
Mwanamuziki nyota nchini Vanes Mdee, akiweka dole gumba
tayari kuchapa kwenye fomu ya kujiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari, (PSS),
wa Mfuko wa Pensheni wa
PSPF wakati wa kongamano lililowakusanya wanafunzi wa
kike wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Shule ya Biashara na kufanyika chuoni
hapo mwishoni mwa wiki. Mamia ya wanachuo walijiunga na mpango huo baada ya
kupata elimu ya faida za kujiunga na mpango huo. Wanaoshuhudia, kutoka kulia ni
Balozi wa PSPF, Flaviana Matata ambaye ni mwanamitindo wa kimataifa anayefanya
kazi zake Ulaya na Marekani, Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, PSS wa
Mfuko huo, Mwanjaa Sembe, na Afisa Masoko na Uhusiano wa PSPF, Rahma Ngassa.
wa Mfuko wa Pensheni wa
PSPF wakati wa kongamano lililowakusanya wanafunzi wa
kike wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Shule ya Biashara na kufanyika chuoni
hapo mwishoni mwa wiki. Mamia ya wanachuo walijiunga na mpango huo baada ya
kupata elimu ya faida za kujiunga na mpango huo. Wanaoshuhudia, kutoka kulia ni
Balozi wa PSPF, Flaviana Matata ambaye ni mwanamitindo wa kimataifa anayefanya
kazi zake Ulaya na Marekani, Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, PSS wa
Mfuko huo, Mwanjaa Sembe, na Afisa Masoko na Uhusiano wa PSPF, Rahma Ngassa.

Naibu
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee Mhe.Hamis
Adrea Kigwangalla akijibu maswali kutoka kwa wabunge mbalimbali katika
kipindi cha maswali na majibu katika kikao cha Tano cha Bunge la 11
linaloendelea Mjini Dodoma. Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO
…………………………………………………………………………………………….
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Serikali
imejipanga kutoa huduma bora za afya kwa wananchi kwa kuwawezesha kila
mwananchi kupata Bima ya Afya itakayosaidia kupata huduma bora za afya
katika zahanati na hospitali mbalimbali.
Akijibu
swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe.Faida Mohammed Bakar(CCM)
lililouliza kuwa bado kuna ukiukwaji wa huduma za afya, haki za afya na
haki za uzazi katika baadhi ya vituo vya kutolea huduma za afya wakati
wa maswali na majibu,Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,
Jinsia,Watoto na Wazee Mhe.Hamis Adrea Kigwangalla amesema katika
kuhakikisha kuwa haki hizi zinapatikana,Serikali kwa kupitia mifumo
yake, ikiwa ni pamoja na mabaraza ya weledi, kurugenzi ya uhakiki na
ubora wa huduma za afya na idara mbalimbali zilizo chini ya Waziri
zinatoa mafunzo kwa watoa huduma za afya kuhusiana na haki za wateja.
Mhe.
Hamis Adrea Kigwangalla amesema katika kutekeleza hili vituo vyote vya
kutolea huduma za afya vina masanduku ya maoni na ofisi za malalamiko
ambazo ni sehemu muhimu ambapo wateja wanaweza kupeleka malalamiko yao
ili hatua zaidi zichukuliwe kukomesha na kutokomeza ukiukwaji wowote wa
haki za wateja.
“
Tutawachukulia hatua wale wote watakaobainika kukiuka haki za wateja kwa
kupitia baraza la wauguzi na wakunga ili kuhakikisha wananchi wanapata
huduma bora zinazostahili ili kuokoa maisha ya wananchi hasa maisha ya
mama na mtoto” Alisema Mhe.Kigwangalla.
Aidha
Mhe. Hamis Adrea Kigwangalla amesema Wizara yake imeandaa rasimu ya
Sheria ya Bima ya Afya ambayo itamuwezesha kila mwananchi kupata bima ya
afya itakayomsaidia kupata huduma bora za afya katika maeneo yao.
Serikali
kupitia Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee
inatoa mafunzo kwa Wakunga wa Jadi ambao wamekuwa wakitumika sana sehemu
ambazo huduma za afya zipo mbali ili kuwezesha wananchi hao kupata
huduma bora za afya kutoka kwa wakunga hao hasa katika afya ya mama na
mtoto.
MKURUGENZI MKUU WA TUME YA USHINDANI AKABIDHI VIFAA VYA MUZIKI KWA JESHI LA MAGEREZA
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo akitoa maelezo mafupi
kwenye hafla ya makabidhiano ya vifaa vya muziki kwa Uongozi wa Jeshi la
Magereza. Hafla hiyo ilifanyikia Bwalo Kuu la Maafisa Magereza, Ukonga
Jijini Dar es salaam, Januari 29, 2016.
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo akimkabidhi Kamishna
Jenerali wa Magereza John Casmir Minja gitaa la muziki ikiwa ni moja
wapo ya vifaa vya muziki vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza.
Kamishna
Jenerali wa Magereza akijaribisha kupiga gitaa la muziki baada ya
kukabidhiwa vifaa vya muziki katika hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo
kutoka kwa Mkurugenzi wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo(wa
kwanza kulia).
Kamishna
Jenerali wa Magereza John Casmir Minja akitoa neno la shukrani kwa
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo kwenye hafla
ya makabidhiano ya vifaa vya muziki ambavyo vitatumika kukuza vipaji vya
Wanamuziki wa Jeshi la Magereza.
Maafisa
Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakisikiliza kwa makini hotuba ya
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo(hayupo
pichani).
Baadhi
ya vifaa vya muziki venye vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza kama
vinavyoonekana katika picha. Vifaa hivyo vitatumika kukuza vipaji vya
Wanamuziki wa Jeshi hilo(Picha na Kitengo cha Habari, Makao Makuu ya
Jeshi la Magereza).
Kundi la Mziki la Navy Kenzo latoa Wimbo na Video Mpya-Kamati
THE INDUSTRY MUSIC LABEL
Baada ya kutamba Mwaka Jana Africa
nzima na wimbo unaoitwa ‘Game’, Kundi la Navy Kenzo limeanza mwaka
vizuri baada ya kutoa wimbo mpya pamoja na video yake unaitwa “Kamatia” ,
Wimbo huo umeshaanza kuwa gumzo sehemu mbali mbali na kuonyeshwa kwenye
TV za kimataifa siku mbili tu baada ya kutoka, Uzinduzi wa Wimbo Huo
ulifanyika Kiaina yake kwa Staili ya ‘Flash Mob’ Kwenye Club ya Rhapsody
kwa kuwasuprise waliokuwa ndani ya Club hiyo.
Kundi la Navy Kenzo linaloundwa na Aika
na Nahreel mpaka sasa wameshatoa nyimbo kadhaa zilizotamba sana kama
Moyoni, Bokodo, Visa na nyingine nyingi.
Navy Kenzo wameamua kutoa Wimbo pamoja
na Video yake moja kwa moja kutokana na ushindani uliopo kwa sasa kwenye
Music wa Bongo Flava, Video imefanyika nchini South Africa na
Muongozaji wa Video wa kimataifa anayeitwa Justin Campos.
Kamatia ni wimbo ambao unaongelea
kuhusu wapenzi wawili waliomua kushikana hasa kwenye mapenzi , Midundo
ya nyimbo hiyo ina mahadhi ya Dancehall na vionjo vya kipekee kutoka kwa
Producer bora Tanzania Nahreel.
Nahreel Ambaye ni mmoja wa Kundi la
Navy Kenzo ni Producer wa Muziki bora Mwenye tuzo ya Kilimanjaro Music,
Ametengeneza nyimbo mbali mbali zilitamba Kama Nana ya Diamond Ft
Flavor, Joh Makini Ft Aka Don’t Bother and Vanessa Mdee’s Nobody but
me, Never ever na Hawajui, pia ndio mpishi wa Nyimbo ya Navykenzo ‘Game’
UNIDO NA CHUO KIKUU CHA MZUMBE WAENDESHA SEMINA KWA WAMILIKI WA VIWANDA VIDOGO VIDOGO VYA UZALISHAJI (SMEs) NA WAHITIMU WA VYUO TANZANIA
Mkuu wa Chuo kikuu cha Mzumbe Kampasi ya Dar es salaam Profesa Ganka Nyamsongoro akifungua Semina kwa ajili ya wamiliki wa viwanda vidogo vidogo vya uzalishaji, wafanyabiashara na wajasiliamali semina iliyolenga programu ya UNIDO wakishirikiana na Chuo kikuu cha Mzumbe kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi kupata mafunzo ya ujuzi wa kazi.
Baadhi
ya wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda vidogo vidogo vya uzalishaji na
wajasiliamali wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa
Peacock Hotel Dar
Mshauri wa UNIDO Bw. Mike Laizer akichangia jambo katika semina hiyo
Bw. Deosdadit Bernad Msimamizi wa Programu kutoka UNIDO akielezea kwa undani juu ya Programu hiyo
Baadhi ya wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda vidogo vidogo vya uzalishaji na wajasiliamali wakiendelea kufuatilia Semina
Profesa
Prosper Ngowi Msimamizi Mkuu wa Programu hiyo akieleza kwa kina nia na
malengo ya wao kufanya hivyo kwa kushirikiana na ‘SMEs’ ili kuwapa ujuzi
wa kazi wahitimu na wahitimu kutoa ujuzi wao waliokuwa nao ili kuweza
kukuwa zaidi
Wafanyabiashara,
wamiliki wa viwanda vidogo vidogo vya uzalishaji na wajasiliamali
wakiwa wanaendelea kufuatilia semina hiyo kwa makini
Baadhi
ya wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda vidogo vidogo vya uzalishaji na
wajasiliamali wakiwa wanauliza maswali na kuchangia mawazo katika
Semina hiyo
Mmoja
wa ‘Mentor’ katika programu hiyo Bw. Kaaya akiwa anatoa maelezo kwa
wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda vidogo vidogo vya uzalishaji na
wajasiliamali jinsi ambavyo watashirikiana katika kuwafundisha kazi
wahitimu hao pamoja na kushirikiana katika mambo mbalimbali
Picha
ya Pamoja kati ya wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda vidogo vidogo
vya uzalishaji na wajasiliamali, Chuo kikuu cha Mzumbe na wawakilishi
kutoka UNIDO
Mkuu
wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Profesa Ganka akifungua semina fupi na
wahitimu kutoka vyuo mbalimbali ambao ni watanzania katika programu
iliyo andaliwa na UNIDO ikiratibiwa na Chuo Kikuu cha Mzumbe juu ya
Mafunzo ya kazi ‘Internship’ ambayo yataanza hivi karibuni ambapo
wahitimu hao watatakiwa kufanya kazi kwa miezi minne katika viwanda
vidogo vidogo vya uzalishaji, wafanyabiashara na wajasiliamali
Msimamizi Mkuu wa Programu kutoka chuo kikuu cha Mzumbe Profesa Prosper Ngowi akiwaelezea wahitimu juu ya Programu hiyo
Baadhi
ya wahitimu wakiwa wanauliza maswali na kutaka ufafanuzi katika baadhi
ya maeneo ambayo walikuwa hawajayaelewa katika semina hiyo iliyofanyika
katika Chuo kikuu cha Mzumbe
Dkt.
Darleene Mutalemwa akitoa neno la Shukurani kwa wote wahitimu wote
waliofika katika semina hiyo kwa niaba ya UNIDO na Chuo kikuu cha Mzumbe
Wahitimu
wakiwa katika semina hiyo ya kupata maelekezo juu ya Programu ambayo
inalenga kuwapa Mafunzo ya kazi wahitimu iliyo andaliwa na UNIDO
ikiratibiwa na Chuo kikuu cha Mzumbe
Mfuko wa Dharura wa UN watoa Dola Milioni 11 kusaidia wakimbizi wa Burundi na jamii ya Tanzania
Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo ametoa dola za Marekani
milioni 100 (US$ 100m, sawa na shilingi za Tanzania bilioni 220) kutoka
katika Mfuko Mkuu wa Kushughulikia Dharura wa Umoja wa Mataifa (CERF)
kwa shughuli za misaada katika maeneo tisa yenye dharura duniani na
yasiyo na fedha za kutosha. Tanzania—ambayo kihistoria imepokea
mamilioni ya wakimbizi kutoka nchi jirani kwa miaka mingi—imetengewa
dola za Marekani milioni 11 (Sawa na shilingi za Tanzania bilioni 24)
kutoka katika kiasi hicho kwa lengo la kushughulikia mahitaji ya
wakimbizi kutoka Burundi.
Waziri
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akitoa msaada katika kambi ya
wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo mkoani Kigoma wakati alipofanya ziara
mkoani humo
Zaidi
ya raia 126,000 wa Burundi wamekimbilia nchini Tanzania tangu mwezi
Aprili, 2015, kufuatia machafuko ya kisiasa nchini humo. Huku tayari
wakimbizi 64,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) wakiwa
tayari nchini. Tanzania hivi sasa ina zaidi ya wakimbizi 193,000.
Kutokana na ukweli kwamba takribani wakimbizi 1,500 wanawasili nchini
kila wiki, inabashiriwa kwamba huenda idadi jumla ya wakimbizi ikafikia
230,000 hadi mwisho wa mwaka 2016. Hali hii inasababisha changamoto
nyingi hasa katika kutoa msaada na kinga ya kutosha kwa wakimbizi.
Mchango
huu mkubwa kutoka CERF utakuwa muhimu sana katika kutoa misaada ya
kiutu kwa wakimbizi wa Burundi wanaoishi katika kambi za Nyarugusu,
Nduta na Mtendeli katika mkoa wa Kigoma, Kaskazini Magharibi mwa
Tanzania, na vilevile kwa jamii za wenyeji ambazo zinahitaji kwa haraka
huduma bora za maji safi, usafi wa kutosha, matunzo ya afya, chakula na
makazi. Sehemu ya fedha hizo pia itatumika kushughulikia mlipuko uliopo
wa ugonjwa wa kipindupindu ambao umeathiri mikoa 19 nchini. Fedha za
CERF kwa hiyo zitasaidia kuhakikisha kwamba maeneo muhimu zaidi katika
dharura yanafanyiwa kazi na kwamba wakimbizi wanapewa kinga na huduma za
msingi.
Baadhi ya wakimbizi waliopo katika kambi ya Nyarugusu iliyopo mkoani Kigoma
“Shirika la Kushughulikia Wakimbizi (UNHCR) linakaribisha mchango huu
wenye ukarimu mkubwa kutoka CERF ambao unakuja katika kipindi mwafaka
kabisa. Utoaji msaada kwa wakimbizi ulikuwa ukikabiliwa na upungufu
mkubwa wa fedha katika mwaka 2015, hali iliyoathiri sana uwezo wetu wa
juhudi za pamoja katika mwaka 2015. Tuna imani kwamba hii ni ishara ya
kwanza kwa upatikanaji wa fedha nyingi zaidi kwa utoaji msaada katika
mwaka 2016. Kwa hakika, mchango huu utasaidia kuziba upungufu mkubwa
uliojitokeza katika wito wetu wa sasa na hivyo kushughulikia mahitaji
makubwa zaidi ya wakimbizi na jamii za wenyeji,” alisema Mwakilishi wa
UNHCR nchini Tanzania, Bi. Joyce Mends-Cole.
Kadiri
mahitaji ya kiutu yanavyoongezeka, mchango kutoka katika Mfuko Mkuu wa
Kushughulikia Dharura wa Umoja wa Mataifa (CERF) umetoa matumaini ya
kuendelea kushughulikia dharura ya wakimbizi kutoka Burundi. Tangu mwaka
2006, Nchi 125 Wanachama wa Umoja wa Mataifa na waangalizi, wahisani
kutoka sekta binafsi na serikali katika kanda zinazohusika wameendelea
kuusaidia Mfuko huo hadi sasa. CERF hadi sasa imetoa jumla ya dola za
Marekani bilioni 4.2 (US$ 4.2bn, sawa na shilingi za Tanzania trilioni
9) kwa miradi ya kiutu katika nchi 94. CERF hupokea michango ya hiyari
katika mzunguko wa mwaka ili kutoa msaada wa kifedha kwa hatua za kiutu
za kuokoa uhai. CERF inapata fedha zake kutoka kwa washirika wengi huku
michango mingi zaidi ikitoka: Uingereza, Swideni, Norwei, Uholanzi na
Kanada.
President Kikwete Statement
ADDIS ABABA, Ethiopia, 31 January 2016,
It is my pleasure to announce
today that I have accepted the invitation from the Confederation of
African Football and from Gavi, the Vaccine Alliance to serve as
Champion for Immunization and as Global Ambassador of Africa United.
Africa United is a pan-African innovative initiative led by Gavi, the
Confederation of African Football, the African Union, the World Bank
Group and the CDC Foundation. This initiative leverages sport to
catalyze action on critical health issues facing the continent.
Africa United was first deployed
during the Ebola crisis, enlisting influencers like Kei Kamara of Sierra
Leone to spread Ebola prevention messages and to encourage the
population to trust and seek care within the health system. Africa
United spokespeople also brought increased attention to the crisis
through an African Union-led awareness and fundraising campaign called
Africa Against Ebola.
Under my leadership, Africa
United will focus on promoting universal health access, beginning with a
focus on Universal Immunization. Immunization is crucial to saving the
lives of children across Africa – and the world. Immunization will be
key to preventing over 1.5 million deaths each year. Universal
vaccination will also play a fundamental role in developing a healthy,
resilient population and in ensuring that we develop the economies we
need to face the challenges of the next century.
Today, as I announce my
commitment to the health of the African continent, I call on every Head
of State across Africa to prioritize access to vaccination in each and
every community.
Africa United will formally
launch its universal immunization initiative next week in Kigali at the
4th Edition of the Orange African Nations Championship – Rwanda 2016. In
Kigali, my esteemed partner in this fight, CAF, will remind everyone
that “Every Shot Counts” as we look achieve our goal of Universal
Immunization.
Please join me and Africa United as we fight for a more secure future through universal access to immunization.MAUAJI YA RUBANI WA HELIKOPTA ILIYOTUNGULIWA NA MAJANGILI WA TEMBO
DKT.SHEIN AZINDUA MIAKA 39 YA KUZALIWA CCM.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali
mbali Chama cha Mapinduzi CCM mara alipowasili katika viwanja vya Ofisi
kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar, katika Mkutano wa hadhara wa Mikoa
minne ya Unguja katika Uzinduzi wa sherehe za miaka 39 ya kuzaliwa kwa
CCM.
MHE. NAPE AIPONGEZA BLOG YA VIJIMAMBO KWA KUTIMIZA MIAKA 6
Blog ya Vijimambo imekuwa mstari wa mbele kwa kutoa habari za uhakika na kwa wakati.
Pia imekuwa daraja zuri kati ya nchi yetu na Watanzania na wapenda Kiswahili duniani.
Imekuwa na mchango mkubwa katika kupeleka utamaduni wa kitanzania nje ya nchi yetu!
Nawatakia kila la heri na mafanikio mema .
MAJALIWA AHUDHURIA IBADA YA KUMUINGIZA KAZINI MKUU WA KKKT ASKOFU SHOO MJINI MOSHI
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Frederick
Sumaye na mkewe Esther katika Ibada ya kumuingiza kazini Mkuu wa
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Askofu Frederick Shoo
iliyofanyika kwenye kanisa kuu la KKKT mjini Moshi Januari 31, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Mkuu wa Kanisa la Kilutheri Tanzania
(KKKT), Askofu Frederick Shoo (kulia) na Mkuu wa Kanisa hilo mstaafu,
Askofu Alex Malasusa katika Ibada ya kumuingiza kazini Askofu Shoo
iliyofanyika kwenye kanisa kuu la KKKT mjini Moshi januari 31, 2016.
(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
TANROAD YA BOMOA NYUMBA ZILIZOJENGWA KATIKA HIFADHI YA BARABARA MAENEO YA BUZA, LUMO TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM
Maofisa
wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) na Polisi , wakisimamia
ubomoaji wa nyumba zilizojengwa kwenye hifadhi ya barabara maeneo ya
Buza kwa Lulenge Temeke jijini Dar es Salaam jana. Imeelezwa kuwa
wamiliki wa nyumba hizo walikwisha lipwa fidia na Tanroad lakiwa wakawa
wameshindwa kuondoka huku wengine wakiendeleza ujenzi.
Wakazi wa Buza Sigara wakiondoa mabaki ya mbao baada ya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad), kubomoa nyumba hizo.
Kijana akipita jirani na nyumba iliyobomolewa.
Mkazi wa Buza akiondoa mabaki ya mbao baada ya nyumba yake kubomolewa.
Moja ya nyumba iliyobomolewa.
Wananchi wakiangalia moja ya Baa iliyobomolewa.
Tingatinga likiwa kazini.
Watoto wakiangalia zoezi la ubomoaji lilivyokuwa likiendelea.
Ofisa wa Tanroad akisimamia ubomoaji huo.
Wananchi wakiangalia zoezi la ubomoaji.
Tingatinga likiisambaratisha moja ya nyumba iliyojengwa kwenye hifadhi ya barabara eneo la Buza kwa Lulenge.
Wananchi wakiangalia ubomoaji huo.
Tingatinga likifanya vitu vyake bila huruma.
Askari wa kutuliza ghasia wakiwa eneo la tukio kuimarisha ulinzi.
Umati wa watu ukiwa eneo la tukio.
(Imeandaliwa na www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
(Imeandaliwa na www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
TAARIFA KWA WANANCHI KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA ZIKA (ZIKA VIRUS)
Kumekuwepo na taarifa kupitia
vyombo mbalimbali vya habari vya Kitaifa na Kimataifa kuhusu Homa ya
Zika ambao ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi kijulikanacho kama “Zika Virus”. Ugonjwa huu uligundulika kwa mara ya kwanza nchini Uganda katika miaka ya 1947 kwenye wanyama aina ya sokwe/nyani (rhesus macaque)
ndani ya Misitu ya Zika, karibu na Ziwa Victoria. Mnamo mwaka 1952,
ugonjwa wa zika uligundulika kwa binadamu nchini Uganda na Tanzania, na
mwaka 1968 uligunduliwa nchini Nigeria. Kuanzia mwaka 1951 hadi 1981,
ugonjwa huu umeshatolewa taarifa katika nchi takribani sita (6) za
Afrika ambazo ni Afrika ya Kati, Egypt, Gabon, Sierra Leone, Tanzania na
Uganda. Vile vile, ugonjwa huu umeshatolewa taarifa katika nchi za
India, Indonesia, Malaysia, Philipine, Thailand na Vietnam na pia nchi
za Amerika na Pacific.
Kuanzia mwezi Mei 2015, ugonjwa
huu ulianza kutolewa taarifa ambapo hadi sasa umeathiri zaidi Bara la
Amerika ya Kusini. Kuna takribani nchi 22 ambapo Wagonjwa
wamethibitishwa kimaabara kuwa na ugonjwa wa Zika. Nchi hizo ni Brazil
(Majimbo 14 yameathirika), Colombia, Suriname, El Salvador, Guatemala,
Paraguay, Mexico, Venezuela, Panama, Cape Verde, Honduras, Panama,
France (French Guiana na Martinique, United States of America (Puerto
Rico), Guyana, Barbados, Ecuador, Bolivia, Haiti, Ujerumani, France
(Saint Martin and Guadeloupe na Dominican Republic.
Ugonjwa huu unaenezwa na mbu aina
ya Aedes ambaye (huwa ana tabia ya kuuma asubuhi na pia nyakati za
mchana/jioni). Aina hii ya kirusi ipo katika familia ya “Flavirus”
ambapo pia wapo virusi vya ugonjwa wa Dengue, Homa ya Manjano (Yellow Fever), Japanese ancephalitis na West Nile Virus.
Kirusi cha homa ya Zika kama kile
cha Dengue kinaambukizwa kutoka mtu mmoja hadi mwingine kwa kuumwa na
mbu wa jamii ya Aedes hasa Aedes aegypti. Mbu huyu anaishi katika
mazingira ya makazi ya binadamu, huuma wakati wa mchana ndani ya nyumba
au kwenye maeneo yenye viwili, hususani majira ya asubuhi na jioni kabla
ya jua halijazama. Mbu huyu anazaliana katika maji yaliyotuama hasa
kwenye vyombo vya nyumbani, makinga maji ya paa za nyumba, matairi ya
gari, ndoo, makopo nk.
- Dalili za Homa ya Zika
Dalili za ugonjwa huu zinafanana
na za homa ya Dengue, ambazo ni homa, kuumwa na kichwa, maumivu ya
viungo, macho kuwa mekundu na vile vile kupata vipele vidogo vidogo kama
harara (Skin rashes). Dalili hizi huanza kujitokeza kuanzia kati siku ya 2 hadi 7 tangu mtu alipoambukizwa kirusi cha homa ya Zika.
Wachina waishio nchini waadhimisha mwaka mpya 2016 “Ngedere”
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Nape Nnauye akifungua Mwaka Mpya Kichina wa 2016
unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo
mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kushoto
ni mshereheshaji ajiyejitambulisha kwa jina la “Sharobaro”.
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Nape Nnauye (kushoto) akibadilishana mawazo na Waziri
Mkuu Mtaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Salim Ahmed
Salim (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016
unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo
mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Nape Nnauye (kulia) akifuatilia michezo mbalimbali
wakati wa wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016
unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo
mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kushoto
ni Mshauri wa Mambo ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini
Tanzania Gao Wei.
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Nape Nnauye (katikati) akifuatilia michezo mbalimbali
wakati wa wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016
unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo
mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kulia
ni Waziri Mkuu Mtaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Salim Ahmed Salim na kushoto ni Mshauri wa Mambo ya Utamaduni kutoka
Ubalozi wa China nchini Tanzania Gao Wei.
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Nape Nnauye (kushoto) akisalimiana na Waziri Mkuu
Mtaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda
(kulia) alipowasili viwanja vya Mnazi Mmoja wakati wa hafla ya uzinduzi
wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere”
kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi
Mmoja jijini Dar es salaam
Baadhi ya wageni waliohudhuria
hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka
wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki
viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Baadhi ya raia wa Kichina
wakiendelea na kujipamba kabla ya kuanza kwa hafla ya uzinduzi wa Mwaka
Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na
utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini
Dar es salaam.
Baadhi ya michezo iliyooneshwa
wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana
kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa
wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Waziri Mkuu Mtaafu wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akichanganya tiketi za
bahatinasibu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016
unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo
mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Vimulimuli vy fataki zilizowashwa
kuashiria kuzinduliwa kwa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama
mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki
viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.(Picha na Eleuteri
Mangi-MAELEZO)
………………………………………………………………………………………………
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Jumuiya ya Wachina wanaoishi
nchini wamezindua na kuukaribisha kwa shamrashamra mwaka Mpya wa 2016
unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo
mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
Akizindua shamrashamra hizo,
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye alisema kuwa
Wachina na Watanzania ni ndugu ambao uhusiano wao ni wa kudumishwa
milele na milele.
“Uhusiano wa Tanzania na China ni
wa kihistoria ambao ni wa muda mrefu katika mambo mbalimbali ikiwamo
kijamii, kiuchumi, kisiasa, kielimu na kiutamaduni Utamaduni na
kimawasiliano kati ya nchi hizi mbili” alisema Waziri Nape.
Kihistoria, uhusiano wa China na
Tanzania ni wa kidugu na kirafiki wakati wote iwe wa dhiki au faraja
katika maisha ya kila siku kati ya Watanzania na Wachina.
Ni wakati muafaka kuongeza
jitihada za kuimarisha uhusiano na ushirikiano wan chi hizo mbili ili
kuwaenzi waasisi wa ushirikiano huo ambao ni Rais Mwalimu Julius Nyerere
na Mao Tse Tung.
Kwa upande wake Mshauri wa Mambo
ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania Gao Wei alisema
kuwa wanajisikia faraja wakati wote wanapofanya kazi na Watanzania kwa
kuwa wanamengi ya kujivunia katika historia ya nchi hizo.
Aidha, shamrashamra za mwaka mpya
wa Kichina zilihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo Mawaziri Wakuu
Wastaafu Salum Ahmed Salum, Mizengo Pinda, viongozi mbalimbali na
wenyeji wa sherehe hizo ambao ni raia wa Kichina wanaoishi nchini
wakiongozwa na viongozi kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania.
Mwaka huu unajulikana kama
“Ngedere” wakati mwaka 2015 ulijuklikana kama “Kondoo” ambapo
maadhimisho ya Mwaka Mpya wa “Ngedere” yalipambwa na michezo mblimbali
ikiwemo bahatinasibu, sarakasi, nyimbo, muziki wa ala, mazingaombwe na
ngoma.
MKUU WA WILAYA YA KINONDONI, PAUL MAKONDA AISHUKURU TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE, WANANCHI WA KINONDONI JIJINI DAR ES SALAAM
| DC. Paul Makonda |
Mnamo
tarehe 23 wilaya yangu iliamua kufanya upimaji wa bure wa magonjwa ya
moyo, upimaji ambao niliamini ungebeba faida kubwa nne: moja, kujenga
utamaduni wa kupima afya mara kwa mara miongoni mwa wananchi, pili
kubaini watu ambao tayari wanasumbuliwa na magonjwa ya moyo, tatu
kuchukua hatua za awali za kuwasaidia wale ambao tayari
wameshashambuliwa na magonjwa hayo na mwisho kutoa elimu juu ya namna ya
kujikinga dhidi ya magonjwa yote ya moyo.
Ugonjwa
wa moyo ni ugonjwa unaoweza kuzalisha magonjwa mengi sana na kama
hujafanya vipimo sahihi ni rahisi kushughulika na matokeo ya ugonjwa
huku ukiacha chanzo kikizaa magonjwa mengine. Mathalani, unaweza
kujikuta unahangaika na kuvimba kwa miguu au kuhangaika na macho ama
figo aukisukari na hata kupoteza nguvu za kiume ukifikiri ndio tatizo
kumbe tatizo la msingi ni moyo.
Kimsingi
ni kwasababu hizo nilizozianisha nilichukua hatua ya kukiomba taasisi
ya moyo ya Jakaya Kikwete kinachosimamiwa na Profesa Janabikinisaidie
kutoa huduma hiyo bure ndani ya wilaya yangu.
Napenda
kuchukua nafasi hii kuwashukuru na kuwapongeza sana madaktari kutoka
taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete pamoja na mwananyamala kwa kuitikia
wito na kushiriki kikamilifu kulifanya zoezi hilo. zoezi ambalo lilikuwa
kubwa na zito kwani kwa makadirio ya awali tulitegemea kupata watu
wasiozidi 2000 ila badala yake walijitokeza wananchi zaidi ya 7000 ila
kutokana na umahiri wa madaktari hao tuliweza kuhudumia zaidi ya
wananchi 5900 ingawa tulilazimika kulifanya zoezi hilo kwa siku ya pili
yake ambayo ilikuwa ni tarehe 24.
Na
kwa watu wengine zaidi ya 1200 waliokuwa wamebaki, zoezi lao
tulilipanga na kulifanya tarehe 30 ya mwezi huu huu wa kwanza. Ukweli ni
kwamba, mambo mengi yalijitokeza kwa siku hizi tatu za upimaji; wapo
waliolazimika kukimbizwa kwa ambulance kuelekea hospitali za
mwananyamala na muhimbili, wapo waliolazimika kupewa appointments za
kuwaona madaktari, wapo waliopewa ushauri wa matumizi ya dawa na wengine
kubadilishiwa dawa sambamba na maelekezo ya utumiaji wa chakula na
ufanyaji wa mazoeziili kupunguza uzito.
Nichukue
tu fursa hii kuwapongeza wanakinondoni kwa kuitikia wito na kuniamini
mkuu wao wa wilaya na serikali yangu kwa ujumla kwamba tuna nia njema na
tunawapenda wananchi wetu kwa kuwahakikishia afya zao zinastawi na
kuendelea kuwa bora siku zote.
Kutokama
na maelezo niliyoyatoa hapo juu sambamba na sababu zilizonisukuma
kufanya zoezi hilo na kutokana na muitikio mkubwa wa wananchi bila
kusahau matokeo ya vipimo vilivyofanyika na kupata majibu ya kwamba watu
wengi wanahitaji matibabu, kubadilishiwa dawa, maelekezo ya matumizi
sahihi ya vyakula pamoja na mazoezi nimefanya uamuzi wa kulifanya zoezi
hili la kudumu na tayari nimeshafanya mazungumzo na hospitali kubwa na
nimetafuta njia na utaratibu bora zaidi wa kulifanya zoezi hili kuwa ni
zoezi la kudumu.
Sasa
basi, natamka rasmi kuwa serikali ya wilaya ya kinondoni inaanza
utaratibu wa kupima bure mara tatu kwa mwaka, utaratibu ambao utaanza
katikati ya mwezi wa nne. Zoezi hili litafanyika kwa kupima zaidi ya
magonjwa kumi ikiwemo yafuatayo: moyo, kisukari, kansa, macho, figo,
meno, kifua kikuu (TB), typhoid, magonjwa ya ngozi, presha, animonia,
kansa ya kizazi, kansa ya matiti, mabusha na matende.
Kama nilivyosema hapo awali ya kwamba, nimeshafanya mazungumzo na hospitali kubwa na kila hospitali itatoa vitengo viwili au vitatu na utaratibu utakuwa hivi. Kwa mfano, utakuta banda limeandikwa Jakaya Kikwete Cardiac Institute ndani ya banda hilo utakuta madaktari waliobobea kwenye upande wa moyo na upimaji wa presha kwahiyo mtu anayetaka kupima moyo ama presha atakwenda moja kwa moja kwenye banda husika.
Kama nilivyosema hapo awali ya kwamba, nimeshafanya mazungumzo na hospitali kubwa na kila hospitali itatoa vitengo viwili au vitatu na utaratibu utakuwa hivi. Kwa mfano, utakuta banda limeandikwa Jakaya Kikwete Cardiac Institute ndani ya banda hilo utakuta madaktari waliobobea kwenye upande wa moyo na upimaji wa presha kwahiyo mtu anayetaka kupima moyo ama presha atakwenda moja kwa moja kwenye banda husika.
Ama
unaingia kwenye banda limeandikwa Ocean Road hospital kwahiyo yeyote
anayetaka kupima kansa ataingia humo…hivyo hivyo kwa magonjwa mengine
yote: kutakuwa na mabanda tofauti yaliyoandikwa ni hospitali gani na
wanapima magonjwa gani, lengo ikiwa ni kumpa urahisi mpimaji
atakayejitokeza.
Mwisho
ila si kwa umuhimu niwashukuru sana wananchi wote wa wilaya nyingine na
wale waliotoka mikoa mbalimbali ikiwemo Tanga, Pwani, Morogoro, Lindi
na Dodomakwa imani yao kubwa juu ya tukio hili iliyowafanya kutoka mbali
na kujisogeza mpaka viwanja vya leaders wakiwa na imani ya kupatiwa
huduma hata kama zoezi hili lilikuwa limewalenga wakazi wa wilaya ya
Kinondoni.
Sambamba
na kuwashukuru wananchi niwashukuru pia waandishi wa habari ambao
wamekuwa mstari mbele kulitangaza tukio na kuhakikisha wananchi wanapata
taarifa kwa wakati.
Imetolewa na:- Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda
Imetolewa na:- Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda
MTAA WA GONGO LA MBOTO MANISPAA YA ILALA JIJINI DAR ES SALAAM WAENDELEA KUUNGA MKONO KAULI YA RAIS DK.MAGUFULI YA KUFANYA USAFI
Mwenyekiti
wa Kikundi chaYetu Envorotec Group kinachojishughulisha na kufanya
usafi katika Mtaa wa Gongo la Mboto Manispaa ya Ilala, Ali Mwinyimkuu
(kulia), akishiriki kufanya usafi na wananchi Dar es Salaam jana, ikiwa
ni utaratibu waliojiwekea wa kufanya usafi kila baada ya wiki mbili ili
kuunga mkono kauli Rais Dk. John Magufuli ya kufanya usafi katika maeneo
tunayoishi na kufanyia shughuli zetu nchini.
Kazi ya usafi ikiendelea.
Mwenyekiti
wa Kikundi chaYetu Envorotec Group kinachojishughulisha na kufanya
usafi katika Mtaa wa Gongo la Mboto Manispaa ya Ilala, Ali Mwinyimkuu
Omari akiwaongoza wenzake kufanya usafi.
Hapa ni kazi tu tunaukataa uchafu.
Wanawake wakishiriki kufanya usafi eneo la relini.
Mwenyekiti
wa Mtaa huo, Bakari Shingo (Aliyevaa kaputura), akishiriki kufanya
usafi na wananchi wake Dar es Salaam jana, ikiwa ni utaratibu
waliojiwekea wa kufanya usafi kila baada ya wiki mbili ili kuunga mkono
kauli Rais Dk. John Magufuli ya kufanya usafi katika maeneo tunayoishi
na kufanyia shughuli zetu nchini.
Usafi ukiendelea.
Wasanii wa Kikundi cha Rock Star wa Mtaa huo nao walishiriki kufanya usafi.
…………………………………………………………………………………..
Na Dotto Mwaibale
WANANCHI
wa Mtaa wa Gongolamboto Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam
wameendelea kumuunga mkono Rais John Magufuli kwa kufanya usafi katika
eneo hilo kwa wiki mara mbili ili kuyaweka mazingira yao katika hali ya
usafi.
Akizungumza
na waandishi wa habari waliotembelea mtaa huo Dar es Salaam jana
kujionea shughuli za usafi katika eneo Mwenyekiti wa mtaa huo Bakari
Shingo alisema lengo lao kubwa ni kuiunga mkono kauli ya Rais Magufuli
ya kufanya usafi ambapo wao wameamua kufanya usafi kwa wiki mara mbili.
Alisema
lakini wao walianza kufanya usafi katika eneo kabla ya rais kuanza
kuhimiza lakini kauli ya Magufuli ilichochea zaidi moto wa kufanya usafi
kwa wananchi wa eneo hilo.
Shingo
alisema katika mtaa wao kunavikundi ambavyo vinasaidia kufanya usafi
ambapo wamegawa maeneo na utaratibu huo umesaidia kuyaweka mazingira
katika hali ya usafi.
Mwenyekiti
wa Kikundi chaYetu Envorotec Group kinachojishughulisha na usafi katika
mtaa huo Ali Mwinyimkuu Omari alisema kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa
katika suala zima la usafi katika eneo hilo kutokana na utaratibu
waliojiwekea.
Alisema
wanamshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Issaya Mngulumi kwa
kujitoa kwake kuwapa gari la kusomba takataka kila wanapofanya usafi
hali ambayo inawapa moyo wananchi wa kufanya usafi hivyo kumungana mkono
Rais Dk. John Magufuli katika suala zima la usafi nchini.
Dar Swim Club mabingwa washinda mashinano ya kuogelea ya Taliss
wachezaji na makocha wa timu ya
Dar Swim Club wakishangilia baada ya kutwa ushindi wa jumla katika
mashindani ya Taliss yaliyofanyika jana kwenye bwawa la kuogelea la
shule ya kimataifa ya Tangangika (IST Upanga) na kushirikisha jumla ya
timu tisa.
Celina Itatiro wa Dar Swim Club na Ema Imhoff wa
Mwanza wakichuana katika mashindamo ya Taliss kwenye bwawa la kuogelea
la shule ya kimataifa ya Tangangika (IST Upanga) na kushirikisha jumla
ya timu tisa.
waogeleaji waki-dive kwenye maji katika mashindano hayo.
waogeaji wakichuana katika mashindano hayo
…………………………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu
Dar es Salaam. Timu ya Dar Swim
Club (DSC) imeshinda mashindano ya kuogelea ya Taliss baada ya kuzipiku
klabu nyimgine nane zilizoshiriki katika mashindano hayo yaliyofanyika
kwenye bwawa la kuogelea la Shule yaKimataifa ya Upanga.
Dar Swim Club ilijikusanyia
pointi 2,421 katika mashindano hayo yaliyoshirikisha timu za wanawake na
wanaume. Katika mashindano hayo, wanawake wa DSC walikusanya jumla ya
pointi 1,526 huku wanaume wakijikusanyia pointu 895 kushinda nafasi ya
kwanza katika mashindano hayo yaliyokuwa na ushindani mkubwa.
Waogelaji wa kike Smriti
Gokarn, Celina Itatiro na Maia Tumiotto walichangia zaidi ushindi wa
timu hiyo kwa kukusanya pointi nyingi na akwa upande wa wavulanai
walikuwa Matt Golembeski, Marin De Villard na Carter Golembeski.
Nafasi ya pili ilinyakuliwa na
wenyeji Taliss kwa kupata jumla ya pointi 2,298 huu waogelaji wao wa
kiume, Adil Dharmal na Oliver Mclntosh wakiongoza kwa kuchangia pointi
nyingi katika ushindi huo.
Nafasi ya tatu ilikwenda kwa
Shule ya Kimataifa ya Moshi ambayo ilichanganyika nay a Arusha kwa
kupata pointi 1,111 huku waogeleaji wake, Josephine Oosterhuis na Pieter
De Raadt wakichangia pointi nyingi.
Timu ya kuoglea ya Mwanza
ilimaliza katika nafasi ya nne chini ya waogeleaji nyota Elia Imhoff na
Emma Imhoff na kufuatiwa ma shule ya kimataifa ya Morogoro chini ya
nyota wake, Dennis Mhini na Charlotte Sanford.
Timu ya Bluefins ilishika
nafasi ya sita kwa pointi 553 ambapo waogelaji wake Sahal Harunani
alishinda medali ya shaba. Nafasi ya saba ilikwenda kwa timu ya Wahoo
iliyokuwa chini ya Ellis Underson na Rania Karume kwa kupata pointi 303
na huku Champions Rise na Kennedy House wakimaliza katika nafasi mbili
za mwisho.
Mhasisi wa Dar Swim Club Ferick
Kalengela alisema kuwa siri kubwa ya ushindi wao ni kujituma na kufanya
mazoezi ya kisasa huku Katibu mkuu wa klabu hiyo, Inviolata Itatiro
akiwapongeza wachezaji wake na kusema huo ni mwanzo tu na makubwa
yatafuatia katika kuendeleza mchezo wa kuogelea nchini.
WAZIRI MAKAMBA ATOA MSAADA MABATI 300 KWA WAHANGA AMBAO NYUMBA ZAO ZILIZOEZULIWA NA UPEPO JIMBONI KWAKE.
NA RAISA SAID,BUMBULI
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshugulikia Muungano na
Mazingira,January Makamba ametoa msada wa mabati 300 kwa wananchi
ambao nyumba zao zimeezuliwa na upepo uliosababishwa na mvua kubwa
iliyonyesha maeneo mbalimbali jimboni humo.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshugulikia Muungano na
Mazingira,January Makamba ametoa msada wa mabati 300 kwa wananchi
ambao nyumba zao zimeezuliwa na upepo uliosababishwa na mvua kubwa
iliyonyesha maeneo mbalimbali jimboni humo.
Nyumba hizo zilikuwa 40 ikiwemo Kanisa na Msikiti zimeezuliwa mapaa
katika kijiji cha Msamaka kilichopo wilayani Bumbuli kufuatia Mvua
kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha.
katika kijiji cha Msamaka kilichopo wilayani Bumbuli kufuatia Mvua
kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha.
Mvua hiyo imesabisha kaya hizo kukosa mahali pa kuishi , huku
wengi wa waathirika wakipewa hifadhi kwenye nyumba za majirani
zao.
wengi wa waathirika wakipewa hifadhi kwenye nyumba za majirani
zao.
Akizungumza na waandishi wa habari hapo Jana Afisa Mtendaji wa kijiji
cha Msamaka Mbazi Shemhando alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo
January 27 mwaka huku saa kumi jioni.
cha Msamaka Mbazi Shemhando alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo
January 27 mwaka huku saa kumi jioni.
