Pages

Thursday, September 24, 2015

PAPA FRANCIS AKUTANA NA OBAMA MAREKANI, NI WAKATI WA ZIARA YAKE YA KIHISTORIA NCHINI HUMO


Pope Francis is scheduled to address Americans on the front lawn of the White House on Wednesday. Pictured above on Tuesday at the airport, being welcomed to the U.S. by President Obama  and his family
Baba Mtakatifu Papa Francis akiwa katika mapokezi chini ya  Rais Obama na familia yake
Kwa kawaida marais wa Marekani huwapokea wageni rasmi Ikulu ya nchi hiyo, lakini alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Kijeshi wa Andrews ulioko nje kidogo ya jiji la Washington, Baba Mtakatifu alipata heshima ya kulakiwa na Rais Obama na familia yake.
Mbali na gwaride la heshima, miongoni mwa waliokuweko kwenye mapokezi hayo rasmi ni pamoja na Makamo wa Rais wa Marekani Bwana Joe Biden na aila yake, watoto wa shule, na viongozi wa Kanisa Katoliki.
Akiwa jijini Washington, Baba Francis atafanya mazungumzo na Rais Obama, kukhutubia kikao cha pamoja cha Mabaraza ya Bunge la Marekani pamoja na kuongoza Ibada mbalimbali.
Ziara yake hiyo ya siku sita, pia itamfikisha kwenye miji ya New York na Philladelphia.
Akiwa jijini New York, Baba Francis ambaye ni kiongozi wa nne wa Vatican kuitembelea Marekani, atatembelea Umoja Wa Mataifa na eneo la Kituo Cha Biashara kiclichoteketezwa kwenye mashamulizi ya Septemba 11, 2001.
Kiongozi huyo wa Kanisa la Katoliki, atamalizia ziara yake katika jiji la Philladelphia, ambako anatarajiwa kuhudhuria kwenye Mkutano wa Familia wa Wakatoliki Duniani.
Miongoni mwa mambo yatakayopewa kipaumbele katika mzungumzo na khotuba zake nchini humu, ni pamoja na utoaji mimba, ndoa za jinsia moja, usawa katika maswala ya kiuchumi na kijamii, mazingira na uhamiaji.

 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika mkutano wake wa kampeni  uliofanyika katika uwanja wa shule ya Msingi Kalangalala mjini Geita leo na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi.
Mgombea Urais Huyo amewaambia wananchi wa Geita kuwa mara atakapoingia Ikulu, moja ya changamoto anazotarajiwa kuzipa kipaumbele ni pamoja na suala la kutatua mgogoro wa wachimbaji madini wadogo wadogo.
Magufuli ameasema kuwa akiingia madarakani atawapa maeneo wachimbaji wadogo wa madini nchini ikiwa ni pamoja na kuwakopesha mitaji na kuwapa vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi zao pamoja na mafunzo kwa ajili ya  kuboresha uchimabaji wao ili uwe wa kisasa zaidi na kupandisha  kiwango cha  ufanisi wa kazi zao za uchimbaji.
Dkt. Magufuli leo amehutubia mikutano katika miji ya Runzewe wilayani Bukombe, Katoro wilayani Chato na Geita mjini akiendelea na kampeni zake za kwaomba wananchi kumpa kura za ndiyo ili aweze kuingia Ikulu na kuwafanyia kazi Watanzania kama kiongozi na Amiri Jeshi mkuu wa Tanzania. 
 Sehemu ya umati wa wakazi wa Geita na vitongoji vyake wakiwe kwenye mkutano wa kampeni wa Dkt John Pombe Magufuli uliofanyika jioni ya leo mjini humo. PICHA ZOTE NA MICHUZI JR-GEITA
Wananchi wa mji wa Geita na vitongoji vyake wakiwa wamefurika kwenye uwanja wa shule ya msingi ya Kalangalala,wakimsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi na kumwaga sera zake mbele za wananchi hao ikiwemo pia na kuwaomba ridhaa ya kuwa Rais kwa kushinda kura nyingi ifikapo Oktoba 25 mwaka huu,ambapo uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwandani Wagombea Ubunge wa jimbo la Busanda Mh.Lolensia Bukwimba na Dkt Meedad wa Chato mapema mchana huu alipokuwa akiwahutubia wananchi wa mji mdogo wa Katoro mkoani Geita, kwenye viwanja vya mnada wa Ng'ombe,katika mkutano wa hadhara wa kampeni,ambapo maelfu ya Wananchi wamehudhuria.Dkt Magufuli atahutubia jioni ya leo mjini Geita kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa mji mdogo wa Katoro mkoani Geita mapema leo mchana kwenye viwanja vya mnada wa Ng'ombe,kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni,ambapo maelfu ya Wananchi wamehudhuria.
Wananchi wa Runzewe wilaya ya Mbongwe mkoani Geita wakimsikiliza kwa makini Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akizinadi sera zake na kuwaomba ridhaa ya kuiongoza Tanzania katika kipindi cha awamu ya tano,kwenye viwanja vya mnada wa Ng'ombe,katika mkutano wa hadhara wa kampeni,ambapo maelfu ya Wananchi wamehudhuria. 
 Wananchi wa Runzewe wakimsikiliza Dkt Magufuli alipokuwa akihutubia kwenye mkutano wa kampeni
 Wananchi wa Runzewe wakimshangilia Dkt Magufuli alipokuwa akijinadi na kuomba kurra za ushindi ili aweze kuwa Rais wa Tanzania katika awamu ya tano
 Wakiwa na mabango yao wakishangilia ujio wa Magufuli
 Wananchi wa Runzewe wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alipokuwa akijinadi na kuomba kurra za ushindi ili aweze kuwa Rais wa Tanzania katika awamu ya tano.
Magufuli Style ilitikisa pia ndani ya Geita kwenye mkutano wa kampeni wa Dkt John Pombe Magufuli jioni ya leo????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akikumbatiana kwa furaha na kijana mlemavu wa ngozi Albino Lazaro Malendeka ambaye alikuwa mtumishi wa kikundi cha Red Briged cha Chadema baada ya kujiunga na CCM mjini Geita leo.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwapokea  mlemavu wa ngozi Albino Lazaro Malendeka kushoto ambaye alikuwa mtumishi wa kikundi cha Red Briged cha Chadema baada ya kujiunga na CCM mjini Geita leo na William Mabula Msalaba aliyekuwa mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Geita.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwanadi wagembea ubunge wa mkoa wa Geita katika mkutano wa kampeni uliofanyika mjini Geita leo.
 Wananchi wa Katoro wakiushangilia msafara wa Dkt Magufuli alipokuwa akielekea kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
 Msafara wa Mgombea Urais ukielekea kwenye mkutano wa hadhara ndani ya mji Mdogo wa katoro mkoani Geita. 
 Nyomi
 Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Geita Mama Fatma Mwasa,pichani kati ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza na Mjumbe wa kamati ya ushindi ya CCM mjini Geita wakati wa mkutano wa kampeni leo
 Wakazi wa Geita wakishangilia jambo kwenye mkutano huo wa kampeni.
 Wananchi wa Geita mjini wakifuatilia mkutano wa kampeni
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita na mgombea ubunge wa jimbo la Geita vijijini Ndugu Joseph Kasheku a.k.a King Msukuma akihutubia malefu ya wananchi wa Geita mjini kwenye mkutano wa kampeni wa Urais,ambapo Ndugu Joseph aliwaomba wakazi wa Geita na vitongoji vyake kumchagua Dkt John Pombe Magufuli awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya tano,katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25 mwaka.
 Mgombea Ubunge wa jimbo la Shinyanga mjini Ndugu Steven Masele akimwombea kura Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kwa wakazi wa Geita
 Nyomi la watu likishangilia
 Wananchi wa Geita mjini wakimsikiliza Dkt Magufuli alipokuwa akiwahutubia jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi wa Nyakahura,wilaya ya Biharamulo alipokuwa akielekea mkoani Gieta kuendelea na kampeni zake.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Victoria Mwakasege, ofisini kwake jijini Dar es salaam Septemba 23, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Victoria Mwakasege kabla ya mazunguzo yao ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Septemba 23, 2015


 Balozi wa China nchini Tanzania Bw. Lu Youqing (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC- wa kwanza kulia), Bw. Clement Mshana pamoja na Makamu wa Rais wa Makampuni ya StarTimes, Bi. Guo Ziqi (wa kwanza kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vyombo vya Habari, Uchapishaji, Redio, Filamu na Luninga, Bi. Yang Peili (wa pili kulia) wakifurahia zawadi za vitambaa vilivyonakshiwa na wabunifu wa Tanzania wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Filamu na Tamthiliya za Beijing kupitia kwenye Luninga ya mwaka 2015. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa ni jitihada za kukuza filamu pamoja na uhusiano wa kiutamaduni baina ya nchi hizo mbili.
 Makamu wa Rais wa Makampuni ya StarTimes, Bi. Guo Ziqi (kushoto) akipokea zawadi ya kinyago kilichochongwa na wasanii wa Tanzania kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC- wa kwanza kulia) Bw. Clement Mshana wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Filamu na Tamthiliya za Beijing kupitia kwenye Luninga ya mwaka 2015. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa ni jitihada za kukuza filamu pamoja na uhusiano wa kiutamaduni baina ya nchi hizo mbili.
 Balozi wa China nchini Tanzania Bw. Lu Youqing (katikati) akifurahia jambo na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya StarTimes Tanzania, Bw. Lanfang Liao (kulia) wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Filamu na Tamthiliya za Beijing kupitia kwenye Luninga ya mwaka 2015. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa ni jitihada za kukuza filamu pamoja na uhusiano wa kiutamaduni baina ya nchi hizo mbili.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC- wa kwanza kulia) Bw. Clement Mshana (kulia), akikabidhiwa zawadi ya kinyago.
 Hapa ni furaha tupu katika uzinduzi huo.
Waigizaji wa filamu ya’The Young Doctor’ Zhang Yi na Zhou Fang wakifuatilia matukio wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Filamu na Tamthiliya za Beijing kupitia kwenye Luninga ya mwaka 2015. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa ni jitihada za kukuza filamu pamoja na uhusiano wa kiutamaduni baina ya nchi hizo mbili.

Na Dotto Mwaibale
KAMPUNI ya StarTimes Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vyombo vya Habari, Uchapishaji, Redio, Filamu na Luninga ya Beijing wamezindua maonyesho ya mfululizo wa filamu na tamthiliya mwaka 2015 ambayo yatajumuisha filamu na tamthiliya za kusisimua za kichina barani Afrika.

Kuendelea kwa kukua kwa muingiliano wa tamaduni baina ya watu wa Tanzania na China kumefanya filamu na tamthiliya za China kwenye luninga zijizolee umaarufu mkubwa na kuwa kichocheo kikubwa katika kukuza mahusiano baina ya nchi hizi mbili.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vyombo vya Habari, Uchapishaji, Redio, Filamu na Luninga, Bi. Yang Peili amebainisha kuwa Tanzania itabaki kuwa mshirika wake mkubwa na wataendelea kuimarisha mahusiano yao ya kitamaduni kupitia matangazo ya maudhui ambayo yana nafasi ya kipekee kuwafikia watu wengi zaidi.

”Maonyesho haya ambayo kwa kawaida yatakuwa ni ya filamu na tamthiliya kutoka Beijing kwa kiasi kikubwa yataonyeshwa nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla. Kwa makadirio, jumla ya filamu na tamthiliya 30 za kwenye luninga zitaonyeshwa nchini Tanzania na nchi nyingine za Afrika. Dhumuni kuu ni kuimarisha muunganiko wa maingiliano ya kiutamaduni baina ya marafiki zetu wa Afrika na watu wa China.” Alisema Bi. Peili

Mamlaka ya Vyombo vya Habari, Uchapishaji, Redio, Filamu na Luninga itatoa fursa ya kipekee kwa watazamaji wa barani Afrika kama vile Tanzania, Kenya na Afrika ya Kusini kukutana na washiriki maarufu wa filamu ya ‘The Young Doctor’. Pia wakurugenzi wa mamlaka hiyo watakuwa na wasaa wa kuzungumza na kuyahoji makampuni ya kimataifa ya uzalishaji wa vipindi barani Afrika kwa nchi hizo tatu.

