Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli
akiongea na Viongozi na Wawakilishi wa Umoja wa Sekta Binafsi nchini
(Tanzania Private Sector Foundation – TPSF) katika ukumbi wa mkutano wa
Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 3, 2015. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA
FULLSHANGWE-IKULU) Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli
akiongea na Viongozi na Wawakilishi wa Umoja wa Sekta Binafsi nchini
(Tanzania Private Sector Foundation – TPSF) katika ukumbi wa mkutano wa
Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 3, 2015 PICHA NA IKULU
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli
akiongea Dk Reginand Mengi Mwenyekiti wa Umoja wa Sekta Binafsi nchini
(Tanzania Private Sector Foundation – TPSF) wakati wa mkutano na
wafanyabiashara Ikulu leo.
Dk
Reginand Mengi Mwenyekiti wa Umoja wa Sekta Binafsi nchini (Tanzania
Private Sector Foundation – TPSF) akisoma hotuba yake katika mkutano huo
uliofanyika Ikulu leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya
CRDB Dk. Charles Kimei akitoa salamu zake Kwa Rais Dk John Pombe
Magufuli kwa niaba ya wawakilishi wa Mabenki.
Baadhi ya watendaji kutoka
serikalini wakiwa katika mkutano huo Kulia ni Katubu Mkuu Wizara ya
Habari, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel .
Mkurugenzi Mtendaji wa TSN Bw. Farouqh Baghozah katikati akiwa pamoja na wafanyabiashara wenzake katika mkutano huo.
Mmoja wa wajumbe akitoa shukurani zake katika mkutano huo. kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Irene Isaka, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Shabani Mwinjaka na mfanyabiashara Nicola Angelo wakiwa katika mkutano huo.
Bw. Octavian Mshiu Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya OpenSanit Limited akiwa pamoja na wafanyabiashara
wenzake katika mkutano huo.
Bw. Issa Hango kutoka kampuni ya madawa ya Shelys pamoja na wafanyabiashara mbalimbali wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu Bw. Gerson Msigwa akielezea ratiba ya mkutano huo kabla ya kuanza.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli
akiingia kwenye mkutano huo huku akiwa ameongozana na Katibu Mkuu
Kiongozi Ombeni Sefue.
Lukaza Blog yaleta Tunzo Nyumbani. Asanteni Wasomaji, watembeleaji na Bloggers wenzangu
Mmiliki wa Lukaza Blog, Josephat Lukaza akiwa ameshikilia Tunzo aliyoshinda katika Kipengele cha Blog Bora ya Siasa katika Shindano la African Blogger Awards 2015 lililofanyika nchini Africa Kusini .Tutembelee kwa kufuata link hii http://www.josephatlukaza.com
Shindano
la African Blogger Awards linaloendeshwa na Kampuni ya Webfluential ya
Nchini Afrika Kusini lilianzishwa mnamo mwaka 2014 huku Lukaza Blog
ikishiriki Kwa Mara ya Kwanza na kuibuka kuwa mshindi wa Pili wa Blog
bora ya Kuelimisha kwa mwaka 2014.
Kwa
Awamu ya Pili ya Shindano la African Blogger Awards liliofanyika mwaka
2015 Lukaza Blog pia iliweza kushiriki katika Vipengele vitatu huku
ikiibuka Mshindi katika Kipengele Kimoja tu cha Blog Bora ya Siasa
ambapo ushindi huo ulitangazwa tarehe 5 May 2015 kupitia Kurasa ya
Twitter ya African Blogger Awards.
Katika
Kinyanganyiro hiko Cha African Blogger Awards nilikua nikichuana na
bloggers wengine kutoka Mataifa mbalimbali ya Africa na kuweza
kuwagaragaza na hatimaye kuibuka Mshindi wa Kipengele cha Blog bora ya
Siasa huku mshindi wa Pili akitokea Afrika Kusini.
Uendeshaji
wa Shindano hili ulifanyika kwa kutumia njia ya Kitaalamu zaidi
ijulikano kama Impartial Judgement ambapo hakuna kupiga kura wal kutaja
jina la blog bali ni mfumo wenyewe wa mtandao ndio unaoweza kutoa
majibu.
Ni
mara ya Kwanza kabisa nchini Tanzania Mmiliki wa blog ya Lukaza, ndg
Josephat Lukaza kuweza kuleta tunzo kutoka Kwenye mashindano yanayohusu
blogs ambapo Kwa Tanzania hakuna shindano lililowahi kufanyika Wala
kuandaliwa zaidi ya mashindano kama hayo kufanyika Nchi nyingine
Duniani.
Sisi
Kama Lukaza Blog tunajivunia kuibuka na Ushindi huu ambapo Kiukweli
umetupa changamoto sana na kutuonyesha kuwa kumbe Blog zetu hata nje ya
nchi zinatembelewa na zina wapenzi wengi sana lakini pia imetupa hali ya
kujituma zaidi na zaidi na kuhakikisha tunafanya kile tunachoweza
kuhakikisha tunaipasha Dunia kuhusiana na kile kitokeacho Duniani,
Hususani Tanzania.
Lukaza
Blog imeweza kuandika historia kwa kushinda katika shindano hilo la
Africa Blogger awards na kufanikiwa kuleta Tunzo Nyumbani.
Tunzo
hii iwaendee Wasomaji wangu wote kwa maana bila nyie Lukaza Blog
isingeweza Kunyakua tunzo hii katika Shindano la African Blogger Awards
lililomalizika Mnamo mwezi May 2015 huko Afrika ya Kusini. Lukaza Blog
iliweza Kuibuka Mshindi wa Kwanza katika Kipengele cha Blog Bora ya
Siasa na kuwashinda wapinzani wake ambapo Mshindi wa Pili akiwa ni
Blogger kutoka Afrika Kusini.
Vilevile
Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru sana wafuatiliaji wa Lukaza
Blog kwa sapoti yao kwangu na timu nzima kwa maana Mafanikio haya Madogo
tu yaliyopatikana wao pia wamehusika.
Shukrani
zangu za Dhati kabisa Ziwaendee pia Bloggers Wenzangu Kiukweli
Ushirikiano wao Kwangu napo kumeongeza tija na msukumo wa hali ya juu
katika Kushinda tunzo hii hatimaye Tunzo hii imekuwa sio ya Lukaza Blog
tu bali ni Kwa Tanzania Nzima na Watanzania Wote.
Asanteni
sana na hapa sio mwisho tunaendelea kupambana na Changamoto ambapo sisi
kama Lukaza Blog kwetu changamoto ni nafasi ya mafanikio.