Alitaja sehemu zilizo athirika zaidi kuwa ni Vitongoji vya Kwemchaa,
Nazareti,CCM, Kwakorosi pamoja na kitongoji cha Kwamingojo ndio
vimeweza kuathirika na maafa hayo.
Nazareti,CCM, Kwakorosi pamoja na kitongoji cha Kwamingojo ndio
vimeweza kuathirika na maafa hayo.
Hata hivyo aliongeza kuwa waathirika watukio hilo Kwa sasa
wamehifadhiwa kwenye nyumba za Jirani wakati utaratibu mwingine wa
kuwasaidia ukiendelea kuwekwa.
wamehifadhiwa kwenye nyumba za Jirani wakati utaratibu mwingine wa
kuwasaidia ukiendelea kuwekwa.
Akikabidhi msaada huo Makamba alisema kuwa kutokana na tukio hilo
anatanguliza msaada huo kwanza wakati akiendelea kutafuta msaada
zaidi.
anatanguliza msaada huo kwanza wakati akiendelea kutafuta msaada
zaidi.
“Nimejikusanya Kwa hiki kidogo ili kiweze kusaidia pale penye uhitaji
Kwa haraka wakati tukiendelea na utaratibu mwingine” alisema Makamba
Kwa haraka wakati tukiendelea na utaratibu mwingine” alisema Makamba
Makamba aliwataka wananchi wote kupanda miti ili kuepuka upepo
mkali unaosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika
maeneo tofauti
mkali unaosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika
maeneo tofauti
SUALA LA ADA ELEKEZI KUHUSISHA WADAU WOTE – WAZIRI MKUU
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizunguza katika ibada ya kumuingiza kazini Mkuu wa Kanisa la Kiinjili
la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick Shoo iliyofanyika kwenye
kanisa Kuu la KKKT mjini Moshi Januari 31, 2016.
………………………………………………………………………………………..
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
amesema suala la ada elekezi linaendelea kufanyiwa kazi na Serikali na
likifika hatua nzuri litahusisha wadau wote ili kupata maoni yao.
Ametoa ahadi hiyo leo mchana
(Jumapili, Januari 31, 2016) wakati akizungumza na mamia ya waumini
walioshiriki ibada ya kumuingiza kazini Mkuu Mpya wa Kanisa la Kiinjili
la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Fredrick Onaeli Shoo
iliyofanyika kwenye usharika wa Moshi Mjini, Dayosisi ya Kaskazini.
Waziri Mkuu Majaliwa ambaye
alihudhuria ibada hiyo kwa niaba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli alikuwa
akijibu baadhi ya hoja zilizotolewa na Dk. Shoo ambaye alisema kama
Serikali inataka kuondoa ada elekezi haina budi kuziimarisha shule zake
ili ziwe kama zilivyokuwa zamani.
Akijibu hoja kuhusu miundombinu ya
reli, Waziri Mkuu alisema Serikali imeamua kufufua miundombinu hiyo na
kwamba hivi sasa inafanya mapitio ili kujua gharama halisi kwa maeneo
husika. Alisema Serikali imepanga kuanza na maeneo manne ambapo la
kwanza alilitaja kuwa ni reli ya kutoka Dar es Salaam – Mwanza – Tabora –
Kaliua – Mpanda hadi Karema.
“Eneo la pili ni reli ya ukanda wa
Kaskazini ambayo itatoka Dar es Salaam – Tanga – Arusha hadi Musoma. Ya
tatu ni ya kutoka Tabora – Kahama – Kigali (Rwanda) na kuishia nchini
Burundi ambayo tunataka isaidie kusafirisha mizigo kutoka bandari ya Dar
es Salaam. Reli ya nne ni ile ya kutoka Mtwara kupitia Tunduru kwenda
Songea hadi Mbamba Bay,” alisema.
Kuhusu ulinzi wa demokrasia ndani
ya Bunge, Waziri Mkuu alisema anakubaliana na Askofu Dk. Shoo juu ya
mihimili yote mitatu kuheshimiana na kwamba ameshukuru kwamba ameonya
juu ya lugha zinazotumika ndani ya Bunge.
“Bunge ni eneo linaloweza kujenga
jamii mpya kwa sababu Bunge ni kioo na jamii ya Watanzania inatuangalia
sisi tuliomo mle. Ni vema tuwe na lugha nzuri, tabia njema na hata jinsi
tunavyovaa ili wanaotuona wapate hamu ya kuiga,” alisema.
Kuhusu ombi la kuibuliwa upya
mchakato wa Katiba mpya, Waziri Mkuu alisema suala hilo amelichukua na
anaenda kulifanyia kazi. “Nakuhakikishia Baba Askofu ushauri ulioutoa
kwa Serikali tumeupokea,” alisisitiza.
Mapema, akitoa hotuba yake, Askofu
Mkuu Dk. Shoo alisema Bunge ni nyumba ya demokrasia kwa hiyo jamii
inatarajia kuona hoja zikijadiliwa kwa haki na amani badala kutumia
ubabe na mabavu au nguvu ya dola.
“Nimewaona baadhi ya wabunge mko
hapa… hili ninalolisema ni lenu na linawahusu ninyi na spika wenu.
Wabunge tunzeni heshima yenu na Mungu awasaidie kulitimiza hilo. Wewe
Waziri Mkuu ni Msimamizi wa shughuli za Serikali bungeni kwa hiyo una
kazi ya kusimamia. Kila mhimili unapaswa utunze heshima yake…,”
alisisitiza.
Kuhusu Katiba mpya, Askofu Dk.
Shoo alisema Watanzania wengi wana kiu ya kuona mchakato huo ukiibuliwa
upya na kukamilishwa ili nchi ipate Katiba mpya yenye kukidhi kiu ya
watu wake na inayoheshimu matakwa ya wengi.
“Mchakato huo ukianza utumike
kuganga majeraha yote yaliyopita. Tukifanya hivyo tutakuwa tumeisaidia
Serikali ya Awamu ya Tano kuipelekea nchi yetu kule ambako imedhamiria.
Yote yanawezekana tukitaka na tukipenda,” alisisitiza.
Kwa upande wake, Askofu ambaye
amemaliza muda wake wa kuliongoza kanisa hilo, Dk. Alex Malasusa alisema
anamshukuru Mungu kwa kupata kibali cha kushuhudia Mkuu mpya wa kanisa
hilo akipokea kijiti cha uongozi kutoka kwake.
“Si kwa akili na uwezo wangu bali
ni kwa uweza wa Mungu kwamba nimeweza kuishuhudia siku ya leo.
Ninamuomba Mungu akusaidie kuongoza kanisa hili, akusaidie kukemea na
kuonya kwa upole. Najua Mungu atakupunguzia hata marafiki kwa sababu ya
matamshi utakayokuwa ukiyatoa, lakini si wewe bali ni uweza wa Bwana na
roho mtakatifu anayekuongoza,” alisema.
Aliahidi kuendelea kuwaombea Rais
Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Majaliwa katika majukumu waliyonayo.
“Msiogope kwa ajili ya majukumu mliyopewa, msihofu tunaendelea kuwaombea
kwa sababu tuko pamoja na sisi ni sehemu ya utumishi wa Taifa,”
alisema.
Waziri Mkuu anarejea Dodoma jioni hii kuendelea na vikao vya Bunge.
IMETOLEWA NA: OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, JANUARI 31, 2016.
MAJALIWA AHUDHURIA IBADA YA KUMUINGIZA KAZINI MKUU WA KKKT TANZANIA ASKOFU SHOO MJINI MOSHI
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea picha aliyopewa na Askofu Mkuu Mpya wa
Kanisa la Kiinjili la Kilutheli,Askofu Frederck Shoo katika ibada ya
kumuingiza kazini askofu huyo ilyofanyika kwenye kanisa kuu la KKKT
mjini Moshi Januari 31, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizunguza katika ibada ya kumuingiza kazini Mkuu
wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick
Shoo iliyofanyika kwenye kanisa Kuu la KKKT mjini Moshi Januari 31,
2016.
Waziri
MkuuKassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa
katika ibada ya kumuingiza kazini Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania, Askofu Frederick Shoo kwenye kanisa Kuu la KKKT
mjini Moshi Januari 31, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili
la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick Shoo (kulia) na Askofu
Mkuu wa KKKT Mstaafu Alex Malasusa baada ya ibada ya kumuingiza kazini
Askofu Shoo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Moshi Januari
31, 2016.
(PICHA NA OFISI YA WAZIRI MUU)
NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT. KIGWANGALA AZINDUA DUKA LA DAWA LA MSD JIJINI ARUSHA
Naibu
Waziri wa Afya akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD
Prof. Idris Mtulia alipowasili duka la MSD Mount Meru, Arusha kwa ajili
ya kulizindua rasmi jana. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean
Bwanakunu, akifuatiwa na Mkurugenzi wa Shughuli za Kanda na Huduma kwa
Wateja Bw. Cosmas Mwaifwani.
NaibuWaziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Hamis Kigwangalla (wa pili kulia),
akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa duka la Dawa la MSD jijini
Arusha, ambalo liko ndani Hospitaliya Mount Meru.
Msimamizi
wa Duka la MSD Arusha Twaha Kabandika akitoa maelezo kwa Naibu Waziri
Kigwangalla wa namna mfumo unaotumika kwa mauzo unavyofanya kazi.Kulia
ni M/Kiti wa Bodi MSD, Prof Idris Mtulia, Mkurugenzi wa MSD Laurean
Bwanakunu (Kushoto0 na Mkuu wa Wilaya ya Arusha mjini Fadhili Nkuru.
………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu, Arusha.
NaibuWaziriwaAfya, MaendeleoyaJamii, Jinsia, WazeenaWatotoMhe. Dkt HamisKigwangalla amezindua rasmi duka la Dawa la MSD jijiniArusha, ambalo liko ndani Hospitaliya Mount Meru na kuiagiza MSD mbali na kuweka alama ya GoT kwenye vidonge vyake iangalie pia utaratibu wa kuweka rangi maalumu kwenye vidonge na vifungashio, ilikurahisha udhibiti wa upotevu na ufuatiliaji wa dawa hizo.
Naibu Waziri huyo pia amewahimiza watendaji wa MSD kuwa waadilifu, kuwajali na kuwasilikiza wateja na kutumia lugha nzuri wakati wa kuwahudumia wateja, huku akitoaangalizo kwa wale wanao kiuka taratibuza ajira kuwa watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Kwa upande Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhaminiya MSD Prof. IdrisMtulia ameeleza kuwa MSD inaweza kufanya vizuri zaidi endapo changamoto za sheria ya manunuzi, mgawo mdogo wafedha kwa vituo vya Afya, hospitali na zahanati, na mgawo wafedha kuja kwa mafungu zitafanyiwa kazi.
Naye Mkurugenzi Mkuuwa MSD Bwana Laurean Bwanakunu ameeleza kuwa MSD itakuwa na maduka manne tu mkoani Dares Salaam, Mwanza, A Arusha na Mbeya ambapo kwa mikoa mingine MSD wanaafanyama wasiliano na hospitali za mikoa ziwe na maduka ya hospitali wanayoendesha wenyewe na kisha MSD iwauzia dawa na kuwawezesha utaalamu wakuendesha maduka hayo.
NaibuWaziriwaAfya, MaendeleoyaJamii, Jinsia, WazeenaWatotoMhe. Dkt HamisKigwangalla amezindua rasmi duka la Dawa la MSD jijiniArusha, ambalo liko ndani Hospitaliya Mount Meru na kuiagiza MSD mbali na kuweka alama ya GoT kwenye vidonge vyake iangalie pia utaratibu wa kuweka rangi maalumu kwenye vidonge na vifungashio, ilikurahisha udhibiti wa upotevu na ufuatiliaji wa dawa hizo.
Naibu Waziri huyo pia amewahimiza watendaji wa MSD kuwa waadilifu, kuwajali na kuwasilikiza wateja na kutumia lugha nzuri wakati wa kuwahudumia wateja, huku akitoaangalizo kwa wale wanao kiuka taratibuza ajira kuwa watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Kwa upande Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhaminiya MSD Prof. IdrisMtulia ameeleza kuwa MSD inaweza kufanya vizuri zaidi endapo changamoto za sheria ya manunuzi, mgawo mdogo wafedha kwa vituo vya Afya, hospitali na zahanati, na mgawo wafedha kuja kwa mafungu zitafanyiwa kazi.
Naye Mkurugenzi Mkuuwa MSD Bwana Laurean Bwanakunu ameeleza kuwa MSD itakuwa na maduka manne tu mkoani Dares Salaam, Mwanza, A Arusha na Mbeya ambapo kwa mikoa mingine MSD wanaafanyama wasiliano na hospitali za mikoa ziwe na maduka ya hospitali wanayoendesha wenyewe na kisha MSD iwauzia dawa na kuwawezesha utaalamu wakuendesha maduka hayo.
Wananchi watahadharishwa juu ya homa ya Zika
……………………………………………………………………………………
Na Raymond Mushumbusi Maelezo
Wananchi wa Tanzania
watahadharishwa juu ya ugojwa wa homa ya Zika uliripotiwa kutokea katika
nchi za Amerika ya kusini hivi karibuni.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Mijini Dodoma na Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii, Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu alipokuwa akitoa tamko juu ya uvumi ulioenea kuhusu homa ya Zika iliyoenea katika nchi za Amerika ya kusini.
Mhe.Ummy Mwalimu amewaasa watanznia kuwa na tabia ya kwenda hospitali kila wanapojisikia dalili za homa na kupima kwani sio kila homa ni malaria kwani dalili za homa ya malaria zinafanana kabisa na dalili za ugonjwa wa homa ya Zika.
“ Nawaomba ndugu zangu watanzania tuzingatie usafi ili kuzuia mazalia ya mbu kwani ugonjwa huu unatokana na virusi vinavyoenezwa na mbu na hao mbu wanapatikana sana nyakati za asubuhi mchana na jioni hivyo nawasihi kutumia dawa za kuua mbua na vyandarua wakati wa kulala.”
“Napenda kutoa tamko kuwa ugonjwa huu wa homa ya Zika haujaingia Tanzania na tunawaomba watanzania kuwa makini sana na waripoti dalili zozote ambazo sio za kawaida zitakazojitokeza na mpaka jana kwa taarifa tulizonazo hakuna mgonjwa aliyegundulika kuwa na homa ya Zika” Alisema Mhe.Mwalimu.
Aidha naye Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Dodoma Dkt Zainabu Chaula amesema wamejiandaa kukabiliana na kesi zozote zinatazojitokeza za homa ya Zika na wana mfumo mzuri wa kubaini magonjwa ya mlipuko na pia kuna maabara ya NIMR ambayo inafanya uchunguzi juu ya magonjwa mbalimbali.
“ Nawaomba watanzania kutopuuzia dalili zozote za homa na kuamua kujitibia manyumbani au kunywa dawa bila kupima na kujua hiyo homa ni ugonjwa gani kwani yaweza kuwa homa ya Zika” Alisema Dkt Chaula.
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Watoto na Wazee wa kushirikiana na Shirika la Afya Dunianoi (WHO) wanafatilia kuhusu ugonjwa huu na watatoa maelekezo ya kuzingatia ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu ila mpaka sasa ugomjwa huu haujaingia Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Mijini Dodoma na Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii, Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu alipokuwa akitoa tamko juu ya uvumi ulioenea kuhusu homa ya Zika iliyoenea katika nchi za Amerika ya kusini.
Mhe.Ummy Mwalimu amewaasa watanznia kuwa na tabia ya kwenda hospitali kila wanapojisikia dalili za homa na kupima kwani sio kila homa ni malaria kwani dalili za homa ya malaria zinafanana kabisa na dalili za ugonjwa wa homa ya Zika.
“ Nawaomba ndugu zangu watanzania tuzingatie usafi ili kuzuia mazalia ya mbu kwani ugonjwa huu unatokana na virusi vinavyoenezwa na mbu na hao mbu wanapatikana sana nyakati za asubuhi mchana na jioni hivyo nawasihi kutumia dawa za kuua mbua na vyandarua wakati wa kulala.”
“Napenda kutoa tamko kuwa ugonjwa huu wa homa ya Zika haujaingia Tanzania na tunawaomba watanzania kuwa makini sana na waripoti dalili zozote ambazo sio za kawaida zitakazojitokeza na mpaka jana kwa taarifa tulizonazo hakuna mgonjwa aliyegundulika kuwa na homa ya Zika” Alisema Mhe.Mwalimu.
Aidha naye Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Dodoma Dkt Zainabu Chaula amesema wamejiandaa kukabiliana na kesi zozote zinatazojitokeza za homa ya Zika na wana mfumo mzuri wa kubaini magonjwa ya mlipuko na pia kuna maabara ya NIMR ambayo inafanya uchunguzi juu ya magonjwa mbalimbali.
“ Nawaomba watanzania kutopuuzia dalili zozote za homa na kuamua kujitibia manyumbani au kunywa dawa bila kupima na kujua hiyo homa ni ugonjwa gani kwani yaweza kuwa homa ya Zika” Alisema Dkt Chaula.
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Watoto na Wazee wa kushirikiana na Shirika la Afya Dunianoi (WHO) wanafatilia kuhusu ugonjwa huu na watatoa maelekezo ya kuzingatia ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu ila mpaka sasa ugomjwa huu haujaingia Tanzania.
JAJI MKUU WA TANZANIA MHE.OTHMAN CHANDE AFUNGUA MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA NCHINI.
Watumishi
wa Mahakama ya Tanzania na wadau mbalimbali wa wakiingia katika viwanja
vya Mnazi mmoja kwa maandamano leo jijini Dar es salaam wakati wa
Ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria.
