafuta mwandishi wa habari wa NIPASHE ili aweze kurusha habari ya shule hiyo na jinsi gani wanafunzi wanavyopata shida wakati wa masomo wanapokuwa juani.

“Si wanafunzi tu bali hata walimu ambao ndio wasimamizi wakuu wa maendeleo ya watoto pindi wanapokuwa shuleni lakini nao walikuwa wakikumbana adha kubwa kama hiyo ya kufundishia juani,hii ni aibu kubwa sana kwani jengo hilo lilimalizwa na wananchi kwa muda wa miaka zaidi ya 3 na kukaa tu huku wanafunzi wakisomea juani alisema”

Kwa upande wake Christina Joseph ni mkazi wa kitongoji cha nyawa anaeleza kuwa wanampongeza mbunge wa jimbo la Busega Dr Raphael Chegeni kwa kuweza kujitolea kwa kuezeka shule hiyo.

Bi Chrisitina aliongeza kuwa wanajipongeza wao kama wananchi kwa kufanya kitu ambacho kimewaletea maendeleo ya haraka katika shule yao,kwani bila kuiezeka shule hiyo kwa majani basi mpaka leo kusingekuwa na dalili za kuezekwa kwa shule hiyo.

Aidha tunalipongeza gazeti la NIPASHE kwa umakini wake wa kuandika habari za watu wa chini kama ilivyo sera ya Rais Magufuli ya kuwahudumia watanzania wa hali ya chini na hii imejionyesha kwa gazeti hilo kwani limetenda haki kwa jamii ya chini.

Na kwa upande wake mbunge huyo wa Busega Dr Raphael Chegeni alipopigiwa simu alisema kuwa suala la wananchi kuezeka nyasi shule ni kitendo cha ujasiri sana kwao ingawa ni aibu kwa serikali lakini tumelimaliza na sasa mabati yameshaezekwa shuleni hapo ili kuweza kuwasaidia wanafunzi hao.

Aliongeza kuwa pesa za mfuko wa jimbo atazipeleka zote katika kuhakikisha majengo yote yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi anaziezeka ili wanafunzi wapate mahali pa kusomea.

“Nimemuomba mkurugenzi aweze kunipatia idadi ya majengo yote ambayo bado ayajaezekwa ili pesa za jimbo zimalizie kero hiyo

No comments :

Post a Comment