Asanteni
sana Bloggers, Wasomaji, Taasisi za Ndani ya Nchi na Hata Barclays
Africa kwa kuona tija na kutuamini Lukaza Blog Kuweza Kufanya kazi na
Nyinyi kwa Kipindi chote cha Miezi Sita kuanzia July hadi December yote
hii ni njia ya kuelekea Kwenye kilele cha Mafanikio huku Juhudi,
Heshima, Busara na ushirikiano vikitawala kichwa kwangu.
Tunzo
hii ni heshima pia Kwetu Tanzania kwasababu tumeanza kuonyesha Dunia
kuwa na Sisi Tupo tumeanza kwenye Muziki, Filamu na Sasa ni Blogs. Pia
unaweza kututembelea kwa Kubofya hapa
MABONDIA THOMASI MASHALI NA FRANSIC CHEKA WATAMBIANA, KUDUNDANA DESEMBA 25 MOROGORO
Mabondia Fransic Cheka kushoto na
Thomas Mashali wakiangaliana kwa usongo wakati wa kutambulisha mpambano
wao wa Desemba 25 utakaofanyika katika uwanja wa Jamuhuri Morogoro Picha
na SUPER D BOXING NEWS
………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Thomas Mashali wa Dar es
salaam na Fransic Cheka wa Morogoro wamendelea kutambiana kuelekea
mpambano wao wa Desemba 25 utakaofanyika katika uwanja wa Jamuhuri
Morogoro uzito wa kg 76
Akiongea na waandishi wa habari
Mashali amesema kuwa hii ni vita ya Dar na Moro hivyo kawaomba wapenzi
wa mchezo wa masumbwi wa Dar es salaam waweze kuhamia morogoro kwa muda
kwa ajili ya kumsapoti siku hiyo ambayo kwake atakuwa na kibarua kigumu
ambapo atapigana na Cheka mkoani Morogoro
Naye Bondia Cheka alijibu mapigo
hayo kwa kusema siku zote anamweshimu bondia anayetaka mpambano wa
marudiano hata hivyo dozi ya mashali ipo pale pale na nitampiga katika
raundi za awali tu kwa kuwa nipo vizuri na naendelea na mazoezi
Kocha wa Mashali Ramadhani Uhadi
amesema kuwa cheka ni bondia wa kawaida sana hivyo wapenzi waje waone
mchezo mzuri utakaochezwa na Mashali atakavyo msambaratisha Cheka siku
hiyo mjini Morogoro
Naye kocha wa bondia Cheka Bw.
Abdallah Salehe amesema Cheka yupo vizuri sana kwa sasa nimempika
ameshaiva ata kama mpambano utakuwa leo Mashali atapigwa mapema sana
Katika mpambano huo kutakuwa na
mipambano mingine yaUtangulizi itakayowahusisha bondia Ibrahimu Class
‘King Class Mawe’ ambaye atapambana na Twaha Kassimu Kg 63 na Vicent
Mbilinyi Kg 63 atakumbana na Deo Njiku wakati Pius Kazaula Kg 66
atamenyana na Seba Temba mpambano mwingine utawakutanisha mabondia Epson
John Kg 57 na Sadiq Momba na wana dada Lulu Kayage Kg 51 atapambana na
Mwanne Haji kugombania ubingwa wa taifa
Iceland yawezesha TGDC kutafiti Jotoardhi
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja
(katikati), sambamba na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la
Maendeleo la Iceland (ICEIDA), Engilbert Gudmundsson, wakisaini Mkataba
wa Makubaliano utakaowezesha Tanzania kunufaika na msaada wa kiasi cha
Dola za Marekani 1,565,000 kwa ajili ya kupata mtaalam mwelekezi kufanya
tafiti katika maeneo yenye viashiria vya Jotoardhi katika maeneo ya
Luhoi na Kibiti, Mkoa wa Pwani na Kiejo/Mbaka Mkoa wa Mbeya.
Wanaoshuhudia ni Meneja Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe na Afisa
Sheria kutoka Wizara ya Nishati na Madini Yese Malolela.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Iceland (ICEIDA),
Engilbert Gudmundsson, (aliyenyoosha mkono), akieleza jambo wakati wa
kikao cha kusaini wakisaini Mkataba wa Makubaliano utakaowezesha
Tanzania kunufaika na msaada wa kiasi cha Dola za Marekani 1,565,000 kwa
ajili ya kupata mtaalam mwelekezi kufanya tafiti katika maeneo yenye
viashiria vya Jotoardhi katika maeneo ya Luhoi na Kibiti, Mkoa wa Pwani
na Kiejo/Mbaka Mkoa wa Mbeya; kuwajengea uwezo wataalam wa ndani katika
tasnia hiyo ikiwemo pia kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya utafiti wa
nishati hiyo. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na
Madini, Mhandisi Paul Masanja (katikati), wanaoshuhudia ni Meneja
Mipango wa ICEIDA (kushoto), David Bjarnason, kulia ni Wataalam kutoka
Wizara ya Nishati na Madini na Kampuni ya TGDC .
Mkurugenzi
Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe (wa kwanza kulia) akisaini
Mkataba wa Makubaliano sambamba na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Kimataifa la Maendeleo la Iceland (ICEIDA), Engilbert Gudmundsson.
Mkataba huo utawezesha Tanzania kunufaika na msaada wa kiasi cha Dola za
Marekani 1,565,000 kwa ajili ya kupata mtaalam mwelekezi kufanya tafiti
katika maeneo yenye viashiria vya Jotoardhi katika maeneo ya Luhoi na
Kibiti, Mkoa wa Pwani na Kiejo/Mbaka Mkoa wa Mbeya. Vilevile msaada huo
utawezesha pia kuwajengea uwezo wataalam wa ndani katika tasnia hiyo
ikiwemo na kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya utafiti wa nishati hiyo.
Wanaoshuhudia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,
Mhandisi Paul Masanja (katikati), Kamishna Msaidizi wa Nishati
anayeshugulikia Nishati Jadidifu Edward Ishengoma (Wa kwanza kulia) na
Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini na ICEIDA
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Iceland (ICEIDA),
Engilbert Gudmundsson (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini , Mhandisi Paul Masanja (kulia) wakibadilishana
Mkataba wa Makubaliano utakaowezesha Tanzania kunufaika na msaada wa
kiasi cha Dola za Marekani 1,565,000 kwa ajili ya kupata mtaalam
mwelekezi kufanya tafiti katika maeneo yenye viashiria vya Jotoardhi
katika maeneo ya Luhoi na Kibiti, Mkoa wa Pwani na Kiejo/Mbaka Mkoa wa
Mbeya. Vilevile, Mkataba huo utawezesha kuwajengea uwezo wataalam wa
ndani katika tasnia hiyo.
