Pages

Friday, July 20, 2018

WEMA SEPETU AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MWAKA MMOJA JELA, AU FAINI YA SH. MILIONI 2



MSANII wa filamu Wema Sepetu, maarufu kama “Madame” amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja (1) jela baada ya kupatikana na hatia ya kutumia madawa ya kulevya aina ya Bangi.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imetoa hukumu hiyo leo Julai 20, 2018 na kwamba Wema pia anayo nafasi ya kulipa faini ya shilingi milioni 2 ili kukwepa kifungo hicho.

Aidha Mahakama imewaachia huru watumishi wake wawili baada ya kuwaona hawana hatia.

Msanii Wema Sepetu alijikuta matatani baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, kuanzisha operesheni kali ya kuwasaka watumiaji, wauzaji, waingizaji na wasambazaji wa dawa za kulevya za aina zote, ambapo watu kadhaa walijikuta matatani akiwemo Wema.
Hata hivyo Wema aliweza kulipa faini hiyo na kuachiwa huru.

No comments:

Post a Comment