Pages

Thursday, September 24, 2015

Changamoto zinazoikabili mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii Tanzania



Majengo pacha yenye ghorofa 35 kila moja yaliyojengwa na mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii PSPF kama mojawapo ya vitega uchumi kwa kuwekeza kwa malengo ya kulinda thamani ya michango ya wanachama, kupata fedha za uendeshaji wa shughuli za mfuko, kuboresha mafao kwa wanachama na kuchangia juhudi za serikali katika kuinuia uchumi wa nchi.

Na Christian Gaya Mwananchi alhamisi Septemba 24,2015
Wiki iliyopita tuliona baadhi ya changamoto zinazoikabili mifumo ya mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii hapa nchini. Na kwamba mifuko hii ya hifadhi ya jamii mara nyingi imekuwa ikiwekeza kwenye rasilimali ambazo haziwezi kuleta ongezeko bora zaidi, kama vile kwenye ujenzi wa nyumba kwa malengo yanayoyajua wao wenyewe. Na uwekezaji umekuwa ukitolewa kisiasa na siyo kiuakinifu wa miradi.
Kwa wakati fulani imesikika kutoka katika vyombo vya habari mbalimbali ya kwamba kumekuwepo na gharama kubwa zaidi kwa ajili ya kuendesha baadhi ya mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii na ukosefu wa vipingamizi vya matumizi ya utawala na hii imechangia kupungua kwa fedha za akiba au limbiko la mfuko kwa ajili ya majanga na afya na ustawi wa mfuko kwa hatarishi za sasa na siku za usoni
Ukija kwa upande wa utoaji wa huduma bora kwa wateja ni sehemu ambayo imesababisha kutoridhika kwa wanachama wengi na wadau wengine wa mifuko hii ya pensheni ya hifadhi ya jamii.
Na mara nyingi malalamiko haya yamehusisha kwa mafao kidogo yanayotolewa kwa wanachama hasa wastaafu, kuchelewesha kulipa mafao ya muda mfupi kwa wakati muafaka, kukosa taarifa au kumbukumbu muhimu za wakati muafaka zinazohusu mfuko wa pensheni na idadi ya michango iliyochangwa na wanachama na, kiasi cha pensheni na mafao anayotakiwa kulipwa mwanachama au mrithi yaani maelezo ya akaunti ya mwanachama ya uhakika yaani muamala. Mara nyingi kumbukumbu za michango zimekuwa hazijakamilika na wala hazijawekwa kwenye kompyuta na pensheni kutokwenda na mfumko wa gharama ya bei wakati huo inapolipwa.
Kwa upande wa chanya, matumizi ya teknolojia ya habari na masiwasiliano na kampeni za uhamasishaji wa umma juu ya mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii inachangia sana katika kutoa huduma za kijamii
Taratibu na kanuni za mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii zingeliweza kuchangia kiasi kikubwa katika kulazimisha taasisi hizi za hifadhi ya jamii kufanya kazi kulingana na viwango vinavyotakiwa na hivyo kujenga uaminifu wa taasisi hizi kwa wanachama na wadau wengine wa sekta ya hifadhi ya jamii
Kanuni za mazingira ya taasisi za umma na watu binafsi ni za muhimu sana katika kuongeza ukweli na uwazi na kuwalinda wanachama na wadau wa mifuko hii ya hifadhi ya jamii. Pamoja na hayo, kuna uzoefu mdogo sana wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya juu ya jambo la uwazi na ukweli hapa nchini.
Kwa kawaida mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii imeshikiliwa na sheria na kuangaliwa na wizara mama kama vile wizara ya fedha, wizara ya serikali za mitaa na wizara ya kazi na ajira kama wizara mama ingawa zinatakiwa kuangaliwa na wizara moja kama vile wizara ya kazi na ajira na kusimamiwa na kudhibitiwa na wakala wa serikali kuhusiana na masuala yote ya sekta ya hifadhi ya jamii. Pamoja na hayo kuna ongezeko wa mifano ya chambo cha usimamizi na mdhibiti kama vile mdhibiti na msimamizi wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii Tanzania (SSRA)
Pamoja na haya yote, kuna vitu vingine vya msingi ambavyo vinatakiwa kufikiriwa ambavyo ni muhimu na ambavyo vitachangia kuunda muundo wa mfumo wa kisasa na vinavyoweza kukubalika na wanachama na wadau wengine wa sekta ya hifadhi ya jamii
Fikirio la kwanza linahusiana na mahitaji ya kuwa na mfumo wa pensheni wa hifadhi ya jamii unaohusisha pamoja kazi zisizo rasmi, hifadhi ya jamii isiyo rasmi, na kukinga hatarishi zote kama vile mfumuko wa bei, kiwango  cha riba ya uwekezaji, uzee, magonjwa, miaka ya kuishi, kiwango cha kodi, ulemavu, msongo wa mawazo na mfumo wa hifadhi ya jamii unaotekeleza kwa muda muafaka mahitaji yayohitajika kwa sasa na mlengwa kwa haraka kinyume na kukinga majanga ya baadaye au mambo mengine ya hatarishi au majanga, unahitajika mfumo wa hifadhi ya jamii unaojumuisha pamoja familia zaidi ya moja na bila kuwepo mfumo dume.
Na jambo la pili linalogusa na linalosababisha kuwagusa sana wachangiaji wa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii ni pale wanapokuwa wanapoteza uanachama na kinga yao ya hifadhi ya jamii pale wanaondoka au kuhamia mfuko mwingine wa pensheni ya hifadhi ya jamii wakiwa ndani ya nchi na akivuka mpaka na kwenda nchi nyingine. 

Christian Gaya ni mwanzilishi wa kituo cha HakiPensheni Tanzania, mshauri na mtaalamu wa masuala ya pensheni. Kwa maelezo zaidi wasiliana kwa barua pepe: gayagmc@yahoo.com na kwa habari zaidi za kila siku juu ya HakiPensheni unaweza kutembelea tovuti www.hakipensheni  simu namba +255 655 13 13 41

No comments:

Post a Comment