Pages

Friday, March 2, 2018

HALMASHAURI KUUNGA TAASISI ZA UMMA NA REA


PICHA 01
PICHA 02
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani akikagua moja ya maeneo ya mashamba ya wanna vijijini zitakapopitaa nguzo za kusafisha umeme wa REA III.
PICHA 06
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani (katikati) akigawa bure kifaa cha umeme tayari(UMETA) kwa wazee 8 ambapo wanne wanatoka Kijijiji cha Miguha Wilayani Nzega na na wengine 4 kutoka Kijiji cha Matinje Wilayani Igunga mkoani Tabora ikiwa Ni ishara ya kuwahamasisha Wananchi wengine kununua vifaa hivyo.
PICHA 010
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani (katikati) akigawa bure kifaa cha umeme tayari(UMETA) kwa wazee 8 ambapo wanne wanatoka Kijijiji cha Miguha Wilayani Nzega na na wengine 4 kutoka Kijiji cha Matinje Wilayani Igunga mkoani Tabora ikiwa Ni ishara ya kuwahamasisha Wananchi wengine kununua vifaa hivyo.
PICHA 012
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani (kushoto) akiteta Jambo na mbunge wa Manonga katika Kijiji cha Matinje baada ya kukagua Mradi wa REA III, katika wilaya ya Igunga mkoani Tabora.
……………….
Na Zuena Msuya Tabora,
Halimashauri za Wilaya nchini zimeshauriwa kutenga fedha kwa ajili ya kuziunganishia Taasisi za umma huduma ya umeme ya umeme unaotokana na Mradi wa kusambaza wa umeme Vijijini REA  Awamu ya Tatu.
Ushauri huo ulitolewa na Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani wakati wa ziara yake ya
kikazi ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi REA III katika Kijiji cha Miguha Wilayani Nzega na kijiji cha Matinje  wilayani Igunga mkoani Tabora.
Dkt. Kalemani alisema kuwa licha ya Taasisi za umma kupewa kipaumbele katika kuunganishwa na huduma za umeme lakini halmashauri nyingi zimekuwa hasitengi fedha wala kutandaza nyaya katika Taasisi hizo zilizopotiwa na Mradi wa REA III na kusababisha changamoto katika kutekeleza mradi huo pamoja kuwaleta adha wananchi.
Alisisitiza kuwa ni vyema halmashauri zikatumia fursa ya umeme wa REA katika kuziungasha Taasisi za Umma kwa kuwa huduma ya umeme huo hupatikana kwa bei nafuu zaidi tofauti na kuunganishwa kwa gharama za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) .
” Mradi wa REA unapita katika kila Kijiji, Halmashauri zote zinafahamu hili cha ajabu hasitengi fedha kwa hiyo Shule, hospitali na Taasisi zote zinazotoa huduma kwa jamii haziunganishwi na huduma ya umeme, halmashauri tengeni fedha wananachi wapate huduma Bora na kisasa”, alisema Kalemani.
Aliwasisiza Wananchi hasa wasio na nyumba zinazohitaji wiring kuchangamkia fursa ya mradi wa Umeme Vijijini REA III, kwa kutumia kifaa cha Umeme tayari (UMETA) kitakachopatikana bure kwa wateja 200 wa mwanzo watakaolipia na kuunganishwa na huduma ya umeme.
Katika ziara hiyo Dkt. Kalemani alisema kuwa kuanzia mwezi Septemba mwaka huu nguzo za zege zitaanza kutumika ili kumaliza tatizo la kudondoka kwa nguzo zilizochakaa au kuchomwa Moto wakati wa kuandaa msimu wa kilimo.
Aliweka wazi kuwa nguzo hizo zitatengezwa hapahapa nchini ambapo Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) litakuwa na kiwanda cha kutengeneza nguzo hizo pia wawekaji wa ndani na nje wanaalikwa kuanzisha viwanda vyao nchini.
“Nguzo yoyote ya umeme itakayoanguka iwe kwa upepo,kuoza au kuchomwa Moto kuanzia mwezi Septemba mwaka huu mbadala wake itasimamishwa nguzo ya zege hizo zitamaliza kabisa tatizo la nguzo kuangua Mara kwa Mara, nguzo hizi za zege zinadumu muda mrefu japo zinatengezwa kwa gharama kubwa”, alisisitiza Dkt.Kalemani.
Katika hatua nyingine DKt.Kalemani amewaalika wawekazi wa nje na ndani kuwekeza katika mkoani Tabora kwa kuwa Mkoa huo una Nishati ya umeme ya kutosha na ziada ambayo wakazi wake hawawezi kuitumia yote.
Alisisitiza kuwa ni marufuku kwa mkoa huo kuwa na tatizo la Kukatikakatika umeme na endapo itatokea Basi Wananchi waelezwe Nini kimesababisha.

No comments:

Post a Comment