Pages

Thursday, September 24, 2015

WAZIRI CELINA KOMBANI AFARIKI DUNIA, ALIKUWA NCHINI INDIA AKIPATIWA MATIBABU YA MALERIA ILIYOAMBATANA NA HOMA KALI

NA K-VIS MEDIA 
CELINA Ompeshi Kombani, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Utumishi), amefariki dunia akiwa kwenye matibabu nchini India. Kwa mujibu wa Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai, Marehemu Kombani alipelekwa nchini India mwezi mmoja uliopita akisumbuliwa na malaria iliyoambatana na homa kali.
Kwa mjujibu wa Ndugai, Mh. Kombani ambaye mara ya mwisho alikuwa mbunge wa jimbo la Ulanga Mashariki, amefariki jioni hii ya Septemba 24, 2015 na mwili wake utawasili jijini Dar es Salaam, Jumamosi Septemba 26, 2015.
Mh. Kombani aliyezaliwa 19 June 1959,
alipata elimu yake ya msingi Kwiro kuanzia mwaka 1968 hadi 1975, na baadaye kujiunga na shule ya sekondari Kilakala mwaka 1975 hadi 1978. Mnamo mwaka 1979 alijiunga na shule ya sekondari ya wasichana ya Tabora, (Tabora Girls), na kuhitimu mwaka 1981.

Mwaka 1982, Mh. Kombani alijiunga na Chuo cha IDM Mzumbe na kujipatia shahada ya Utawala wa Umma (B.A in Public Administration mnamo mwaka 1982 hadi 1985. Mwaka 1994 hadi mwaka 1995 Mh. Kombani alichukua shahada ya pili ya Utawala wa Umma, chuo Kikuu ch Mzumbe 

HOUSE GIRL ATOKOMEA NA MTOTO WA BOSI WAKE, HAIJULIKANI ALIKO NA MTOTO HUYO


Picha ya hivi karibuni ya mtoto Loveness C. Jullu
Familia ya Jullu ya Wazo Hill kwa Msabaha jijini Dar es Salaam inaomba msaada kutoka kwa raia wema ili kufanikisha kumpata mtoto wao Loveness Coletha Jullu aliyepotea nyumbani na msichana aliyekuwa akimlea na kusaidia shughuli za nyumbani.

Wawili hao hawajaonekana tangu juzi Jumanne. Taarifa zimefikishwa katika kituo cha polisi na RPC wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni amekiri kupata taarifa za tukio hilo.

Ikiwa una taarifa zozote zitakazosaidia kupatikana kwao tafadhali zitoa kupitia namba hizi: 0715797920 na 0786977615.

Asante.
Binti msaidizi wa kazi za nyumbani (house-girl)

Picha ya awali ya mtoto

 Pichani kutoka kushoto ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Shekh. Khamis Haji Khamis, Rais wa Zanzibar, Dkt. Alhaj Ali Mohammed Shein, Waziri wa Sheria na Katiba wa Zanzibar,Abubar Khamis Bakary Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, na Rais mstaaffu wa Zanzibar, Aman Abeid Karume, wakiwa kwenye baraza la Eid El Hajj, mjini Zanzibar leo Septemba 24, 2015. Waislamu kote Duniani wanasherehekea sikukuu ya Eid El Hajj
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Waziri wa katiba na Sheria Mhe,Abubar Khamis Bakary mara alipowasili katika viwanja vya Chuo cha Amali Mkokotoni katika Mkutano wa Baraza la Eid El Hajj akiwa mgeni rasmi katika baraza hilo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame mara alipowasili katika viwanja vya Chuo cha Amali Mkokotoni katika Mkutano wa Baraza la Eid El Hajj akiwa mgeni rasmi katika baraza hilo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame mara alipowasili katika viwanja vya Chuo cha Amali Mkokotoni katika Mkutano wa Baraza la Eid El Hajj akiwa mgeni rasmi katika baraza hilo leo kabla ya kukagua gwaride rasmi la Sherehe hizo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein akipokea salamu ya heshma ya Gwaride la KIKOSI cha Polisi FFU mara alipowasili katika viwanja vya Chuo cha Amali Mkokotoni katika Mkutano wa Baraza la Eid El Hajj akiwa mgeni rasmi katika baraza hilo leo (kushoto)Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akitoa hutuba yake kwa wananchi wa Zanzibar katika Baraza la Eid El Hajj lililofanyika leo katika Ukumbi wa Chuo cha Amali Mkokotoni Wilaya ya Kaskazini A,Mkoa wa Kaskazini  Unguja ikiwa ni katika sherehe za Sikukuu ya Eid El Hajj
 Mke wa Makamo wa Pili wa rais wa zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi (mwenye miwani) pamoja na Viongozi wengine mbali mbali wakiwa katika ukumbi wa  Chuo cha Amali Mkokotoni katika Mkutano wa Baraza la Eid El Hajj lililofanyika leo,mgeni rasmi katika baraza hilo akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein



Baadhi ya Viongozi na wananchi walioalikwa katika mkurano wa Baraza la Eid El Hajj wakiwa katika ukumbi wa Chuo cha Amali Mkokotoni Wialaya ya Kaskazini A mkoa wa kakskazini Unguja,palipofanyika Baraza  hilo katika kusherehekea Sikukuu ya Eid El Hajj wakati mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Ali Mohamed Shein 
IBADA YA HIJA ENEO LA MINA, NI WAKATI WA KUMRUSHIA MAWE SHETANI
  
KWA uchache Waislamu 717 wamefariki dunia kwa kukanyagana wakati wakitekeleza ibada ya Hija nje kidogo ya Maka (Mecca).
Watislamu wengine 863 wamejeruhiwa kwenye kadhai hiyo iliyotokea wakati Waislamu wanaoshiriki ibada ya Hija, walipokuwa wakitekeleza tendo la kumrushia mawe shetani.
Mkanyagano huo ambao umetokea kwenye daraja la bonde la Minna, kilomita chache kutoka mji mtakatifu wa Maka nchini Saudi Arabia ambapo takriban mahema  160,000, yanayohifadhi mamilioni ya  waumini wa Kiislamu wanaoshiriki ibada ya Hija mwaka huu.
Tukio hilo lilitokea wakati makundi makubwa mawili ya watu, waliokuwa wakijiandaa kutekeleza moja ya matukio ya mwisho ya ibada yalipokutana kwenye “njia panda” (makutano ya barabara), Maafisa wa Saudi Arabia wameviambia vyombo vya habari leo Septemba 24, 2015
Mkanyagano huo uliacha mlundikano wa maiti na majeruhi kwenye mitaa huku joto kali likitawala eneo hilo, Picha za video zimeonyesha.
Zaidi ya waokoaji 4,000 wamepelekwa eneo la tukio ili kusaidia shughulia za uokoaji na kutoa huduma ya kwanza ambapo mamia ya watu waliojeruhiwea vibaya walichukuliwa kwa helikopta na wengine kwenye mamia ya magari ya kubeba wagonjwa.
Vifo hivyo ni vingi mmno kutokea kwenye eneo hilo kwa wakati kama huu, ambapo mnamo mwaka 1990, mahujaji 1,400 walifariki dunia baada ya kutokea mshtuko miongoni mwa mahujaji wakiwa kwenye njia ya chini ya kupitia kuelekea eneo hilo la kumrushia mawe shetani
Lakini pia ni tukio la pili kutokea katika kipindi hiki cha hija, ambapo mwanzoni mwa mwezi huu, zaidi ya watu 100 walipoteza maisha baada ya winchi kubwa lililokuwa kwenye eneo la ujenzi kwenye msikiti mkuu wa Maka, kukatika na kuangukia majengo na watu.
Watu wengine zaidi ya 200 walijeruhiwa kwenye tukio hilo.


Profesa Ibrahim Lipumba, akisalimiana na Hujaji mwenzake kwenye msikiti mkuu wa Mecca, Saudi Arabia, wakati wa ibada ya Hija. 

