Pages

Wednesday, February 27, 2019

SERIKALI YAIGIZA FEDHA ZA MAKUSANYO ZIPELEKWE BENKI KABLA YA KUPANGIWA MATUMIZI


NYAMHANGA MHAND.NYAM
Katibu  Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga,akizungumza  wakati wa kupokea mashine 270 za kieletroniki za ukusanyaji wa mapato (POS) zilizotolewa kwa ajili ya halmashauri 18 za mikoa ya Dodoma na Kigoma kupitia mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (LIC) unatekelezwa kwa ushirikiano baina ya ofisi ya TAMISEMI na Ubalozi wa Dernmark.
OLSEN 1
????????????????????????????????????
Kiongozi wa Mradi Maboresho ya Mazingira ya Biashar Flemming Olsen,akitoa taarifa baada ya kukabidhi  mashine 270 za kieletroniki za ukusanyaji wa mapato (POS) zilizotolewa kwa ajili ya halmashauri 18 za mikoa ya Dodoma na Kigoma kupitia mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (LIC) unatekelezwa kwa ushirikiano baina ya ofisi ya TAMISEMI na Ubalozi wa Dernmark.
MAZUNGUMZO
Baadhi ya Makatibu Tawala wa Mikoa waliohudhuria hafla ya upokeaji wa mashine za Kielektronic POS 270  kutoka kwa Serikali ya Dernmark
????????????????????????????????????
Mkurugenzi wa TEHAMA OR-TAMISEMI Erick Kitali,akitoa  wito kwa halmashauri zilizokabidhiwa Mashine za Kielektronic POS 270 kwa ushirikiano baina ya ofisi ya TAMISEMI na Ubalozi wa Dernmark.
????????????????????????????????????
Kiongozi wa Mradi Maboresho ya Mazingira ya Biashar Bw.Flemming Olsen,(kulia) akimkabidhi Mashine Ya Kielektronic POS kwa Katibu  Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga
????????????????????????????????????
 Katibu  Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga akionesha juu mashine ya Kielektronic POS kwa makatibu Tawala wa mikoa (hawapo pichani) baada ya kupokea mashine 270 zilizotolewa na ubalozi wa Dernmark kwa kushirikiana na Ofisi ya TAMISEMI kulia kwake ni Kiongozi wa Mradi Maboresho ya Mazingira ya Biashar Bw.Flemming Olsen
MCHATTA
Kiongozi wa Mradi Maboresho ya Mazingira ya Biashar Bw.Flemming Olsen akimkabidhi mashine za Kieletronic Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Bw.Rashid Mchatta (katikati) ni Katibu  Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga
????????????????????????????????????
Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw.Kessy Maduka akipeana mkono na Katibu  Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga wakati wa hafla ya kupokea mashine za Kieletronic zilizotolewa na ubalozi wa Dernmark kwa kushirikiana na Ofisi ya Tamisemi (kulia) ni Kiongozi wa Mradi Maboresho ya Mazingira ya Biashar Bw.Flemming Olsen
????????????????????????????????????
Katibu  Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi mara baada ya kupokea mashine za Kieletronic POS 270 zilizotolewa na Ubalozi wa Dernmark kwa kushirikiana na Ofisi ya Tamisemi
NENO LA SHU MCHATTA
Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Bw.Rashid Mchatta akitoa neno la shukran kwa niaba ya wenzake baada ya kukabidhiwa mashine 270 za Kieletronic POS zilizotolewa na Ubalozi wa Dernmark kwa kushirikiana na Ofisi ya Tamisemi.
Picha na Alex Sonna-Fullshangweblog
…………………..
Na.Alex Sonna,Dodoma
Katibu  Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanga amezielekeza mamaka za serikali za mitaa kote nchini kuhakikisha kuwa fedha zote zinazokushwanywa zinawekwa benki kabla ya kupangiwa matumizi.
Mhandisi Nyamhanga alitoa marufuku hiyo wakati wa kupokea mashine 270 za kieletroniki za
ukusanyaji wa mapato (POS) zilizotolewa kwa ajili ya halmashauri 18 za mikoa ya Dodoma na Kigoma kupitia mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (LIC) unatekelezwa kwa ushirikiano baina ya ofisi ya TAMISEMI na Ubalozi wa Dernmark.
Mhandisi amesema kuwa  wakurugenzi wa halmashauri kote nchini wanatakiwa kuhakikisha fedha zote zinazokusanywa zinakwenda benki kabla ya kupangia matumizi.
“Makatibu Tawala wa Mikoa kuweni makini katika ukusanyaji wa mapato ili  kutimiza azma ya serikali ya kuongeza udhibiti na kuleta tija katika ukusanyaji wa mapato katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuhakikisha fedha ilokusanywa inahifadhiwa benki kabla ya matumizi yoyote”Amesema Mhandisi Nyamhanga.
Aidha Mhandisi Nyamhanga ameongeza kuwa jitihada hizi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano zitasaidia kuongeza kipato katika Mamlaka za Serikali za Mitaa na kupunguza utegemezi na kuboresha utoaji wa huduma za kijamii kwa watanzania wote.
Kwa  upande wake Mkurugenzi wa TEHAMA OR-TAMISEMI Erick Kitali ametoa wito kwa halmashauri kuwa na kifaa maalumu cha kuzuia radi ili kutatua changamoto ya mitandao ya mifumo ya mapato kaharibiwa radi kipindi cha mvua  katika halmashauri hizo.
Naye Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa, Dk Charles Mhina amesema kuwa  mradi wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji katika halmashauri za mikoa ya Dodoma na Kigoma, umefadhiri miradi mbalimbali yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 11.013.
Akifafanua baadhi ya miradi iliyotekelezwa kupitia mradi huo, Dk Mhina amesema kuwa wameweza kununua POS 235 kwa thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.95, ambazo zimechangia ongezeko la makusanyo kwenye halmashauri za Mkoa wa Kigoma kwa asilimia 88 katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba 2018 na kwa asilimia 130 kwa Mkoa wa Dodoma.
Aidha amesema kuwa pia umewezesha kujengwa kwa vituo 13 vya utoaji huduma za biashara na uwekezaji kwa gharama ya zaidi ya Sh bilioni 1.45 ambavyo vimepunguza urasimu wa utoaji wa huduma za biashara na uwekezaji na kuongeza idadi za biashara na mapato ya halmashauri.
Naye Kiongozi wa Mradi Maboresho ya Mazingira ya Biashar Flemming Olsen ametoa wito kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania  kuhakikisha mapato yanakusanywa kwa ufasaha kwani kuna wafanya biashara wanabidhaa ya thamani kubwa lakini wanalipa ushuru mdogo.
Wakati huo huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Rashid Mchatta amesema kuwa atakwenda kusimamia vyema mashine hizo ili zifanye kazi ipasavyo na itasaidia kuongeza mapato katika maeneo yao ya kazi.
Katika hafla hiyo Mhandisi Nyamhanga amehitimisha kwa kutoa shukurni za dhati  kwa niaba ya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wananchi wa Serikali ya Denmark kupitia Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania na kusema kuwa ushirikiano wa nchi hizi mbili utaleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment