Monday, November 28, 2016

UJUMBE KUTOKA CHAMA CHA CPC CHA CHINA WATUA NCHINI KUJIFUNZA KAZI ZA CCM


 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),  Mkoa wa Dar es Salaam Ramadhani Madabida (kushoto), akimkabidhi Ilani ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015,  Mkurugenzi wa Idara ya Mahusiano ya Kimataifa, Maendeleo na Mafunzo wa Chuo cha Viongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China, Jia Bo,  Dar es Salaam leo asubuhi, ambaye yupo nchini na wajumbe wenzake sita kwa zaiara ya siku saba ya kichama kukitembelea Chama Cha Mapinduzi (CCM).
 Mkutano ukiendelea.
 Wajumbe hao wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida.
 Makada wa CCM wakijumuika na wajumbe wenzao kutoka china.
 Mratibu wa Masuala ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Pindi Chana (kushoto), akizungumza na wajumbe hao.
 Madabida akiwakaribisha wajumbe hao.
Karibuni wajumbe kutoka China.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kabla ya makabidhiano ya picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli iliyochorwa na kikundi cha Angavu Youth Group leo Novemba 28, 2016 jijini Dar es Salaam. Picha hiyo imekabidhiwa kwa Waziri huyo  kwa niaba ya Mhe. Rais. kushoto ni Mwenyekiti wa Angavu Youth Group Bw. Athumani Salum na kulia ni Katibu wake Bi. Oliver Charles.

(PICHA NA ANITHA JONAS – MAELEZO)



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye (kulia) akisikiliza kwa makini hotuba iliyokuwa ikisomwa na Katibu wa Angavu Youth Group Bi.Oliver Charles (katikati) wakati wa makabidhiano ya picha ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye (kulia) akipokea picha ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutoka kwa Mwenyekiti wa Angavu Youth Group Athumani Salum (kulia) leo jijjini Dar es Salaam. Picha hiyo imechorwa kwa ustadi na kikundi cha Angavu Youth Group.



Wanafunzi wa shule ya Academic International school, Harshvardhan Kabla (kushoto) ambaye ameshika nafasi ya kwanza duniani katika somo la Kompyuta kwa wanafunzi wa “A Level” kwa mitihani ya Cambridge na Abishek Sankaranarayanan(kulia) ambaye ameshinda nafasi ya kwanza kwa somo la hisabati kwa mitihani ya Cambridge kwa wanafunzi wa kidato cha nne wakiwa katika picha ya pamoja katika sherehe maalum ya kuwapongeza.Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Inder Jit Sagar akimkabidhi cheti na kombe mwanafunzi wa Shule ya Academic International, Harshvardhan Kabla (kulia) kwa kushinda nafasi ya kwanza duniani katika somo la Kompyuta kwa wanafunzi wa “A Level” kwa shule zinazofuata mtahala wa Cambridge.Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Inder Jit Sagar akimkabidhi cheti na kombe mwanafunzi wa Shule ya Academic International, Abishek Sankaranarayanan(kulia) kwa kushinda nafasi ya kwanza duniani katika somo la Hisabati kwa wanafunzi wa “O Level” kwa shule zinazofuata mtahala wa Cambridge.Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Inder Jit Sagar (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na walimu wawili wa shule ya Academic International, Walter Mlowe ambaye anafundisha somo la Hisabati na Thadei Mwinuka ambaye anafundisha somo la kompyuta. Walimu hao walitunukiwa vyeti kwa kazi nzuri ya ufundishaji.Mkurugenzi wa shule ya Academic International, Yusuf Kalindaga akizungumza katika hafla maalum ya kuwapongeza wanafunzi , walimu na wafanyakazi wa shule hiyo kwa kufanya vyema katika mitihani ya Cambridge.Mkuu wa shule ya ya Academic International, Shyama Santhosh ( wa kwanza  kushoto) akisema jambo katika sherehe hiyo ya kuwapongeza wanafunzi hao  na walimu.


Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Academic International wakishiriki katika hafla hiyo.
Baadhi ya wazazi na wanafunzi wa shule ya Academic International wakiwa katika hafla hiyo 


Wanafunzi wawili wa shule ya Academic International ya Tanzania wameweka historia katika mitihani ya mtahala wa Cambridge baada ya kushinda nafasi ya kwanza duniani katika masomo ya hisabati na kompyuta.

No comments :

Post a Comment