Thursday, December 3, 2015

Tanesco kuondolewa katika uzalishaji umeme, Wind EA kuanza kuzalisha mwishoni 2017

maj1

 

Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Mhandisi, Hosea Mbise akizungumza katika mkutano wa tatu wa wawekezaji na wadau wa nishati ya umeme ujulikanao kwa jina la  Powering Africa uliodhaminiwa na kampuni ya Wind East Africa.
maj2
Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kampuni ya Six Telecoms Rashid Shamte akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mradi wa umeme wa upepo wa Singida kupitia kampuni ya Wind EA ambao unatarajiwa kuanza uzalishaji rasmi mwishoni mwa mwaka 2017. Shamte alisema hayo wakati wa mkutano  wa tatu wa kimataifa wa kuiwezesha Afrika katika utatuzi wa nishati ya umeme umefanyika Dar es Salaam leo.  Kulia ni Mkurugenzi wa Mradi huo, Mark Gammons.
maj3
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa kampuni ya Wind East Africa John Chaggama akifafanua jambo kuhusiana na uwekezaji wao wa Umeme wa Upepo uliopo mkoani Singida. Chaggama alisema mradi huo utatatua tatizo la nishati hiyo hapa nchini mara utakapoanza rasmi uzalishaji mwishoni mwa mwaka 2017.
maj4
Wadau na wawekezaji mbali mbali wa nishati ya umeme wakimsikiliza Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Mhandisi, Hosea Mbise hayupo pichani wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa wawekezaji na wadau wa nishati ya umeme ujulikanao kwa jina la  Powering Africa uliodhaminiwa na kampuni ya Wind East Africa.
……………………………………………………………………………
Na Mwandishi wetu
Wakati Serikali ikibainisha kuliondoa Shirika la umeme nchini (Tanesco) katika uzalishaji wa umeme, kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo (Wind East Africa) imesema itaanza uzalishaji wa nishati hiyo mwishoni mwa mwaka ujao.
Wakizungumza katika mkutano wa kimataifa wa uwekezaji katika sekta ya umeme, Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Mhandisi, Hosea Mbise na Mwanzilishi na Mkurugenzi wa wa kampuni ya Wind East Africa, Rashid Shamte walieleza mkakati uliopo katika kuboresha sekta ya umeme nchini ambapo baada ya muda, Tanesco itakuwa na kazi ya usafirishaji tu huku kazi ya uzalishaji ikifanywa na kampuni kama Wind EA.
Mbise alisema kuwa alisema uzalishaji wa umeme unahitaji uwekezaji wa hali ya juu ikiwamo kutoa fursa kwa kampuni mbalimbali kuanza kuzalisha umeme kwa manufaa ya Taifa.
Kwa mujibu wa Mbise, hatua za awali za kuliondoa Shirika hilo la umeme nchini kuwa mzalishaji wa nishati hiyo umeanza na ifikapo 2022, Shirika hilo halitajihusisha na uzalishaji wa umeme zaidi ya kazi ya usafirishaji tu.
“Kwa utaratibu huu, Tanesco sasa itaondoshwa katika mchakato wa kuzalisha umeme na kubaki kuwa msambazaji, hatua tayari zimeanza kwa kuangalia madeni yaliyopo Tanesco na jinsi ya kuyafuta sanjari na kuwachukua watumishi wa Tanesco.
“Ifikapo 2022 hatutakuwa na Tanesco katika uzalishaji wa umeme bali umeme utazalishwa na kampuni mbalimbali na mkakati uliopo ni kwamba hadi kufikia 2030, asilimia 70 ya Watanzania wawe wamefikiwa na huduma ya umeme,” alisema Mbise.
Kwa upande wake, Shamte alieleza kuwa mradi wa umeme wa upepo wa Singida kwa sasa upo katika maandalizi ya kina kuanza na mwaka ujao watakamilisha taratibu mbalimbali kwa mujibu wa sheria za uwekezaji.
Shamte alisema kuwa mradi huo ambao utazalisha 100 Mega Watts mbali ya kutatua tatizo la umeme, utaufanya mkoa wa Singida kubadilika kwa kupata maendeleo makubwa kiuchumi, biashara na hata kijamii.
Alisema kuwa mkataba mikataba ya kumalizia uwekezaji wamradi huo itasainiwa mwanzoni mwa mwezi ujao (Januari 2017).
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa kampuni ya Wind East Africa, John Chagama alisema, mradi wa umeme wa upepo utakapokamilika utawanufaisha Watanzania hasa wakazi wa Singida ambako mradi huo unaanzishwa.
 
“Kwanza utasaidia kutoa ajira kwa wakazi wa Singida, lakini pia utawanufaisha Watanzania hasa wa kipato cha chini kwani umeme utakuwa wa gharama nafuu,” alisema.
Chagama alisema kuwa umeme wa upepo ni mradi wa kudumu na utawafanya watanzania kupunguza gharama za maisha kwani bei ya umeme itashuka.

MAADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA YAFANYIKA SOKO LA TEMEKE STERIO JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Mwenyekiti wa Soko la Temeke Sterio Amani Mtemi akiwatambulisha wageni waalikwa katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyika katika soko hilo Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Temeke, John Bwana.
 Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Grace Mathe akisoma risala ya Shirika hilo kwa mgeni rasmi.
 Mdau Mwajuma Issa akichangia jambo kuhusu masuala ya ukatili wa jinsia hasa matusi wanayofanyiwa na wanaume katika soko hilo.
 Kijana Andrew Kamtu akielezea chanzo cha ukatili wa kijinsia kuwa kinaanzia kwa wazazi wenyewe.
 Ofisa wa EfG, Charles akigawa vitabu vya msaada wa kisherea kuhusu ukatili wa kijinsia.
 Maofisa wa Jeshi la Polisi wa Dawati la Jinsia kutoka Mkoa wa Kipolisi Temeke wakiwa kwenye maadhimisho  hayo.
 Wakina mama wakiserebuka kwenye maadhimisho hayo.
 Maadhimisho yakiendelea.
 Wananchi wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
 Wawezeshaji sheria masokoni wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
 Burudani zikiendelea kutoka kwa kundi la Machozi Theatre Group.
 
 Ngoma ya mganda ikichezwa ikiongozwa na chipukizi kutoka kundi la Machozi Theatre Group.
 Burudani ya Sarakasi hiyo ikifanyika.
 Mwezeshaji Sheria  Kashindye Kapambala akichangia jambo kuhusu ukatili wa jinsia.
 Wanawake wakitembea katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyika katika Soko la Temeke Sterio Dar es Salaam leo. Maadhimisho hayo yaliandaliwa na Shirika la Equality for Growth (EfG)
 Wasanii wa Kikundi cha Sanaa cha Machozi Theatre Group wakitoa burudani kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyika katika Soko la Temeke Sterio Dar es Salaam leo. Maadhimisho hayo yaliandaliwa na Shirika la Equality for Growth (EfG)
Mwezeshaji wa sheria masokoni akichangia jambo kuhusu ukati wa kijinsia masokoni unavyofanyika.
 ……………………………………………………………………………………….
Na Dotto Mwaibale
 
MASHIRIKA yasiyo ya kiserikali yamesaidia kwa kiasi kikubwa kuhamasisha  jamii kuhusu kujua vitendo vya ukatili wa kijinsia hivyo kusaidia kupunguza vitendo hivyo nchini.
 
Hayo yalibainishwa na Ofisa wa Polisi Dawati la Jinsia Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Meshack Mpwaga katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyika Soko la Temeke Dar es Salaam leo mchana yaliyokuwa na kauli mbiu ” Funguka chukua hatua mlinde mtoto apate elimu”
 
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye maadhimisho hayo yaliyoa andaliwa na Shirika la Equality for Growth (EfG), Mpwaga alisema mashirika yasiyo ya kiserikali kwa kiasi kikubwa yameisaidia nchi katika kutoa elimu na kuhamasisha jamii juu ya vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia ambapo uelewa umekuwa mkubwa.
 
“Uelewa kwa jamii kuhusu vitendo hivyo ni mkubwa mno wito wangu jamii iendelee kutoa taarifa polisi pale inapobaini kuwepo kwa vitendo hivyo nasi tutachukua hatua stahiki” alisema Mpwaga.
 
Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Temeke, John Bwana,  ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo ametoa mwito kuwa siku 16 za kupinga ukatili wa jinsia jamii izitumie kuelimishana  na kupambana na ukatili huo wa kijinsia.
 
Alisema ni muhimu sasa jamii kuelimika na kuachana na vitendo vya udhalilishaji sehemu yoyote ili kupata taifa la watu waliostaraabika.
 
Alisema serikali hasa idara ya maendeleo ya jamii imekuwa ikisaidia na taasisi binafsi katika kupiga vita vitendo hivyo vya ukatili wa kijinsia jambo linalosaidia jamii kufanya shughuli za maendeleo kwa uhuru.
 
Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Grace Mathe alisema utafiti uliofanywa na shirika juu ya ukatili dhidi ya wanawake masokoni unaonesha asilimia 90.32 ya wanawake katika sekta isiyo rasmi wanafanyiwa ukatili mara kwa mara wa kingono, kimwili na matusi katika maeneo yao ya kazi.
 
 
Alisema mradi huo unatekelezwa katika wilaya ya Temeke na Ilala ndani ya masoko sita ambayo ni Feri, Kisutu, Mchikichini, Gezaulole, Tabata Muslimu na Temeke Sterio na kuwa umelenga kuwalinda wanawake katika sekta isiyo rasmi hususani wafanyabiashara masokoni dhidi ya ukatili wa kijinsia.
 

Serikali kuendelea kuimarisha Sekta ya Uvuvi

uv1 
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na uvuvi Bi Judith Mhina akifafanua kwa waandishi wa habari kuhusu mradi wa udhibiti wa uvuvi na maendeleo shirikishi Kusini Magharibi mwa bahari ya Hindi “SWIOFISH” leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Bi Fatma Sobo.
uv2 
Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Bw. Silas William akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuwainua wavuvi wadogo hapa nchini ili kushiriki katika kukuza uchumi wa Taifa. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Bi Fatma Sobo.mwisho kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na uvuvi Bi Judith Mhina.
uv3 
Baadhi ya Maafisa kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi wakifuatalia mkutano wa Wizara hiyo na waandishi wa habari uliofanyika leo Jijini Dar es salaam.
uv4 
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia mkutano kati yao na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambao pamoja na mambo mengine ulibainisha kuwa Serikali imejipanga kukomesha uvuvi haramu hapa nchini hasa kwa kutumia mabomu kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais,Wizara ya Mali asili na Utalii, Wizara ya Nishati na Madini,Wizara ya mambo ya Ndani na ile ya Katiba na Sheria.
(Picha na Frank Mvungi-Maelezo)

Rais Dkt. Magufuli atoa siku saba kwa wafanyabiashara wakwepa kodi.

index 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wadau wa Sekta  Binafsi na kuwaahidi kuwapa ushirikiano mkubwa kwani anatambua mchango wao katika ukuaji wa  uchumi na kuwasihi kuwa wazalendo katika suala la utoaji kodi ili kulipeleka taifa katika nchi yenye  uchumi wa Kati Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.(Picha na Hassan Silayo Maelezo)
………………………………………………………………………………………………….
Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli amewapa siku saba kuanzia tarehe 03/12/2015 wafanyabiashara wote ambao waliingiza mizigo yao bila kulipa kodi wakalipe kwani baada ya hapo watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Hayo yamesemwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam na Mheshimiwa Rais katika mkutano wake na wadau wa sekta binafsi alipoamua kufanya mazungumzo nao pamoja na kuwasikiliza maoni yao ikiwa ni sehemu ya ahadi zake katika kipindi cha kampeni za kuomba kura za kiti cha Urais,lengo likiwa ni kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta binafsi.
Mheshimiwa Rais aliendelea kusema kuwa katika kipindi hichi cha miaka mitano amedhamiria kuijenga nchi na watu wasimuelewe vibaya kwa maamuzi anayofanya kwani ni kwania njema ya kuleta maendeleo na siyo ujeuri.
“Tutaangalia namna ya kupunguza utitiri wa ushuru katika bidhaa mbalimbali,mfano katika kipindi cha kampeni niligundua katika Mkoa wa Kagera na Kilimanjaro wanakolima zao la Kahawa,wamekuwa wakitozwa tozo 26 kwa zao hilo na hiyo imechangia kusababisha wafanyabiashara wa zao hilo kufanya biashara haramu ya kupeleka zao hilo kwa magendo kuuza katika nchi jirani”,alisema Mheshiwa Rais Dkt. Magufuli.
Pamoja na hayo Mheshimiwa Dkt.Magufuli amewaahidi wadau wasekta binafsi ushirikiano mkubwa kwani anatambua mchango wao katika kukuza uchumi na pia amewataka wadau hao kuwa wazalendo na kuliacha kukwepa kulipa kodi ili tuweze kujenga taifa lenye maendeleo makubwa ya kiuchumi.
Mheshimiwa Rais Dkt.Magufuli ameendelea kusema kuwa kama kutakuwa na mfayabiashara yeyote atakayetaka kuwekeza na akakwamishwa na mtu aliyechini ya uteuzi wake basi mtu huyo ataondoka kwani sasa ni wakati wa wadau wa sekta binafsi kuanza kuanzisha viwanda mbalimbali vitakavyo toa ajira.
Pamoja na hayo Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli amewapa mawazo ya kibiashara wadau wa sekta binafsi kuanzisha kampuni ya kutenganisha udongo unaotoka kwenye machimbo ya madini,kuanzisha viwanda vya samaki pembezoni mwa bahari pamoja na kutengeneza samani zitokanazo na mazao ya misitu.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) Bw.Regnald Mengi amesema kuwa wako tayari kumpa ushirikiano mkubwa Mheshimiwa Rais katika kuhakikisha uchumi watanzania unakuwa kwa haraka na pia amemuomba mheshimiwa rais kuendelea kukemea masuala ya rushwa pamoja kusaidia kupunguza utitiri wa kodi.
 
John Bukuku 
(johnbukuku@gmail.com)
Displaying TPSF-COUNCIL IKULU.docx.

No comments :

Post a Comment