UONGOZI wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, chini ya Mkurugenzi wake Mkuu, Bw. Adam Mayingu, umefanya ziara ya kutembelea vyombo vya habari hapa jijini Dar es Salaam, ili kuimarisha ushirikiano miongozi mwa taasisi hiyo ya umma na waandishi wa habari.
Bw.
Mayingu na timu yake walitembelea vyombo vya habari vya kampuni ya Mwananchi
Communications Limited, MCL, yenye makao yake makuu, barabara ya Mandela eneo
la Tabata reline, na kampuni ya Business Times, wachapishaji wa gazeti la
Majira, yenye makao yake makuu eneo la Gerezani.
Pichani
Bw. Mayingu (kulia), akimpatia zawadi Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, Bw. Francis
Nanai, mara baada ya mazungumzo baina ya uongozi wa PSPF, na ule wa MCL. (Picha
zote na Abdul Njaidi wa PSPF)
Meneja
Mkuu wa
Business Times Limited Bw. Aga Mbuguni,(kushoto)
akipokea machapisho mbalimbali ya Mfuko wa Pensheni wa PSPF
kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo Bw. Adam Mayingu baada kikao cha
watendaji wakuu wataasisi hizo kilichofanyika Makao Makuuya
Business Timesjijini Dar es Salaam.
Bw. Mayingu (katikati) akiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa MCL
Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa PSPF, Bw.
Gabriel Silayo (wanne kushoto) akisisitiza jambo katika kikao kazi kilichowakutanisha watendaji wa kuu wa Mfuko wa Pensheni wa
PSPF na Business Times.
Wadau waliohudhuria uzinduzi huo wakisikiliza kwa mageni hotuba zilizokuwa zikitolewa. |
Mgeni rasmi, mkuu wa mkoa wa Morogoro Dr Rajab Rutengwe akisalimiana na mkurugenzi wa Tigo kanda ya Mashariki Goodluck Charles, katikati ni Afisa wa maendeleo ya masoko Shavkat Berdiev. |
Wafanyakazi wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Suleiman Bushagama (Kushoto) Mutalemwa (katikati) na Ben Mponzi (kulia) wakibadilishana mawazo wakati wa uzinduzi huo. |
Wafanyakazi
wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Suleiman Bushagama (Kushoto)
Mutalemwa (katikati) na Ben Mponzi (kulia) wakibadilishana mawazo wakati
wa uzinduzi huo.MAGEREZA KUHAMASISHA UTALII WA NDANI KATIKA MIAKA 54 YA UHURU WA TANGANYIKA
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Magereza John Minja akiwasilia katiki viwanja vya
Magereza Mkoa wa Kilimanjaro kwa ajili ya hafla ya kukabishi bendera kwa
watumishi 39 wa Jehi hilo wanaotarajia kuadhimisha miaka 54 ya Uhuru wa
Tanganyika kwa kupanda Mlima Kilimanjaro.
Kamishna
Jenerali wa Magereza John Minja akikabidhi bendera ya Magereza kwa
kiongozi wa Msafara Kamishna Msaidizi wa Magereza Alexander Mmasy leo
tarehe 04/12/2015 wakiwa wanajiandaa kupanda Mlima tarehe 06/12/2015 ili
ifikapo tarehe 09 siku ya Uhuru wa Tanganyika wawe kileleni
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza John Minja akitoa nasaha kwa wapanda mlima wa Jeshi la Magereza (Hawapo pichani)
Baadhi
ya wadau wa Magereza Utalii Klabu walio tayari kupanda Mlima
Kilimanjaro wakisikiliza kwa makini nasaha za Kamishna Jenerali wa
Magereza John Minja katika hafla ya kukabidhiwa bendera ya Jeshi hilo
kuipeleka katika Kilele cha Mlima huo.
Baadhi
ya wadau wa Magereza Utalii Klabu walio tayari kupanda Mlima
Kilimanjaro wakiimba nyimbo za hamasa baada ya kupokea bendera kutoka
kwa Kamishna Jenerali wa Magereza John Minja katika hafla ya kukabidhiwa
bendera ya Jeshi hilo kuipeleka katika Kilele cha Mlima huo.
Wapanda
Mlima Kilimanjaro wa Jeshi la Magereza wakiwa katika picha ya pamoja na
Mkuu wa Jeshi la Magereza John Minja (Katikati),wa tatu kulia ni Mkuu
wa Magereza Mkoa wa Arusha SACP Hamis Nkubasi, na Mkuu wa Magereza Mkoa
wa Kilimanjaro SACP Venant Kayombo, wa tatu kushoto ni Mnadhimu Mkuu wa
Magereza Mkoa
Wadau
wa Magereza Utalii Klabu wakiwa katika mazoezi mbalimbali ya kukimbia
na kutembea katika viunga vya mji wa Moshi ikiwa ni maandalizi ya
kuelekea katika kilele cha Mlima Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya
kuadhimisha miaka 54 ya Uhuru wa Tanganyika sambamba na kuamasisha
utalii wa ndani.
Picha zote na Mrakibu Msaidizi wa Magereza Deodatus Kazinja na Koplo Mfaume Abdalah wa Jeshi la Magereza
……………………………………………………………………………………………..
Na Deodatus Kazinja
Katika kuadhimisha miaka 54 ya uhuru wa Tanganyika tarehe 9 Desemba watumishi wapatao 39 Jeshi la Magereza wakiwa katika uwiano wa wanaume 30 na wanawake 9 wataadhimisha siku hiyo kwa kupanda mlima Kilimanjaro na kutembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro. Washiriki hawa wanatoka katika vituo vya Makao Makuu ya Magereza, Chuo cha Taaluma ya urekebishaji Ukonga Dar es salaam, Kikosi Maalum cha Kutuliza Gasia Magereza (KMKGM), Pwani, Dar es salaam, Iringa, Mbeya, Mara, Tabora, Tanga, Kilimanjaro na Arusha ambao kwa gharama zao wameamua kuadhimisha miaka 54 ya uhuru wa Tanganyika kwa kufanya utalii wa ndani. Akiongea na waandishi wa habari Kamishna Jenerali wa Magereza nchini John Casmir Minja katika hafula fupi ya kuwakabidhi bendera watumishi hao katika viwanja vya Magereza Mkoa wa Kilimanjaro amesema amefurahishwa mno na uamuzi wa askari hao kwa vile unalitangaza Jeshi la Magereza nje ya mipaka yake. Kamishna Minja alisema pia mbali na kulitangaza Jeshi la Magereza unawaweka timamu watumishi hao katika kufanya kazi zao vizuri ikiwa ni kuunga kauli mbiu ya serikali ya Awamu ya Tano ya Hapa Kazi tu. Aidha Kamishna huyo alitumia fursa hiyo kuishukuru serikali kwa namna ambavyo imekuwa ikijitolea kulisaidia Jeshi la Magereza ambapo alitoa taarifa kuwa tayari mikataba ya kununuliwa magari yapatayo 905 na ujenzi wa nyumba za watumishi zipatazo 9500 imesainiwa na magari yataanza kuingia mapema Januari 2016. Kwa upande wake mwenyekiti wa Magereza Utalii Klabu ambaye pia ni Mhasibu Mkuu wa Jeshi la Magereza Ndugu Estomih Hamis mbali na kumshuruku Kamishna Minja akwa namna ambavyo amejitolea katika kufanikisha uanzishwaji wa Klabu hiyo kuelezea dhima nzima ya utalii huo. “ Tumeamua kuadhimisha miaka 54 ya uhuru wa Tanganyika kwa mfumo huu kwa sababu kadhaa. Mosi , ni kuunga mkono jitihada za serikali za muda mrefu za kuhamasisha utalii wa ndani ambacho ni chanzo kimojawapo cha kuongeza mapato ya ndani ya serikali” “Pili, ni kuleta mwamko kwa watumishi wa umma na watanzania kwa ujumla katika kutembelea vivutio vya utalii vya ndani kuliko ilivyo sasa ambapo sehemu kubwa ya watalii ni wageni kutoka nje ya Tanzania” Aidha, ndugu Hamis aliongeza kuwa zoezi la upandaji mlima Kilimanjaro ni zuri kwa kuimarisha afya za watumishi hivyo kujiepusha na magonjwa kama vile kisukari, shinikizo la damu na utimamu wa mwili na hasa kwa askari wanaotakiwa kuwa hivyo muda wote. Tukio la watumishi wa Magereza kupanda mlima Kilimanjaro litakuwa ni la pili kwa mwaka huu ambapo mara ya mwisho walipanda mlima tarehe 6 March, 2015 wakiwa ni jumla ya watumishi 20 ambapo 16 walifanikiwa kufika kileleni na wanne kurudia njiani kwa sababu mbalimbali. Zoezi la upandaji mlima lililopita lilifanyika kwa mafanikio makubwa kiasi cha kuibua hoja y wa unndwaji wa chombo cha pamoja kinachoweza kuratibu shughuli za utalii ndani ya Jeshi la Magereza kwa kuwaunganisha watumishi wote. Hoja hiyo ilifanikiwa kwa kuundwa kwa Klabu ya Utalii ya Magereza, klabu ambayo iko katika hatua za mwisho za usajili. Tayari Klabu hiyo inao viongozi wakiongozwa na Mwenyikiti ndugu Hamis, katibu wake akiwa ni Mkaguzi wa Magereza Dominick Mshana na Mweka Hazina ni Mrakibu Msaidizi wa Magereza Erasto Kipingu. Nani analipa gharama za utalii huo? Akijibu swali hilo katibu wa Klabu hiyo Mkaguzi Mshana alisema kwa hivi sasa watumishi hao wanapanda kwa gharama zao wenyewe kutoka katika mishahara yao ambapo karibu kila mshiriki amechanga wastani wa shilingi 300,000. Mshana amesema ni matumaini yake kuwa katika siku za mbeleni kama watapatikana wadhamini gharama hizo zinaweza kupungua sana kutoka mifukoni mwa washiri. Aidha amesema gharama za kupanda mlima na kutembelea vivutio vingine kwa ujumla ni kubwa kwa mtu mmoja mmoja lakini kunakuwa na unafuu mkubwa watu wakipanda kama kikundi.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni Prof. Elisante Ole Gabriel wa
pili kutoka kulia akiongea na wanahabari katika maadhimisho ya siku ya
kujitolea duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo,wa kwanza kulia
ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika lisilo la Kiserikali la Volountary
Overseas (VSO) Dkt. Philip Goodwin.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole
Gabriel akiongea na vijana wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za
kujitolea katika taasisi mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya
kujitolea duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Bi
Ritha Mushi (VSO Volunteer) akiongea na Vijana wenzake juu ya umuhimu
wa kujitolea katika kongamano la siku ya kujitolea duniani lililofanyika
jijini Dar es Salaam leo.
Bw. Ian Tarimo anaejitolea katika Shirika lisilo la Kiserikali la Youth
For Change akiongea na Vijana wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali
za kujitolea katika taasisi mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya
kujitolea duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Dr
Ven kutoka DFID akiwaasa vijana wanaojishughulisha na shughuli
mbalimbali za kujitolea katika taasisi mbalimbali wakati wa maadhimisho
ya siku ya kujitolea duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Kijana
akipata maelezo juu ya utendaji kazi wa shirika lisilo la Kiserikali la
JICA wakati wa kongamano la siku ya kujitolea lililofanyika jijini Dar
es Salaam leo.
WAISHTAKI MAHAKAMA YA ICTR WAKISTAHIKI ZAO
Mahmoud Ahmad Arusha
WALIOKUWA wafanyakazi wa
mahakama ya kimataifa ya mauaji ya kimbari ya Rwanda, UN –ICTR, ambayo
imemaliza muda wake wakuwepo nchini , wameishitaki mahakama hiyo kwenye
mahakama ya kazi wakidai kutolipwa stahiki zao.
Wafanyakazi hao wakizungumza
kwenye ofisi ya Idara ya kazi mkoa wa Arusha, wamesema wanaishitaki
mahakama hiyo kutokana na kutowalipwa stahiki zao ambazo zinahusisha
Likizo na nyongeza ya mishahara kulingana na mikataba yao.
Wafanyakazi hao wanaidai
mahakama hiyo jumla ya dola za kimarekani, 800,000, ambazo hawajalipwa
hadi leo ambapo mahakama hiyo ya Umoja wa mataifa ambayo imedumu kwa
kipindi cha miaka 21 ilifunguliwa mjini Arusha mwaka 1994 nayo imemaliza
kazi yake mwezi uliopita.
Wafanyakazi hao ambao
waliajiriwa na Mahakama hiyo mwaka 1998 walikuwa wakihudumia wafungwa na
mabusu wa mahakama hiyo iliyopo kwenye gereza kuu la Arusha .
Wamesema walipoaanza kudai na
kufuatilia stahiki zao ndipo walipopewa barua za
kuachishwa waliachishwa kazi Septemba 30 mwaka huu .
Wamesema mara baada ya kupewa
barua zao hawakutakiwa tena kufika ofisi za Mahakama hiyo zilizokuwa
jengo la mikutano ya kimataifa AICC na ndipo walipofika Idara ya Kazi
mkoa kwa ajili ya kufungua shauri la madai yao.
Ofisi hiyo ya Kazi iliandikia
mahakama hiyo barua ya kutaka kufahamu stahiki za wafanyakazi hao lakini
mahakama hiyo haikujibu mpaka leo.
Wafanyakazi hao wamewasiliana na
kituo cha haki za binadamu , LHRC, mjini Arusha ambapo kimewapatia
msaada wa sheria ili kudai stahiki zao.
Akizungumza Wakili wa kituo cha
haki za binadamu, Shirinde Ngalule, amesema Umoja wa mataifa una kinga
ya kutokushitakiwa katika taasisi yeyote ile ikiwemo mahakamani.
Lakini kwa mjibu wa mkataba wa
kuanzishwa kwa mahakama hiyo hapa nchini Mahakama hiyo inatakiwa
kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia sheria za nchi husika zikiwemo
sheria ya mahusiano ya kazi.
Amesema kwa msingi huo mahakama
hiyo inapaswa kuheshimu sheria na haki za binadamu, badala ya
kwanyanyapaa waliokuwa watumishi wake kwa kisingizio cha cha kuwa na
kinga ya kutokushitakiwa.
Amesema mahakama hiyo imekiuka
taratibu katika kuwaachisha watumishi hao ambao taratibu hazikufuatwa
ikiwemo kupewa notisi na badakla yake walipewa barua ya kuachishwa kazi
kitendo ambacho ni kinyume na haki za binadamu.
