Pages

Monday, March 2, 2020

IGP SIRRO AWASILI MKOANI MANYARA KWA ZIARA YA KIKAZI



Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akikagua mradi wa ujenzi wa kituo cha Polisi kilichopo wilaya ya Chemba mkoani  Dodoma, leo 02/03/2020 wakati akiwa safarini kuelekea mkoani Manyara kwa ajili ya ziara ya kikazi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (katikati), akizungumza na Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara, Paul Kasabago, wakati akipokelewa na mwenyeji wake kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi mkoani humo leo 02/03/2020.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akitoka katika Ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara, ambapo alisaini kitabu cha wageni na kuzungumza na maofisa wa vyeo mbalimbali na kuwakumbusha wajibu wao katika utendaji kazi, IGP Sirro yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi. Picha na Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment