Sunday, November 22, 2015

KINANA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA VYAMA VYA SIASA KUSINI MWA AFRIKA MJINI MAPUTO,MSUMBIJI

 

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman  Kinana (kulia)akiwa kwenye picha ya pamoja na Zuma Mwenyekiti wa ANC ya Afrika Kusini Rais Jacob  (kushoto) na Mwenyekiti wa FRELIMO ya Msumbiji Rais Philipe Nyusi  (katikati)
  Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Chama cha SWAPO cha Namibia Rais Hage Gengob,  katika
mkutano wa viongozi wa vyama vya siasa
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto) akizungumza kwenye mkutano wa viongozi wa vyama vya siasa vya Kusini mwa Afrika mjini Maputo, Msumbiji.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa na Makatibu Wakuu wa vyama vya ANC, FRELIMO, MPLA, SWAPO na ZANU PF mjini Maputo.
…………………………..
Katibu Mkuu wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Komredi Abdulrahman Kinana katikati ya wiki iliyopita aliongoza
ujumbe wa Tanzania nchini Msumbiji kuhudhuria mkutano wa Vyama vya Siasa Kusini
Mwa Afrika. 
Mkutano huo uliohudhuriwa
na baadhi ya Wenyeviti na Makatibu Wakuu wa vyama  hivyo, umemalizika mwishoni mwa wiki mjini
Maputo kwa mafanikio makubwa.
Mkutano huo ulijadili
masuala yaliyolenga kutatua changamoto mbalimbali za mataifa hayo na mipango ya
maendeleo kwa ujumla.
Baadhi ya viongozi wa
vyama hivyo vya siasa waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa ANC ya Afrika
Kusini Rais Jacob Zuma, Mwenyekiti wa FRELIMO ya Msumbiji Rais Filipe Nyusi,
Mwenyekiti wa SWAPO ya Namibia Rais Hage Geingob pamoja na Komredi Kinana na
ujumbe wake.
Ujumbe kutoka Tanzania
ulioongozwa na Komredi Kinana umewajumuisha Katibu wa NEC anayeshughulikia
Siasa na Mambo ya Nje Dkt. Asha-Rose Migiro pamoja na Makatibu Wakuu wa Jumuiya
za CCM.