Katika miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia ukuaji wa kasi wa tasnia ya filamu na tamthiliya kwenye luninga na kunufaisha maisha ya watu huku masoko ya tasnia hizo kwa nyumbani yakijulikana kimataifa na kuwa kiungo muhimu katika kukuza muingiliano wa kiutamaduni baina ya nchi husika.

Kama sehemu ya chombo cha uzinduzi wa Maonyesho ya Filamu na Tamthiliya za Beijing kupitia kwenye Luninga ya mwaka 2015, sherehe za uzinduzi zitafanyika nchini Afrika ya Kusini ambapo zitahudhuriwa na mamlaka ya bodi hiyo ya Beijing.

“Maonyesho haya yanafuatilia tukio kama hili ambalo lilifanyika mwaka jana na kuandaliwa na Mamlaka ya Vyombo vya Habari, Uchapishaji, Redio, Filamu na Luninga ambapo Mr. Guo Jinlong,  Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mamlaka ya Kisiasa ya CPC na Katibu wa Kamati ya Mamlaka ya Beijing alihudhuria sherehe ya aina yake alipotembelea nchini Tanzania,” alisema Bi. Peili na kumalizia, “Tamthiliya hizi za Kiingereza za kwenye luninga kama zinavyojulikana miongoni mwa watazamaji wengi zimejizolea umaarufu mkubwa burudani inayopendwa katika nchi nyingi za kiafrika na tunaamini kwa pamoja tunaweza kuziunga mkono tasnia za uzalishaji wa vipindi za nyumbani katika nchi husika ili kuweza kunufaika zaidi kwa pande zote mbili.”

Uzinduzi wa Maonyesho ya Filamu na Tamthiliya za Beijing kupitia kwenye Luninga ya mwaka 2015 utajumuisha vipindi vya luninga maarufu na filamu kama vile ‘The Young Doctor’‘The Sweet Burden’‘The Mi Family’s Marriage’‘Ordinary World’‘Love is Not Blind’’20 Once Again’‘A Wedding Invitation’, na ‘The Left Ear’ambazo zimepangwa kuonyeshwa nchini Tanzania ndani ya kipindi cha mwaka mzima.

Shughuli za kukuza maonyesho haya katika nchi zingine za barani Afrika zikiwemo Kenya na Afrika ya Kusini zitafuatia kulingana na kampuni ya matangazo ya dijitali ya StarTimes ambayo ina mpango wa kuzionyesha kupitia katika ving’amuzi vyao vya antenna na madishi, na kwa uhakika itasaidia kwa kiasi kikubwa itasaidia kukuza utamaduni wa China barani Afrika.
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akijibu baadhi ya maswali kutoka kwa wadau wakati wa kikao cha kujadili rasimu ya Mkakati wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam leo Septemba 23, 2015
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Maimuna Tarishi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali baada ya kufunga kikao cha kujadili rasimu ya Mkakati wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.