Ameongeza kuwa chanzo ni pale walipoanza kudai mkataba wa kazi ndipo walipoaanza kufukuzwa mmoja mmoja
ZAIDI YA MITAMBO 30 YA UMEME JUA YATOLEWA MSAADA KWA JAMII
Na Mahmoud Ahmad Arusha
ZAIDI ya mitambo ya sola 30 imetolewa kwa jamii mbalimbali yenye
uhitaji zikiwemo Zahanati ,vituo vya afya,ofisi za watendaji kata na shule mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia kuboresha huduma zao wanazotoa kwa jamii. Hayo yalisemwa jana na Meneja masoko wa kampuni ya Sola ya Mobisol ,Seth Matemu na Meneja Mauzo ,Joseph Zikhali wakati wakizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kutangaza ofa mpya ya msimu wa sikukuu kwa wateja wake . Alisema kuwa, kampuni hiyo ya sola imekuwa ikisaidia shughuli mbalimbali za kijamii hususani zenye uhitaji ambapo hadi sasa hivi wamekwisha tumia kiasi cha shs 15 milioni kwa ajili ya kusaidia mitambo hiyo . Matemu alisema kuwa, lengo la kuwasaidia jamii hiyo ni mojawapo ya malengo ya kampuni hiyo kuhakikisha kuwa inarudisha sehemu ya faida kwa wananchi wake kwa kugawa mitambo ya sola bure kwa wenye mahitaji. Alisema kuwa,kampuni hiyo ina zaidi ya wateja 20,000 kwa Tanzania nzima ambapo wananchi wengi kwa sasa wana mahitaji ya umeme wa jua kutokana na changamoto kubwa ya umeme unaokatika kila wakati na hivyo kuchangia baadhi ya shughuli kusimama . Naye Meneja wa huduma kwa wateja kutoka kampuni hiyo, Tery Odiko alisema kuwa, kampuni hiyo imejiwekea mikakati zaidi ya kuhakikisha inafikisha huduma zake katika maeneo ya vijijini ambapo huduma za umeme hazijawafikia wananchi. Alisema kuwa,huduma hizo wanazotoa zimekuwa zikisaidia kukuza ajira kwa vijana kwani kwa kumiliki mitambo hiyo wana uwezo wa kuanzisha shughuli mbalimbali za kuwaingia kipato muda wote kama vile salon sehemu ya kuchajia simu kwa kuwa na umeme wa uhakika. Aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kununua mitambo ya sola kwa msimu huu wa sikukuu kwani wanatoa ofa maalumu kwa wateja wake . WANANCHI WATAKIWA KUFANYA ZOEZI LA USAFI ENDELEVU WILAYANI TEMEKE
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(katikati) akitoa
mwongozo jana juu ya suala la kufanya usafi kwa wakuu wa idara(hawapo
pichani) wa Halmashauri wa Manispaa ya Temeke. Wengine katika picha ni
Mkurugezi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Bw. Photidas Kagimbo
(kushoto) na Mkurugenzi wa Utumishi na Raslimali Watu wa TAMISEMI Bw.
Mohamed Pawaga(kulia)
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba akisisitiza juu ya
utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli la usafi wa mazingira ,jana wakati alipotembelea
Ofisi ya Msimamizi wa soko la Temeke Sterio lililopo katika Halmashauri
ya Manispaa ya Temeke.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(aliyetangulia)
akikagua machinjio ya kuku jana katika soko la Temeke Sterio Halmashauri
ya Manispaa ya Temeke.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Bw. Photidas Kagimbo
(wa pili kushoto) akimwongoza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu
Bw. Zuberi Samataba(katikati) kukagua soko la Temeke Sterio lililopo
katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.Zoezi hilo lilifanyika jana
wilayani humo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la usafishaji wa
mazingira.
Katapila
la Halmashauri la Manispaa ya Temeke likizoa uchafu jana katika soko la
Temeke Sterio ikiwa ni utekelezaji agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la usafishaji wa mazingira.
akataka zikiwa zimezagaa mitaani baada ya kutupwa na wananchi wa Kiburugwa katika Manispaa ya Temeke.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(kulia) akitoa
agizo kwa Mkuu wa Idara ya Usafishaji na Manispaa ya Manispaa ya Temeke
Bw. Ally Hatibu ya kuondoa mara moja uchafu katika eneo la barabara ya
Kiburugwa ambayo wakazi wa huko wamegeuza sehemu ya kutupa takataka.
Agizo hilo alilitoa jana wakati alipofanya ziara ya kutekeleza agizo la
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la
usafishaji wa mazingira.
Picha zote na Beatrice Lyimo -MAELEZO
………………………………………………………………………………………..
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Dar es salaam
Serikali imewataka wananchi wote kuwajibika katika
usafishaji wa mazingira na maeneo yanayowazunguka ili kudhibiti magonjwa
mbalimbali ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.
Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya
Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
anayeshughulikia Elimu Zuberi Samataba wakati wa ziara yake katika
Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ya ukaguzi na utoaji mwongozo katika
kutekeleza agizo la Rais la kutumia siku ya Uhuru kufanya usafi.
Alisema kuwa kila mwanachi anapaswa kuhakikisha mazingira
anayoishi na yale yanayomzunguka yanakuwa safi wakati wote ili kupunguza
mlipuko wa kipindupindu.
Samataba alisema kuwa mazingira yanayowazunguka wananchi
yakiwa safi yatapunguza matumizi ya serikali yanatokana na ununuzi wa
dawa za kutibu wagonjwa wa kipindupindu na hivyo fedha hizo kuelekezwa
katika matumizi mengine.
“Kila mmoja akiwajibika mahali pa kazi na mazingira
yanayomzunguka hali hii itasaidia kuimarishwa usafi na hivyo kila mtu
anapaswa awajibike kwa uchafu anaouzalisha nyumbani kwake au sehemu ya
kazi yake kwani jukumu la usafi ni la kila mtu” alisisitiza . Samataba.
Alisema kuwa kila Halmashauri nchini inapaswa kujipanga
vizuri katika kuhakikisha kuwa inaondoa uchafu mitaani na kusafisha
maeneo yake ili kuondokana na tatizo la kipindupindu.
Samataba aliwaagiza viongozi wa Manispaa ya Temeke na
Halmashauri nyingine nchini kusimamia suala la usafi kuhakikisha
linakuwa endelevu kwani jukumu la usimamizi wa usafi ni la kila mtu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya
Temeke Photidas Kagimbo alisema kuwa wananchi wa Halamashauri hiyo
wamelipokea suala la utekelezaji wa agizo la Rais na wanaahidi
kuhakikisha kuwa maeneo yote yanakuwa safi siku zote.
Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda Digitali kwa nchi za SADC wahitimishwa jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Bw. Assah Mwambene
akifunga Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda
Digitali kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za
Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Katibu Mkuu, Wizara ya Habari,
Vijana Utamaduni na Michezo jana. Tanzania imepata heshima ya kuwa
mwenyeji wa mkutano huo baada ya kuonekana kufanya vizuri katika
uhamaji wa matumizi ya mfumo wa analogia kwenda digitali kwa wakati.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji wa Serikali Bw. Assah Mwambene
(katikati) akiwaonesha jambo kupitia Kitumi chake cha Mkononi (IPAD)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Ally
Simba (kulia) na Naibu Mkurugenzi wa Utangazaji wa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania(TCRA) Bw. Fredrick Ntobi (kushoto) kabla ya kufungwa kwa Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda Digitali kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Dar es salaam.
Washiriki wa Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda Digitali kwa nchi za Jumuiya
ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wakifuatilia masuala
mbalimbali wakati wa mkutano huo jijini Dar es salaam.
Mada mbalimbali zikiwasilishwa kwa washiriki wakati wa Mkutano wa 10 wa uhamaji kutoka mfumo wa Analogia kwenda Digitali kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Dar es salaam.Picha Aron Msigwa – MAELEZO.
TAARIFA YA MSIBA WA MAREHEMU WILLY CHIWANGO KUTOKA TASWA
Nasikitika
kuwajulisha kuwa tumepata msiba wa mwanafamilia mwenzetu na
mwanataaluma wa siku nyingi katika uandishi wa habari za michezo nchini,
Willie ‘Willy’ Chiwango,
Chiwango alifariki usiku wa
kuamkia jana katika hospitali ya Massana, Dar es Salaam na msiba upo
nyumbani kwake Ilala Mchikichini, Dar es Salaam, ambapo mipango ya
maziko inafanyika.
Wakati wa uhai wake marehemu
Chiwango alifanya kazi katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo
magazeti ya serikali, Daily News na Sunday News. Pia amepata kufanya
kazi This Day na vyombo vingine.
Kwa wanaohitaji taarifa za msiba huu, namba za wahusika ni mtoto wa marehemu 0659-353006, kama ukimkosa hata mjane wa marehemu pia anazungumza 0652-722173.
Naomba tushirikiane na familia katika kipindi hiki kigumu. Mungu amuweke mahali pema peponi marehemu Mzee Willy Chiwango. Amina.
Ahsanteni,
Katibu Mkuu TASWA.
WAVUVI UKANDA WA PWANI YA BAHARI YA HINDI KUNUFAIKA NA UVUVI WENYE TIJA.
Jovina Bujulu- MAELEZO.
.Dar es Salaam.
Wavuvi
waishio ukanda wa maeneo ya Pwani ya Bahari ya Hindi upande wa Tanzania
Bara na Zanzibar wanatarajia kunufaika na elimu ya ukuzaji viumbe
kwenye maji na teknolojia sahihi ya kupambana na mabadiliko ya tabia
nchi kupitia mradi wa Udhibiti wa Uvuvi na Maendeleo Shirikishi Kusini
Magharibi mwa Bahari ya Hindi (SWIOFISH).
Hayo
yamesemwa jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya
Maendeleo ya Uvuvi, Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Bi. Fatma
Sobo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa
mradi wa Udhibiti Uvuvi na Maendeleo Shirikishi Kusini Magharibi mwa
Bahari ya Hindi, ulioanza kutekelezwa mwezi Juni mwaka huu.
Amesema lengo
la mradi huo ni kuwasaidia wavuvi wadogo wa ukanda huo ili waweze
kunufaika na shughuli hiyo na kuwa na uvuvi endelevu wenye kuongeza
faida kiuchumi, kijamii na kimazingira.
‘Lengo la
mradi huu ni kuhakikisha kuwa wavuvi wa ukanda wa Pwani wanakuwa na
uvuvi endelevu na wananufaika na rasilimali za bahari kwa kuimarisha
uwezo wa Taasisi za Kikanda na Serikali” Amesema.
Ameeleza
kuwa katika kufuatilia utekelezaji wa mradi huo , Wizara ya Maendeleo
ya Mifugo na Uvuvi,imeanzisha mpango wa uongozi na usimamizi wa uvuvi
ambapo wavuvi wanapatiwa elimu kuhusu aina za samaki, aina ya nyavu za
kuvulia, muda wa kuvua, mauzo na uhifadhi wa samaki.
Ameongeza
kuwa mradi huo utaimarisha mfumo wa taarifa za uvuvi kama vile mavuno,
nguvu ya uvuvi inayotumika , mauzo ya ndani na nje nchi yatokanayo na
shughuli hizo.
Bi. Fatma
aliongeza kuwa kipaumbele cha mradi huo kimewekwa katika uvuvi wa samaki
aina ya pelagiska, Jodari, Kamba miti, samaki mwamba, pweza na ukuzaji
viumbe kwenye maji bahari ambapo eneo la majaribio litakuwa katika
wilaya za Mkinga, Pangani, Tanga, Bagamoyo mjini na Lindi Vijijini.
Aidha,
amesema mradi huu utatekelezwa kwa miaka 6, kuanzia 2015 hadi 2021 na
umefadhiliwa na Mfuko wa Mazingira Duniani na Mfuko wa Kimataifa wa
Maendeleo kwa jumla ya Dola za Kimarekani milioni 36,000 ambapo
utazihusisha wilaya 16 kutoka ukanda wa bahari ya Hindi, mkoa wa Tanga
hadi Mtwara.
Ameongeza
kuwa mradi huo ukizishirikisha Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
(Tanzania Bara), Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Zanzibar) na Mamlaka ya
Kusimamia Bahari Kuu utakomesha uvuvi haramu wa kutumia Mabomu.
Taasisi
zitakazotelekeza mradi huo ni Wakala wa Mafunzo ya Elimu ya Uvuvi,
Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Kitengo cha Hifadhi za
Bahari na Maeneo Tengefu, Vikundi vya Ujasiriamali na Jamii za watu wa
Pwani.
Joshua Mlelwa achomoza Tamasha la Krismasi
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha
hilo, Alex Msama Mlelwa anaungana na wenzake Rose Muhando, Upendo
Nkone,Kwaya ya Wakorintho Wapili (Tanzania) na Ephraim Sekeleti wa
Zambia.
Msama alisema Kamati yake inaendelea na mikakati ya
maandalizi ya tamasha hilo ambalo litakuwa na dhamira ya kushukuru baada
ya Tanzania kupita kwenye uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25.
Aidha Msama alitoa wito kwa Watanzania kujitokeza katika tamasha hilo ili kufikisha shukrani ya pamoja kwa Mungu.
TANZANIA YAPEWA CHETI CHA KUTOKUWA NA UGONJWA WA POLIO
Na Magreth Kinabo
Tanzania imetangazwa rasmi kuwa ni mojwapo ya nchi isiyokuwa na ugonjwa wa polio katika nchi za Afrika katika mkutano wa Tume ya Afrika ya kuthibitishwa kutokomezwa kwa polio(Afrika Regional Certification Commission for Polio Eradication).
Kutangazwa kulifanyika katika mkutano huo uliofanyika nchini Madagascar, Novemba 26, mwaka huu.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Donan Mmbando wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kuhusu ugonjwa huo ulifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini Dar es Salaam. “Hii inamaanisha kuwa kwa sasa hatuna ugonjwa wa polio tena nchini kwa sababu tumeweza kuwafikia watoto wengi zaidi kwa kuwapatia chanjo ya polio na hivyo kuongeza kinga kwenye jamii.Kutokana na mafanikio hayo, tunatakiwa bado kuendelea na kutoa chanjo ya polio kwa watoto wote stahiki ili kuongeza kinga kwa jamii pamoja kuimarisha mfumo wa ufutiliaji wa mgonjwa yoyote mwenye ulemavu wa ghafla,” alisema Dkt. Mmbando. Katibu Mkuu huyo alifafanua kwamba mgonjwa wa mwisho wa polio alipatikana Julai mwaka 1996 hapa nchini. Aliongeza kuwa ufuatiliaji wa magonjwa yanayokingwa na chanjo uliimarishwa na kufikia viwango vinavyo kukubalika kimataifa na kuthibitisha kuwa watoto wenye umri chini ya miaka 15 waliopata ulemavu wa ghafla wanapatikana na sampuli zao kuchukuliwa mara moja. Hivyo kuanzia mwaka 1997 mpaka Oktoba 2015 jumla ya sampuli 6,249 za watoto waliopata ulemavu zilipelekwa kwenye maabara za kimataifa na kuthibitishwa kuwa hakuna sampuli iliyoonesha uwepo wa ugonjwa wa polio. COSATO CHUMI AMALIZA TATIZO LA VITANDA HOSPITAL YA MAFINGA MJINI
Pichani
Mbunge wa jimbo la Mafinga mji ni Cotato Chumi akimkabidhi msaada wa
vitanda ,magodoro pamoja na vifaa mbalimbali kaimu mganga mkuu wa
hospitali ya Mafinga Dk Abdul Msuya juzi
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatiliwa ugawaji wa vifaa hivyo wakati wa makabidhiano
Mbunge wa mafinga mjini Cosato Chumi akikabidhi vifaa hivyo kwa vitendo
Baadhi ya wadau na wanachama wa chama cha mapinduzi ccm walihudhulia tukio hilo
…………………………………………………………………………………..
TATIZO la upungufu wa vitanda katika wodi ya
akina mama na watoto katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa ambalo kwa muda mrefu limekuwa chanzo cha msongamano na uwalazimu baadhi ya wagonjwa kulala sakafuni sasa limepatiwa ufumbuzi baada ya uongozi wa hospitali hiyo kupokea msaada wa vitanda na vifaa tiba kutoka kwa mdau wa maendeleo katika sekta ya afya.
Mbunge wa Mafinga Mjini
(CCM) Cosato Chumi alisema kuwa kwa muda mrefu hospitali hiyo ilikuwa ina upungufu wa vifaa mbalimbali ikiwemo vitanda hali iliyofanya kuandika maandiko mbalimbali kwa wahisani wa nje ya nchi ili kuweza kumsaidia kupata vifaa hivyo .
Alisema kuwa umefika
wakati sasa wadau mbalimbali, mifuko ya kijamii na makampuni kujenga utamaduni wa kusaidia watu wenye mahitaji mbalimbali wakiwemo watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na wagonjwa hospitalini kwani kufanya hivyo ni sehemu ya kurudisha kile wanachokitapa kwa jamii.
“Unajua afya ni kila
kitu katika maisha ya binadamu hivyo lazima nitekeleze ahadi zangu nilizotoa wakati wa kampeni na wanachi lazima tufanye kazi kwa kujituma ili tumuunge mkono rais wetu ambaye anania ya ya kutuletea maendeleo na kuwataka wadau mbalimbali kusaidia jamii zenye mahitaji na kuacha kutegemea serikali pekee “ alisema
Chumi aliwaomba wananchi
wa jimbo hilo kuunga mkono kwa kufanya kazi kwa nguvu zote ili walete maendeleo kwa pamoja maana akifanya kazi pekee yake bila wao hawezi kuleta maendeleo pekee yake.
Msaada huo wa vitanda 16 na magodoro 11 na vitu
mbalimbali umetolewa na taasisi binafsi inayojishughulisha na masuala ya afya ya nchini Astralia ijulikanayo kama “Rafiki Surgical Mission” kwa uratibu wa ofisi ya mbunge wa jimbo la Mafinga mjini
Alisema kuwa msaada huo aliopatiwa na rafiki zao hawajatoa hata
senti tano bali huwa marafiki hao wanachangishana fedha na kununua vifaa hivyo na kisha kuvisafirisha mpaka bandari kavu ambapo hapo ndio hutumia garama kusafirisha vifaa hivyo mpaka sehemu husika TAHADHARI KUHUSU KUINGILIA MAWASILIANO YA WATU AU KUFUATILIA
Katika
siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa za kuwepo kwa Programu
(Application) ya simu ikijulikana kama SOFTBOX TANZANIA iliyosemekana
iko kwenye Google PLAYSTORE.
Ilidaiwa kuwa program (Application) hiyo ya SOFTBOX TANZANIA ilikuwa na uwezo wa kunasa au kuingilia mazungumzo ya simu, ujumbe mfupi pamoja na mawasiliano ya WhatsApp kutoka kwenye simu ya mtu binafsi. Kwa yeyote aliyekuwa na nia hiyo ya kunasa au kuingilia mazungumzo ya simu, ujumbe mfupi pamoja na mawasiliano ya WhatsApp kutoka kwenye simu ya mtu mwingine alihitajika kulipia fedha kiasi cha Tshs 35,000/= kupitia mitandao ya simu ili kupata namba ya siri kwa ajili ya kuwezesha nia hiyo. Mamlaka ya Mawasiliano imefanya uchunguzi kubaini kuwepo kwa programu hiyo na ukweli kuhusu uwezo wake wa kufanya kilichodaiwa, ikiwa ni pamoja na kuangalia madhara ya program hiyo na sheria inasema nini kuhusu suala hili. Baada ya kufanya uchunguzi wa kina, Mamlaka ya Mawasiliano ilibaini na imejiridhisha kuwa program (Application) hiyo haina uwezo huo wa kunasa au kuingilia mazungumzo ya simu, ujumbe mfupi pamoja na mawasiliano ya WhatsApp kutoka kwenye simu ya mtu binafsi kama ilivyodaiwa. Aidha Mamlaka imebaini kuwa watengenezaji (Developers) wa programu hiyo walikuwa na nia ya kutapeli na kujipatia fedha hiyo kiasi cha Tshs 35,000/= kwa njia ya udanganyifu wakitumia kivutio cha kunasa au kuingilia mazungumzo ya simu, ujumbe mfupi pamoja na mawasiliano ya WhatsApp kutoka kwenye simu za watu binafsi. Programu (Application) nyingine ya aina hiyo iliibuka tena ikiitwa SIMNET Tanzania ikiwa na maelezo kama ya awali. Wakati Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania pamoja na Jeshi la Polisi wakiendelea na uchunguzi zaidi, tunapenda kuuarifu umma wa Watanzania kuepuka kufanya mambo yafuatayo: 1. Kuvutiwa na matendo yaliyo kinyume na sheria na maadili ya matumizi mazuri ya mawasiliano kama hili la kunasa au kuingilia mazungumzo ya simu, ujumbe mfupi pamoja na mawasiliano ya WhatsApp kutoka kwenye simu ya mtu binafsi. Kitendo hiki ni kosa la jinai kwa mujibu wa kifungu cha 6 na 10 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao ya Mwaka 2015 na kifungu cha 123 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) ya Mwaka 2010. Sheria katika vifungu hivyo inakataza mtu yeyote kuingilia mawasiliano ya mtu mwingine. Adhabu kali ya makosa haya ni faini isiyopungua shilingi milioni tano au kutumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja au vyote kwa pamoja. 2. Mamlaka inawatahadharisha watumiaji wa huduma za mawasiliano kutokuwa wepesi na kudanganyika kufanya malipo yoyote kwa njia ya mitandao kwa huduma wasiyokuwa na uhakika nayo au bila kujiridhisha na uwepo wa huduma hiyo. Ni vizuri kutoa taarifa kwa mtoa huduma wako au kuwasiliana na Mamlaka ya Mawasiliano kupitia barua pepe malalamiko@tcra.go.tz au kupiga simu namba 0784558270/1. Imetolewa na: Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania 04/12/2015 KITUO CHA RADIO CHA HITS FM RADIO CHATIWA MOTO NA WATU WASIO JUULIKANA USIKU WA JUZI
Vifaa
vyote vya kutangazia katika Studio ya Hits FM Radio vilivyoteketea kwa
moto usiku wa juzi katika studio hiyo mara baaada ya kuvamiwa na watu
wasipjuulikana huko Migombani Mjini Zanzibar
Waandishi wa habari wakisikiliza kwa makini maelezo yanayotolewa na
Mkuu wa kituo cha Hits FM Mohammed Abdallah hayupo pichani mara baada
ya kuunguzwa kituo cha Radio hiyo.