UNIDO YAPIGA JEKI VIWANDA VIDOGO VYA MAFUTA YA ALIZETI DODOMA

IMG_2196 
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga akitoa maelezo jinsi kiwanda hicho kinavyofanya kazi zake kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (kushoto), Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum (kulia) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto kukagua miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa mjini Dodoma. (Picha na Modewjiblog).
Na Mwandishi wetu
Kutoratibiwa kwa mbegu za alizeti na ukosefu wa mitaji umeelezwa kuwa changamoto kubwa kwa wasindikaji wadogo wa mafuta ya mbegu ya alizeti katika kuendesha viwanda vyao kwa gharama nafuu.
Hayo yameelezwa na Wakala wa uendelezaji Kongano la Mafuta ya Alizeti wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo la Viwanda (UNIDO) Vedastus Timothy wakati akizungumza na waandishi wa habari walioambatana na Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez.
Mratibu huyo alikuwa Dodoma kwa shughuli mbalimbali za ukaguzi wa miradi pamoja na kuhudhuria shughuli za bunge la Tanzania lililomalizika jana.
Timothy alisema kwamba pamoja kuwepo kwa taarifa za kuwepo kwa mbegu za kutosha nchini Tanzania,hali halisi inayoelezwa na wasindikaji inaashiria kwamba sekta hairatibiwi vyema kwani wasindikaji hukaa muda mrefu bila kuwa na mbegu za kusindika.
Aidha alisema kwamba mbegu za alizeti zinazovunwa kuanzia Aprili hadi Julai na huwa na bei nafuu kipindi hicho lakini kama wasindikaji wakikosa mitaji na kununua mbegu chache, msimu unapoisha hawawezi tena kuendelea kufungua viwanda vyao.
Alisema kwamba wasindikaji hao wanakumbana na kiwango kikubwa cha riba kuanzia asilimia 20 kwenda juu , riba ambayo inakwamisha maendeleo ya viwanda hivyo.
IMG_2202 
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga (kulia), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto), Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (wa pili kushoto), Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum (katikati) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto (wa pili kulia) wakipata picha ya ukumbusho katika matanki ya kuhifadhia mafuta ya alizeti kiwandani hapo.
Hata hivyo alipoulizwa wanafanya nini katika kusaidia wasindikaji hao kukabiliana na hali hiyo alisema kwamba kupitia kongano hilo na Shirikisho la wasindikaji wadogo wa alizeti kanda ya mashariki na kati (CEZOSOPA). wana mipango ya kuwezesha wasindikaji hao kuwa na nguvu katika soko na kuwa na uwezo wa kupata mitaji bila gharama kubwa.
Aidha kupitia kongano hilo chama hicho kitawezeshwa uboreshwaji wa viwanda vya wanachama wake ili viweze kushindana na kukidhi viwango vya Shirika la Viwango nchini Tanzania (TBS).
Wakala huyo alisema hayo katika mahojiano yaliyofanyika kufuatia ziara ya mradi wa Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez kwenye kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products kilichopo katika kijiji cha Nzuguni, manispaa ya Dodoma, kinachonufaika na mradi wa ubia wa uboreshaji viwanda kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) na Wizara ya Viwanda na Biashara (TIUMP).
Kwa mujibu wa taarifa ya UNIDO, taasisi hiyo ya Umoja wa Mataifa inachangia kuimarika kwa sekta ya viwanda vidogo na vya kati vya usindikaji mafuta na kuviweka katika ushindani.
Aidha kupitia UNIDO ni viwanda hivyo vinawekwa katika hali ya kukua kuwa viwanda vikubwa.
IMG_2212 
Mfanyakazi wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya Alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Alpha Manyanga akiwa kwenye mashine ya kuchujia mafuta kiwanda hapo.
Katika ushirika wa aina hiyo ni matarajio ya mradi huo kufanikisha juhudi za kupunguza umaskini kama moja ya malengo ya maendeleo endelevu yanayotarajiwa na dunia.
Aidha katika upunguzaji huo wa umaskini mradi utachangia ongezeko la fursa za ajira na ukuaji wa uchumi.
Mkoa wa Dodoma wenye viwanda vya kusindika mbegu za alizeti vinavyofanyakazi katika mkaazi wakitumia zana dhaifu na vifungashia visivyokuwa na ishara yoyote ile na kuuza bidhaa zao kando mwa barabara wanahitaji mfumo thabiti wa ukuzaji wa shughuli zao na kueleweka.
Kutokana na mazingira hayo wajasirimali hawa hujikuta wakiingia hasara kubwa kwa kupoteza tija na pia soko lenye uhakika.
Kutokana na madhara hayo na pia kukosa hati ya ubora kwa kukosa mazingira yanayoruhusu hati hiyo kutolewa, TIUMP imelenga kusaidia wasindikaji hawa na teknolojia sahihi inayohitajika ili watoke pale walipo na kuwa na viwanda vidogo au vya kati.
Ingawa kwa sasa UNIDO inasaidia viwanda vinane vya mbegu za alizeti ili kuweza kuboresha bidhaa zao na utendaji kuna muonekano wa maendeleo makubwa siku za usoni hasa kwa wanachama wa CEZOSOPA ambao wameuinganishwa pamoja kwa ajili ya misaada mbalimbali ya kuwawezesha kuwa washindani katika soko.
IMG_2216 
Mtaalamu wa Chakula kutoka CEZOSOPA, Sophia Majid (aliyeipa mgongo kamera) akitoa maelezo kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto (kulia) walipokua wakikagua mtambo wa kusafisha mafuta (Semi re-finery) uliofadhiliwa na UNIDO kiwandani hapo.
UNIDO wanatumia maarifa waliyojifunza Ethiopia kuimarisha wanachama wa CEZOSOPA ambao tayari wamekubali kuunda kampuni ya pamoja na kuwekeza katika kitu wanachokifanya kwa pamoja kwa lengo la kuongeza uwezo na ushindani katika soko.
Halmashauri ya Chamwino tayari imekubali kuipa ardhi CEZOSOPA kwa ajili ya uwekezaji huo mkubwa.
Aidha UNIDO imewezesha kupatikana kwa teknolojia rahisi kwa ajili ya usafishaji wa mafuta ya alizeti na teknolojia hiyo inafanyiwa kazi na VETA.
UNIDO wamesema teknolojia hiyo hiyo inasaidia kuweka mafuta katika viwango vinavyotakiwa kitaifa na kimataifa na kwamba teknolojia hiyo tayari inafanyakazi nchini katika viwanda viwili na vingine saba vimeonesha nia ya kupata teknolojia hiyo.
Imeelezwa kuwa fedha za mradi huo zinapatikana kutoka UNIDO na wadau wengine kama SIDA na UNDAP.
IMG_2233 
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto akipozi kwa picha.
IMG_2237 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akifurahi jambo alipokuwa akipewa maelezo na Mtaalamu wa Chakula kutoka CEZOSOPA, Sophia Majid (kulia) ya mtambo mahususi wa kusafisha mafuta (Semi re-finery) uliofahdhiliwa na UNIDO.

KANDA YA KASKAZINI WAZINDUA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili kanda ya Kaskazini na Meneja Miradi wa Shirika lisilo la kiserikali la NAFGEM,Honorata Nasuwa akizungumza na wanahabari(hawako pichani ) juu ya uzinduzi huo,kushoto kwake ni Afisa Ushawishi na utetezi (KWIECO) na mratibu wa maadhimisho hayo kanda,Hilary Tesha.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi ya uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili kanda ya Kaskazini.
Baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Kilimanjaro wakifuatilia taarifa juu ya uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya siku 16 zakupinga ukatili na aliyekuwa Mwenyekiti wa dawati la Jinsia,Grace Lyimo akizungumza jambo katika kikao cha kamati hiyo na wanahabari.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa hiyo. Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MAZISHI YA MAWAZO BADO KIZUNGUMKUTI. CHADEMA KUTINGA MAHAKAMANI.

Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesitisha shughuli za mazishi ya aliekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoani Geita marehemu Alphonce Mawazo, baada ya jeshi la polisi Mkoani Mwanza kuzuia zoezi la kuuaga mwili wake lililokuwa limepangwa kufanyika juzi jumamosi Jijini Mwanza. 
Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Freeman Mbowe alibainisha hayo jana wakati akizungumza na Wanahabari Mkoani Mwanza, ili kutoa msimamo wa Chama baada ya kuwepo kwa mazungumzo baina yake na familia ya marehemu Mawazo. 
Alisema kuwa baada ya mazungumzo hayo, Chadema pamoja na familia ya marehemu Mawazo wamekubaliana kwenda Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kufungua shauri la kuomba tafsiri ya Kimahakama juu ya zuio hilo la jeshi la polisi kuzuia mwili wa marehemu Mawazo kuagwa Jijini Mwanza kabla ya Kwenda kuzikwa Kijijini kwake Chikobe katika Wilaya ya Busanda Mkoani Geita.
Nae Mchungaji Charles Lugiko ambae ni baba mlezi wa marehemu Mawazo, alisema anasikitishwa na hatua iliyochukuliwa na jeshi la polisi ya kuzuia mwili wa marehemu Mawazo kuagwa Jijini Mwanza ambapo ameeleza kuwa na matumaini makubwa ya kwamba mahakama itatenda haki juu ya suala hilo.
Frederick Sumaye pamoja na Edward Lowasa ambao ni Viongozi Waandamizi wa Chadema, walisema hatua ya jeshi la polisi kuzuia mwili wa Mawazo kuagwa Jijini Mwanza si sawa na kwamba inaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani. 
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza kupitia kwa Kamanda wake Charles Mkumbo, lilizuia zoezi la mwili wa marehemu Mawazo Kuagwa Jijini Mwanza, kwa madai kwamba limepokea taarifa za kiitelejensia za kuwepo baadhi ya vikundi vya watu kutumia mwanya huo kufanya fujo na hivyo kuhatarisha usalama wa raia na mali zao. 
Aidha Kamanda Mkumbo aliitaja sababu nyingine kuwa ni uwepo wa mlipuko wa Ugonjwa wa Kipindupindu Mkoani Mwanza, ambao umesababisha jeshi hilo kutoruhusu mikusanyiko ya aina yoyote inayoweza kusababisha ugonjwa huo kuenea zaidi kwa mjibu wa wataalamu wa afya ambapo lilishauri zoezi la kuaga mwili huo kufanyika Mkoani Geita ambapo mazishi ya marehemu Mawazo yatarajiwa kufanyika.
Katika uchaguzi uliomalizika hivi karibuni, marehemu Alphone Mawazo alikuwa mgombea ubunge Jimbo la Busanda Mkoani Geita kupitia Chadema, akiwa pia ni Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo ambapo aliuawa kikatili kwa kukatwa mapanga na mashoka na watu wasiojulikana jumamosi iliyopita ya Novemba 14 mchana huku kifo chake kikihusishwa na uhasama wa kisiasa.

WADAU WAJITOKEZA KUISAIDIA TIMU YA KIKAPU MBEYA

 Na Emanuel Madafa,Mbeya
Wachezaji
22 wa mpira wa kikapu Mkoa wa Mbeya, tayari wamefanikiwa kuondoka mkoani humo
kwa ajili ya  kushiriki mashindano ya
Taifa CUP, yatakayofanyika  Mkoani Dodoma  November 22 hadi November
30 mwaka huu.
Wachezaji
hao walishindwa kusafiri mapema kuelekea mkoani Dodoma
 kushiriki mashindano hayo  kutokana na kukabiliwa na uhaba wa fedha hali
iliyofanya kuwepo na maandalizi hafifu.
Aidha
kufanikiwa kwa timu hiyo kunatokana na kujitokeza kwa  Kampuni ya vinywaji baridi ya Coca Cola, Mkoa
wa Mbeya pamoja na Kampuni ya Tbl , amboa wamechangia kiasi kidogo cha fedha
kilicho fanikisha safari hiyo.
Akizungumzia
juu ya kupokea kwa ufadhiri huo Katibu wa chama  cha mpira wa kikapu mkoani Mbeya ambaye pia ni
mwalimu wa timu hiyo  , Yusuf Nyirenda, amesema
kuwa wanawashukuru wadau hao kwa kujitokeza   kwa kuchangia kiasi hicho
cha fedha .
Amesema kampuni ya  Coca Cola pekee imechangia kiasi cha shilingi
Mil 1.5 ambapo kwa upande wa Tbl  wamechangia kiasi cha shilini laki tano   hivyo
watajitahidi kutumia kaisi hicho kilicho patikana  ili kushiriki mashindano hayo.
Amesema,
tayari timu imekwisha ondoka   Mbeya November 21, ikiwa na wachezaji 22 kati
yao wanawake 11 na wanaume 11 lakini mpaka sasa  wamefanikiwa kupata
shilingi milioni 2  kati ya milioni
4,700,000 zinazohitajika.
“Kiasi
cha shiringi milioni 4,700,000 zinahitajika kwa ajiri ya usafiri wa kwenda na
kurudi, chakula, malazi na ada ya kushiriki mashindano haya,”alisema.
Amesema
kwa dhati kabisa anaipongeza kampuni ya Coca cola kwani ndio kampuni pekee
ambayo imekuwa ikijitoa mara kwa mara kusaidia timu hiyo .
Amesema
kutokana na mazingira hayo baadhi ya wachezaji watalazimika kujigharamia
wenyewe katika eneo la usafiri   hivyo, amewaomba wadau  na mashabiki wa mpira
huo, kuendelea kjitokeza kwa wingi katika kuichangia timu hiyo ili iweze kushiriki
mashindano hayo.
 
( Imeandaliwa na Mtandao wa www.Jamiimoja.blogspot.com- Mbeya 0759406070)

Tigo Yadhamini Gulio la Annual Charity Baazar

Meneja Mawasiliano wa Tigo, John Wanyancha akiongea na waandishi wa habari wakati wa gulio lililoandaliwa na wake wa mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania lenye lengo kusaidia jamii, Tigo ni wadhamini wa gulio hilo.
 
Mtoa huduma wa Tigo, Khalid Omary akitoa huduma kwa wateja wa Tigo kwenye gulio lililoandaliwa na wake wa mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania lenye lengo kusaidia jamii
Watoa huduma wa Tigo, Joshua Samuel na Judith Alfred wakitoa huduma kwa mteja wa Tigo, Justus Ndimbo mkazi wa Yombo Buza kwenye gulio lililoandaliwa na wake wa mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania lenye lengo kusaidia jamii
Kikundi cha sanaa cha Jumping Village kikitoa burudani kwenye gulio la lililoandaliwa na wake wa mabalozi lililofanyika Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST) Masaki.  

Kikundi cha sanaa cha Jumping Village kikitoa burudani kwenye gulio la lililoandaliwa na wake wa mabalozi lililofanyika Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST) Masaki.  

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWASILI DAR

index 
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakipokea shada la maua kutoka kwa Immaculata Warqaso wa Ofisi ya Waziri  baada ya kuwasili kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam Novemba 22, 2015 wakitoka Dodoma.Wapili kulia ni Katibu Mkuuwa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt Florence Turuka. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

ZIARA YA RAIS WA ZANZIBAR FUMBA

SE2
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipata maelezo kwa ufupi kutoka kwa  Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Bw.Said Salim Bakhresa alipowasili Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi jana katika ziara ya kutembelea maeneo ya ujenzi wa Mji mpya wa Nyumba za kisasa zinazojengwa na Kampuni ya Azam Group kwa kushirikiana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,(kushoto) Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar Nd,Salum Khamis Nassor [Picha na Ikulu.]
SE3
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipata maelezo kwa ufupi kutoka kwa  Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Bw.Said Salim Bakhresa alipowasili Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi jana katika ziara ya kutembelea maeneo ya ujenzi wa Mji mpya wa Nyumba za kisasa zinazojengwa na Kampuni ya Azam Group kwa kushirikiana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,(kushoto) Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar Nd,Salum Khamis Nassor [Picha na Ikulu.]
SE4
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kwa ufupi kutoka kwa  Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Bw.Said Salim Bakhresa alipowasili katika eneo linalotarajiwa kujwga kiwanda cha utengezaji wa Lami katika Kijiji cha Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi jana katika ziara ya kutembelea maeneo ya ujenzi wa Mji mpya wa Nyumba za kisasa zinazojengwa na Kampuni ya Azam Group  kwa kushirikiana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
SE5
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Bw.Hudhaifa Yussuf Ali Mchoraji wakati alipokuwa akiangalia zamani za ujenzo wa Nyumba za kisasa zitakazojengwa katika fukwe za Kijiji cha Fumba Mkoa wa Magharibi Unguja alipokuwa katika ziara maalum ya kutembea maeneo hayo jana,ujenzi huo utafanyika kwa ushirikiano wa Kampuni ya Azam Group na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
SE6
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) akifuatana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Bw.Said Salim Bakhresa (katikati) Mkuu wa Wilaya ya Magharibi A. Bw.Ayoub Mohammed Mahmoud (kushoto)   na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar Nd,Salum Khamis Nassor wakati alipofanya ziara maalum  ya kutembelea maeneo ya ujenzi wa Mji mpya wa Nyumba za kisasa zitakazojengwa na Kampuni ya Azam Group kwa kushirikiana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,[Picha na Ikulu.]
SE8
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar Nd,Salum Khamis Nassor wakati alipokuwa akiangalia ramani ya Ujenzi wa Nyuma za Kisasa zitakazojengwa na Kampuni ya Azam Group kwa kushirikiana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika maeneo ya fukwe za Kijiji cha Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja alipofanya ziara maalum,[Picha na Ikulu.]
SE9
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Group Bw.Said Salim Bakhresa alipowasili Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi jana katika ziara ya kutembelea maeneo ya ujenzi wa Mji mpya wa Nyumba za kisasa zinazojengwa na Kampuni ya Azam Group kwa kushirikiana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, [Picha na Ikulu.]
SE10
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na viongozi mbali mbali wakati alipowasili Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi jana katika ziara ya kutembelea maeneo ya ujenzi wa Mji mpya wa Nyumba za kisasa zinazojengwa na Kampuni ya Azam Group kwa kushirikiana na Serikali nya Mapinduzi ya Zanzibar [Picha na Ikulu.]

