Mkuu
wa Masoko na Hazina wa BancABC, Barton Mwasamengo, (kushoto), na Mkuu wa
Kitengo cha Wateja Binafsi na wafanyabiashara wadogo wadogo, Joyce Malai,
wakionyesha kadi inayoonyesha uzinduzi wa ofa ya riba asilimia 16% kwa wateja
wanaofungua akaunti ya amana ya muda maalum msimu huu wa sikukuu. Uzinduzi huo
ulifanyika Desemba 5, 2016 makao makuu ya BancABC jijini Dar es Salaam.
NA MWANDISHI WETU.
BancABC ya
jijini Dar es Salaam, leo Desemba 5, 2016, imezindua ofa ya riba hadi asilimia
16% kwa mteja anayefungua akaunti ya amana ya muda maalum, (Fixed Account),
msimu huu wa sikuku.
Akizungumza
wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika makao makuu ya benki hiyo jingo la
Uhuru Hights jijini Dar es Salaam, Mkuu wa kitengo cha wateja binafsi na
wafanyabiashara wadogo wa benki hiyo, Bi. Joyce Malai, alisema, riba hiyo
itatolewa kwa mwaka na mteja atalipwa riba papo kwa papo ikiwa ni zawadi yake
ya msimu wa sikukuu.
“Hii ni ofa bora
kuliko zote kwenye soko kwa sasa na tunataka kuwashawishi wateja wetu na hata
wale wasiokuwa na akaunti kwetu kutumia fursa ya ofa hii ya msimu wa sikukuu.”
Alifafanua.
Bi. Malai
alisema, “benki inathamini jinsi wateja wetu wanavyotuunga mkono na hiyo ndiyo
sababu sisi kama benki tumeamua kuwazawadia ofa hii kabambe katika msimu huu wa
sikukuu.”
Alisema mteja
anaweza kufika tawi lolote la benki hiyo lililoko Uhuru, Quality Centre,
Kariakoo jijini Dar es Salaam na mkoani Arusha ili kufungua akaunti hiyo ambapo
riba hiyo italipwa papo hapo, lengo ni kumpa mteja uhuru wa kutumia kwa ajili
ya kufanya manunuzi binafsi kama apendavyo.
“Tunajua wakati
huu, watu wengi wanajiandaa kulipa ada, kununua mahitaji mbaimbali kwa ajili ya
sikuu, na wengine kwenda kupumzika kwenye maeneo mbaimbali, hivyo wakati
unasubiri kufanya mambo hayo ni vema fedha zako ukazileta hapa benki na
kuzitunza na muda wa kufanya hayo matumizi ukifika, basi unakuja kuzichukua na
faida.” Aliongeza Mkuu wa Masoko na Hazina wa benki hiyo, Bw.Barton Mwasamengo.
Mkuu
wa Masoko na Hazina wa BancABC, Barton Mwasamengo, (kushoto), na Mkuu wa
Kitengo cha Wateja Binafsi na wafanyabiashara wadogowadogo, Joyce Malai, wakati
wa mkutano na waandishi wa habari, kuzindua ofa ya riba asilimia 16% kwa wateja
wanaofungua akaunti ya amana ya muda maalum msimu huu wa sikukuu. Uzinduzi huo
ulifanyika Desemba 5, 2016 makao makuu ya BancABC jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa
Kitengo cha Wateja Binafsi na wafanyabiashara wadogowadogo, Joyce Malai
Mkuu
wa Masoko na Hazina wa BancABC, Barton Mwasamengo,
Waandishi wa habari
Bi.Upendo Nkini(kulia), akiwakaribisha maafisa hao tayari kuzungumza na waandishi wa habari
No comments :
Post a Comment