Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey
Mwanri akizungumza na wananchi wa mkoa huo wakati alipokuwa akiupokea
msafara wa kijinsia ulifika mkoani humo kwa lengo la kutoa elimu ya
kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Baadhi ya
Wananchi mkoani Tabora waliojitokeza katika kuupokea msfara wa kijinsia
unaolenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya vitendo hivyo.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey
Mwanri akiwa na wasanii Shetta na G nako wakitumbuiza katika Mtaa wa
Toronto Mkoani Tabora wakati Msafara wa kijinsia unaolenga kutoa elimu
ya mapambano dhidi ya vitendo vya kikatili uliposimama mkoani hapo.
Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW
**************************
Na Mwandishi Wetu Tabora
Mkuu wa Mkoa wa
Tabora Aggrey Mwanri amewataka wananchi wa Mkoa huo kuunga
mkono juhudi
za Serikali katika mapambano dhidi ya vitendo vya kikatili hasa kwa
wanawake na watoto.
Mkuu wa mkoa huyo
ameyasema hayo jana mkoani humo wakati akiupokea Msafara wa Kijinsia
kutokomeza ukatili unaolenga kutoa elimu kwa jamii kuhusu madhara ya
kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia kuelekea Maadhimisho ya Siku ya
Wanawake Duniani yatakayofanyika Kitaifa Simiyu Machi 08, 2020.
Mwanri amesema
kuwa Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa inayoendekeza vitendo hivyo
kwani kumekuwa na mimba na ndoa kwa watoto wadogo wa kike na vilikuwa
vinazidi kushamiri ila kwa kiasi kikubwa wamekabiliana navyo.
“Sisi hatuna
utani na wale wanaofanya vitendo hivi nilishasema nitasukuma ndani
wahusika wote watakaohusika na vitendo vya ukatili wa kijinsia” alisema
Ameongeza kuwa
suala la wananchi kushiriki katika kutoa taarifa juu ya matendo ya
ukatili sio suala la hiari bali ni lazima kwani vitendo hivyo vinatokea
na kufanywa na wanafamilia kwa kiasi kikubwa.
“Wanaofanya
vitendo hivi ni watu wa karibu na familia zetu wanawabaka na kuwalawiti
watoto wetu tunanyamaza kisa ndugu haiwezekani tukaruhusu haya” alisema
Pia Mkuu wa mkoa
huyo amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanawapeleka shule watoto
wao hasa watoto wa kike ambao walisahaulika ili kuwawezesha kupata elimu
itakayowasidia kuondokana na vitendo vya kikatili katika ukuaji wao na
ustawi wa maisha kwa ujumla.
Msafara wa
kijinsia kutokomeza ukatili wa kijinsia upo katika mzunguko ulioanzia
mkoa wa Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa na umefika mkoani Tabora
kuelekea Shinyanga na utapokelewa mkoani Simiyu kuelekea Maadhimisho ya
Siku ya Wanawake Duniani.
No comments:
Post a Comment