Pages

Monday, July 23, 2018

WANANCHI WA BUZA WAISHUKURU SERIKALI

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akizungumza na wananchi  alipokuwa akikagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
 Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani) alipofanya ziara ya kukagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akizungumza na wananchi  alipokuwa akikagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
  Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani).
  Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani) alipofanya ziara ya kukagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
 Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani) alipofanya ziara ya kukagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
..............................................................
Wananchi wa eneo la Buza katika  Manispaa ya Temeke Jijini Dar es salaam wameishukuru serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa ujenzi wa kituo cha afya Buza.

Shukrani hizo wamezitoa leo wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo alipofanya ziara ya kushtukiza kituoni akiwa safarini kuelekea wilayani Kibaha kukagua miradi ya  maendeleo.

Alipofika kituoni hapo, Waziri huyo alikutana na umati wa kinamama na watoto wakisubiri kupata huduma katika Majengo yenye changamoto kubwa. 

Akizungumza na wananchi na wagonjwa waliokuwepo Kituoni hapo, Waziri Jafo amesema ameamua kufanya ziara hiyo ili kujionea hali halisi ya wananchi hao wanavyopata huduma ya afya.

“Serikali inatambua changamoto zinazowakabili lakini nimeleta habari njema kwenu kuwa serikali itakiboresha kituo hicho ili kuondoa kero zinazowakabili,”amesema.

Ameeleza kuwa kituo hicho kitajengewa jengo la upasuaji,  wodi,  maabara, jengo la wagonjwa wa nje   ikijumuisha vyumba vya madaktari pamoja na jengo la X-Ray na mradi unaotarajiwa kugharimu zaidi ya sh.Bilioni moja.

Kufuatia hali hiyo, Wananchi hao wameishukuru serikali kwa kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili na kwamba uboreshaji huo utawawezesha waweze kupata huduma bora za afya.

No comments:

Post a Comment