Pages

Monday, April 1, 2019

WADAU WAKUTANA KUJADILI RASIMU YA KANUNI ZA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA


1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akifungua kikao cha Vyama vya Siasa kupitia na kujadili Rasimu ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwaka 2019.
2
Mwenyekiti wa Baraza la vyama vya Siasa, John Shibuda akizungumza wakati wa Kikao cha kujadili rasimu ya kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019.
3
Baadhi wa wajumbe wakifuatilia ufunguzi wa kikao cha kujadili rasimu ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019.
4
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo (Katikati) akiwa katika picha ya mpamoja naMwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa pamoja na viongozi wengine wa vyama vya siasa vilivyoshiriki katika kikao.
…………………………..
Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo wamewataka viongozi na wawakilishi vya vyama vya siasa kuhakikisha wanatoa maoni yenye
tija ili kutengeneza kanuni zilizo bora zitakazo simamia uchaguzi wa serikali za mitaa.
Aidha, Jafo amesema uchaguzi wa serikali za mitaa unatarajia kufanyika muda wote kati ya Novemba au Desemba mwaka huu.
Jafo aliyasema hayo wakati wa kufungua mkutano wa siku mbili uliokutanisha vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu ambao wana kazi ya kujadili rasimu ya uchaguzi wa serikali za mitaa unaofanyika baadaye mwaka huu.
Alisema Tanzania inaongozwa kwa utaratibu wa demokrasia, hivyo Serikali ilioana kutengeneza  jukwaa la kuwakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo vyama vya saisa ili kuwa na kanuni bora zitakazoendesha uchaguzi kwa amani na utulivu.
“ Nikiwa nimepewa mamlaka hii na Rais John Magufuli, nikaona sio vyema kwa mujibu wa utaratibu wa undwaji wa kanuni hizi lazima tuunde kanuni ambazo zinamchango mkubwa wa wadau mbalimbali ambao utasaidia sana katika mwenendo wa uchaguzi tunaoendana nao
“Tunapokea maoni kutoka kwa wadau, na kundi hili ambalo linawakilisha vyama vya siasa vyenye usajili  ni muhimu sana kwasababu ndio kundi ambalo linachakata kwa muda wote katuni hizi na wenye wajibu wa kuteua wagombea wa nafasi mbalimbali.
Alisema kutokana na umuhimu wa vyama vya siasa katika uundwaji wa kanuni za uchaguzi, ofisi yake ilipeleka rasimu hiyo mapema kwa wadau ili kuweza kupata muda wa kupitia na kuja na maoni yaliyobora.
“Ndio maana nimewapa maelekezo ni vyema kanuni kuwafikia wadau siku chache kabla hatujakutana wapate muda wa kuzipitia ili kupata maoni mazuri.
Aliongeza: “ Wakati mwingine tukipeana kanuni ukumbini, inakuwa sio jambo jema sana na inakuwa kama ni jambo la kuviziana, hili ni jambo letu sote kwa ajili ya nchi yetu, mapema kupata ushauri mzuri ulio bora na kanuni ziwe nzuri na imara ili kuweza kushiriki uchaguzi za serikali za mitaa kwa uzuri.
Jafo alisema kanuni hizo zinamaeneo matatu ikiwa ni pamoja na Rasimu ya Kanuni za Uchaguzi wa mwenyekiti wa kijiji, wajumbe wa halmashauri ya kijiji na mwenyekiti wa kitongoji katika mamlaka ya serikali za mitaa za mwaka 2019.
Alisema pia kuna Rasimu ya uchaguzi wa mwenyekiti wa mtaa, na wajumbe wa kamati ya mtaa katika mamlaka ya miji za mwaka 2019 na Rasimu ya kanuni ya uchaguzi wa mwenyekiti  wa kitongozi katika mamlaka za miji midogo za mwaka 2019.
“ Nimatumiani yangu tutatumia muda vizuri katika kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni na michango mbalimbali kusaidia kuboresha rasimu za kanuni kwa lengo la kukuza demokrasia hapa nchini na utawala bora.
“ Taifa letu ni taifa la mfano, pengine mataifa mengine hayapati jukwaa kama hii la kuweza kubadilishana mawazo hivyo kuzidi kuimarisha demokrasia,” alisema.
Aliongeza: “ Ni imani yangu mchakato utaenda vizuri na utakuwa wenye tija kwa wajumbe kutoa maoni bora ili mwisho wa siku shiriki Novemba au mwishoni wa mwaka huu kwa jinsi Mungu atakapotupa kibari.
Naye Mwenyekiti wa Baraza la vyama vya Siasa, John Shibuda alisema watahakikisha wanatengeneza kanuni zitakazojenga taswira nzuri ya nchi Kitaifa na Kimataifa.
Aliomba katika kikao hicho Msajili wa vyama atoe uwianishaji wa kanuni hizo pamoja na Sheria mpya ya vyama vya siasa ili isijeleta msuguano wakati wa uchaguzi huo.
“Ili kuondokana na dukuduku na sintofahamu kuwepo uwianishaji wa sheria ya vyama vya siasa na kanuni hizi za uchaguzi, tuongeze muda wa majadiliano uwe siku tatu ili tumsikie msajili anasemaje kwenye hili ili isitokee misuguano,”alisema.
Pia Shibuda alipongeza juhudi za Rais John Magufuli za kuimarisha uchumi wa nchini na kuwa wao kama vyama siasa hawana upogu wa macho na akili wa kutambua juhudi hizo.
Jana wajumbe walipitishwa katika rasimu hiyo na watatumia siku ya leo kufanya majadiliano na kesho itakuwa zamu ya asasi za kiraia kutoa maoni yake.
Baadhi ya vyama vilivyotuma wawakilishi ni Chama cha Mapinduzi(CCM), Chama cha Wananchi(CUF), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ARA, Union for Multiparty Democracy(UMD), ACT-Wazalendo, NCCR-Mageuzi, National League For Democracy (NLD), United Peoples’ Democratic Party(UPDP), National Reconstruction Alliance(NRA) na Tanzania Democratic Alliance(TADEA).
Tanzania Labour Party(TLP), United Democratic Party(UDP), Demokrasia Makini (MAKINI), Democratic Party(DP), Sauti ya Umma(SAU), Tanzania Farmers Party(AFP), Chama cha Kijamii(CCK), Alliance for Democratic Change(ADC) na Chama cha Ukombozi wa Umma(CHAUMMA).

No comments:

Post a Comment