………………………………………………………………………………………………..
Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam
Serikali kupitia Kampuni Tanzu ya Uendelezaji Jotoardhi Tanzania, (TGDC) na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Iceland (ICEIDA), wamesaini Mkataba wa Makubaliano utakaowezesha Tanzania kunufaika na msaada wa kiasi cha Dola za Marekani 1,565,000 kwa ajili ya kupata mtaalam mwelekezi kufanya tafiti katika maeneo yenye viashiria vya Jotoardhi; kuwajengea uwezo wataalam wa ndani katika tasnia hiyo ikiwemo pia kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya utafiti wa nishati hiyo.
Makubaliano hayo yalifikiwa jijini Dar es Salaam, Makao Makuu ya Wizara ya Nishati na Madini, kati ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja na Mkurugenzi Mkuu wa ICEIDA, Engilbert Gudmundsson, ambapo tukio hilo lilishuhudiwa na Meneja Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe, Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Uendelezaji wa Nishati Jadidifu, Edward Ishengoma, baadhi ya Maafisa kutoka TGDC na Wizara ya Nishati na Madini.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Naibu Katibu Mkuu Mhandisi Paul Masanja alisema kuwa, matarajio ya Tanzania ni kuzalisha kiasi cha megawati 200 za umeme unaotokana na nishati ya jotoardhi ifikapo mwaka 2020 ambapo taarifa za awali zinaeleza kuwa, hazina iliyopo kupitia nishati hiyo ina uwezo wa kuzalisha zaidi ya megawati elfu tano za umeme (5,000), kutokana na nishati ya jotoardhi .
Aidha, Mhandisi Masanja aliongeza kuwa, utayari na ushirikiano iliyouonesha nchi ya Iceland kupitia ICEIDA itakuwa kichocheo kikubwa kufikia malengo ya serikali ya kuwa na nishati ya kutosha ya umeme kutoka vyanzo mbalimbali.
“Tuna malengo yetu mengi kupitia nishati hii, utafiti ndio njia itakayotufanya kufikia malengo yetu hivyo, ushirikiano huu ni mwanzo mzuri kwa upande wetu. Nafahamu Iceland mlianzia katika hatua za chini kabisa lakini sasa mko mbali. Naamini uzoefu wenu utatuwezesha kuweza kufika mahali tunapotarajia,” aliongeza Mhandisi Masanja.
Aidha, Masanja aliitaka Kampuni ya TGDC, kuhakikisha inashirikiana vizuri na nchi ya Iceland ikiwemo shirika la ICEIDA kuhakikisha linafuata ushauri mzuri wa kitaalamu unaotolewa na shirika hilo ili kuweza kupata uzoefu, jambo ambalo litawezesha sekta ya jotoadhi nchini kupiga hatua na hivyo kuifanya jotoardhi kuwa chanzo kingine cha nishati ya umeme.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe, alishukuru utayari wa ICEIDA katika kuhakikisha kwamba Tanzania inafikia malengo yake ya kuendeleza nishati hiyo, utayari ambao utasaidia kufanyika kwa tafiti katika maeneo yenye viashiria vya jotoardhi ya Luhoi, na Kibiti, Mkoa wa Pwani.
Vilevile, Mhandisi Njombe alieleza kuwa, kutokana na utafiti utakaofanywa, utawezesha upatikanaji wa takwimu sahihi ambazo zitafungua njia ya kupata msaada zaidi kutoka katika taasisi ambazo zimejikita katika masuala ya zenye uhusiano na nishati ya jotoardhi, jambo ambalo pia litawezesha uendelezaji wa nishati hiyo nchini.
Aidha, Mhandisi Njombe alitumia fursa hiyo pia kueleza hatua mbalimbali ambazo tayari zimefanywa na kampuni hiyo katika kuhakikisha kwamba, jotoardhi inakuwa chanzo kingine cha uzalishaji umeme nchini na kuongeza kuwa, kupitia makubaliano hayo, ICEIDA itawezesha wataalam wa ndani wa TGDC kupata ujuzi na uzoefu utakaowezesha kufanyika kwa tafiti nyingine katika maeneo ya Kiejo/ Mbaka, Mkoa wa Mbeya.
Naye, Mkurugenzi wa ICEIDA, Engilbert Gudmundsson alieleza umuhimu wa nishati hiyo na unafuu wake wa gharama ikilinganishwa na nishati nyingine na kueleza kuwa, asilimia 25 ya umeme unaozalishwa nchini Iceland unatokana na nishati ya jotoardhi.
“Ilituchukua kipindi cha miaka 25 kufikia mafanikio tuliyonayo katika nishati ya jotoardhi. Kutokana na ubobezi huu ni vema kwetu kutoa uzoefu kwa TGDC kuhakikisha inafakia malengo tarajiwa na kwamba jotoardhi inakuwa chanzo kingine cha umeme kwa Tanzania ambao ni rahisi na nafuu,”aliongeza Engilbert.
Jotoardhi ni mojawapo ya chanzo cha nishati kitokanacho na mvuke unaotoka ardhini, hususan katika maeneo yaliyo katika Bonde la Ufa (Rift Valley). Nchi zilizo katika bonde la Ufa (African Rift Geothemal Facility – ARGeo) ni pamoja na Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.
Tayari Tanzania imefanya jitihada kadhaa za kuendeleza Jotoardhi ikiwemo uanzishwaji wa Kampuni ya TGDC, ambayo ni Kampuni Tanzu ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO), iliyoanzishwa mwezi Juni, 2014. TGDC inatajwa kuwa kichocheo muhimu cha uendelezaji wa nishati ya jotoardhi. Aidha, mwishoni mwa mwezi Oktoba hadi mwanzoni mwa Novemba 2014, Tanzania ilikuwa Mwenyeji wa Mkutano wa Tano wa Kimataifa wa Jotoardhi uliofanyika Jijini Arusha.
Mkutano wa Jotoardhi unatajwa kuinufaisha Tanzania katika kuhamasisha matumizi ya nishati jadidifu ili kuchangia upatikanaji wa nishati hiyo nchini; kubadilishana uzoefu na uelewa na wataalamu kutoka nchi mbalimbali duniani; ikiwemo pia kuharakisha uendelezaji wa jotoardhi
Serikali kupitia Kampuni Tanzu ya Uendelezaji Jotoardhi Tanzania, (TGDC) na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Iceland (ICEIDA), wamesaini Mkataba wa Makubaliano utakaowezesha Tanzania kunufaika na msaada wa kiasi cha Dola za Marekani 1,565,000 kwa ajili ya kupata mtaalam mwelekezi kufanya tafiti katika maeneo yenye viashiria vya Jotoardhi; kuwajengea uwezo wataalam wa ndani katika tasnia hiyo ikiwemo pia kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya utafiti wa nishati hiyo.
