Pages

Monday, March 2, 2020

MKURUGENZI BoT TAWI LA ARUSHA AWAASA WAANDISHI WA HABARI ZA UCHUMI NA BIASHARA KUWA WAZALENDO KWA TAIFA


 

Mkurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania Tawi la Arusha, Bw. Charles Yamo, akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina kwa waandishi wa habari za uchumi na fedha kwenye ukumbi wa BoT jijini Arusha Machi 2, 2020.

Meneja Msaidizi wa Uhusiano na Itifaki BoT, Bi. Vicky Msina (katikati) akitoa maelezo ya awali kuhusiana na semina hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa BoT tawi la Arusha, Bw. Charles Yamo na kulia ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango.

Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tafiti za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Misango, akitoa mada kuhusu mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na dunia na matarajio kwa mwaka 2020.

Baadhi ya waandishi wakiwa katika semina hiyo huku wakifuatilia mada mbalimbali zinazowasilishwa na watoa mada.
………………………………………………
Mkurugenzi wa  Benki Kuu ya Tanzania Tawi la Arusha Bw. Charles Yamo amewaasa waandishi wa habari za Uchumi na Biashara kuwa wazalendo kwa taifa wakati wanapofanya
kazi zao za kiuandishi ili wasije kuibomoa nchi kiuchumi kwa kalamu zao.
Bw. Charles Yamo ameyasema hayo wakati akifungua semina ya siku tano kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuhusu habari za Uchumi na Biashara iiliyoanza leo kwenye  ukumbi wa tawi la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Arusha.
Amewataka waandishi wa habari kwa kutumia kalamu zao kutanguliza uzalendo katika kila wanachoandika  kutoka (BoT) kuhusu uchumi na Biashara wahakikishe kinatolewa na Gavana wa au wasaidizi wake ili wasijeandika habari isiyo na taarifa rasmi na kupotosha umma wa Watanzania.
“Hakikisheni Mnakuwa Wazalendo kwa kila mnachokiandika kuhusu BoT ili kulinda uchumi wa nchi kupitia kalamu zenu mnaweza kubomoa uchumi wa nchi kama msipofuata maadili ya kitaaluma na kuwa Wazalendo kwa taifa” Amesema Bw. Charles Yamo.
Bw. Yamo amewataka waandishi wa habari kujiendeleza kielimu na kitaaluma hasa wakibobea katika eneo fulani badala ya kugusa hapa na pale, hii itawafanya kila mnachoandika kiwe makini na kisicho na mashaka kwa wasomaji.
“Naomba mkawe makini kusikiliza kile mtakachoambiwa na watoa mada kuhusu mambo mbalimbali ya Benki Kuu ya Tanzania BoT ikiwa ni pamoja na Sera ya Fedha, Masoko pamoja na Mabenki
Katika Ratiba yenu inaonyesha mtakuwa na ziara ya kutembelea vivutia vya utalii ni jambo zuri.  lakini mimi nawashauri kama itawapendeza mtakapofanya ziara yenu mtembelee viwanda kwa sababu kauli mbiu ya  Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli ni Uchumi wa Viwanda, hivyo ingekuwa ni jambo zuri kama mtatembelea viwanda kadhaa katika jiji la Arusha ili kuona shughuli za kiuchumi zanavyokwenda.
Benki Kuu inathamini kazi inayofanywa na waandishi wa habari katika kuwaelemisha wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya uchumi na biashara ndiyo maana tumekuwa tukipata taarifa mbalimbali kupitia vyombo vyenu vya habari.
Ameongeza kuwa Benki Kuu ya Tanzania itaendelea kushirikiana na vyombo vya habari ili kupitia vyombo hivyo elimu ya shughuli za uchumi na Biashara iawafikie wananchi wengi zaidi hapa nchini hivyo kuelewa kazi za BoT na kuchochea maendeleo katika sekta ya fedha nchini.
Amemaliza kwa kuishukuru idara ya Itifaki na Uhusiano kwa Umma Benki kuu ya Tanzania kwa kuandaa semina hiyo na kufanyika kwenye tawi la (BoT) jijini Arusha ambalo ni tawi kongwe sana , tawi hilo ni la kwanza kati ya matawi yote ya (BoT) nchini na lilianzishwa mwaka 1977.

No comments:

Post a Comment