Pages

Wednesday, January 30, 2019

MGUNDUZI WA MADINI YA TANZANITE MZEE NGOMA AFARIKI DUNIA

 
tanzanittmann_87929-768x576 
Mvumbuzi wa madini ya Tanzanite, Jummane Ngoma amefariki dunia leo Jumatano Januari 30, 2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.
 
Mtoto wa marehemu, Hassan Ngoma amesema, “Ni kweli Mzee amefariki leo jioni hii hapa Muhimbili,” amesema Ngoma 
Hassan amesema kinachofanyika kwa sasa ni kuuhifadhi mwili wa baba yake kisha baadaye watatoa taarifa rasmi ikiwamo utaratibu wa msiba utakuwa wapi na mazishi yatafanyika wapi baada ya kikao cha familia.
 
Aprili 6 mwaka jana, Rais John Magufuli akizindua ukuta wa mgodi wa Tanzanite, Mirerani mkoani Manyara alimzawadia Sh100 milioni kama shukrani kwa mchango wake kwa kugundua madini hayo.
 
m16
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wenginme wakimsikiliza Mzee Jumanne Ngoma akitoa shukurani zake kwa kutambuliwa na serikali na kupewa shilingi milioni 1000 na Rais kama ahsante yake wakati wa sherehe za kuzindua rasmi ukuta kuzunguka migodi ya Tanzanite eno la Mirelani wilaya ya Simanjiro mkoa wa Manyara  Aprili 6, 2018. Picha na Maktaba 

No comments:

Post a Comment