               Na Veronica Kazimoto wa MAELEZO

Usajili wa Raia una jukumu la msingi katika kutekeleza matakwa ya utawala bora na maendeleo ya kiuchumi katika taifa lolote lile duniani.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba Maimuna Tarishi wakati akifungua mkutano wa wadau wa kujadili Rasimu ya Mkakati wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Tarishi amesema Usajili wa Raia ni wajibu wa kisheria kwa kuwa unasaidia katika upangaji wa mipango madhubuti ya maendeleo pamoja na kuiletea maendeleo jamiii kulingana na Mkakati wa Kuondoa Umaskini na Kukuza Uchumi Tanzania (KUKUTA II).
Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Katiba na Sheria amebainisha kuwa mfumo wa Usajili wa Raia uliopo sasa Tanzania Bara umekuwa ukifanya kazi kwa kusuasua na hivyo kusababisha baadhi ya wananchi kutotambulika katika kumbukumbu rasmi za kiutawala.
“Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi iliyofanyika mwaka 2012, ni asilimia 15 tu ya watanzania ndio waliosajiliwa na kupata vyeti, hali inayowaacha wengi pasipo kutambulika popote katika kumbukumbu rasmi za kiutawala,” amesema Tarishi.
Ameongeza kuwa usajili ya vifo ndio uko katika hali mbaya zaidi ambapo ni matukio machache ya vifo yanayoandikishwa na sababu za vifo hivyo hazibainishwi kwa usahihi au hazibainishwi kabisa hali inayosababisha ugumu katika kutekeleza majuku kwa upande wa sekta ya afya nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa ambaye ofisi yake ni mdau muhimu wa mfumo huu, amesema lengo la mkakati huu ni kuanzisha mfumo wa Usajili wa Raia ambao unakidhi vigezo vya kimataifa ambao ni wa kudumu na unaofikia watu wote katika kusajili matukio muhimu ya binadamu na kuzalisha takwimu za matukio hayo katika namna ambayo ni endelevu na ya kuaminika.
Dkt. Chuwa amesema mfumo huu wa Usajili wa Raia ukikamilika utasaidia kupata huduma zote za usajili katika sehemu moja kwa vituo vyote vya usajili nchini.
Nae Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi (RITA) Emmy Hudson amesema mfumo uliopo sasa uko mbali na wananchi walio wengi hasa wa maeneo ya vijijini kwasababu ngazi ya chini ya usajili ni ofisi ya  Katibu Tawala wa Wilaya.
Changamoto hii na nyingine inasababisha huduma hii ya usajili kutofika kwa urahisi kwa wananchi walio wengi hali ambayo inaleta uhitaji wa mabadiliko ambayo ili tufanikiwe, RITA inahitaji peke yake haitamudu kuzikabili changamoto za mfumo pasipo kuhusisha wadau mbalimbali katika kuboresha mfumo huu.
Usajili wa Raia ulianzishwa na sheria ya kikoloni mnamo mwaka 1917. Kwa mujibu wa sheria hiyo usajili ulikuwa ni lazima kwa wakazi wa Tanganyika na baada ya uhuru, sheria hii ilirithiwa ambapo licha ya mabadiliko kadhaa ambayo yamekuwa yakifanyika bado wananchi wamekuwa na kasumba ya kutokuona umuhimu wa Usajili wa Raia nchini.

 Mtakwimu Mkuu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Emilian Karugendo, akifafanua jambo wakati wa uwasilishaji wa mada iliyohusiana na hatua za kuandaa Mkakati wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu wakati wa kikao cha wadau kilichofanyika katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam
 Meneja wa Usajili kutoka RITA Angela Anatory akiwasilisha rasimu ya Mkakati wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu katika kikao cha wadau kilichofanyika katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.

 Mwakilishi wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO) Dkt. RufaroChatora akiongea kwa niaba ya wawakilishi wengine wa mashirika ya Umoja wa Mataifa waliohudhuria kikao cha wadau wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.
Picha ya pamoja
LOWASSA ATUA LINDI NA KUIPA "MAUMIVU" CCM, WANACHAMA KADHAA WAKIHAMA
 Waziri Mkuu wa zamani, Fredrick Sumaye, akionyesha kadi za wananchama  3000 wa Chama cha Mpinduzi(CCM)waliohamia Chadema katika mkutano wa kampeni  wa Mgombea Urais wa anayeungwa mkono na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa, (kulia), katika Jimbo la Mtama mkoani Mtwara leo Jumatano Septemba 23, 2015
 Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia Wananchi, katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili,Lindi Mjini , leo Septemba 23, 2015. (Picha na Othman Michuzi na Fidelis Felix).
 Mfuasi wa CCM, akifurahia jambo wakati wa mkutano huo


 Mgombea Urais wa anayeungwa mkono na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),Edward Lowassa akiwa amekaa kwenye kiti maalumu alichopewa kama zawadi  katika mkutano wa kampeni  kwenye jimbo la Mtama mkoani Mtwara