RAIS DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI BAADA YA KUMUAPISHA WAZIRI MKUU MHE. MAJALIWA KASSIM MAJALIWA MJINI DODOMA

index1
Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu mpya Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa mara baada ya kumuapisha mwishoni mwa wiki katika Ikulu Ndogo ya Chamwino mjini Dodoma. Wengine kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zandibar Dkt Abdulhamid Yahya Mzee, Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Balozi Ombeni Sefue, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe Mohamed Chande Othman, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Pandu Ameir Kificho na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Mkungu.
index2
Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu mpya Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa mara baada ya kumuapisha mwishoni mwa wiki katika Ikulu Ndogo ya Chamwino mjini Dodoma.
PICHA NA IKULU

DC MAKONDA AZUNGUMZIA KIFO CHA KATIBU WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI MADEREVA TANZANIA (TADWU) 

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye ni mlezi wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi nje ya chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa ya kuhusu kifo cha utata cha aliyekuwa Katibu wa chama hicho Tanzania, Rashid Saleh kilichotokea hivi karibuni pamoja na ratiba ya mazishi yake yatakayofanyika jijini Mwanza.
 Marehemu, Rashid Saleh
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye ni mlezi wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADU), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Pubrishers LTD, Eric Shigongo (katikati), na wadau wengine kuhusu taratibu za mazishi za katibu huyo.
 Mjumbe wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Stanley Kilave (kulia), akizungumza na Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Clement Masanja (kushoto), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Pubrishers LTD, Eric Shigongo (katikati), wakati wa taratibu za mazishi zikifanyika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dar es Salaam leo.
 Msemaji wa familia ya marehemu, Jonas Marinyizu (katikati), akitoa shukurani kwa DC Makonda na wadau wengine kwa kuwezesha msiba huo pamoja na utaratibu wa mazishi utakavyo kuwa. Mwenyekiti wa Chama hicho, Shaban Mdem akizungumza katika mkutano na wanahabari
 Ndugu na jamaa wa marehu wakiwa katika chumba za kuhifadhi maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakisubiri kufanyika taratibu cha uchunguzi wa mwili huo kabla ya kusafirishwa kwenda jijini Mwanza kwa mazishi.
Ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu wakiwa katika chumba za kuhifadhi maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakisubiri kufanyika taratibu cha uchunguzi wa mwili huo kabla ya kusafirishwa kwenda jijini Mwanza kwa mazishi.
…………………………………………………………………………………………………
Na Dotto Mwaibale
 
MWILI wa Katibu Mkuu na Msemaji wa Chama Cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Rashid Saleh umesafirishwa jana kwenda kijijini kwao Kayenze wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza kwa maziko.
 
Saleh alifariki jana Novemba 20 Majira ya saa 8 mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wakati akipata matibabu ya maradhi ya figo ili kuokoa maisha yake baada ya kile kinachodaiwa kushindwa kufanya kazi ipasavyo.
 
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambaye pia ni mlezi wa chama hicho, Paul Makonda alisema kuwa wamepata pigo kutokana na umuhimu na umahiri ambao alikuwa nao marehemu hasa katika kutetea haki za madereva wenzake sanjari na kuibua mambo mbalimbali ambayo yatabaki kuwa historia na kumbukumbu kwao.
 
“Saleh alifariki jana (Novemba 20) baada ya kusikia anaumwa ambapo hali yake haikuwa nzuri na madaktari walishauri nimlete Muhimbili kwa matibabu zaidi ambapo nilimfikisha lakini baada ya muda mfupi wakati madaktari wanahangaika kumtibu na kuokoa maisha yake alifariki,”alisema.
 
Alisema marehemu amekiacha chama sehemu ya mafanikio makubwa zaidi ya mabadiliko na mikataba ya haki za madereva nchi nzima huku akibainisha mazingira ya kifo na kutaka uchunguzi zaidi ili kujiridhisha na kifo chake uliofanywa chini ya uangalizi wa polisi.
 
“Hatukuona kama kuna haja ya kumuhifadhi mwili wa ndugu yetu hadi hapo tutakapojua nini chanzo cha kifo chake kwani majibu ndiyo yatatupa picha ya ugonjwa kwani tumehangaika tangu alipokuwa hospitali ya Kairuki ambapo tulipofika hapa ikabainika kuwa figo zake zote mbili hazifanyi kazi,”alisema.
 
Aliongeza kuwa marehemu alipelekwa hospitalini hapo kwa kitengo maalum huku akibainisha endapo figo zinashindwa kufanya kazi mzunguko mzima wa damu mwilini nao husimama ambapo madaktari walishirikiana lakini hawakuweza kuokoa maisha yake.
 
Mwenyekiti wa Chama hicho, Shaban Mdem alisema kuwa msiba huo umewasikitisha sana kutokana na mazingira ya kifo chake huku akiitaka mamlaka husika kulisimamia suala hilo la kupatika kwa majibu sahihi juu ya kifo chake.
 
“Tunataka uchunguzi ufanyike na majibu yatoke yakiwa sahihi na yanayoridhisha juu ya kifo chake kwani amekufa na madai ambayo yapo ndani yao, hivyo serikali itambue kifo cha Saleh ni katika harakati za kudai haki ambayo tuliyawasilisha mbele ya aliyekuwa waziri mkuu Mizengo Pinda,”alisema. 
Alisema Saleh ni kiongozi wa taifa zima hivyo alimtaka rais Magufuli kuingilia kati suala hilo kwani kutokana na hali hiyo watamaliza wafanyakazi wote kwa kuwauwa katika mazingira kama hayo sambamba na kutenga siku rasmi kwa ajili ya maombezo ya msemaji huyo.
 
Mazingira ya Kifo
 
Akizungumzia mazingira ya kifo Msemaji wa Familia ya Marehemu Jonas Ernest alisema kuwa Novemba 9 mwaka huu marehemu alipokea simu kutoka kwa rafiki yake ma kumtaka waende kwenye kikao, ambapo baada ya hapo mwenzake alidai kuwa na njaa.
 
Alidai baada ya hapo walikwenda kuagiza chakula ambapo mwenzake hakula na kumuacha marehemu akiwa anakula huku mwenzake akiwa amemuaga kwenda msalani.”Baada ya kurudi msalani alimkuta marehemu akilalamika tumbo linamuuma na hivyo kuondoka eneo hilo pasi na huyo rafiki kula chochote,”alisema.
 
Alidai kuwa baada ya kuhisi maumivu makali ya tumbo alianza kuharisha na kutapika na alikimbizwa hospitali lakini uchunguzi ulibaini hakuwa na tatizo na kurudishwa nyumbani ambapo siku inayofuata alirudi hospitali na kuambiwa kuwa ana malaria 4.
 
“Alianza kutumia dawa za malaria na baadaye kujiskia vibaya na kumrudisha tena hospitali ya Kairuki laikini madaktari walidai kuwa anatatizo ndani ya mwili ambalo ni figo kushindwa kufanya kazi vizuri,”alidai na kuongeza kuwa hadi marehemu anafariki alikaririwa akidai kuwa”Nyama inanitenganisha na mwanangu lakini”na kumtaja mmoja wa wafanyakazi wenzake huku akidai kumuona mtoto wake.  
 
Harakati za kudai haki ya madereva
 
Saleh alizaliwa mwaka 1966 Mwanza, ambapo hadi anafariki alikuwa katika harakati za kudai na kutetea haki za madereva ambapo Oktoba 2, mwaka huu alikaririwa akisema wamechoshwa na uozo unaoendelea kufanywa na Mamlaka ya Usafirishaji Majini na Nchi Kavu (Sumatra) na Wizara ya Kazi na Ajira kuhusu kufumbia macho kero zinazoitatiza sekta ya usafirishaji hasa kwa madereva wa mabasi ya abiria na magari ya mizigo.

Wanafunzi wenye mahitaji maalum vyuo vikuu waaswa kutumia vyema utaalamu walioupata kuendesha maisha yao

fr1
Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Balozi Nicholas Kuhanga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu Bora wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) wakati wa Mahafali ya nane ya chuo hicho yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Profesa William Anangisye, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Lwekaza Mukandara na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) Bw. Peter Kuhanga.
 Picha na Frank Shija, MAELEZO
fr5
Baadhi ya wahitimu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) wakifuatilia hotuba mbalimbali wakati wa Mahafali ya nane ya Chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo jana.
fr7
Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ,Balozi Nicholas Kuhanga akiwatunuku Shahada wahitimu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) (hawapo pichani) alipokuwa mgeni wa Chuo katika Mahafali ya nane ya chuo hicho jana jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Bw. Peter Ngumbulu.
fr11
Muhitimu wa mwaka wa tatu ambaye ameongoza kwa ufauli kwa kupata GPA ya 4.8 Bi. Ummul Kheir Mustafa akipongezwa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Bw. Peter Ngumbulu mara baada ya kupokea zawadi yake ikiwemo kukabidhiwa Cheti chake mbele ya hadhara wakati wa Mahafali ya nane ya chuo hicho jana jijini Dar es Salaam. Muhitimu huyo amekuwa mwanafunzi wa kwanza kunufaika na mpango wa chuo hicho wa kutoa fursa ya kuajiriwa chuoni hapo kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katka masomo yao ikiwa ni njia ya kukabiliana na uhaba wa wanataaluma chuo hapo.
fr12 
Muhitimu wa mwaka wa tatu ambaye ameongoza kwa ufauli kwakupata GPA ya 4.8 Bi. Ummul Kheir Mustafa akionyesha Cheti chake cmbele ya hadhara mara baada ya kuwa muhitimu wa kwanza kukabidhiwa cheti wakati wa Mahafali ya nane ya chuo hicho jana jijini Dar es Salaam. Mbali na kukabidhiwa Cheti chake cha Shahada papo hapo muhitimu huyo amekuwa mwanafunzi wa kwanza kunufaika na mpango wa chuo hicho wa kutoa fursa ya kuajiriwa chuoni hapo kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katka masomo yao ikiwa ni njia ya kukabiliana na uhaba wa wanataaluma chuo hapo. 
fr2
Mgeni rasmi  wa Mahafali ya nane ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaama (DUCE) Profesa Martha Qorro akizungumza wakati wa Mahafali hayo yaliyofanyika jana chuoni hapo. Katika mahafali hayo jumla ya wahitimu 1156 walitunukiwa Shahada na Stashahada za juu.
………………………………………………………………………………………………..
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Wanafunzi wenye mahitaji maalum wanaosoma vyuo vikuu nchini wameaswa kutumia elimu wanayoipata kuendesha maisha yao ili waweze kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla.
Hayo yamesemwa na Prof. Mshiriki wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Kituo cha Studi za Mawasiliano Martha Qorro ambaye alikuwa Mgeni Mashuhuri wakati wa Mahafali ya nane ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaama (DUCE) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaaam.
Prof. Qorro alisema kuwa mwamko wa wanafunzi wenye mahitaji maalum kujiunga na elimu ya juu nchini ni mzuri licha ya changamoto zinazowakumba wanafunzi hao wanapokuwa chuoni.
“Hawa ni wanafunzi wenye uelewa mzuri wakipata mahitaji yao ya lazima yakiwemo fimbo nyeupe, vifaa vya kuandikia kwa kutumia nukta nundu, baiskeli za miguu mitatu, viti maalu na mahitaji mengine ya kijamii” alisema Prof.Qorro.
Prof.Qorro aliongeza kuwa ni wajibu wa vyuo vikuu nchini kikiwepo Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam kuwasisitiza kwa kuwauliza wanafunzi wanapojaza fomu za kujiunga waoneshe kuwa wanamahitaji maalum ili waandaliwe mahitaji hayo ikiwemo usafiri wa bajaji ndani ya chuo ili kuwawezesha kuwahi vipindi vyao katika maeneo mbalimbali ndani ya chuo.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Profesa William Anganisye alipokuwa akitoa taarifa fupi kuhusu mafanikio chuo wakati wa Mahafali hayo alisema kuwa chuo hicho kimetimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake ambapo hadi sasa wamehitimu wanafunzi zaidi ya 8000 na jumla ya wahitimu 1156 walitunukiwa Shahada na Stashahada za juu katika mahafali hiyo ya nane.
Naye muhitim wa mwaka wa tatu katika ngazi ya shahada ya ualimu katika masomo ya sanaa Andrea Sanga ambaye pia ni mwanafunzi mwenye mahitaji maalum (mlemavu asiyeona) alisema kuwa mafanikio yake katika masomo yametokana na kuheshimu ratiba kuu ya masomo chuoni hapo pamoja na ratiba yake binafsi ya kujisomea.
Zaidi ya hayo, Sanga alisema kuwa maktaba ya chuo, ushirikiano mzuri kati yake na wanafunzi wenzake na walimu wake, kuhudhuria semina na kufanya kazi kwa wakati na kupunguza msongamano wa kazi nyingine ndiyo vimekuwa dira yake kuu ya mafanikio.