Makubaliano hayo yalifikiwa jijini Dar es Salaam, Makao Makuu ya Wizara ya Nishati na Madini, kati ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja na Mkurugenzi Mkuu wa ICEIDA, Engilbert Gudmundsson, ambapo tukio hilo lilishuhudiwa na Meneja Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe, Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Uendelezaji wa Nishati Jadidifu, Edward Ishengoma, baadhi ya Maafisa kutoka TGDC na Wizara ya Nishati na Madini.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Naibu Katibu Mkuu Mhandisi Paul Masanja alisema kuwa, matarajio ya Tanzania ni kuzalisha kiasi cha megawati 200 za umeme unaotokana na nishati ya jotoardhi ifikapo mwaka 2020 ambapo taarifa za awali zinaeleza kuwa, hazina iliyopo kupitia nishati hiyo ina uwezo wa kuzalisha zaidi ya megawati elfu tano za umeme (5,000), kutokana na nishati ya jotoardhi .
Aidha, Mhandisi Masanja aliongeza kuwa, utayari na ushirikiano iliyouonesha nchi ya Iceland kupitia ICEIDA itakuwa kichocheo kikubwa kufikia malengo ya serikali ya kuwa na nishati ya kutosha ya umeme kutoka vyanzo mbalimbali.
“Tuna malengo yetu mengi kupitia nishati hii, utafiti ndio njia itakayotufanya kufikia malengo yetu hivyo, ushirikiano huu ni mwanzo mzuri kwa upande wetu. Nafahamu Iceland mlianzia katika hatua za chini kabisa lakini sasa mko mbali. Naamini uzoefu wenu utatuwezesha kuweza kufika mahali tunapotarajia,” aliongeza Mhandisi Masanja.
Aidha, Masanja aliitaka Kampuni ya TGDC, kuhakikisha inashirikiana vizuri na nchi ya Iceland ikiwemo shirika la ICEIDA kuhakikisha linafuata ushauri mzuri wa kitaalamu unaotolewa na shirika hilo ili kuweza kupata uzoefu, jambo ambalo litawezesha sekta ya jotoadhi nchini kupiga hatua na hivyo kuifanya jotoardhi kuwa chanzo kingine cha nishati ya umeme.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe, alishukuru utayari wa ICEIDA katika kuhakikisha kwamba Tanzania inafikia malengo yake ya kuendeleza nishati hiyo, utayari ambao utasaidia kufanyika kwa tafiti katika maeneo yenye viashiria vya jotoardhi ya Luhoi, na Kibiti, Mkoa wa Pwani.
Vilevile, Mhandisi Njombe alieleza kuwa, kutokana na utafiti utakaofanywa, utawezesha upatikanaji wa takwimu sahihi ambazo zitafungua njia ya kupata msaada zaidi kutoka katika taasisi ambazo zimejikita katika masuala ya zenye uhusiano na nishati ya jotoardhi, jambo ambalo pia litawezesha uendelezaji wa nishati hiyo nchini.
Aidha, Mhandisi Njombe alitumia fursa hiyo pia kueleza hatua mbalimbali ambazo tayari zimefanywa na kampuni hiyo katika kuhakikisha kwamba, jotoardhi inakuwa chanzo kingine cha uzalishaji umeme nchini na kuongeza kuwa, kupitia makubaliano hayo, ICEIDA itawezesha wataalam wa ndani wa TGDC kupata ujuzi na uzoefu utakaowezesha kufanyika kwa tafiti nyingine katika maeneo ya Kiejo/ Mbaka, Mkoa wa Mbeya.
Naye, Mkurugenzi wa ICEIDA, Engilbert Gudmundsson alieleza umuhimu wa nishati hiyo na unafuu wake wa gharama ikilinganishwa na nishati nyingine na kueleza kuwa, asilimia 25 ya umeme unaozalishwa nchini Iceland unatokana na nishati ya jotoardhi.
“Ilituchukua kipindi cha miaka 25 kufikia mafanikio tuliyonayo katika nishati ya jotoardhi. Kutokana na ubobezi huu ni vema kwetu kutoa uzoefu kwa TGDC kuhakikisha inafakia malengo tarajiwa na kwamba jotoardhi inakuwa chanzo kingine cha umeme kwa Tanzania ambao ni rahisi na nafuu,”aliongeza Engilbert.
Jotoardhi ni mojawapo ya chanzo cha nishati kitokanacho na mvuke unaotoka ardhini, hususan katika maeneo yaliyo katika Bonde la Ufa (Rift Valley). Nchi zilizo katika bonde la Ufa (African Rift Geothemal Facility – ARGeo) ni pamoja na Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.
Tayari Tanzania imefanya jitihada kadhaa za kuendeleza Jotoardhi ikiwemo uanzishwaji wa Kampuni ya TGDC, ambayo ni Kampuni Tanzu ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO), iliyoanzishwa mwezi Juni, 2014. TGDC inatajwa kuwa kichocheo muhimu cha uendelezaji wa nishati ya jotoardhi. Aidha, mwishoni mwa mwezi Oktoba hadi mwanzoni mwa Novemba 2014, Tanzania ilikuwa Mwenyeji wa Mkutano wa Tano wa Kimataifa wa Jotoardhi uliofanyika Jijini Arusha.
Mkutano wa Jotoardhi unatajwa kuinufaisha Tanzania katika kuhamasisha matumizi ya nishati jadidifu ili kuchangia upatikanaji wa nishati hiyo nchini; kubadilishana uzoefu na uelewa na wataalamu kutoka nchi mbalimbali duniani; ikiwemo pia kuharakisha uendelezaji wa jotoardhi
TAZARA yapokea mabehewa 18 na vichwa 4 kutoka Serikali ya Watu wa China
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaabani Mwinjaka akipanda kwenye moja
ya vichwa 4 vya treni ya Tazara vilivyotolewa na Serikali ya China.
Mwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing akizungumza kabla ya makabidhiano
Balozi wa Zambia nchini Tanzania Judith Kapijimpanga akizungumzia umuhimu wa reli ya TAZARA kwa Tanzania na Zambia.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaabani Mwinjaka akizungumzia mustakbali wa TAZAMA katika kujenga uchumi wa Tanzania.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Mamlaka ya Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) Ronald Phiri
akibadilishan hati za makabidhiano ya mabehewa 18 na vichwa 4 vya treni
na Makamu wa Rais wa CCECC kutoka Serikali ya Watu wa China Lin
Zhiyong.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaabani Mwinjaka (katikati) akikata
utepe pamoja na Balozi wa Zambia nchini Tanzania Judith Kapijimpanga
(kushoto) na Mwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania, wakikata
utepe kuashiria kukabidhiwa kwa kwa mabehewa 18 na vichwa 4 kutoka
Serikali ya China.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaabani Mwinjaka na Balozi wa Zambia
nchini Tanzania Judith Kapijimpanga, wakielekea kupanda kwenye treni ya
kichwa na mabehewa mapya ya TAZARA.
Moja ya mabehewa mapya
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaabani Mwinjaka na Balozi wa Zambia
nchini Tanzania Judith Kapijimpanga (kulia) wakibadilishana mawazo
wakiwa ndani ya sehemu ya kulia chakula iliyomo kwenye moja ya behewa
jipya.Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji TAZARA, Ronald Phiri na Mwakilishi
wa Balozi wa China.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaabani Mwinjaka na Balozi wa Zambia
nchini Tanzania Judith Kapijimpanga, wakiteremka kutoka kwenye moja ya
behewa jipya baada ya kusafiri nalo kwa dakika kumi kufanyia majaribio.
Moja ya kichwa kipya na mabahewa 18 mapya yaliyokabidhiwa kwa TAZARA.
Baadhi
ya maafisa kutoka Serikali ya Watu wa China na wafanyakazi wa Mamlaka
ya Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA), wakishuhudia utiaji saini wa
makabidhiano ya mabehewa 18 na vichwa 4 kutoka Serikali ya Watu wa
China.
Picha na Hussein Makame-MAELEZO
…………………………………………………………………………………………………………
Picha na Hussein Makame-MAELEZO
…………………………………………………………………………………………………………
TGDC yatarajia kuzalisha umeme Megawati 200 ifikapo 2020.
Meneja
Mkuu wa Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC),
Mhandisi Boniface Njombe akichangia mada wakati wa Warsha ya siku mbili
inayofanyika Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka
Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia
njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo
pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo
katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika
yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la
Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha
Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi
pamoja na Indonesia.
Mkurugenzi
wa Mipango na Maendeleo ya Biashara wa Shirika la Uendelezaji wa
Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Bwana Kato Kabaka akitoa mada
wakati wa Warsha ya siku mbili inayofanyika Jijini Dar es Salaam
inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia
masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika
kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji wa huduma tofauti
zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika la TGDC nchini
Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya
Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la
Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi,
TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia.
Mtaalamu
wa masuala ya nishati toka Benki Kuu ya Dunia (ESMAP) Bwana Thrainn
Fridriksson (aliyesimama mbele) akitoa mada wakati wa Warsha ya siku
mbili inayofanyika Jijini Dar es Salaam inayowakutanisha wadau kutoka
Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia
njia zilizotumiwa na baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo
pamoja na uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo
katika kulisaidia shirika la TGDC nchini Tanzania, mashirika
yaliyohudhuria warsha hiyo ni yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la
Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha
Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi
pamoja na Indonesia.
Mtaalam
wa masuala ya nishati ya jotoardhi toka Shirika la Pertamina Geothermal
Energy la nchini Indonesia Bwana Hendrik Kurniawan Sinaga (kulia)
akitoa mada wakati wa Warsha ya siku mbili inayofanyika Jijini Dar es
Salaam inayowakutanisha wadau kutoka Mashirika mbalimbali
yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi kujadilia njia zilizotumiwa na
baadhi ya mashirika kufanikiwa kupata nishati hiyo pamoja na uanishaji
wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo katika kulisaidia shirika
la TGDC nchini Tanzania, mashirika yaliyohudhuria warsha hiyo ni
yakiwemo ya Benki ya Dunia (ESMAP), GDC la Kenya, JICA la Japan, BGR la
Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha Umoja wa Mataifa kinachofundisha
nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi pamoja na Indonesia. Kuhsoto ni
Mtaalam mwenzie wa masuala hayo Bwana Agus Zuhro.
……………………………………………………………………………………………………………..
Na Benedict Liwenga, Maelezo.
TGDC imepewa
lengo na Serikali la kuhakikisha kuwa inazalisha umeme wa Megawati 200
na kuuingiza katika gridi ya Taifa kufikia mwaka 2020.
Kauli hiyo
imetolewa jana na Meneja Mkuu wa Shirika la Uendelezaji Nishati ya
Jotoardhi Tanzania (TGDC) Mhandisi Boniface Njombe wakati wa warsha ya
siku mbili iliyofanyika Jijini Dar es Salaam ambayo iliwakutanisha wadau
kutoka Mashirika mbalimbali yanayoshughulikia masuala ya jotoardhi.
Mhandisi
Njombe alisema kuwa warsha hiyo ina lengo la kujadili njia mbalimbali
zilizotumiwa na baadhi ya mashirika hayo hadi kufanikiwa kupata nishati
hiyo ikiwemo uanishaji wa huduma tofauti zifanywazo na mashirika hayo
katika kulisaidia shirika la TGDC.
“Matokeo ya
warsha hii tuliyoifanya tumeweza kuwasiliana na wenzetu wa Benki ya Duni
(ESMAP) kwa kukusanya wataalam toka taasisi mbalimbali pamoja na
Mashirika mbalimbali ambayo yamewahi kufanya kazi hii ya utafutaji wa
nishati ya jotoardhi na lengo letu ni kutaka kufahamu njia ambazo
wenzetu walizitumia mpaka kufanikiwa ili na sisi tupate kujifunza”,
alisema Njombe.
Aidha,
aliongeza kuwa warsha hiyo itawezesha rasilimali chache zilizopo ziweze
kutumika ipasavyo katika kuleta matokeo ambayo TGDC inatarajia kuyapata
ili kuhakikisha kuwa lengo la upatikanaji wa nishati hiyo linafikiwa.
Sambamba na
warsha hiyo TGDC kupitia Wizara ya Nishati na Madini wametiliana saini
Mkataba wa makubaliano na Shirika linaloshughulikia nishati ya Jotoardhi
la nchini Iceland (ICEIDA) utakaoisadia Tanzania kupatiwa vifaa
mbalimbali vitakavyotumika katika maeneo ambayo jotoardhi inasadikiwa
kupatikana.
