Friday, May 1, 2015

UCHAGUZI CCM 2015: Profesa Sospeter Muhongo, Mbunge wa Kuteuliwa

WASIFU Umri:  61 Elimu: Shahada ya Uzamivu (PhD) ya Jiolojia, Chuo Kikuu cha Ufundi cha Berlin, Ujerumani. Kazi: Mbunge wa Kuteuliwa 
Na Julius Mtatiro
Kwa ufupi
  • Profesa Muhongo amewahi kuwa Makamu wa Rais wa Tume ya Ramani ya Jiolojia ya Dunia (CGMW), Mhariri Mkuu wa Jarida la Afrika la Sayansi za Miamba na Madini (The Journal of African Earth Sciences, Elsevier) na hadi sasa ni mjumbe wa bodi kadhaa za uhariri wa majarida ya sayansi, teknolojia na ubunifu.


Historia yake
Profesa Sospeter Muhongo alizaliwa katika Wilaya ya Musoma Mjini, mkoani Mara Juni 25, 1954 (atatimiza miaka 61 Juni mwaka huu). Alianza shule ya msingi mkoani Mara na kuendelea na masomo ya sekondari (kidato cha I – VI) katika shule mbalimbali hapa nchini.
Alichaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuhitimu Shahada ya Jiolojia. Kwa sababu ya ufaulu wa hali ya juu, alipata ufadhili kirahisi, kwenda kusoma shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Gӧttingen, Ujerumani na baada ya kuihitimu, aliendelea na Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Ufundi cha Berlin akibobea katika eneo hilohilo la jiolojia ambako alihitimu.
Katika maisha yake ya kitaaluma, amewahi kupokea na kutunukiwa tuzo nyingi, achilia mbali ushiriki wake katika mambo mengi ya kitafiti. Serikali ya Ufaransa ilimtunukia Cheo cha Ofisa Mwenye tunu ya Kitaaluma Iliyotukuka - Ordre des Palmes Académiques (Iliyoanzishwa na Mfalme Napoleon Mwaka 1808).
Mwaka 2004, alipokea tuzo inayoheshimika kwa jamii ya wanajiolojia wa Afrika ya Profesa Robert Shackleton (UK) (Geological Society of Africa’s prestigious Professor Robert Shackleton Award), kwa ajili ya utafiti wa kipekee kuhusu jiolojia ya Afrika ya miamba yenye umri wa zaidi ya miaka milioni 500 (Precambrian Geology of Africa).
Amekuwa Mshiriki wa Ngazi ya Juu (Fellow) wa Akademia ya Sayansi ya Nchi zinazoendelea (FTWAS), Chama cha Wanajiolojia wa Afrika (FGSAf), Akademia ya Sayansi ya Afrika (FAAS) na Akademia ya Sayansi ya Tanzania (FTAAS).
Profesa Muhongo amewahi kuwa Makamu wa Rais wa Tume ya Ramani ya Jiolojia ya Dunia (CGMW), Mhariri Mkuu wa Jarida la Afrika la Sayansi za Miamba na Madini (The Journal of African Earth Sciences, Elsevier) na hadi sasa ni mjumbe wa bodi kadhaa za uhariri wa majarida ya sayansi, teknolojia na ubunifu.
Pia, Profesa Muhongo amewahi kuwa Rais wa Chama cha Wanajiolojia wa Afrika (1995-2001), Mkurugenzi Mwanzilishi (2005-2010) wa Ofisi ya Sayansi ya Kanda ya Afrika (ICSU) yenye Makao Mkuu yake Pretoria, Afrika Kusini, Mwenyekiti wa Bodi ya Unesco-IUGS-IGCP Programu ya Kimataifa ya Sayansi ya Jiolojia (2004 - 2008) na Mwenyekiti wa Kamati ya Programu ya Kisayansi (SPC) ya Mwaka wa Kimataifa wa Sayari ya Dunia uliotangazwa na Umoja wa Mataifa (UN-IYPE) mwaka 2007-2010.
Mwaka 2009, Profesa Muhongo aliteuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa mgombea wa nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Unesco na alikuwa miongoni mwa wasomi mashuhuri wanne walioingia kwenye mchujo wa mwisho, japokuwa hakupewa wadhifa huo.
Mwaka 2014, alishinda tuzo ya Heshima ya Jamii ya Wanasayansi wa Jiolojia na Uchimbaji Petroli na Gesi Asilia ya Nigeria (NMGS)/AMNI ya Profesa M.O. Oyawaye.
Nguli huyu anazungumza lugha nne kubwa, Kiswahili, Kiingereza, Kijerumani na Kifaransa na amemuoa Bertha Mamuya - wana kijana aitwaye Rukonge na wanawalea watoto yatima watatu.
Mbio za ubunge
1 | 2 | 3 | 4 | 5 Next Page»

No comments :

Post a Comment