MSD YAPELEKA MOI VIFAA VYENYE THAMANI YA SH.MILIONI 251 ZILIZOKUWA ZITUMIKE KUJIPONGEZA WABUNGE

 Magari ya Bohari ya Dawa (MSD), yakishusha vifaa tiba Taasisi ya Moi kufuatia agizo la Rais Dk.John Magufuli kulitaka Bunge kutumia sh.milioni 15 kwa ajili ya kujipongeza na fedha zilizobaki kuzipeleka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kukabiliana na uhaba wa vifaa tiba na magodoro. 
Na Dotto Mwaibale
…………………………………………………………………………
BOHARI ya Dawa (MSD) imeanza kupeleka Vifaa Tiba kwenye Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI), Vifaa ambavyo vimenunuliwa na Ofisi ya Bunge kwa agizo alilotoa Rais Dk. John Magufuli.
 
Vifaa hivyo vilianza kupelekwa juzi katika Taasisi hiyo ili kukabiliana na uhaba alioubaini Rais  Magufuli baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika mapema mwezi huu.
 
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu akizungumzia kuhusu vifaa hivyo jijini Dar es Salaam juzi wakati wa usambazaji alisema  hivyo vyenye gharama ya sh.milioni .251 ni pamoja na vitanda 300, magodoro 300, viti vya kusukuma (Wheel Chairs) 30, vitanda vya kubebea wagonjwa (Stretchers) 30, mashuka 1,695 na mablanketi 400.
 
Alisema MSD ilianza kupeleka Vifaa hivyo MOI mwishoni mwa wiki na kuwa itaendelea kutoa vifaa hadi wiki hii inayoanza leo.
 
Fedha hizo zilizotumika kununulia vifaa hivyo zilitokana na agizo la Rais Dk.John Magufuli alilolitoa wakati akilihutubia bunge mjini Dodoma mwishoni mwa wiki ambapo alilitaka bunge kutumia sh.milioni 15 tu kwa ajili ya kujipongeza na kiasi hicho kilichobaki kitumike kununulia vifaa hivyo

MKUTANO WA WANASHERIA MAWAKILI AFRIKA MASHARIKI KUFANYIKA ZANZIBAR

AAEAAQAAAAAAAAKIAAAAJDVhYzk2MDUyLTgzZTgtNDUxMi05ZmRlLWE3NDRmMzYyMmY1Mg
Na RAMADHANI ALI/MAELEZO ZANZIBAR  
Chama cha Wanasheria Mawakili Zanzibar kimepata heshma ya kuwa mwenyeji wa Mkutano wa siku mbili wa mwaka wa Wanasheria Mawakili wa Nchi za Afrika Mashariki utakaoanza  tarehe 27 Mwezi huu katika Hoteli ya Sea Cliff Resort.
Akizungumza na waandishi wa Habari Ofisini kwake Bwawani, Katibu Mkuu wa Chama cha Wanasheria Mawakili Zanzibar Omar Said Shaaban amesema mkutano huo utawashirikisha zaidi ya Wanasheria 400 kutoaka Nchi zote wananchama wa Afrika Mashariki na Mataifa mengine Duniani.
Amesema kwa kawaida Jumuiya ya Wanasheria Mawakili wa Nchi za Afrika Mashariki inawachama wa aina mbili ambao ni wanasheria wenyewe binafsi na Jumuiya za kila Nchi nazo huwa ni mwanachama wa pili.
Katibu Mkuu wa Wanasheria Mawakili Zanzibar amesema Mkutano huo utakuwa na malengo ya kubainisha kuwa Taaluma ya sheria kama kichocheo cha Biashara na Uwekezaji ambapo mada mbali mbali zitawasilishwa.
Amezitaja baadhi ya mada zitakazowakilishwa katika mkutano huo ni pamoja na Kada ya Sheria kama biashara, muundo mzima wa Biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki na mada nyengine ni masuala ya rushwa na vipato visivyohalali.
Ametoa wito kwa wananchi wa Zanzibar kuupokea ugeni huo mkubwa wa wanasheria na kuonyesha ukarimu uliozoeleka kwa wageni na kutumia fursa ambazo zitapatikana kutokana na kuwepo kwao hapa nchini.
Amesema chama kwa upande wake tayari kimeliarifu Jeshi la Polisi kuhusu ugeni huo kwa lengo la kuimarisha hali ya usalama wakati wote wa mkutano.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wanasheria Zanzibar amesema Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu atakuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano huo.

WAZIRI MKUU MAJLIWA AKISALIMIANA NA VIONGOZI WA MOROGORO

index 
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakisalimiana na viongozi wa mkoa wa Morogoro wakati waliposimama kwa muda mjini  Morogoro wakiwa njiani kuelekea Dar es salaam wakitoka Dodoma Novemba 22, 2015. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Rajabu Rutengwe (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments :

Post a Comment