Utiaji saini
wa mkataba huo ulifanywa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na
Madini, Mhandisi Paul Masanja na kwa upande wa nchi ya Iceland ulifanywa
na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la ICEIDA Bwana Engilbert Gudmundsson
ukushuhudiwa na Meneja Mkuu wa Shirika la Uendelezaji Nishati ya
Jotoardhi Tanzania (TGDC) Mhandisi Boniface Njombe na Wanasheria.
Akiongea mara
baada ya utiaji saini wa mkataba huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja alilishukuru shirika la ICEIDA
la nchini Iceland kwa mchango wao mkubwa wa kukubali kulisadia shirika
la TGDC ili kuhakikisha kuwa nishati hiyo inapatikana.
Naye
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la ICEIDA Bwana Engilbert Gudmundsson
ameahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza nishati
hiyo kwa kuendelea kutoa msaada wa kiufundi na vifaa vinavyotumika
katika utafutaji na uchimbaji wa nishati hiyo.
Warsha hiyo
ilihusisha wadau mbalimbali wakiwemo watu wa Benki ya Dunia (ESMAP), GDC
la Kenya, JICA la Japan, BGR la Ujerumani, ICEIDA la Iceland, Chuo cha
Umoja wa Mataifa kinachofundisha nishati ya Jotoardhi, TNO la Uholanzi
pamoja na Indonesia kwani hawa wote wameweza kufanikiwa kuipata nishati
hiyo, hivyo watatoa mchango mkubwa kuliwezesha shirika la TGDC kupata
mafanikio na hatimaye nishati hiyo kuweza kupatikana.
TGDC NI
Shirika Tanzu la Tanesco lililoanzishwa Desemba 2013 na kuanza rasmi
kufanya kazi zake mwezi Julai 2014 ili kuharakisha upatikanaji wa
nishati ya jotoardhi nchini.
MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA AFANYA ZIARA SOKO KUU SHINYANGA,MAZINGIRA YA SOKO YANATISHA
Desemba
02,2015- Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameendelea na
ziara za kushtukiza kwenye maeneo ambayo ni kero katika wilaya
hiyo.Ilikuwa majira ya saa tano asubuhi,mkuu huyo wa wilaya akaabukia
katika soko kuu la manispaa ya Shinyanga lililojengwa kabla ya uhuru wa
Tanganyika..Ikawa faraja kwa Wafanyabiashara wa soko hilo waliodai kwa
kipindi kirefu wamekuwa wakiilalamikia halmashauri ya manispaa kutokana
na kushindwa kulifanyia ukarabati soko hilo.Akiwa katika soko hilo
Josephine Matiro amesikiliza kero nyingi kutoka kwa wafanyabiashara hao
ikiwemo ukosefu wa mitaro,kalo la maji,uchafu sokoni.Mwandishi
mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo eneo la
tukio..Anatusimulia kwa picha 40 kilichojiri mwanzo hado mwisho..Tazama
hapa chini
UN, SERIKALI ZATAKA VIJANA KUONGOZA KATIKA KUKABILI MABADILIKO TABIA NCHI SINGIDA
Mkuu
wa wilaya ya Ikungi, Chigulu Charles akitoa neno la ukaribisho kwa
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa
Singida, Dkt. Parseko Kone katika ziara ya kukagua miradi inayofadhiliwa
na Mashirika ya Umoja wa Mataifa mkoani Singida.
Na Modewjiblog team, Singida
MRATIBU
wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi mkazi wa Shirika
la Mipango ya Maendeleola umoja huo (UNDP) Bw.Alvaro Rodriguez, amezuru
mradi wa ufugaji nyuki uliopo Ikungi mkoani Singida.
Katika
Ziara hiyo kwenye mradi unaofadhiliwa na UNDP, Mratibu huyo aliambatana
na Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone, na Ofisa wa Mambo ya Nje
kutoka Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa wizara ya Mambo ya Nchi za
Nje, Bi. Maulidah Hassan.
Viongozi
hao walifika katika mradi huo kuangalia mafanikio ya mradi huo
unaotekelezwa chini ya mpango wa miaka mitano wa Msaada wa Maendeleo wa
Umoja wa Mataifa, (UNDAP).
Mradi huo uliofadhiliwa na UNDP kwa thamani ya Shilingi milioni 224 umewanufaisha wafugaji 2,000 huku wanawake wakiwa ni 1,100.
Mradi huo ulianza kutekelezwa kuanzia mwaka 2013 na 2014 umelenga kuendeleza shughuli za ufugaji nyuki wilayani Ikungi.
Aidha
mradi huo umelenga kupunguza umaskini kutunza mazingira kwa njia ya
uragibishi na kufunza wananchi kuhusu suala la ufugaji nyuki na utunzaji
wa mazingira.
Kutokana
na mradi huo, fursa za ajira zilitengenezwa, hasa vijana wa kijijini,
kuwepo na eneo la kisasa la kutengeneza mizinga ya nyuki na uchomaji
moto uliokuwa unafanywa katika misitu ukapungua sana.
Akizungumza
katika eneo la mradi Bw. Rodriguez, aliusifu utawala wa mkoa wa Singida
kwa kufanyakazi na UNDP kwa lengo la kujenga uwezo kwa wananchi na
wakati huo huo kutunza mazingira.
Mwakilishi
wa Mratibu Mkuu wa Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI)
ya wilayani Ikungi, inayosimamia mradi wa ufugaji nyuki kisasa, Boniface
Mathew akitoa maelezo ya mradi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja
wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro
Rodriguez. Pamoja na mambo mengine Shirika la Maendeleo la Umoja wa
Mataifa UNDP limeshiriki katika ufadhili wa utengenezaji wa mizinga bora
pamoja na kutoa semina mbalimbali kwa wafugaji nyuki uliogharimu kiasi
cha Shilingi milioni 224 hadi sasa.
“Ninafuraha
sana kuona matokeo mema ya mradi huu; ni lengo letu kutunza mazingira
huku tukifaidika na uhifadhi huo. Mafanikio haya yanastahili kuigwa na
wengine,” alisema Rodriguez akiongeza kuwa wanawake walifaidika sana na
mradi huu kiasi cha kustahili kufanyiwa kazi katika eneo jingine.
Mkuu
wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone alisema mradi wa UNDP una matokeo
yenye tija kubwa na kuwataka waliofadhiliwa kutumika kufunza jamii
nyingine umuhimu wa ufugaji na hifadhi ya misitu.
“leo
tunashuhudia ufugaji nyuki wa kisasa ambao umebadilisha sekta ya ufugaji
nyuki, tija katika ufugaji huu imeongezeka maradufu. Hiyo imesaidia
kaya zaidi ya 1000 kupata kipato cha kukabiliana na umaskini.” Alisema
Mkuu wa mkoa.
Aidha
alisema kwamba wafugaji nyuki wameweza kuwa pamoja na kujipatia asali
na mazao mengine kutokana na shughuli ya ufugaji nyuki kama nta, sumu ya
nyuki, uchavuaji na kadhalika.
Mwakilishi
wa Mratibu Mkuu wa Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI)
ya wilayani Ikungi, Boniface Mathew (kulia) akikabidhi taarifa ya mradi
kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa
Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Kutokana
na shughuli hizo za ufugaji zaidi ya fursa 2,500 za ajira
zilitengenezwa.nafasi hizo ni kama za mfugaji, wachongaji mizinga, wauza
asali, wasafirishaji na wachakati wa asali.
Wilaya ya Ikungi imejaliwa kuwa na misitu ya Miombo na Minanga ambayo ni chanzo kizuri cha chavua.
Mradi wa ufugaji nyuki Ikungi umelenga kufungua njia zote za uzalishaji
asali na kupiga vita umaskini kwa kuanzisha fursa za ajira za
kujitegemea.
Mwakilishi huyo wa UNDP na Mkuu wa mkoa pia walitembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ambayo ipo katika awamu ya mwisho ya ujenzi.
Itakuwa ni moja ya hospitali kubwa itakayohudumia mikoa mitano katika ukanda wa kati.
Katika mazungumzo yake Mratibu wa UN alimpongeza Mkuu wa mkoa kwa juhudi zake za kuhudumia wanawake waume na watoto wa Tanzania.
Baadhi
ya mizinga ya kisasa iliyofadhiliwa na UNDP ikiwa kwenye karakana ya
kutengeneza mizinga ya nyuki tayari kugawiwa kwa vikundi mbalimbali vya
wanawake na vijana iliyopo kwenye Taasisi ya Kijamii ya Fursa za
Kimaendeleo (Fu-DI) ya wilayani Ikungi.
Mwakilishi
wa Mratibu Mkuu wa Taasisi ya Kijamii ya Fursa za Kimaendeleo (Fu-DI)
ya wilayani Ikungi, Boniface Mathew akimwonyesha mizinga ya kisasa ya
ufugaji nyuki Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
(katikati). Kushoto ni “Programme Assistant- Global Environmental
Facility Small Grant”, UNDP, Stella Zaa.
Mwanakikundi
cha Uaminifu kinachojihusisha na ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa, Juma
Simbu akikabidhi taarifa ya kikundi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini,
Alvaro Rodriguez.
Sehemu ya eneo la shamba darasa la kuzalisha makundi ya nyuki lilipo katika kijiji cha Mahambe tarafa ya Ikungi mkoani Singida.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akisaidiana na wanakikundi cha
Uaminifu kinachojihusisha na ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa
kupandisha moja kati ya mizinga iliyofadhiliwa na UNDP katika shamba
darasa la kuzalisha makundi ya nyuki lilipo katika kijiji cha Mahambe
tarafa ya Ikungi mkoani Singida.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez pamoja na Mkuu wa Mkoa wa
Singida, Dkt. Parseko Kone wakipandisha moja kati ya mizinga
iliyofadhiliwa na UNDP kwenye shamba hilo.Kwa matukio zaidi bofya hapa
Tanzania yawa mwenyeji wa mkutano wa kumi wa SADC
Na Immaculate Makilika -MAELEZO
Tanzania imekuwa mwenyeji wa mkutano wa kumi wa nchi za
Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wa uhamaji kutoka
mfumo wa analogia kwenda digitali, imepata heshima hiyo baada ya
kuonekana ni kati ya nchi zilizofanya vizuri katika uhamaji wa analogia
kwenda digitali.
Mkutano huo wenye kauli mbiu
inayosema ‘Digital Broadcasting Dynamics: Building a suistainable
Future’ unaofanyika kuanzia tarehe 2 hadi 3 Desemba, 2015 jijini Dar es
salaam, una lengo la kubadilishana uzoefu kwa nchi wananchama wa SADC
ambazo zimepiga hatua katika uhamaji wa mfumo wa analogia kwenda
digitali .
Katibu Mkuu wa Wizara ya
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Dkt. Yamungu Kayandabila alitoa
shukrani kwa niaba ya Serikali ya Tanzania kwa heshima iliyopewa na
sekretarieti ya SADC kwa kuifanya Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huu
muhimu.
‘Serikali ya Tanzania imewekeza
kwa kiasi kikubwa katika miundombinu ya teknolojia ya habari na
mawasiliano (TEHAMA) na imetumia mkongo wa Taifa wa mawasiliano
(National ICT Broadband Backbone – NICTBB) uliopo zaidi ya kilomita
7,560 ambao umeenea katika makao makuu ya miji yote nchi nzima, ikiwa ni
pamoja na mikongo 4 ya kimataifa inayopita baharini na hivyo tuna
kila sababu ya kutarajia mafanikio makubwa ya TEHAMA katika kipindi cha
miaka mitano ijayo’ alisema Bwana. Kayandabila
Tanzania ilifanikiwa kumaliza
uhamaji wa mfumo wa analogia kwenda digitali katika miji 20, tarehe 30
mwezi aprili, 2015, ikiwa ni kabla ya muda wa makubaliano ya
‘International Telecommunications Union’( ITU) , yaliyozitaka nchi
kuhama kabla ya kufikia tarehe 17 Juni,2015.
Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka
ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Ally Y. Simba alisema pamoja na
changamoto mbalimbali kama gharama kubwa za huduma hizi, zinazozikuimba
nchi katika uhamaji wa mfumo wa analogia kwenda digitali, katika nchi
zilizo kusini mwa jangwa la Sahara Tanzania imekuwa kati kati ya nchi 3
zilizofanya vizuri ikitanguliwa na Rwanda pamoja na Visiwa vya
Shelisheli.
Alitaja baadhi ya sababu
zilizosadia Tanzania kufikia hatua hiyo ambazo ni utayari wa viongozi
na ushirikishwaji wa wadau katika kila hatua ya mchakato.
Aidha, faida za kuhamia katika
mfumo wa digitali ni pamoja na fursa za uandaji wa maudhui, namna ya
kuwasilisha maudhuui hayo kwa hadhira, vile vile mfumo huo umesaidia
kufikisha maudhui kwa hadhira kupitia njia mbalimbali za mawasiliano,
ambazo zinaweza kuleta mchango katika sekta za kijamii na uchumi.