 Wananchi wa Jimbo la Mtama, Mkoani Lindi wakifatilia Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Soko la Majengo, leo Septemba 23, 2015
 Waziri Mkuu wa zamani, Fredrick Sumaye, akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni  wa Mgombea Urais wa anayeungwa mkono na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),Edward Lowassa(kulia) katika Jimbo la Mtama mkoani Mtwara

Wabunge wa  jimbo la Mtama mkoani Mtwara, Isihaka Mchinjita (CUF) na Seleman Luongo(chadema) kulia wakijinadi mbele ya mgombea Urais wa Ukawa, Edward Lowassa 
Umati wa Wananchi wa Lindi Mjini, wakiwa katika Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili, Mkoani Lindi leo Septemba 23, 2015.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI, LINDI.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia Wananchi, katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili,Lindi Mjini, leo Septemba 23, 2015.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini kwa tiketi ya Chama cha Wananchi CUF kupitia Mwamvuli wa UKAWA, Salum Barwany, akimueleza Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, changamoto mbalimbali za wananchi wa Lindi, katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili,Lindi Mjini, leo Septemba 23, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini kwa tiketi ya Chama cha Wananchi CUF kupitia Mwamvuli wa UKAWA, Salum Barwany, katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili,Lindi Mjini, leo Septemba 23, 2015.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini kwa tiketi ya Chama cha Wananchi CUF kupitia Mwamvuli wa UKAWA, Salum Barwany, akiwahutubia Wananchi wa Jimbo lake hilo, katika Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili,Lindi Mjini, leo Septemba 23, 2015.
Sehemu ya Wananchi wa Jimbo la Lindi Mjini, wakimshangilia Mgombea Ubunge wao, Salum Barwany, alipokuwa akihutubia na kukonga nyoyo zao kwa kugusa moja kwa moja changamoto zinazowakabili na namna watakavyoweza kuzitatua iwapo watapata ridhaa ya uongozi.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akifurahi jambo na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini kwa tiketi ya Chama cha Wananchi CUF kupitia Mwamvuli wa UKAWA, Salum Barwany.
Uwanja wa Pilipili ulikuwa ni shangwe tupu, muda wote wa Mkutano.
Waziri Mkuu wa zamani, Mh. Fredrick Sumaye, akiwahutubia wananchi wa Jimbo la Lindi Mjini, kabla ya kumkaribisha Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, katika Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili,Lindi Mjini, leo Septemba 23, 2015.
Sehemu ya Wananchi wa Jimbo la Lindi Mjini, wakiwa katika Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Pilipili,Lindi Mjini, leo Septemba 23, 2015.
Wananchi wa Jimbo la Mtama, Mkoani Lindi wakionyesha furaha yao kwa ujio wa Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Soko la Majengo, leo Septemba 23, 2015.
Vinaja wa Jimbo la Mtama Mkoani Lindi wakiishangilia Chopa anayoitumia Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, kawati ikiwasili kwenye eneo la Mkutano uliofanyika kwenye Uwanja wa Soko la Majengo, leo Septemba 23, 2015.
Pipozzzzzzz........ Pawaaaaa......






Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia Wananchi wa Jimbo la Mtama, Mkoani Lindi, katika Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Soko la Majengo, leo Septemba 23, 2015.
Wananchi wa Jimbo la Mtama, Mkoani Lindi wakifatilia Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Soko la Majengo, leo Septemba 23, 2015.
kadi za wanancha wa CCM zaidi ya elfu tatu (3000) wa Jimbo la Mtama, Mkoani Lindi walioamua kuunga mkono mabadiliko ya UKAWA, zikiwekwa kwenye kiroba baada ya kukabidhiwa.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Waziri Mkuu wa zamani, Mh. Fredrick Sumaye wakionyesha kwa wananchi wa Jimbo la Mtama, Mkoani Lindi, lundo la kadi za wanancha wa CCM zaidi ya elfu tatu (3000) walioamua kuunga mkono mabadiliko ya UKAWA, wakati wa Mkutano wa Kampeni za Mgombea huyo, uliofanyika kwenye Uwanja wa Soko la Majengo, Mtama leo Septemba 23, 2015.







No comments:

Post a Comment