Watumishi
wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), Askari
wa Jeshi la Magereza na Watumishi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka
(DPP) wakiwa wamebeba mabango ya Ofisi zao wakati wa Ufunguzi wa
maadhimisho ya Wiki ya Sheria Nchini leo jijini Dar es salaam.
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande (Mwenye T-shirt nyeupe kulia), Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Said Mecki Sadiki (wa Pili kulia) na Watendaji
wa Mahakama ya Tanzania wakishiriki mazoezi ya viungo ya pamoja na wadau
mbalimbali wa Mahakama leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja wakati wa
Maadhimisho ya Wiki ya Sheria Nchini.
Jaji
Kiongozi Mhe. Shaban Lila (katikati) akiongoza mazoezi ya pamoja ya
Wadau wa Mahakama leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
salaam wakati wa Ufunguzi wa Wiki ya Sheria nchini.
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akizungumza na wadau mbalimbali wa
Mahakama waliohudhuria Ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria mwaka
2016 katika viwanja vya Mnazi mmoja leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa Ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria.
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akiwa katika picha ya pamoja na
Watumishi wa Tume ya Utumishi wa Mahakama wakati wa Ufunguzi wa
maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini leo jijini Dar es salaam. Wengine
katika picha ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omary Othman Makungu (wa tatu
kutoka kulia), Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki (wa tatu
kutoka kushoto) na Jaji Kiongozi Mhe. Shaban Lila (wa pili kutoka
kushoto).
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akiwa katika picha ya pamoja na
viongozi na Watendaji wa Mahakama, Viongozi na Askari wa Jeshi la Polisi
wakati wa Ufunguzi wa Wiki ya Sheria leo jijini Dar es salaam.
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande (katikati) Mkuu wa Mkoa wa Dar es
salaam Saidi Meck Sadiki (wa tatu kutoka kushoto), Jaji Mkuu wa Zanzibar
Mhe. Omary Othman Makungu (wa tatu kutoka kulia) na Jaji Kiongozi Mhe.
Shaban Lila (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Chama cha
Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA) leo katika viwanja vya Mnazi Mmmoja
wakati wa Ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini.
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. Othman Chande akiwa katika picha ya pamoja na
Askari wa Jeshi la Magereza leo wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya
Wiki ya Sheria nchini.
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AMUWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE MKUTANO WA WAKUU WA AFRIKA masuala ya Usalama Barani Afrika.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Viwanda la
Umoja wa Mataifa UNIDO lenye makamo makuu yake Nchini Vienna Ausria Bw.
Li Yong walipokuta katika Ofisi za Umoja wa Afrika (AU) Addis Ababa leo
Januari 31,2016, Makamu wa Rais yupo Nchini Addis Ababa Ethiopia
kumuwakilisha Rais John Magufuli kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za
Afrika unaojadili kuhusu masuala ya Usalama Barani Afrika.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akizungumza na Ujumbe wa Shirika la Maendeleo la Viwanda la Umoja wa
Mataifa lenye Makao Makuu yake Nchini Vienna Austria uliongozwa na
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Bw. Li Yong, leo Januari 31,2016 kwenye
Ofisi za Umoja wa Afrika (AU) Addis Ababa, katika mazungumzo yao
Viongozi hao walizungumzia juu ya kuendeleza ushirikiano kwenye
maendeleo ya Viwanda utakaotolewa na UNIDO kwa Serikali ya Tanzania ili
kuifanya Tanzania iwe Nchi ya Viwanda kuanzia mwaka 2015/2020, ambapo
Mkurugenzi huyo ameahidi kuitembelea Tanzania wakati wowote kuanzia
sasa. Makamu wa Rais yupo Nchini Addis Ababa Ethiopia kumuwakilisha Rais
John Magufuli kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika unaojadili
kuhusu masuala ya Usalama Barani Afrika.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akipokea taarifa yenye mipango ya Maendeleo ya Viwanda kutoka kwa
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda la Umoja wa Mataifa
Bw. Li Yong baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao yaliyofanyika leo
Januari 31,2016 katika Ofisi za Umoja wa Afrika (AU) Addis Ababa, Makamu
wa Rais yupo Nchini Addis Ababa Ethiopia kumuwakilisha Rais John
Magufuli kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika unaojadili kuhusu
masuala ya Usalama Barani Afrika.
(Picha na OMR)
Tamasha la Pasaka kufanyika Mwanza
……………………………….
TAMASHA la Pasaka 2016 linaloandaliwa na Kampuni ya Msama Promotions jijini Dar es Salaam linatarajia kufanyika Machi 27 katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama mkoa wa Mwanza umepata bahati hiyo baada ya wakazi wake kuomba kwa kipindi kirefu kufikiwa na tamasha hilo.
“Kamati yangu huwa inasikia matakwa ya mashabiki wa muziki wa Injili kwa sababu tamasha hilo ni lao ni vizuri kuwasikiliza,” alisema Msama.
Msama alisema, Kamati yake imekaa na imechunguza Tamasha la mwaka huu lifanyikie jijini humo, hivyo anatoa wito kwa wakazi wa jiji hilo kujiandaa vilivyo kwa ajili ya tamasha hilo.
“Tamasha letu linawahusu wenye uhitaji maalum ambao ni walemavu, wajane na yatima ambao misaada yao inatokana na tamasha hilo, hivyo wajipange na kujitokeza kwa wingi,” alisema Msama.
Msama alisema wamesikia kilio cha Wananchi Mwanza baada ya maombi yao ya muda mrefu, tamasha litafanyikia jijini humo ikiwa ni heshima yao.
“Wakazi wa Mwanza walipokee, waimbaji mbalimbali wa mataifa mbalimbali, ni sherehje, raha, vifijo,” alisema Msama.
TAMASHA la Pasaka 2016 linaloandaliwa na Kampuni ya Msama Promotions jijini Dar es Salaam linatarajia kufanyika Machi 27 katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama mkoa wa Mwanza umepata bahati hiyo baada ya wakazi wake kuomba kwa kipindi kirefu kufikiwa na tamasha hilo.
“Kamati yangu huwa inasikia matakwa ya mashabiki wa muziki wa Injili kwa sababu tamasha hilo ni lao ni vizuri kuwasikiliza,” alisema Msama.
Msama alisema, Kamati yake imekaa na imechunguza Tamasha la mwaka huu lifanyikie jijini humo, hivyo anatoa wito kwa wakazi wa jiji hilo kujiandaa vilivyo kwa ajili ya tamasha hilo.
“Tamasha letu linawahusu wenye uhitaji maalum ambao ni walemavu, wajane na yatima ambao misaada yao inatokana na tamasha hilo, hivyo wajipange na kujitokeza kwa wingi,” alisema Msama.
Msama alisema wamesikia kilio cha Wananchi Mwanza baada ya maombi yao ya muda mrefu, tamasha litafanyikia jijini humo ikiwa ni heshima yao.
“Wakazi wa Mwanza walipokee, waimbaji mbalimbali wa mataifa mbalimbali, ni sherehje, raha, vifijo,” alisema Msama.
ONGEZEKO LA BAJETI KATIKA SEKTA YA UTALII
Katika
mipango ya kukuza uchumi, sekta ya utalii chini ya Prof Jumanne
Maghembe ambaye ni Waziri mpya wa maliasili na utalii imeamua kuanza
kuweka mikakati katika kuongeza bajeti ya kutosha kwa mwaka 2016, ili
kuongeza bidhaa na huduma zenye ubora kwa lengo la kuvutia watalii wengi
zaidi nchini.
Sekta
ya utalii imekuwa na mpango wa kuongeza watalii wa kigeni zaidi ya
Million 3 mpaka kufikia 2018, ambapo mkakati huu utaenda sambambana na
ongezeko la pato la taifa kuongezeka mara mbili ya kinachopatikana kwa
sasa.
kwa upande wake mdau wa masuala ya Utalii, Bw. Andrea Guzzoni, Meneja mkazi wa JovagoTanzania
alifafanua kuwa sekta ya utalii imekuwa mstari wa mbele katika kukuza
uchumi baada ya kilimo, hivyo kama suala hili litatiliwa mkazo basi
tunasubiria Tanzania mpya katika uchumi.
Aliendelea
kwa kufafanua kuwa, “Sekta hii inabidi ikabiliane na matatizo
yanayoikabili katika ukusajji wa kodi, kwa namna moja au nyingine
inaweza kuwa ni kikwazo kikubwa cha maendeleo kama hatuta chukua hatua
yeyote”.
“Hata
hivyo,inabidi tuangalie maboresho katika nyanja tofauti tofauti, bado
kuna wahudumu wasio na ujuzi wa kutosha, ukilinganisha na huduma ukiwa
nje ya nchi na hapa ni tofauti, hivyo tujaribu kuweka mafunzo ya ziada
kwa waajiriwa na waajiri ili kuongeza ufanisi katika kazi”

No comments :
Post a Comment