Nchi wanachama wa SADC
walioshiriki katika mkutano huo ni pamoja na Zimbabwe, Tanzania,
Botswana, Namibia, Afrika ya Kusini, Malawi, Visiwa vya Shelisheli,
Zambia, Lesotho na Swaziland. Ambapo washiriki walipata fursa ya
kujadiliana na kuuliza maswali juu ya mada zilizowasilishwa katika
mkutano huo uliojumuisha pia wadau wa sekta ya utangazaji nchini. Aidha,
mkutano huu ni matokeo ya mkutano wa 9 wa ‘SADC Digital Terrestrial
Television Forum ’uliofanyika mwezi Juni, 2015 nchini Namibia.
UGONJWA WA MTUHUMIWA WAKWAMISHA KUENDELEA KWA KESI
Mahmoud Ahmad,Arusha
Mahakama ya hakimu mkazi mkoani Arusha mwishoni mwa
wiki iliyopita ililazimika kuhairisha kesi ya kuidhinisha jumla ya
kiasi cha sh,24 milioni kinyume na sheria inayomkabili mkurugenzi mkuu
wa kituo cha zana za kilimo na teknolojia vijijini(Carmatec),Elfariji
Makongoro na wenzake wawili hadi Januari 18 mwakani baada ya upande
mshtakiwa kudai Makongoro ni mgonjwa.
Kesi hiyo ilihairishwa mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo
mkoani Arusha,Patricia Kisinda baada ya wakili wa mshtakiwa Arnold
Laiser kuiambia mahakama hiyo kwamba Makongoro bado ni mgonjwa na
anaendelea kupata matibabu.
Wakili huyo aliiomba mahakama hiyo kuhairisha kesi hiyo nambari
1195 ya mwaka 2015 kwasababu mteja wake bado ni mgonjwa na anaendelea
kupata matibabu katika hospitali ya Regency iliyopo jijini Dar es
salaam.
Kutokana na hali hiyo kesi hiyo ilikuwa isikilizwe Oktoba 12 na
20 mwaka huu mfululizo lakini kutokana na sababu hiyo hakimu alilazimika
kuiharisha hadi Januari 18 mwaka ujao.
Hatahivyo,kabla ya kuiharisha kesi hiyo hakimu Kisinda alimtaka
wakili wa mtuhumiwa huyo kuwasilisha vyeti vya ugonjwa wa mtuhumiwa
mahakamani hapo ifikapo Januari 18 mwakani wakati kesi hiyo
itakapoletwa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa.
Awali,mwendesha mashtaka kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana
na Rushwa(Takukuru) mkoani Arusha ,Rehema Mteta aliiambia mahakama hiyo
kwamba Makongoro akiwa kama mkurugenzi wa kituo hicho na wenzake wawili
mnamo Juni 26 mwaka 2012 waliipatia zabuni karakana ya Mbilinyi Auto ya
jijini Arusha bila kufuata sheria za zabuni.
Mteta,alisema kwamba Makongoro ambaye ni mkurugenzi wa kituo
hicho,Absolom Nko ambaye ni afisa manunuzi sanjari na Pythias Ntella
ambaye ni kaimu ofisa usafirishaji wa kituo hicho walitumia madaraka ya
kinyume na sheria kwa kuipatia zabuni karakana hiyo kukarabati gari aina
ya Toyota Landcruiser Hardtop mali ya serikali kwa kiasi cha sh,24
milioni.
MKOA WA MBEYA WATEKELEZA AGIZO LA RAIS KUHUSU UNUNUZI WA VIFAA TIBA KWA FEDHA ZA MAADHIMISHO YA UKIMWI
Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mbeya Ndugu Stella Kategile akitoa taarifa ya UKIMWI kwa mkoa wa Mbeya kwa ujumla wake. |
Dawa pamoja na vifaa tiba vilivyo nunuliwa kutoka katika fedha zilizo changishwa na wadau kwa ajili ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani. |
Na Mwandishi wetu,Mbeya
Siku
chache mara baada ya Serikali kutangaza kuahirisha shughuli za
maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani ambayo yalipangwa kufanyika Kitaifa
mkoani Singida mwaka huu na badala yake pesa hizo zikatumike kununua Vifaa tiba
pamoja na Dawa za ARV hatimaye agizo hilo limetekelezwa na uongozi wa Mkoa wa
Mbeya .
chache mara baada ya Serikali kutangaza kuahirisha shughuli za
maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani ambayo yalipangwa kufanyika Kitaifa
mkoani Singida mwaka huu na badala yake pesa hizo zikatumike kununua Vifaa tiba
pamoja na Dawa za ARV hatimaye agizo hilo limetekelezwa na uongozi wa Mkoa wa
Mbeya .
Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbasi kandoro, amesema
pesa zilizokusanywa na kamati ya inayoratibu maadhimisho hayo kwa mkoa wa mbeya
ni kiasi cha shilingi milioni 3.5 ambazo
zimetumika kwa ajili ya kutekeleza agizo hilo la rais Magufuli kwa ununuzi wa
ununuzi wa vifaa tiba pamoja na dawa hizo za ARV.
pesa zilizokusanywa na kamati ya inayoratibu maadhimisho hayo kwa mkoa wa mbeya
ni kiasi cha shilingi milioni 3.5 ambazo
zimetumika kwa ajili ya kutekeleza agizo hilo la rais Magufuli kwa ununuzi wa
ununuzi wa vifaa tiba pamoja na dawa hizo za ARV.
Amesema, kiasi hicho cha fedha kilipatikana
baada ya wahisani mbalimbali kuchangia na kwamba kiongozi huyo amewataka wadau
ambao hawakupata fursa ya kuchangia waendelee kwani mahitaji bado ni makubwa
hususani katika suala nzima la chakula.
baada ya wahisani mbalimbali kuchangia na kwamba kiongozi huyo amewataka wadau
ambao hawakupata fursa ya kuchangia waendelee kwani mahitaji bado ni makubwa
hususani katika suala nzima la chakula.
Aidha, Mkuu huyo alitoa shukrani za pekee kwa
kanisa la Anglikan mkoa wa Mbeya kwa kuchangia boksi saba za kondomu na
kuwataka wananchi kuendelea kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya ugonjwa
wa ukimwi kwani hali ya takwimu bado si nzuri kwa Mkoa wa Mbeya.
kanisa la Anglikan mkoa wa Mbeya kwa kuchangia boksi saba za kondomu na
kuwataka wananchi kuendelea kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya ugonjwa
wa ukimwi kwani hali ya takwimu bado si nzuri kwa Mkoa wa Mbeya.
No comments :
Post a Comment