Mwandishi
wa habari akimuhoji Mkuu wa Utawala wa Afisi kuu ya CCM FM Salum
Khatibu Reja alipofika katika kituo cha Radio ya Hits FM na kujionea
hali ya kituo hicho.
Waandishi
wa habari wakisikiliza kwa makini maelezo yanayotolewa na Mkuu wa kituo
cha Hits FM Mohammed Abdallah hayupo pichani mara baada ya kuunguzwa
kituo cha Radio hiyo.
Mwenyeki
ti wa MCT Suleiman Seif katikati akifafanuwa jambo kwa waandishi wa
habari kuhusiana na kutiwa moto Hits FM Radio usiku wa juzi iliyopo
Migombani Mjini Zanzibar.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abaas Mwinyi Atimiza Ahadi Zake kwa Kituo cha Afya Fuoni
Mbunge
wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe A bass Ali Hassan Mwinyi, akitembelea
Kituo cha Afya cha Fuoni Zanzibar kinachotowa huduma kwa Wananchi wa
Jimbo hilo na jirani wakati akitimiza ahadi yake kwa kutuo hicha,
akipata maelezo kutokwa kwa mdhamini wa kituo hicho Muuguzi wa Afya ya
Jamii Bi Mwaka Pandu Makame akitowa maelezo ya eneo lao la kuchomea taka
za kituo hicho.
Mbunge
wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassan Mwinyi akitembelea
kituo hicho cha Afya Fuoni Zanzibar akiwa katika ziara yake katika jimbo
lake kujiuonea ufanisi wa kituo hicho na kukabidha Madawa na kuvifanyia
mategenezo vyoo vya kituo hicho ni moja ya kero za Wananchi wanaofika
kituoni hapo.
Mbunge
wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Adass Mwinyi akitembezwa katika kituo
hicho na Madaktari wa Kituo hicho, akiwa katika ziara yake ya
kukamilisha ahadi yake juu ya kituo hicha kikifanyia mategenezo sehemu.
Mbunge
wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Mwinyi akimsikiliza daktari wa
kitengo cha kungolea meno katika Kituo hicho cha Fuoni Zainab Seif na
Khadija Khamis, wakimueleza Mbunge huyo baadhi ya vifaa vinakosekana
katika kitengo chao kwa ajili ya huduma ya kungolea meno Wananchi
wanaofika kituoni hapo. Kituo hicho kinatowa huduma za Uzalishaji wa
Kinamama kupiga Utra saund na huduma nyengine za matibabu
Mbunge
wa Fuoni Mhe Abass Mwinyi akizungumza wa Wafanyakazi wa Kitengo cha
Meno katika Kituo cha Afya Fuoni wakati wa ziara yake kutimia ahadi
alizotowa kwa Wananchi wa Jimbo hilo katika kituo hicho na kufanikisha
upatikanaji wa vifaa hivyo wanavohitaji katika kituo hicho kuondoa kero
kwa Wananchi wake wanaofika kituoni hapo kupata huduma ya meno na
nyeginezo.
Mhe
Abass Mwinyi akizungumza na Wafanyakazi wa Kituo cha Afya Fuoni
Zanzibar wakati wa ziara yake kutembelea Kituo hicho na kukabidhi madawa
kwa ajili ya kituo hicho, Kinachotowa huduma kwa Wananchi wa Jimbo lake
na Wananchi wa jirani.ili kuboresha ufanisi wa huduma ya Afya kituoni
hapo.
Mbunge
wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe. Abass Mwinyi akizungumza na wafanyakazi
wa Kituo hicho na Wananchi wa Jimbo lake wakati wa ziara yake ya kwanza
katika jimbo hilo na kukabidhi vifaa na Madawa kwa kituo hicho. Mhe
Mbunge Abass amesema sasa Hapa Kazi Tu, ili kuwaletea maendeleo Wananchi
wa Jimbo lake na kuondoa kero zote katika jimbo hilo na kuwa Jimbo la
mfano katika majimbo yote ya Zanzibar.
Daktari
Dhamana wa Kituo cha Afya Fuoni Said Fadhili Abass akizungumza wakati
wa mkutano huo na Mbunge wa Jimbo la fuoni na kumshukuru kwa msaada wake
huo kwa Kituo chao. na kusema dawa hizo zitatumika kwa wananchi wa
Jimbo hilo wanaofika kituoni hapa kupata huduma mbalimbali za Afya.
Wauguzi wa Kituo cha Afya Fuoni
wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Fuoni Mhe Abass Mwinyi wakati
akizungumza na Wafanyakazi hao katika ziara yake kutembelea Kituo hicho
na kukabidhi madawa kwa ajili ya Wananchi wanaofika kupata huduma
kituoni hapo.
Mbunge
wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassaan Mwinyi akimkabidhi
fedha shilingi milioni moja Dakt. Dhamani wa Kituo cha Afya Fuoni
Zanzibar Said Fadhil Abass, kwa ajili ya kutatua makero zinazokikabili
kituo hicho cha Afya Fuoni ili kufanya kazi zao kwa kuwahudumia Wananchi
kwa ufanisi zaidi.
Mbunge
wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassaan Mwinyi akimkabidhi
vifaa kwa akili ya vyoo vya kituo hicho Dakt. Dhamani wa Kituo cha Afya
Fuoni Zanzibar Said Fadhil Abass na kulia Muuguzi wa Afya ya Jamii
Kituoni hapo Mwaka Pandu Makame.
Mzee
wa Jimbo la Fuoni Mzee Takrima akizungumza wakati wa hafla hiyo ya
kukabidhi madawa na vifaa katika Kituo cha Afya Fuoni Zanzibar.
Wananchi wa Jimbo la Fuoni wakimsikiliza Mbunge wao.
Wauguzi
wa Kituo cha Afya Fuoni wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Fuoni Mhe
Abass Mwinyi wakati akizungumza na Wafanyakazi hao katika ziara yake
kutembelea Kituo hicho na kukabidhi madawa kwa ajili ya Wananchi
wanaofika kupata huduma kituoni hapo.
Imetayarishwa na othmanmapara.Blogspot
Zanzinews.com
Email othmanmaulid@gmail.com.
Mobile 0777424152 or 0715424152.
MRATIBU UN ARIDHISHWA NA MATUMIZI YA UFADHILI TABORA
Ofisa
Kilimo na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Samaluku Joseas
(kushoto) akisoma taarifa ya maendeleo ya miradi mbalimbali
inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa katika mkoa wa Tabora.
Pichani wa pili kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa
Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez
pamoja na Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa
katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah
Hassan (wa tatu kushoto) wakipitia taarifa hiyo kwa pamoja kabla ya
kuelekea kukagua miradi hiyo.
Na Modewji blog team, Tabora
MRATIBU
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika
la Mipango ya Maendeleo la Umoja huo Bw.Alvaro Rodriguez, amesema kwamba
umoja huo utaendelea kufadhili miradi ya maendeleo katika mkoa wa
Tabora yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi.
Hayo alisema jana baada ya kuzuru miradi inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa mkoani Tabora.
Miradi
hiyo ni ya ujenzi wa bwawa la nguvumoja kwamtindo wa utoaji wa chakula
kwa kazi inayofanywa na mradi wa misitu ya miyombo.
Katika
ziara hiyo ambayo alikuwa na Ofisa kutoka Kitengo cha ushirikiano wa
kimataifa wizara ya mambo ya nchi za nje, Bi. Maulidah Hassan Mratibu
huyo aliridhishwa na mafanikio ya miradi hiyo ambayo imelenga kupiga
vita umaskini na kutunza mazingira.
Ziara
ya Mratibu huyo mkoani Tabora ni moja ya ziara yake ndefu ya kutembelea
miradi inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa katika mikoa ya
Singida, Tabora na Kigoma.
Alipotoka
Singida jana asubuhi alifika katika moja ya Wilaya kame nchini, Wilaya
ya Igunga na kuona mradi unaofadhiliwa na Shirika la Mpango wa Chakula
la Umoja wa Mataifa (WFP) wa ukarabati wa bwawa la Charco.
Bwawa
hilo ambalo litahudumia watu takribani 6,100 kutoka vijiji vya
Nguvumoja, Ndembezi na Iborogelo lilijengwa awali na miradi ya TASAF
lakini wakati wa mvua za Elnino tuta lake lilivurugika vibaya.
Akizungumzia
bwawa hilokaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Igunga ambaye pia ni Ofisa
Kilimo na Ushirika wa Wilaya ya Igunga, Samaluku Joseas, akizungumza
alisema kwenye bwawa hilo kwamba Umoja wa Mataifa kupitia WFP
wanawezesha ukarabati wa bwawa hilo kwa kutoa chakula kwa wachimbaji.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa tatu kushoto) aliyeambatana na
Afisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (wa
pili kushoto) walipowasili kukagua mradi wa ujenzi wa
Bwawa la Charco la Nguvumoja kwa mtindo wa utoaji wa chakula kutoka
Shirika la Chakula Duniani (WFP) kwa kazi inayofanywa na mradi wa misitu
ya Miyombo. Kushoto ni Ofisa Tawala msaidizi anayeshughulikia Uchumi na
Tija wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Dkt. Phillips Mtiba pamoja na
Ofisa Kilimo na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Samaluku
Joseas (wa pili kulia).
Aidha
imeelezwa kuwa tuta hilo likikamilika litakuwa na uwezo wa kuhudumia
kaya 1,200 na Ng’ombe elfu moja na kuweza kuhifadhi maji kwa mwaka
mzima.
Imeelezwa
kuwa wajenzi wanapewa debe moja la Mahindi kwa kina cha mita moja na
urefu wa mita nne na upana wa mita tatu na nusu lita ya mafuta ya kula
na Njegere kilo tatu.
Kumalizika kwa bwawa hilo kutasaidia kupunguza umbali wa wananchi katika kutafuta maji.
Awali wananchi walilazimika kusafiri kilomita 30 kupata maji katika bwawa la Manzugi kuchota maji na kunywesha mifugo.
Aidha imeelezwa kuwa baadae wanyama watatengewa eneo la kunywa maji.
Aidha
alitembelea kikundi cha ufugaji nyuki, utunzaji wa mazingira pamoja na
usindikaji wa matunda pori cha Membo , wilayani Uyui.
Kikundi
hicho kilichopo wilayani Uyui kimeanzishwa Mei 8,2007 na Katibu wa
kikundi Nasibu Baraka alisema kikundi hicho chenye wanachama 30
kimefanyakazi kubwa ya kupiga vita umaskini.
Alisema
ili kukabiliana na adui njaa na umaskini kikundi hicho kwa ufadhili wa
UNDP kimewezesha kujiajiri wenyewe, Kusindika matunda ya asili kwa ajili
ya jamu na divai,kilimo cha bustani, kilimo cha chakula na biashara,
ujenzi wa majikobanifu,usagaji wa unga na kupika keki za Muhogo mbichi
kwa Karanga na Asali.
Akisoma
risala kwa Mratibu wa UN Tanzania alisema kwamba wamekuwa na mafanikio
makubwa kutokana na ruzuku mbalimbali za UNDP ikiwamo mafunzo.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendelea kupata maelezo ya mradi
huo.
Aidha amesema kwamba kwa sasa wanatumia sola badala ya mafuta ya taa huku mradi wa Miyombo ukiendelea kuleta neema.
Aidha ametaka umoja huo kuwasaidia kuwa na mshine za kisasa cha kusindika matunda na chakula.
Viongozi
hao walifika katika mradi huo kuangalia mafanikio ya mradi huo
unaotekelezwa chini ya mpango wa miaka mitano wa Msaada wa Maendeleo wa
Umoja wa Mataifa,(UNDAP).
Aidha
mradi huo umelenga kupunguza umaskini kutunza mazingira kwa njia ya
uragibishi na na kufunza wananchi kuhusu suala la ufugaji nyuki na
utunzaji wa mazingira.
Naye
Ofisa utawala msaidizi wa mkoa anayeshughulikia Uchumi na Tija Dk.
Phillips Mtiba akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa Tabora, Ludovick
Mwananzila ambaye hakuwepo kutokana na majukumu mengine kwenye mikutano
na wananchi kuhusu miradi ya TASAF, alisema baada ya kumaliza kukagua
miradi kwamba wameridhika na miradi inayofadhiliwa na UN katika mkoa
huo.
Alisema
pamoja na kwamba walitembelea miradi michache lakini ni dhahiri mkoa wa
Tabora umefurahishwa na misaada iliyotolewa ambayo inatia moyo na
kusaidia harakati za serikali za kukomboa wananchi wake kutoka katika
lindi la umaskini na ukosefu wa huduma muhimu kama za maji na hifadhi ya
mazingira.
Pamoja
na kushukuru kwa misaada hiyo kwa wanatabora na maendeleo yao, alitaka
UN isiwachoke kusaidia vipaumbele vya mkoa huo ambavyo ni kujitokeza kwa
chakula na hifadhi ya misitu.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendelea na ukaguzi wa Bwawa hilo.
“
Nashukuru sana kwa msaada tunaoendelea kupata kutoka UN kwa ajili ya
maendeleo ya wana Tabora na Tabora kwa ujumla na niseme tu kwamba kama
wana Tabora kuna vitu ambavyo tunaweza kufanya na mengine hatuwezi
kuyafanya na hapo ndipo sasa tunapoweza kuona umuhimu wa nafasi ya
wafadhili na wadau mbalimbali katika shughuli za maendeleo.” Alisema Dk.
Phillips.
Alisema
ingawa walikuwa na muda mfupi na kutembelea miradi michache , alitamani
waje kurudi kuona miradi mingi zaidi ili watambue kwamba miradi hiyo
inabadilisha wana Tabora na hawachezei fedha za ufadhili.
Muonekano wa mradi wa ujenzi wa Bwawa la Charco la Nguvumoja.
Alisema
suala la uhakika wa chakula kwa wananchi ni muhimu kwao kutokana na
ukweli kuwa wananchi wakiwa na chakula hata fedha zao zitakaa mfukoni na
kufanya kazi nyingine za maendeleo. Alisema kutokana na hali hiyo
wataendelea kuomba kusaidiwa katika eneo hilo.
Aidha
alitaka mkoa wa Tabora kuendelea kusaidiwa kutunza misitu ya Miyombo
kwa ajili ya manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho kwa kuwa misitu ni
kivuta mvua na maji ndio pembejeo namba moja katika uzalishaji wa
chakula.
Alishukuru
UNDP kwa kusaidia kuhifadhi misitu hiyo ili kuwapo na uvunaji endelevu
kwa kusaidia jamii kuitunza na kuismamia rasilimali hiyo na kuitumia
katika fursa za kiuchumi kama ufugaji nyuki.
Leo Mratibu huyo ataendelea na ziara yake katika mkoa wa Kigoma.
Wananchi wakiendelea kuchimba bwawa hilo.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akizungumza na wananchi wa kijiji cha
Nguvumoja watakaonufaika na mradi wa bwawa hilo.
HapaKaziTu; ndio maneno aliyokuwa akiyasema Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakati akichimbia sehemu ya bwawa
hilo alipofanya ziara ya kukagua mradi huo wa Bwawa la Charco la
Nguvumoja.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akichimba udongo na sururu huku Afisa
wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan akijaza
udongo unaochimbwa kwenye ndoo.
HapaKaziTu;
Wanakijiji pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez
wakishangilia kwa pamoja huku wakiunga kauli ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ya #HapaKaziTu
sambamba na mabango 17 ya malengo ya maendeleo endelevu (Sustainable
Development Goals-SDGs) walioyowafikia wanakijiji wa Nguvumoja. Kwa matukio zaidi bofya link hii
Uzinduzi wa mtandao wa intaneti ya kasi zaidi wa Tigo 4g LTE mkoani Morogoro wafana
MANISPAA YA KIONONDONI NA USAFI WA MAZINGIRA
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Kinondoni Injinia, Musa Natty akieleza jambo wakati wa
mkutano na wadau wa usafi wa mazingira kuhusu mkakati wa kufanya usafi
katika Manispaa hiyo kufuatia agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambapo siku ya sikuu ya Uhuru,
inayoadhimishwa kila Desemba 9 kuwa siku ya kufanya usafi ,kulia kwake
ni Mkurugenzi wa Idara ya Tawala za Mikoa Dodoma Bi.Susano Chekani .
Mkurugenzi
wa Idara ya Tawala za Mikoa Dodoma Bi.Susano Chekani akifafanua jambo
kwa wajumbe wa mkutano wa mkakati wa usafi (hawapo katika picha) namna
ya kushirikiana katika kuhakikisha mazingira ya jiji la Dar es Salaam
yanakuwa safi na salama ili kuepukana na magonjwa ambukizi ikiwemo
kipindupindu katika kutekeleza agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli kuadhimisha siku ya sikuu ya Uhuru,
Desemba 9 kuwa siku ya kufanya usafi , kulia kwake ni Katibu Tawala
Afya Daktari.Grace Magembe.
Wajumbe
wa mkutano wa usafi ambao pia ni wadau kutoka taasisi mbalimbali
zikiwemo Taasisi za kifedha, Mazingira,Jeshi la
Magereza,Wanamazingira,Vikundi vya Usafi na Wafanyakazi wa Manispaa ya
Kinondoni wakisikiliza mada zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo
ikiwa ni kutekeleza agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli kuadhimisha siku ya sikuu ya Uhuru, Desemba 9
mwaka huu kuwa siku ya kufanya usafi .
Wajumbe
wa mkutano wa usafi ambao pia ni wadau kutoka taasisi mbalimbali
zikiwemo Taasisi za kifedha, Mazingira,Jeshi la
Magereza,Wanamazingira,Vikundi vya Usafi na Wafanyakazi wa Manispaa ya
Kinondoni wakisikiliza mada zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo
ikiwa ni kutekeleza agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli kuadhimisha siku ya sikuu ya Uhuru, Desemba 9
mwaka huu kuwa siku ya kufanya usafi .
Mkurugenzi
wa Idara ya Tawala za Mikoa Dodoma Bi.Susano Chekani akikagua Soko la
Magomeni lilipo Manispaa ya Kinondoni wakati ziara ya kuangalia hali ya
usafi ikiwa ni kutekeleza agizo lililotolewa na Rais wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli kuadhimisha siku ya
sikuu ya Uhuru, Desemba 9 kuwa siku ya kufanya usafi,kulia kwake ni
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Injinia Mussa Natty.
Mkurugenzi
wa Idara ya Tawala za Mikoa Dodoma Bi.Susano Chekani akiongea na
wachuuzi wa Soko la Magomeni katika Manispaa ya Kinondoni katika ziara
ya kuangalia hali ya usafi katika soko hilo.
Mkurugenzi
wa Idara ya Tawala za Mikoa Dodoma Bi.Susano Chekani akiwa ameongoza na
viongozi mbalimbali kutoka Manispaa ya Kinondoni katika ziara ya
kuangalia hali ya usafi ya soko la magomeni kandokando ni sehemu ya
kukusanyia taka za soko hilo na baadaye huchukuliwa na gari maalum la
kubebea taka kwa ajili ya kupelekwa dampo kuu.
Mkurugenzi
wa Idara ya Tawala za Mikoa Dodoma Bi.Susano Chekani akiwa ameongoza na
viongozi mbalimbali kutoka Manispaa ya Kinondoni katika ziara ya
kuangalia hali ya usafi ya soko la magomeni kandokando ni sehemu ya
kukusanyia taka za soko hilo na baadaye huchukuliwa na gari maalum la
kubebea taka kwa ajili ya kupelekwa dampo kuu.
Mkurugenzi
wa Idara ya Tawala za Mikoa Dodoma Bi.Susano Chekani(Kulia)
akimsikiliza Mwenyekiti wa Soko la Tandale Mohamed Mwikya(Kushoto)
wakati wa ziara ya kukagua hali ya usafi wa soko hilo
Gari
la Kuzoa taka kutoka katika Manispaa ya Kinondoni likiwa limebeba taka
kutoka Soko la Tandale tayari kwenda kuzihifadhi katika dampo kuu,
Manispaa hiyo imekuwa ikihakikisha hali ya usafi katika masoko yake kwa
kupeleka magari ya kuzoa taka kila siku ili kuepukana na magonjwa
ambukizi ikiwemo kipindupindu.
Sehemu ya Soko lilipo kwenye kituo cha Daladala cha Simu 2000 eneo la
Sinza kikiwa katika hali nzuri ya usafi huku uongozi wa eneo hilo
wakiendelea kuisimamia hali hiyo kama ambavyo ilivyoagizwa na Rais wa
Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli kuwa siku
ya sherehe ya Uhuru ambayo huadhimishwa kila Desemba 9, mwezi wa 12 kuwa
ni siku ya usafi wa mazingira ili kuepukana na magonjwa amukizi
kikiwemo kipindupindu.
Sehemu
ya Daraja la Tegeta Manispaa ya Kinondoni ikiwa imegeuzwa Dampo na
wakazi wa eneo hilo kwa ambapo Mkurugenzi wa Idara ya Tawala za Mikoa
Dodoma Bi.Susano Chekani aliagiza uchafu huo kutolewa haraka kwa kuwa
inahatarisha hali ya afya kwa wakazi wa maeneo hayo .
(Picha na Lorietha Laurence-Maelezo) |
No comments :
Post a Comment