Monday, March 4, 2013

Mchango wa wazee kwenye uchumi wa taifa



 PHOTO | PHOEBE OKALL Voters queue to cast their ballots on March 4, 2013 at Garissa Township Primary School in Garissa County.
 By NATION TEAM newsdesk@ke.nationmedia.com  
 na Christian Gaya majira Machi 05,2013
Zaidi ya asilimia hamsini ya milioni mbili ya watoto yatima na watoto wanaishi kwenye mazingira hatarishi wanategemea wazee kupata mahitaji muhimu kama vile chakula, tiba na mahitaji muhimu ya elimu. Kwa maana hiyo wazee ni msingi wa muhimu sana kwa makuzi ya mamilioni ya watoto kwa sasa na siku zijazo. Pamoja na hayo ingawa mtandao usio rasmi wa hifadhi ya jamii unaendelea kubadilika lakini unazidi kumwachia akina bibi wazee kuwa ndiyo wanatunza watoto ambao hata shule hawajaanza hata madarasa ya awali au darasa la kwanza.

Uchumi wa kizazi cha vijana wa sasa unawafanya vigumu kufanya  maamuzi ya kujikimu wenyewe na familia zao kwa vile kwa sababu kila siku jamii ya kitanzania inazidi kuongezeka kumomonyoka na kutawanyika, mwongezeko wa idadi ya wazee inafanya kuwa ni msingi imara wa familia pana.

Wazee wanaume kwa wanawake wametoa mchango mkubwa kwa jamii ya kitanzania kwenye mabadiliko mbalimbali katika ngazi ya kanya, jumuia na kitaifa. Wazee wameweza kuchangia katika uchumi wa taifa moja kwa moja au kupitia katika maisha yao yote waliyokuwa wakifanyia kazi serikalini, kwenye makampuni ya watu binafsi, kazi za kilimo na ufugaji na madini lakini pamoja na hayo karibu asilimia sabini na tano ya wazee wanaendelea kuchapa kazi vizuri kabisa pamoja na umri    w a uzee waliokuwa nao.  

 Kipato cha wazee mara nyingi imekuwa ikiwekezwa kwa ajili ya maendeleo ya vizazi vya vijana. Ingawa wazee wengi wanaishi maeneo ya vijijini na kufanya kazi sehemu za sekta zisizo rasmi ni muhimu kutambuliwa kuwa wengi wao bado wanaendelea kuchangia kwenye pato la taifa kwa njia ya kutoa kodi za aina mbalimbali kama vile kwa njia ya bidhaa zenye kodi ambazo wazee wanazinunuliwa sokoni kila siku.

Katika ngazi ya kaya wazee wanaume kwa wanawake wanatoa mchango mkubwa kwa ajili ya mtaji na rasilimali ya maendeleo watu katika nchi. Mara nyingi wazee wamejishughulisha katika kazi zisizo na malipo yeyote hasa zile za kuangalia watoto kwa ajili ya familia zao, kwa kufanya hivyo wamekuwa wakisaidia kaya nyingi kuongeza uzalishaji na ufanisi wa kazi pamoja na kuongeza maendeleo ya rasilimali mtu. Ingawa hivi karibuni wazee wameonekana kwa muda wote wamekuwa wakiongezeka wakishushughulika na uangalizi wa kulea watoto.  Voters wait their turn to cast the ballot at the Manyatta Primary School polling station in Kisumu on Monday. Experts say a smooth transition will see accelerated economic growth, helping the next government to deal with problems like unemployment. Photo/Tom Otieno

Watoto na wajukuu wanaweza kwenda mijini kutafuta kazi za kujiajiri au kuajiriwa, lakini mara nyingi wanarudi tena kwa wazee. Na mchango mkubwa wa wazee umekuwa ukionekana kwenye ngazi ya jumuia. Hesabu nyingi zinaonekana kutoka kwa madiwani na wajumbe wa jumuiya zinaeleza ni jinsi gani wazee wanavyochangia kutoa elimu muhimu ya malezi inayojenga misingi imara ya kukuza vijana kwa njia iliyokuwa rasmi na ile isiyokuwa rasmi.

Vilevile wanasifiwa kwa kutunza mila na desturi za urithi kutoka kwa mababu na bibi zetu na kwa mchango mkubwa kwa kuhamasisha mshikamano ndani ya jamii katika kutatua migongana. Wazee hasa wanaume wana uzoefu mkubwa wa kutoa upatanisho kati ya mivutano au mgogoro ya kaya na kaya. Kumbukumbu zao za madeni na malipo na ugumu wa uhusiano wa kiuukoo ni mambo muhimu sana kwa jumuia na ambayo inategemea zaidi makubaliano yaliyokuwa sawa sawa kijamii

Akina bibi wazee wanasaidia kaya mabalimbali zisizo kuwa rasmi na zingine zilizoko kwenye jumuia mbalimbali kwa kuwajali na kuwatunza vitoto vichanga na watoto kuwawezesha wanawake wengine wenye nguvu kufanya kazi za uzalishaji mali. Kwa kufanya hivyo rasilimali za kaya zinaweza kuelekezwa kwenye huduma ya matibabu au kulipa gharama za matibabu kuliko kuwekeza kwa watoto.

Utafiti  uliofanywa huko vijijini nchini Tanzania inaeleza kuwa watoto wenye wazazi ambao ni dhaifu kiakiri, na kimawazo ni rahisi sana kusababisha hao watoto kuacha shule na kutumia masaa machache sana kwa ajili ya shule. Lakini ni vizuri kutambua ya kuwa ni mara nyingi hawa wazee ya kwamba wanatunzwa na watoto

No comments :

Post a Comment