Pages

Monday, May 1, 2017

MVUA ZABABISHA MAPOROMOKO YA ARDHI NA MADARAJA KUKATIKA KISIWANI PEMBA

MITI mbali mbali ikiwa imeanguka katika moja ya sehemu ya Barabara ya Chake-Mkoani, kufuatia mvua kubwa iliyonyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA) Kwa hisani ya ZanziNews
MAGUNIA 518 ya Karafuu Kavu zikiwa hazikuharibika katika ghala la kuhifadhia karafuu la Shirika la ZSTC Mkoani, baada ya ghala hilo kuanguka sehemu ya Ukuta na gunia tisa kufukiwa na dongo zikiwa na karafuu kavu.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
SEHEMU ya Ghala la Kuhifadhia karafuu la ZSTC Mkoani, likiwa limebomoka baada ya kuangukiwa na mti uliokuwa katika mlima na kupelekea Gunia Tisa za Karafuu Kavu zenye thamani ya Zaidi ya Milioni 5 kufukiwa na dongo kutokana na mvua kubwa iliyonyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
WATOTO wadogo wakisafisha kwa kutoa dongo nje katika Msikiti wa Mbuyuni Wilaya ya Mkoani, baada ya sehemu kubwa ya msiki huo kuangukiwa na Udongo ulioporomoka na kuharibu Msikiti, kama unavyoonekana katika Picha.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
WATOTO wadogo wakisafisha kwa kutoa dongo nje katika Msikiti wa Mbuyuni Wilaya ya Mkoani, baada ya sehemu kubwa ya msiki huo kuangukiwa na Udogo ulioporomoka na kuharibu Msikiti, kama unavyoonekana katika Picha.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
WANANCHI wa Mbuyuni Wilaya ya Mkoani, wakitoa msaada kwa kuondosha Udongo, ili kutoa Vitu vilivyofukiwa na Fusi baada ya Nyumba ya Fadhil Amour Mohamed kuangukiwa na Udongo na kutokupata hata kitu Kimoja.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
SOMA ZAIDI »

No comments:

Post a Comment