Pages

Friday, July 20, 2018

WAZIRI UMMY MWALIMU APIGA MARUFUKU WATOTO CHINI YA MIAKA MITANO KUTOZWA FEDHA ZA KUMUONA DAKTARI NA VIPIMO HOSPITALI YA MAWENI MKOANI KIGOMA


  WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy mwalimu, ametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma (MAWENI), na kujionea changamoto mbalimbali zinazoikabili hospitali hiyo kongwe kabisa hapa nchini.
Mhe. Ummy Mwalimu ameandika katika ukurasa wake wa Facebook kuwa “Ameridhishwa na hali ya utoaji huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma, Maweni. Ingawa kuna changamoto ya Uhaba wa watumishi na uchakavu wa miundombinu.” Anasema Mhe. Ummy mwalimu.
Mhe. Waziri amesema, Mwaka huu 2018/19 Serikali imetenga shs bilioni 1.1 kwa ajili ya kuboresha Miundombinu. Pia mwezi huuwa saba (July) Wizara yake itapeleka watumishi wapya 34 wakiwemo madaktari 7 na wauguzi 17.
Aidha Mhe. Waziri ameonyesha kuchukizwa na kitendo cha uongozi wa Hospitali hiyo wa kuwatoza fedha watoto chini ya miaka mitano kitu ambacho ni kinyume na miongozio ya wizara hoyo.
“Naagzia ni marufuku kuwatoza fedha wagonjwa wenye umri chini ya miaka mitano za vipimo au kumuona daktari.” Alisema na kuamuru mkazi mmoja aliyefika hospitalini hapo akiwa na motto wake mwenye umri chini ya miaka mitano (5), ambaye alilipa fedha za kumuona daktari na vipimo, arudishiwe fedha zake mara moja.
Hata hivyo Mheshimiwa Waziri amefurahi kuona Madaktari Bingwa wakitoa huduma ktk Hospitali hiyo.
Aidha Mhe. Waziri amesema Wizara yake imedhamiria kuboresha huduma ktk Hospitali za Rufaa za Mikoa. "Moja ya mikakati yetu ni kuhakikisha uwepo wa Madaktari Bingwa ktk fani za kipaumbele ambazo ni Upasuaji (General Surgery), Magonjwa ya Wanawake na Uzazi (Obstetrics & Gynaecology), Magonjwa ya Watoto (Paediatrics & Child Health), Magonjwa ya ndani (Internal Medicine), Magonjwa ya Kinywa na Meno (Dentistry) na Radiolojia (Radiology). Hivi sasa tunaweka mazingira mazuri kuvutia Madaktari Bingwa na Watumishi wengine wa Afya kufanya kazi mikoa ya pembezoni ikiwemo Kigoma. Aidha Ninawataka Watumishi wapya wote waliopangwa kufanya kazi mikoa ya pembezoni ikiwemo Kigoma waripoti katika Vituo Vyao. Hatutabadilisha Vituo. Utumishi wa Umma ni Popote. Muhimu zaidi watu wa mikoa hii nao wana haki ya kupata huduma bora za Afya" Alibainisha 




Mhe. Waziri Umy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na  Dkt. Osmund Dyegura (Upasuaji), Dkt. Lameck Mdengo (Magonjwa ya Wanawake na Uzazi), Dlt. Macrive Yakayashi (Magonjwa ya Watoto), Dlt. Sunday Dominico (Magonjwa ya Wanawake na Uzazi
Waziri wa Afya,Maendekeo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akipanda kivuko kuelekea kijiji cha Mwamgongo ziwa Tanganyika kuweka jiwe la Msingi katika Zahanati ya kijiji hicho pia kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika zahanati hiyo.Waziri Ummy Mwalimu akiendelea na ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya Mkoani Kigoma

No comments:

Post a Comment