WAISLAMU WASALI SALA YA EID EL-HAJJ NCHINI
 Waislamu wakiwa kwenye sala ya Eid al-Hajj kwenye uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma, leo Septemba 24, 2015.
 Muumini wa Kiislamu, akichinja mbuzi, ikiwa ni utekelezwaji wa sikukuu ya Eid Al-Hajj, amnbayo inawataka Waislamu kutekeleza sherehe hiyo kwa kuchinja wanyama wanaoruhusiwa kuliwa




 Sheikh Abdu Kadri akiongoza swala ya Idd El Haji katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam leo asubuhi. Waislam wa Tanzania leo waliungana na wenzao duniani kote kusherehekea Sikukuu ya Idd El Haji.
 Sheikh Nurudin Kishki alitohotuba baada ya swala hiyo.
 Sheikh  Othman Dishi akitoa maelekezo kabla ya kuanza kwa swala hiyo.
 Waumini wa dini ya kiislam wakiwa katika swala.
 Wanawake na watoto wakiwa kwenye swala hiyo.
 Mazuria ya kuswalia yakitandikwa kabla ya kuanza ibada.
 Hapa wakitawaza kabla ya kuinza kwa swala hiyo.
Abdurahi Suleiman (kulia), akiuza mafuta na manukato mbalimbali katika viwanja hivyo.
 Ibada ya swala ya Idd El Haji ikiendelea.
 Biashara ya Balaghashia ikiendelea katika viwanja vyao.
 Swala ikiendelea katika viwanja hivyo.
 Pikipiki na baiskeli zikiwa zimewekwa kwa pamoja kwa ajili ya usalama.
 Mwanahabari akichukua picha katika ibada hiyo.
 Waumini wa kiislam wakiwa katika viwanja hivyo wakati wa ibada hiyo.
 Hapa salamu zikiendelea.
 Sheikh Othmani Dishi (kushoto), akisalimiana na Sheikh Abdu Kadri kabla ya kuanza kwa swala hiyo.
 Swala ikifanyika katika viwanja hivyo.
 Swala ikifanyika kwa unyenyekevu mkubwa.

Shirika la Maendeleo Tarime SHIMATA chini ya ufadhiri wa Taasisi ya TWAWEZA kupitia mradi wake wa UWEZO ambao umelenga kufanya kazi ya kutathimini hali ya kielimu katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda linatarajia kufanya tathimini kwa watoto (Wanafunzi na wasio wanafunzi) walio na umri kati ya miaka saba hadi 16 katika Wilaya ya Tarime Mkoani Mara kwa lengo la kubaini hali ya kielimu na changamoto zake ilivyo wilayani humo.
Na:Binagi Media Group
Ili kufanikisha zoezi hilo, SHIMATA imetoa semina kwa wahojaji watakaofanya tathimini hiyo ambayo pia itawafikia wenyeviti wa Mitaa na Vijiji pamoja na Wanakaya pamoja na kupima kiwango cha madini joto katika kaya hizo.

Akifunga semina hiyo iliyoanza juzi Septemba 22,2015 na kutamatika jana Septemba 23,2015 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime, Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Tarime John Marwa ambae alimwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo aliwataka washiriki wa semina hiyo (wahojaji) kuhakikisha wanafanya tathimini hiyo kwa ukweli na uwazi ili kupata majibu sahihi ya kiwango cha elimu katika Wilaya hiyo.
Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Tarime John Marwa
Mwenyekiti wa SHIMATA Joseph Magabe akizungumza katika semina hiyo
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Baada ya semina, mgeni rasmi alikabidhi vyeti vya ushiriki kwa wanasemina
Mratibu wa Twaweza Wilayani Tarime akipokea Cheti cha utambuzi kutoka TWAWEZA
Mwenyekiti wa SHIMATA akipokea cheti cha utambuzi kutoka TWAWEZA
Picha ya pamoja kati ya washiriki wa semina na mgeni rasmi
Picha ya pamoja kati ya washiriki wa semina na mgeni rasmi
Viongozi na Wajumbe wa SHIMATA

No comments:

Post a Comment